Wewe ni nani?
“Jijaribuni wenyewe kwamba
mmekuwa katika Imani…”
2 Wakorintho 13: 5
Wewe umezaliwa na Mungu kwa mujibu wa Neno
la Mungu, kwa kuwa linaonyesha
vizuri kuwa wewe ni mtoto
wake. Moyo wako uwe na uhakika mbele zake. Kila aliyeligundua Neno la Mungu,
hatahisi na kujua ukweli katika kipindi hicho, katika uwepo wa Mungu, kuwa ni
mtoto wake. Swali, siyo wewe? Ni nani
sasa? Je, Roho ya uwana imo moyoni mwako sasa? Chunguza moyo wako sasa, wewe ni
hekalu la Roho Mtakatifu? Anaishi ndani yako?
Haupo kwenye
kipindi cha pumziko kupitia ubatizo, lakini roho wa Kristo na utukufu wake hayupo
juu yako? Au ule mwanga uliokuwa ndani yako umebadilika na kuwa giza? Kwako
ninasema, “Lazima uzaliwe mara ya pili”. Umesoma alama za
watoto wa Mungu. Wote wasio nazo mioyoni mwao haijalishi wamebatizwa au
hawajabatizwa, lazima wataangamia milele.
Njia ya Maombi
“Basi
ninyi saline hivi”
Mathayo 6: 9
Yeye anayejua
vizuri namna tunavyotakiwa kusali na jinsi tunavyotakiwa kusali, hitaji gani,
jinsi anavyowasilisha. Litampendeza yeye mwenyewe na mazuri yatakuwa yetu. Haya
ndiyo maombi (sala) sahihi na yanayojulikana. Yanaelezea mahitaji yetu yote,
yanaelezea shauku zetu zote kisheria na mwongozo kamili na Roho Mtakatifu yupo
kutuongoza kuomba, kwa vitu; muda mwingine, kwa Neno kwa kifupi, kwa ukaribu,
kikamilifu. Maombi ya sehemu tatu, Utangulizi na hitimisho.
Utangulizi: “Baba
yetu wa mbinguni”. Inajenga msingi wa maombi. Inahusisha jinsi
tunavyomjua Mungu kabla hatujaomba kwa ujasiri, inaonyesha imani yetu, na upendo
wa Mungu na mtu anayemwendea Mungu kwa maombi. “Baba yetu” ambaye ni mwema na
wa neema kwa wote, Muumbaji, anayetutunza, Baba wa
Bwana wetu, tupo kwa ajili yake, ni watoto wake kwa neema, siyo Baba yangu tu
bali Baba wa ulimwengu, malaika na watu wote. “Wa mbinguni” – amekaa
mbinguni na duniani na anatawala kila kitu mbinguni na duniani, anajua kila kimbe
na kazi yake, na kila tukio milele na milele.
Bwana mwenyezi na
mtawala wa kila kitu. Kuomba mkate wa kila siku:- Chakula na neema utupe leo
riziki yetu, Mathayo 6:11, “Jina lako litukuzwe”. Naomba, Ooh Baba, ujulikane
na viumbe vyote kwa ufahamu mzuri, uheshimiwe, upendwe uogopwe
na
watu mbinguni na duniani, na malaika wote na watu wote, “Ufalme wako uje” –
Ufalme wako uje haraka na umeze falme zote za dunia, watu wote wakupokee,
kristo, ufalme wako uaminiwe kwa jina lako.
Watu wafunikwe na
haki, amani, furaha, utakatifu na shangwe mpaka utakapokuja kutuchukua kwenye
ufalme wenye utukufu na kukaa na wewe milele. “Mapenzi yako yatimizwe hapa
duniani kama huko mbinguni” naomba viumbe vyote vinavyoishi duniani vifanye
mapenzi yako kama malaika watakatifu!.
Kanuni ya kila
uhitaji (tamaanio) katika moyo wa mkristo ni utukufu wa Mungu.
(Mathayo 6:9-10) na unachohitaji kwa ajili yako ni mkate, riziki ya kila siku
na nguvu ya ukombozi dhidi ya dhambi (mathayo 6:11-13) hakuna zaidi ya hivyo,
mkristo akafanya mapenzi yake. Kwa hiyo sala hiyo inapeleka matamaanio yetu
yote. Maisha ya milele ni matokeo ya utakatifu.
Mwisho; Ufalme ni
wako “Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu na utukufu hata milele, amina” Mathayo
6:13.
Maombi ya mtu aliyeamka
“Hivyo
husema, amka, wewe usinziaye, ufufuke katika wafu, na
kristo atakutangaza”
Waefeso 5: 14
Jitambue mwenyewe!
Kama wewe ni miongoni mwa maskini wanaojidanganya wenyewe, Amka! Je, ujasiri
wako ni ujasiri unaotokana na nafsi yako mwenyewe ili kukupa ushuhuda kwamba
wewe ni mtoto wa Mungu, na kwamba umewashinda maadui
zako?
Mlilie ili maganda
yaliyopo katika macho yako yadondoke katika macho yako ili uweze
kujijua, kama Mungu anavyokujua wewe: maskini,
usiyestahili, mwenye dhambi. Omba ili uweze kupokea ile hali ya hukumu ya
dhambi mpaka utakaposikia Sauti inayofufua katika wafu,
ikisema “changamka”. Dhambi zako zimesamehewa. Enenda kwa amani; imani yako imekuponya:.
Na Roho wake atakushuhudia kuwa wewe ni mtoto wake.
Omba,
Tafuta, Bisha
“Nami
nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona;
bisheni, nanyi mtafunguliwa”
Luka 11: 9
Wale ambao
wanashauku na neema ya Mungu wanapaswa kuingojea, kwanza, kwa njia ya maombi;
hiki ni kielelezo cha moja kwa moja cha Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe. Katika
hotuba ya mlimani, baada ya kuelezea kwa marefu kila kilichomo ndani ya dini na
kuelezea mapana yake, aliongeza, “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata bisheni, nanyi mtafunguliwa” (Mathayo 7: 7 – 8 na Luka 11: 9-10).
Kwa uwazi zaidi,
tunaelekezwa hapa kwamba ili tuweze kupokea, au kama njia ya kupokea, kutafuta,
ili kupata neema ya Mungu, lulu ya thamani kubwa; bisheni, yaani - endelea kuomba na kutafuta, ikiwa tutaingia katika ufalme wake. Ili
kusiwepo na mashaka yoyote. Bwana wetu anatupa mithali ya pekee ya Baba mwenye
shauku ya kutoa vipawa vyema kwa watoto wake, akimalizia na maneno, “Je, Baba
yenu aliye mbinguni hatawapa Roho Mtakatifu wale wamwombao?” (Luka 11: 13).
Yesu anatupa maelekezo
ya kuomba, pamoja na ahadi ya hakika kwamba kwa njia hii tutapata majibu ya
maombi yetu: “Ingia katika chumba chako cha ndani ... bali mbele za
Baba yako aliye sirini; na ... Baba yako aonaye
sirini atakujaza” (Mathayo 6: 6).
Omba na kuvumilia
“Bwana,
tufundishe sisi kusali”.
Luka 11: 1-2
Mara baada ya Bwana
wetu kujibu ombi (hapo juu) la wanafunzi wake, akiwaonyesha ulazima wa kutumia
maombi, ikiwa tunataka kupokea kipawa kutoka kwa Mungu. Aliwaeleza habari za
mtu alimwomba rafiki yake usiku wa manane, amkopeshe mikate mitatu. Ingawa
rafiki yake hakuamka na kumpa kwa sababu alikuwa ni rafiki yake, bali kwa
sababu ya bughudha isiyokoma. Rafiki yake ataamka na kumpa. Yesu alisema, “Nami
nawaambia, ombeni, nanyi mtapewa”.
Bwana wetu mwenyewe
aliwahakikishia wale wanaolia mchana na usiku; “nawaambia,
atawapatia hiki upesi; walakini atakapokuja mwana wa Adamu, Je! Ataiona imani
duniani?” (Luka 18: 8).
Maombi yanapokuwa uponyaji wa
nafsi yenye giza
“Ee
Bwana, unijaribu na kunipima: unisafishe mtima wangu na moyo wangu:
Zaburi
26: 2
Kwa kufikiri kwamba
uponyaji ni ule ule katika maeneo yote ni kosa kubwa - lakini
linalofahamika kwa wengi. Uponyaji wa kiroho, kama ulivyo wa kimwili-magonjwa
huwa ya namna mbalimbali kama vyanzo vyake visivyofanana. Jambo la kwanza,
kuchunguza kilichosababisha (chanzo). Kilichosababisha ugonjwa
ndicho kinachotoa au kueleza ni tiba gani inayohitajika.
Kwa mfano: Je, ni
dhambi ndiyo iliyosababisha giza? Je, ni dhambi gani? Je, dhamiri yako
inakushitaki kwa kutenda dhambi yoyote ambayo humhuzunisha Roho Mtakatifu? Je,
unaweza kutarajia nuru na amani kurudi bila kuondoa kitu hicho na kupokea
msamaha? Au pengine ni baadhi ya kutofanya uliyopaswa
uyafanye (sin of omission). Je, unawakemea wanaotenda dhambi
mbele yako? Je, unatembea kwa kutumia njia ambazo Mungu amekupa: mbele za watu,
familia, katika maombi ya faragha? Kama ki-mazoea, umekataa majukumu
yanayojulikana, mpaka dhambi (yakutofanya ulipaswa kufanya, au kufanya
uliyokuwa hupaswi kuyafanya) itakapoondolewa, faraja yote ni batili na ya
uongo. Usitafute kuwa na amani moyoni mpaka umekuwa na amani ya mungu, ambayo
haiweze kuwepo bila mazingira ya toba sahihi.
Au je, kuna baadhi
ya dhambi (ndani) ambazo zinainuka kukusumbua? Je, umewahi kufikiri zaidi
kuhusu nafsi yako zaidi ya jinsi ikupasavyo kufikiri? Je,
umejitukuza zaidi kuhusu kitu fulani kuliko Yesu Kriso?
Je, umekuwa na fikra ya kuwa na mafanikio uliyo nayo ni matokeo ya nguvu,
hekima, na ushujaa wako mwenyewe? Kama ni hivyo, ona njia
unayopaswa kuiendea: jinyenyekeze chini ya mkono wa Mungu, na kwa wakati
wake atakuinua.
Maombi ya asubuhi na mapema
“Ee
Mungu, nitakutafuta mapema”
Zaburi 63: 1
Je, unaiona namna
gani siku yako? Wakristo wengi, kama hawana majukumu ya kila siku ya kwenda
kazini, huamka saa bili au saa tatu asubuhi baada ya masaa manane, tisa au
zaidi ya kulala usingizi. Sisemi kwamba wote wanaofanya hivi wanakwenda kuzimu.
Lakini hata hivyo siwezi kusema wanakwenda mbinguni, au wamejikana wenyewe
na kubeba msalaba wao kila siku. Kutokana na uchunguzi wa zaidi ya
miaka sitini, kwa wastani wanaume wanapaswa kulala (kupumzika) si zaidi ya masaa sita mpaka saba, na wanawake wenye afya wanapaswa
kulala (kupumzika) si zaidi ya masaa saba mpaka nane katika saa 24.
Huu muda wa kulala
(kupumzika) unafaida kwa mwili na nafsi; ukilinganisha na madawa yoyoyte
ninayoyajua; madawa ya kinga, na kuondoa dosari za mishipa ya fahamu.
Kumtafuta
Mungu
“Basi
si zaidi damu yake Kristo ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi wa
Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhambi zenu na matendo mafu, mpate
kumwabudu Mungu aliye hai?”
Waebrania 9: 14
Liweke neno hili
ndnai ya moyo wako, kwamba matendo ya kawaida hayawezi kutoa faida. (manufaa
katika maisha ya kiroho) Hakuna nguvu iwezayo kuokoa katika matendo hayo, isipokuwa
katika Roho wa Mungu, na katika damu ya Kristo. Hata kile
ambacho hukitoa kwetu pasipo neema ndani ya nafsi zetu hakiwezi kuwa na faida
bila kumtegemea Mungu pekee. Kwa upande mwingine, yeye anayemtegemea Mungu kwa
dhati hawezi kupungukiwa neema ya Mungu, hata kama ataondolewa katika kila
jambo linalowafanya watu wasiomcha Mungu kuishi duniani.
Katika kutumia njia
zote, mtafute Mungu peke yake na kupitia kitu chochote, tazama pekee nguvu za
Roho wake, na kazi ya ukombozi pale msalabani. Jihadhari, usije ukabaki katika
matendo pekee; ikiwa utafanya hivyo, yote itakuwa
ni kazi isiyokuwa na matunda. Katika neema, hakuna kitu kisichokuwa na Mungu,
kinachoweza kuitosheleza nafsi yako. Kwa hiyo mwangalie yeye katika mambo yote, na yote kupitia yeye, na juu ya yote. Kwa kuwa nguvu zote, na
mafanikio yote yatolewa kwake pekee.
Pia, kumbuka
kutumia njia zote kama njia au namna – kama zilivyokusudiwa na Mungu
na siyo kama jinsi zilivyo kwa namna yake, lakini kwa ajili ya kufanya upya
nafsi (NIA) katika haki na utakatifu wa kweli. Kwa hiyo, kama kweli
zimekusudiwa kufanya hivyo, ni vema; lakini kama si hivyo, ni sawa na kinyesi
(mavi), na hasara.
Ona umuhimu wa kuwa Mtakatifu
“Angalieni
msimkatae yeye anenaye, (kutoka mbinguni)
Waebrania 12: 25
Jitahidi kuingia
katika mlango ulio mwembamba. Strive, (Jitahidi, weka bidii, au juhudi)
katika hali ya uchungu wenye kumcha Mungu imetolewa ahadi ya kuingia katika
starehe au pumziko lake (Angalia Waebrania 4: 9-11). Jitahidi ili
usije ukaikosa starehe au pumziko, jitahidi; yaani katika hali ya kuwa
na shauku, kiu, au kuugua kusikoweza kutamkwa. Jitahidi katika maombi pasipo
kukoma. Wakati wote, mahali popote, uinue moyo wako kwa Mungu. Usimwache
apumzike, kama mwimba zaburi, “Amka na mfano wa Mungu” na kwa njia hii unaweza
kupata utoshelevu.
Hitimisho: Jitahidi kuingia katika
mlango ulio mwembamba. Jitahidi, siyo tu kwa uchungu wa nafsi, wa kushuhudiwa,
wa huzuni, wa aibu, wa shauku, wa hofu, wa maombi yasiyokoma. Jitahidi, vivyo
hivyo kwa kuweka vema mazungumzo yako yote, maisha yako yote, kwa kutembea
kwa nguvu zote katika njia zote za Mungu – njia ya kutokuwa na hatia, kuwa na
rehema. Ondoa kila namna ya uovu. Tenda mema yaliyo ndani ya uwezo wako kwa
watu. Kana (kataa) mapenzi yako katika mambo yote, na kisha chukua msalaba
wako kila siku. Uwe tayari kujitenga na kila kitu kinachoweza kukuzuia, na
kukitupa mbali nawe. Uwe tayari kupata hasara ya mali, marafiki, kiafya katika
mambo yote – hapa duniani – ili uweze kuingia katika ufalme.
Mngojee Bwana
“Nafsi
yangu yamngoja Mungu peke yake”
Zaburi 62: 11
Kwa ujumla wakristo
wamekuwa na mapokeo ya kutumia baadhi ya sala au maombi. Sasa, labda wewe ni
mmoja ambaye bado unaendelea kutumia namna hiyo ya maombi kama ulivyokuwa
mtoto. Lakini, hakika kuna “njia iliyo bora” (1 Wakorintho 12: 31)
ya namna ya kuwa mbele za Bwana Mungu. Tathmini hali yako ya ndani naya nje na
kisha ulinganishe na maombi unayoomba.
Kwa mfano, wewe ni
mtu mwenye afya, mtulivu, na una aina za mahusiano,
majirani wema, na uhusiano mzuri na marafiki. Ni wazi kwamba, haki yako ya nje
huwafanya watu wakusifu na kuona kwamba wewe ni mtu mwema na mwenye sifa kwa
Mungu.
Upande mwingine,
kama umo katika dhiki (maskini), au mhitaji, udhia, hatari, au katika maumivu
au Ugonjwa, na utamimina moyo wako mbele za Mungu kupitia maombi sambamba na
hali yako.
Vivyo hivyo,
kujitoa katika maombi yako kutaendana na hali yako ya ndani, au hali ya ufahau
wako. Je, wewe ni mzito, pengine
kutokana na hali ya dhambi au kutokana na majaribu mbalimbali? Hivyo maombi
yako sharti yawe na sehemu ya kuungama, kusali na dua ambazo zinakubaliana na
hali ya ufahamu ulio na taabu.
Tofauti na hapo,
je, una amani katika nafsi yako? Je, unamfurahia Mungu? Je, faraja zake ni kuu
juu yako? Basi, useme na mwimba zaburi “wewe ni Mungu wangu, na nitakupenda.. nitakusifu”.
Kusoma na kutafakari zaburi ya sifa kwa kawaida kuinua moyo wa shukurani “Njia
iliyo bora zaidi” kuliko yoyote.
Usijisumbue kwa lolote
“Kwa
kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme”
Luka 12: 32
Ni kwa kiasi gani inaweza
kupendeza Baba wa mbunguni kutupatia vyakula na mahitaji yetu? Kwa kuwa mna
urithi huu, msifikiri au kusumbuka na mali za dunia. Vivyo hivyo, Mtume Paulo
aliwaandikia (Wafilipi 4: 6), “Msijisumbue kwa neno
lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba pamoja na kushukuru na haja
zenu zijulikane na Mungu”. Kama wanadamu hawatakuwa wanyenyekevu kwako, hata
kama si katika hili au jambo jingine lolote, usijisumbue, lakini omba.
Uangalifu na maombi
haviwezu kukaa pamoja. “katika kila neno omba” liwe kubwa au dogo “haja zenu na
zijulikane na Mungu”; na wale kwa ajili ya aibu au kujifunika na
kutokuwa waaaminifu, wakiendelea katika shauku zao, kama kwamba walikuwa wadogo
sana au wakubwa sana, lazima waangaliwe kwa makini. “Kwa Mungu” - mara zote si sahihi kuyaweka wazi (kuwajulisha wanadamu) mbele za watu
“kwa kusali” ambayo ni kwa mapana na kuzidi kusihi kwa dua “Na kushukuru” - uhakika wa hali ya juu wa nafsi iliyo huru kutoka katika taabu na
maombi ya kudhiri kwa kweli.
Na hii hali ya
shukurani hufuatwa na amani. Amani na shukurani huwekwa pamoja (Wakolosai 3: 15).
“Kesho itajisumbukia yenyewe”. Hivyo uwe mwangalifu an kesho ijapo. Leo uwe
huru mbali na masumbufu.
Ukane au ukatae u-mimi ili
kumtii Bwana
“Mkiwa
na juhudu katika roho … katika kweli”
Warumi 12: 11-12
Huyu ni mmoja
ambaye hajaitupia mbali (kuikana) iman. Ambaye bado ana roho ya kufanywa mwema,
ambayo huendelea kushuhudia na roho yake kuwa yeye ni mwana wa Mungu. Hata
hivyo haendelei katika ukamilifu. Haendelei, kama hapo awali, akiwa na njaa na
kiu kuifuata haki; akitaka sana kuwa na sura ya Mungu na utimilifu
wa wote wa kumfurahia Mungu kama Ayala aioneavyo
shauku mito ya maji (zaburi 42: 1). Vinginevyo ni udhaifu na
amezimia na kuchoka katika ufahamu wake, akiwa ameatamia kati ya Uhai na mauti.
Kwa nini yako
hivyo? Kwa sababu amelisahau neno la Mungu, ambalo husema kwamba “na kwamba
imani ile ilikamilishwa kwa njia ya matendo yake” - (Yakobo 2: 22). Hatumii bidii
yake yote katika kufanya kazi ya Mungu. Wala haendelei katika maombi ya mara
kwa mara – yeye binafsi au kujumuika na wengine. Vile vile amepungua katika
kushiriki ushiriki wa meza ya Bwana, au kusikia Neno la Mungu, katika
kutafakari, kufunga, na kuhudhuria makongamano ya kikristo. Kama huwaachii
baadhi ya njia hizi za neema, angalau huwa hazitumii kwa bidii.
Kwa nini sasa,
haendelei katika maombi? Kwa sababu katika nyakati za ukame, ni ngumu na ni
taabu kwake. Huwa hawaendelei kusikiliza neno la Mungu katika nafsi
zote huupenda usingizi. Kwa hiyo imani yake si kamilifu, wala hawezi kukua
katika neema, kwa sababu hataweza kujikana mwenyewe na kuubeba msalaba wake.
Maombi – silaha ya kuvaa kama
taji
“Kwa
sala zote na maombi – mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo… na
kudumu kuwaombea watakatifu”
Waefeso 6: 18
Kielelezo cha
silaha zote za Mungu kinatuonyesha jinsi inavyopendeza kuwa mkristo. Upungufu
wa kimojawapo hutufanya tusiwe wakamilifu. Ingawa anaweza kuwa na kweli
ki-imani, akawa na dini, viatu miguu, ngao ya imani, upanga wa Roho; hata hivyo
kitu kimoja zaidi kinahitajika: mkisali kila wakati: wakati wote na katika
matukio yote, katikati ya matendo (shughuli zote, kwa ndani “Omba bila kukoma”
“By the spirit” - kupitia ushawishi.
“Kwa sala zote”
yaani maombi ya namna zote: katika ibada, faragha, katika ufahamu, kwa sauti.
Usiwe na bidii tu katika aina moja ya maombi na kisha ukaweka aina
nyingine; ikiwa tunataka shauku za maombi yetu kujibiwa, tutumie njia zote.
Baadhi hutumia maombi ya akili (ufahamu) tu, wakidhani kwamba ni njia ya
kuabudu iliyo bora kuliko nyingine. Lakini inahitaji neema ya juu zaidi ili
kuwezeshwa kumiminika maombi ya kung’anga’ania na yanayoendelea
– kuliko kutumia maombi ya akili.
“Kuomba” – kurudia
na kuhojiana katika maombi kama Kristo alivyofanya katika bustani ya Edeni’
“kesheni” - kwa ndani haya maombi yamekusudia Mungu, kujua
mapenzi yake, na kupata nguvu za kuyafanya hayo mapenzi ya Mungu na kufikia
Baraka tunazozionea shauku. “Kudumu katika kuwaombea watakatifu wote” endelea
mpaka mwisho katika zoezi hili takatifu ili wengine waweze kufanya mapenzi ya
Mungu na kuwa imara. Pengine tunapokea majibu machache ni kwa sababu hatufanyi
maombezi ya kutosha kwa ajili ya wengine.
Furahini siku zote: Omba
shukurani
“Furahini
siku zote; Ombeni bila kukoma:
Wathesalonike 5: 16-18
“Furahini siku zote”. Katika furaha
isiyoingiliwa katika Mungu. “Ombeni bila kukoma” ambayo ni tunda la “furahini siku zote” katika Bwana. “Shukuruni kwa kila jambo”,
ambalo ni tunda la yote yaliyopita. Huu ni utimilifu wa
kikristo. Zaidi ya hapa hatuwezi kwenda, na hatupaswi kupungukiwa vitu hivi - (furaha na maombi).
Bwana wetu alinunua
furaha na haki, kadhalika, kwa ajili yetu. Ni mtindo wa
Injili, kwamba kuokolewa katika hatia, tunapaswa kuwa na furaha katika Kristo.
Maombi yanaweza kusemwa, kama pumzi ya maisha yetu ya kiroho, yeyote anayeishi
hawezi kuacha kupumua. Hivyo ni zaidi sana tunapokuwa tumefurahia uwepo wa
Mungu, ni zaidi sana katika maombi na sifa tuzitoazo “Bila kukoma”,
vinginevyo furaha yetu itakuwa kama kiini macho tu.
Shukurani haiwezi
kutengwa na maombi ya kweli, imeunganishwa ki umuhimu na maombi. Yeyote
anayeomba hutoa sifa, iwe ni kwa raha au maumivu au kwa sababu ya mafanikio, au
kwa shida nzito. Humbariki Mungu kwa mambo yote, huwatazama
wanapokuwa wakimwendea, naye huwapokea kwa ajili yake mwenyewe tu si kwa
kuchagua, wala kukataa, kwa kupanda, au kwa kutopanda, iwe chochote, lakini tu
kama inakubaliana au kutokukubaliana na mapenzi yake
makamilifu.
“Katika hili” –
kwamba mnapaswa kufurahi, kuomba, kutoa shukurani, “ni mapenzi ya Mungu” wakati
wote ni mema, mara zote hutuelekeza kwenye wokovu wetu!.
Maombi na neema
“Mkiishi
kujitakasa roho zetu kwa kutii kweli”
1 Petro 1: 22
Ni jambo
lisilopingika kwamba kristo ndiyo njia pekee ya neema. Nina jibu, hii ni njia
ya kawaida ya kutumia maneno. Elezea neno lenyewe, na hali ya kupinga ukweli
huu hutoweka. Tunaposema” maombi ni njia ya neema”, unamaanisha kuwa yeye ndiye
gharama na mnunuzi wa neema hiyo, kwamba “hakuna ajae kwa Baba isipokuwa kwa
njia ya yeye”. Ni nani anayeikana kweli hii?
Lakini andiko
(limepingwa pia) halitudekezi kungojea wokovu? Je, Daudi hasemi “nafsi yangu
yamngoja Bwana; na kutoka kwake napaka wokovu? Je, Isaya hatufundishi jambo
lile lile, akisema, “Ee Bwana tumekungoja?” haya yote hayawezi kupingwa,
kukanika. Bila mashaka, tunapaswa kumngoja Bwana, lakini tutamngoja kwa namna
gain? Je, tumeweza kupata njia iliyo bora zaidi ya kumngoja Bwana kuliko ile
ambayo yeye mwenyewe ameichagua? Tafakari vema maneno ya Nabii Isaya. Sentensi
yote inasema, “naam katika njia ya hukumu zako (maagizo) sisi tumekungoja
ee Bwana”. Na Daudi naye alimngoja Bwana kwa mamna hiyo: “Ee Bwana unifundishe
njia ya amri zako, nami nitaishika hata mwisho”
(Zaburi 119: 33).
Omba kwa Imani
“Ila
na aombe kwa imani pasipo shaka yoyote”
Yakobo 1: 6
Kuhusu matumizi ya
maombi kama njia ya neema, maelekezo ambayo Mungu ametupa kupitia Mtume Yakobo
yako wazi kabisa. Pamoja na maombi ya kila aina, ya kusanyiko au faragha, na
Baraka huambatana naye, anasema, “Lakini mtu wa kwenu amepungukiwa na hekima, na
aombe dua kwa Mungu, awapaye wote kwa ukarimu, wala hakemei naye atapewa”
(Yakobo 1:5). Kama wakiomba; vinginevyo “wala hamna
kitu kwa kuwa hamuombi” (Yakobo 4:2). Ikiwa wataomba, hawakemei, lakini
anasema, “naye atapewa” - (Yakobo 1:5).
Kwa sababu Mtume
anaongeza, “aombe kwa imani” baadhi wanaweza kupinga na kusema kuwa haya siyo
maelekezo kwa wasio amini (wanaotafuta), kwa wale wasiojua neema ya msamaha wa
Mungu. Nimejibu, maana ya neon “FAITH” (Imani) katika sehemu hii limewekwa na
Mtume Mwenyewe, kwa kusudi la kudhibiti upinzani huo. Maneno yanayofuata baada
ya hapa ni “Kutokuchukuliwa na mawimbi”, bila mashaka. Asione shaka lakini
Mungu asikie maombi yake na kutimiza shauku ya moyo wake; kutampa
neema, kwa hekima anayoomba.
Lazima tuhitimishe,
kuomba andiko linaloonyesha kwamba wote walio na shauku ya neema wanapaswa
kuingoja kwa njia ya maombi.
Maombi ya familia
“Na
hao walio wenye hekima katika watu watafundisha wengi”
Daniel 11: 33
Tunandaa nyumba
zetu katika utumishi kwa kuwafundisha watu wa familia zetu. Tunahakikisha kuwa
kila mtu katika dari zetu anakuwa na maarifa ya msingi ili kupata wokovu. Ni
wajibu wetu kuona kwamba wenzi na watoto wetu wamefundishwa mambo ambayo
yanahusiana na amani ya milele. Panga, hasa katika siku ya Bwana, ili kwamba
wote waweze kuhudhuria ibada kwa ajili ya mafundisho. Vile vile kuhakikisha kwamba wana muda wa kusoma Neno, kutafakari, na
kuomba. Isipite siku yoyote pasipo familia kuomba kwa kumaanisha.
Kadhalika, unapaswa
kujitahidi kuwafundisha watoto wako mapema, waziwazi, mara kwa mara na kwa
uvumilivu. Mtoto anapoanza kuongea, unaweza kuwa na uhakika
kwamba lengo la mafundisho linaanza kufanyiwa kazi kuanzia muda huo, usipoteze
muda wa kusema mambo ya Mungu. Lakini ongea kwa uwazi, ukitumia
maneno ambayo watoto wanaweza kuyaelewa-ambayo hutumiwa na watoto.
Fanya hivyo mara
kwa mara, inua moyo wako kwa Mungu ili afungue ufahamu wao
na kumimina nuru yake ndani yao. Lakini haya yote hayawezi kuwa na ufanisi bila
kuvumilia. Kamwe usiache mpaka umeona matunda ya mafundisho yako kwa
watoto. Kufanya hivi, unahitaji kuvikwa uweza kutoka juu. Pasipo hili,
ninashawishika kusema, hakuna yeyote ambaye anaweza kuwa na utoshelevu wa
uvumilivu kwa kazi hiyo.
Kujenga kwa maombi na Imani
“Kwa
maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki”
Warumi 10: 10
Rafiki, chukua
hatua zaidi, usiridhike na matendo mema: kuwalisha wenye njaa, kuwavika walio
uchi, kuwatembelea yatima na wajane katika dhiki zao, au wagonjwa na hao wali
magerezani, na wageni. Je, una hubiri kweli ya Yesu katika jina la
Kristo? Je, ushawishi wa Roho Mtakatifu na nguvu za Mungu hukuwezesha kuwaleta
wenye dhambi katika nuru, kuwatoa katika nguvu za shetani na kuwaleta katika
nguvu za Mungu?
Kisha nenda na
ujifunze ulichofundisha: kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani;…
wala si kwa matendo…. Bali kwa rehema zake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa mara ya
pili na (Waefeso 2:8, Tito 3:5)
Jifunze kuweka yote
juu ya msalaba, huku ukihesabu yote uliyofanya kuwa ni uchafu na kinyesi. Kama
unaamini, omba, bwana Oo niongezee imani. Au kama huna imani, omba nipe imani
hii, ingawa imekuwa ni kama punje ya haradari. Ni imani tu iokoayo, imani
ambayo hujenga juu ya mwamba, simama imara wakati mafuriko
na upepo vinapovuma. Na hii imani iokoayo ndiyo hasa
hudhihirika katika matendo mema ya haki.
Baba yako anajua
“Maana
Baba yenu anajua mnayoyahitaji kabla ninyi hamjamwomba”.
Mathayo 6: 8
Katika maneno yake,
kabla ya maneno hayo, Bwana wetu alikuwa akionya dhidi ya kurudia rudia.
Kurudia maneno yeyote pasipo kumaanisha ni kurudia bure. Kwa hiyo, tunapaswa
kuwa waangalifu katika maombi yote ili kumaanisha tunachosema na tunasema tu
kile tunachomaanisha katika mioyo yetu.
Hii ni sababu ya
msingi kwa nini wengi hukiri kidini, ni aibu. Hakika
maneno yote katika ulimwengu si sawasawa na shauku takatifu. Maombi mazuri au
yaliyo bora ni yale yanayotokana na maneno yanayorudiwa ambayo ni lugha ya
Mungu ndani ya moyo wa mwamini.
“Na Baba yenu
anajua yale mnayoyahitaji”. Hatuombi ili kumjulisha Mungu mahitaji yetu. Anayajua
yote kama alivyo, hahitaji kujulishwa kitu chochote ambacho hakukijua hapo
kabla. Na mara zote yuko tayari kutupatia mahitaji yetu. Kitu kikubwa
tunachopungukiwa ni ili nafsi ya kupokea neema na Baraka zake. Na kusudi moja
kuu la maombi ni kuonyesha hali ya kutokustahili ndani yetu ili kumtegemea
Mungu, na kuongeza shauku ya vitu tuviombavyo, na kutufanya makini na mahitaji
yetu ili tusije tukaacha kupambana mpaka tupate ushindi ili kupata Baraka zetu
(Mwanzo 32:24- 30).
Kuomba ili kuondoa giza
“Maana
moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu, wala kuwahuzunisha”
Maombolezo 3: 33
Pamoja na sababu
mbalimbali za hali ya jangwa, siwezi kuthubutu kupinga au kwenda kinyume na
mapenzi ya Mungu kwa sababu yeye hufurahishwa na mafanikio ya watumishi wake na
hapendi kuwahuzunisha au kuwatesa wanadamu. Mapenzi yake huleta utakaso katika
maisha yetu, kamwe hapendi kuondoa vipawa katika maisha yetu. - (Warumi 11:29); kamwe hatuachi, kama baadhi wanavyosema bali sisi ndiyo
tunaomwacha.
Sababu kuu na
inayofahamika ya kuwa na giza ndani yetu ni dhambi za namna Fulani, pengine ya
kutotenda tuliyopaswa, au kutenda tusiyopaswa.
Hii dhambi huwa na
lengo la kutia giza katika nafsi ya mtu, hasa kwa ile dhambi inayojulikana, kwa
makusudi; lakini mara kwa mara, nuru hutoweka ili kuipa nafsi dhambi ya
kutotenda aliyopaswa mtu kutenda. Mara nyingi dhambi hii Roho Mtakatifu huiondoa kwa haraka, lakini ni kwa taratibu sana. Iwapo
Kutokuwa
na maombi ya faragha, au kuomba kwa kurashiarashia. Pengine
inaweza kuwa ni dhambi ya kutotenda yaliyopaswa kutendwa. Upungufu huu hauwezi
kutokana na njia nyingine; na matokeo yake ni uhai wa Mungu huanza kuoza na
kutoweka kwa taratibu.
Kutokutenda kwa
namna nyingine ambako kunaweza kuleta giza ndani ya nafsi ya mwamini ni
kutokumkemea “jirani” tunapomwona amekosa lakini tunachukua dhambi kwa ajili
yake - (Mambo ya walawi 19:17). Kwa kuacha kumrudi au
kumuonya, tunaifanya dhambi yake kuwa yetu. Hivyo tunawajibika kwa hilo. Kwa
sababu hiyo tumekuwa tukimhuzunisha Roho Mtakatifu, na kupoteza nuru ya
mwangaza wa sura yake.
Maombi kama ya neema
“Lakini,
kueni katika neema na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo”
2 Petro 3: 18
Njia kuu za neema
ni maombi (yawe ya faragha au katika kusanyiko); kuchunguza
maandiko (ambako hujumlisha kusoma, kusikiliza, na kutafakari Neno la Mungu);
kushiriki meza ya Bwana (kula mkate na kunywa divai kwa kumbukumbu
ya Bwana Yesu). Haya yanaaminika ni njia za kuleta maana
yake katika nafsi zetu.
Ndivyo ilivyokuwa
katika kanisa la kwanza, lakini kadri muda ulivyokuwa unaendelea upendo wa
wengi ukapoa. Baadhi wakaanza kukosa kwa kutumia vibaya, na kuiweka dini kwa
kufanya yale mambo yaliyoonekana kwa macho badala ya kufanya
yale ambayo ni matokeo ya moyo uliofanywa upya katika sura ya Mungu. Sasa,
uthamani wa njia hutegemea hasa utumishi wao wa kidini. Hivyo njia hizi
zote-zinapoondolewa au kutengwa zinakuwa hazina maana. Ikiwa hazituleti au
kutuongoza katika kumjua na kumpendeza Mungu hazikubaliki mbele za
Mungu. Hazina tofauti na machukizo na uvundo katika pua zake. Huchoshwa nazo.
Na zinapotumika ili kujaribu kutimiza matakwa ya kidini ambayo wanapaswa kuyatumikia,
huugeuza mkono wa Mungu kinyume chao na kuuondoa ukristo
nje ya moyo badala ya kuwa njia inayoingia ndani ya mioyo.
Kuomba rehema
“Si
kwa katika uwezo wa yule atakaye, bali wa Yule arehemuye, yaani Mungu:
Warumi 9: 19
Wokovu kwa njia ya
imani ni fundisho lisiloleta furaha kwa wale ambao hujihesabia haki - (self-righteousness). Shetani huongea kama alivyo
bila (kweli au aibu) anapotamka kutokufurahishwa, kwa kuwa wokovu kwa njia ya
imani ndiyo fundisho pekee lenye kufurahisha, limejaa faraja kweli, kwa wote
walijiharibu maisha yao, na wanaojihukumu kwa dhambi zao, yeye amwaminiye hata
aibika: na Bwana yule yule ni juu ya wote
– ni tajiri kwa wote wamwitao. Hii ni faraja iliyo juu zaidi ya mbingu, yenye
nguvu kuliko mauti!.
Kwa nini!
Huwarehemu wote? Kwa zakayo, aliyekuwa mtoza ushuru kwa udanyanyifu? Kwa
mariamu Magdalena, na kwa mwanamke mzinifu? Hivyo, mtu anaweza kusema, “Ni mimi,
naweza kutarajia rehema zake!” Na wewe unaweza, uliyeteswa,
usiyekuwa na mtu wa kukufariji Mungu hatayadharau maombi yako.
Labda anaweza
kusema, sasa ijayo, “changamka, dhambi zako zimesamehewa” Umesamehewa kiasi
kwamba hazitakutawala tena. Ndiyo, na Roho Mtakatifu
atakushuhudia katika roho yako kwamba wewe ni mtoto wa Mungu.
Habari njema ya
furaha ku iliyoletwa kwa watu wote! Kwake yeye aliye na kiu, njoo unywe
maji; na wewe usiyekuwa na pesa, njoo, ununue, na ule - (Isaya 55:1). Dhambi zako zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama
sufu, ikiwa zitakuwa zaidi ya nywele au kichwa chako (idadi), mrudie Bwana, na
atakurehemu; naye atakusamehe.
Maombi kupitia majaribu
“Basi, Bwana ajua kuwaokoa
watauwa na majaribu”
2 Petro 2: 9
Kama giza
limesababisha majaribu mengi, mazito na yasiyo tarajiwa; njia pekee ya kuondoa
na kuzuia ni kuwafundisha wakristo kutarajia majaribu wakati wowote. Wanaishi
katika ulimwengu wenye uovu, katikati ya waovu, wenye roho za uchafu, na wenye
mioyo ya kutenda uovu. Wanapaswa kushawishika kwamba kazi yake ya utakaso kwake
si timilifu kwao, kama wanavyodhani; bali ni mchakato kupitia mambo hayo
wanapoamini mara ya kwanza, kama watoto wachanga ambao hukua taratibu.
Wanapaswa kutarajia dhoruba nyingi kabla ya kufikia utimilifu wa kimo cha
kikristo.
Zaidi ya yote
wafundishwe, dhoruba hii inapokuwa juu yao, hawapaswi kutafakari
pamoja na shetani bali ni kuomba. Na wamimine mioyo yao kwa Mungu na
kumwonyesha shida zao. Watu wa jinsi hii wanapaswa kutumia ahadi kuu na za
thamani. Siyo kwa wajinga, mpaka ujinga utakapoondolewa.
Kwa wale
waliojaribiwa, tunaweza kutangaza wema wa Mungu wetu. Unategemeana
na uaminifu na nguvu zake katika damu iliyomwagika kwa ajili yetu ili kutusafisha
dhambi zetu. Mungu atalishuhudia neon lake na kuwatoa katika shida zao.
Atasema, “Amka, uangaze; kwa maana nuru yako imekuangazia”. Hakika, hiyo nuru,
ikiwa utatembea kwa unyenyekevu na kuwa na Mungu, itakuangazia
zaidi katika siku kamilifu (Ona Mithali 4:18).
Maombezi ya Yesu kwa ajili
yetu
“Na
tukaribie wenye moyo wa kweli, kwa utimilifu wa Imani”
Waebrania 10:22
Kwa hiyo imani
katika maisha, kufa na maombezi kwa ajili yetu tunazidi kufanywa upya kila
mara, na tunazidi kufanywa weupe na safi. Siyo tu kwamba hatuhukumiwi, lakini
pia hakuna adhabu mbaya kama ilivyokuwa hapo kwanza, Bwana
akitusafisha mioyo yetu na maisha yetu.
Kwa imani hiyo
hiyo, tunahisi nguvu ya Kristo ikiwa juu yetu kila
wakati, ambayo kwa hiyo tuko kama tulivyo leo. Kwa hii imani pekee,
tunawezeshwa kuendelea katika maisha ya kiroho. Na pasipo hiyo, bila kujali
utakatifu wetu wa sasa, tungepaswa kuwa mashetani muda mchache ujao.
Maadam tumewaka
imani yetu kwake, tunateka maji kutoka katika visima vya wokovu. Tunamtegemea
mpendwa wetu, Kristo ambaye ni tumaini la utukufu wetu, ambaye
hukaa ndani ya mioyo yetu kwa imani.
Kadhalika yeye
anaendelea kufanya maombezi kwa ajili yetu ikiwa mkono wa kuume wa Mungu;
tunapokea msaada kutoka kwake ili kufikiri, kuongea, na kutenda au kufanya yote
yanayopaswa mbele ya macho yake.
Yeye hututangulia
katika yote tuyatendayo, ili kuomba mtindo, maisha, mazungumzo
na matendo yalioanza, yaliyoendelea na yaishie katika yeye. Yeye pia husafisha
mawazo ya mioyo yetu kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu, ili tuweze kumpenda
kikamilifu, na kwa kumhimidi kwa kumstahi kupitia jina
lake Takatifu.
Je, tunapaswa kumngoja kwa
namna gani?
“Mtafuteni Bwana, maadam anapatikana,
mwiteni maadam, yu karibu?
Isaya 55: 6
Fikiri mtu amejua
wokovu ni kipawa na ni kazi ya Mungu, na akafikiri baadaye kwamba ameshawishika
pia kwamba hana kipawa, je, anawezaje kukipata?
Kama ukisema,
“Amini, na utaokoka” wajibu, “kweli, lakini je,
nitaamini namna gani” Unawajibu, “mngoje Bwana”.
“Vema, lakini
ninapaswa kumngoja Bwana jinsi gani? Ukitumia njia ya neema, au hapana? Je,
ninapaswa kuingoja neema ya Mungu, ambayo huleta wokovu, kwa kutumia njia ya
neema, au kwa kuitupia mbali neema, au kwa kuitupia mbali
neema hiyo?”
Haiingiliki akilini
kwamba neno la Mungu haliwezi ktuoa maelekezo katika suala muhimu kama hili au
kwamba mwana wa Mungu, ambaye alikuja kutoka mbinguni kwa ajili
yetu na kwa ajili ya wokovu wetu, anaweza kuwa ametuacha bila maelekezo hasa
kuhusu wokovu unaotuhusu.
Na ki urahisi, hakutuacha
pasipo maelekezo; ametuonyesha njia ambayo tunapaswa kuiendea. Tunapaswa
kulisoma Neno la Mungu. Na kuuliza kwa kutafuta kilichoandikwa. Tukifanikiwa
kukua katika hicho, hakuna shaka litakalosalia ndani yetu.
Kwa mujibu wa
maandiko matakatifu, wote wenye shauku na neema ya Mungu wanapaswa kuingoja kwa
kupitia njia ambazo Mungu ameziandaa – kwa kuzitumia, na siyo kuziweka mbali,
maombi, kusikiliza, kusoma, na
kutafakari maandiko; na kushiriki meza ya Bwana.
Upendo katika moyo
“Pendo
la Mungu limemiminwa ndani ya mioyo yetu na Roho Mtakatifu
tuliyepewa sisi”
Warumi 5: 5
Alama ya tatu ki
maandiko ya wale waliozaliwa mara ya pili, na ambayo ni kuu kuliko zote, ni
upendo. Ni upendo wa Mungu, ambao umemiminwa ndani ya mioyo yetu na
Roho Mtakatifu tunapozaliwa mara ya pili na roho wa Mungu. “Kwa
sababu ninyi ni wana”. Mtakatifu Paulo aliwaandikia Wagalatia, “Mungu alimtuma Roho
wa mwanaye mioyoni mwetu, aliyae “Abba, yaani Baba” - (Wagalatia 4:6) kwa njia ya huyo Roho, wanamwangalia Mungu
kwa bidii kama mpatanishi wa Baba mpendwa.
Wanamlilia kwa
ajili ya (riziki) mkate wa kila siku, kwa ajili ya mahitaji yote yawe ni ya kiroho
nay a kimwili. Wanamimina mioyo yao
kwa dhati mbele ya Bwana Mungu, wakijua kwamba wanazo haja wamwombazo - (Ona 1 Yohana 5:14-15) furaha yao ni katika yeye; ni furaha ya mioyo
yao. Shauku ya nafsi zao ni kumwendea yeye; kufanya mapenzi yake huleta utoshelevu
mkuu ndani yao. Wanampenda Mungu kama mwokozi wao.
Wanampenda Yesu Kristo kwa dhati; wameungwa na Bwana na kuwa roho mmoja. Nafsi
zao zinamtegemea Bwana Yesu na humkubali yeye ni mkuu miongoni mwa maelfu.
Wanajua kile alichokiandika mwandishi wa Zaburi kina maana gani; wewe mzuri
sana kuliko wanadamu; Neema imemiminwa midomoni mwako - (Zaburi 45:2).
Mungu ni mtoaji
“Kila
kutoa kuliko kwema na kitolewacho kilichokamilika ….. hutoka juu, hushuka kwa
Baba wa mianga”
Yakobo 1: 17
Ni kweli kwamba
dini kwa nje haina thamani (maana) pasipo na dini ndani ya moyo; “Mungu ni
Roho; na hao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli” - (Yohana 4:24). Kwa hiyo ibada ya nje ni kazi bure pasipo moyo uliojitoa
kwa Mungu. Maagizo ya Mungu katika mambo ya nje huwa na hatua na thamani ikiwa
yatakuwa yalianzia ndani katika utakatifu. Lakini hayakuanzia ndani (badiliko)
hayana faidia na utupu. Ikiwa yatatumika katika nafsi inayopaswa kutumiwa na
mambo ya ndani ya roho ya mwanadamu, mambo hayo ni chukizo.
Njia zote kwa nje
bila kujali ni zipi ikiwa ziko mbali na Roho Mtakatifu
haziwezi kuwa na faida kabisa, haziwezi
kutuongoza kumjua au kumpendeza Mungu. Pasipo utata, msaada unaofanyika juu ya
uso wan chi, anafanya yeye mwenyewe. Ni yeye pekee ambaye, kwa nguvu zake kuu,
anatenda ndani yetu yanayompendeza mbele zake. Mambo yote ya nje, Mungu
asipotenda ndani yako, yana hali ya kawaida na
yaliyodhaifu. Tunajua kwamba hakuna nguvu ya kawaida katika maneno yatumikayo katika
sala katika kusoma maandiko, katika mkate na divai
inayopokelewa katika ushirika wa meza ya Bwana. Ni Mungu pekee ambaye
hutoa kila kilicho chema, na mwanzilishi wa neema. Nguvu zote ni zake, na kwa
hiyo kupitia chochote – kati ya hivi, kuna Baraka yoyote ambayo huachiliwa
ndani yetu.
Maombi ya ahadi za Mungu.
“Ijapokuwa
sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mnahuzunishwa kwa majaribu ya namna
mbalimbali”.
1 Perto 1: 6
Wakati wa magonjwa
na maumivu, shetani hutusonga sana kwa nguvu zote, “Je, Mungu hasemi, ‘pasipo
utakatifu hakuna mtu atakaye muona Bwana”’, unajua utakatifu
ni utimilifu wa sura ya Mungu, na jinsi jambo hili lilivyo mbali na macho yako!
Huwezi kuingia katika hali ya utakatifu huu. Umeteseka katika mambo yote bure.
Na bado upo katika dhambi zako, na hatimaye lazima
utaangami”.
Ikiwa macho yako
hayakumwangalia yeye (Bwana) aliyezibeba dhambi zako zote, shetani atakuleta
tena chini ya hofu ya kifo ambamo uliwahi kuwa katika utumwa kwa njia hii
hudhoofisha, kama siyo kukuharibu kabisa, Amani na furaha yako katika Bwana.
Sasa amani ya Mungu ndani ndiyo njia ya thamani ya kuendelea katika siura
ya Mungu. Kuna msaada kidogo kutuleta katika utakatifu kuliko huu-ufahamu, na
roho iliyomwelekea mungu, kupata pumziko katika damu ya Yesu.
Pasipo hii, ni
shida kukua katika neema na katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
Kwa hiyo, shika sana mwanzo wa ujasiri ulioimarika mpaka mwiso. Bila shaka
utapokea ahadi ya Mungu, kwa wakati huu na kwa ajili ya umilele. Usijisumbue
kwa lolote. Pia mahitaji yako yajulikane bila shaka au hofu, lakini kwa
shukurani kwake yeye aliyeahidi ahadi hizi zote (Angalia Wafilipi 4:6)..
Ninyi kwa ujumla
‘Mungu
kwa amani mwenyewe awatakase kabisa”.
1Thesalonike 5: 23
Mungu wa amani
hutakasa kwa kutumia amani ambayo huitumia kutenda kazi ndani yetu, ambayo ni
njia kuu ya utakaso. Neno lililotumika katika tafsiri ya asili linamaana, ‘kwa
ujumla na kikamilifu” - kila sehemu na yote
yanayohusiana nasi “Ujumla wenu” Mtume anaendelea,
“roho na nafsi ya mwili” mhifadhiwe mwe kamili bila lawama” Anaonyesha kwamba
alitaka hali yao ya kiroho ihifadhiwe kikamilifu, vile vile akiwa
na shauku kuona afya ya hali yao ya asili.
Ili kuelezea hili
zaidi: nafsi na mwili pekee ni sehemu za asili ya kibinadamu lakini kipawa cha
Ki-Mungu, kinachopatikana ndanai ya wakristo
pekee. Ili kuwatia moyo wakristo wa Thesalonike, Mtakatifu Paulo
aliongeza “yeye aliyewaita, ni mwaminifu, naye atafanya’ (Mstari 24); Ikiwa
hamtazimisha Roho, ambaye kwa yeye alikuwa ameandika kusudi
lake (Mstari 19). Mahali popote alipo Roho amani hii huwepo. Huwepo katika
pendo takatifu, katika furaha, katika maombi; na shukurani.
Oh, usimzimishe,
kwa kumwacha pembeni, au kwa kukataa, kutenda mema, au kwa kutenda ouvu! Kama
njia kuu ya kujiepusha na hili, aliondoka. “furahini siku zote;
omba bila kukoma; shukuruni kwa kija jambo” Onyo la Baraka, hata
katika siku zetu!
Je, hasira yako ya ndani ni
ipi?
“Kwamba
watubu…. wakiyatenda matendo yanayopatana na kutubu kwao”
Matendo 26: 20
Kama dhamiri
ya waaminio iko hai, dhambi kiasi gani hutamani matendo yao? Matendo yao siyo
kwa ajili ya utukufu wa Mungu; na mara kwa mara hawakukusudia kutenda kwa ajili
ya utukufu wa Mungu. Wengi hufanya mapenzi yao wenyewe na wakitafuta
kujipendeza wenyewe kama siyo kumpendeza Mungu.
Wakati wakijitahidi
kutenda wema kwa jirani yao, je, hawajisikii hisia za hasira ya namna Fulani?
Hata hivyo, matendo yao mema, mambo yao ya rehema yamechafuliwa na mchanganyiko
wa uovu. Je, si suala hilo hilo wanapokuwa wakitoa sadaka ya maombi kwa Mungu,
katika mkusanyiko au katika faragha, au kujiingiza katika huduma muhimu? Je,
mioyo yao mara zote haitangitangi kuelekea miisho ya dunia?
Tena, dhambi ngapi
za kutotenda waliyopaswa kuyatenda zinazowahukumu! Tunajua maneno ya mtume
Yakobo, “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake
huyo ni dhambi”. - (Angalia Yakobo 4:17). Je,
hawaoni kupungukiwa au kutowepo kwa upendo ndani yao,
na hasira takatifu, na makosa mengine ya ndani yasiyokuwa na idadi; ili kwamba
walie pamoja na Ayubu, “kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu,
na kutubu katika maumivu na majivu”. (Ayubu 42:6).
Maombi na kujikana mwenyewe
“Na
ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku anifuate”
Luka 9: 23
Ufahamu wa neema ya
Bwana wetu katika meno haya ni wa muhimu sana. Kila hatua ya maisha ya kiroho,
kuna aina mbalimbali za vizingiti vinavyozuia kupata neema na kukua katika
neema hiyo. Hata hivyo, yote yanategemeana na mjumuisho wa maneno hayo:
kutokujikana wenyewe, au kutokuibeba
msalaba wetu.
Hili suala ambalo
hupigwa sana na maadui wengi na wenye nguvu. Asili zetu huinuka kinyume
na kweli hii. Wala ambao huchukua asili kuliko neema kwa ajili ya mwongozo huiharibu kweli hili; Adui mkubwa
wa nafsi zetu anajua fika umuhimu wake na mweka kikwazo dhidi ya kweli ya
kujikana na kuubeba msalaba.
Hata wale ambao kwa kiasi Fulani
wameitikisa na kuiharibu nira ya shetani na kupata ujuzi wa neema ndani ya
mioyo yao si marafiki wa hili fundisho la kikristo. Ijapokuwa limesisitizwa kwa
upekee na Bwana wao, baadhi yao ni wajinga kabisa kana kwamba hakukuwepo na
neno kama hilo katika Biblia.
Wengine huendelea katika hali ya
kutokufahamu na hivyo kuwa kinyume na kweli hii ya kujikana na kubeba msalaba. Hueleza fundisho
la kujikana na kubeba msalaba katika namna na sura mbalimbali. Huliita
fundisho hili “kuutafuta wokovu kwa matendo au kutafuta kujithibitisha sisi
wenyewe”. Uko katika hatari endelevu ya kunyanyaswa, au kuwa mjinga wa fundisho
hili muhimu la Injili. Maombi yenye
bidii yakutangulie, yakiambatana na kufuata kile ambacho anatarajia.
Mungu anafanya mambo makuu
“Kwa
sababu hiyo, msiwe wajinga, bali mfahamu nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.
Waefeso 5: 17
Ufalme wa mbinguni
kwa ndani hukaa ndani ya mioyo ya wote waliotubu na kuamini injili, ni haki,
amani na furaha katika Roho Mtakatifu. Lakini hayo matunda au matokeo tu.
Wakati hizi Baraka zinapokuwa kwa uchache, hata hivyo bado tunategemea kuona
makuu zaidi.
Tunategemea
kumpenda Bwana Mungu wetu siyo tu kama tunavyofanya
sasa, kwa udhaifu ingawa kwa uthabiti wa moyo, bali kwa mioyo yetu yote, akili
zetu zote, nafsi zetu zote na nguvu zetu zote. Ni kweli tunatarajia kufanywa
kamili katika Upendo” (1Yohana 4:18). Tunatafuta nguvu ili tufurahi siku zote,
kuomba bila kukoma, kutoa shukurani kwa kila jambo. Tunaamini kwamba ile nia
iliyokuwepo ndani ya Kristo itakuwa ndani yetu pia (Angalia
Wafilipi 2:5) Na tunatarajia kutakaswa kutoka katika sanamu zote na kuokolewa kutoka
katika uchafu wetu wote wa ndani wan je pia (Angalia Ezekieli 36:29) - ili kutakaswa, kama yeye alivyo Mtakatifu.
Tunatafuta ongezeko
la jinsi hiyo katika ujuzi wa kumjua na kumpenda Mungu mwokozi
wetu ili atuwezeshe kutembea katika nuru wakati wote kama yeye alivyo katika
nuru. Tunatumaini katika ahadi zake yeye asiyeweza kusema uongo kwamba wakati
utafika ambapo yote tunayotenda yatakuwa
yakitendeka kwa ajili ya utukufu wa Mungu Lengo la shetani katika kuharibu ni
kuharibu kazi ya Mungu ndani ya nafsi zetu, au kuzuia ongezeko lake, kwa taraja
letu katika hiyo kazi kubwa. Hata hivyo kuna njia ya kudhibiti hiyo mishale na
kuinuka juu zaidi dhidi ya kile alichokikusidia ili
kutuangusha.
Njia za wokovu.
“Wakati
wa usiku nimelikumbuka jina lako, Ee bwana, nikaitii sheria yako’
Zaburi 119: 55.
Tayari imegundulika
kwamba kuna utaratibu ambao katika huo Mungu kwa ujumla amependezwa kutumia
njia hizi katika kuwaleta wenye dhambi kwake. Japokuwa
hatupati amri katika maandiko Matakatifu kwa ugunduzi uliofanyika. Njia za
jinsi watu tofauti walivyoongozwa, na jinsi walivyopata Baraka za Mungu,
zinatofautiana kiviwango, na njia hizi zikiwa na utofauti mara maelfu.
Hata hivyo hekima
yetu ni kufuata uognozi wa ki-ungu na Roho wake zaidi sana kama jinsi njia
zilivyo ni sisi wenyewe kutafuta neema ya Mungu. Kwa sababu
yeye hutuongoza kwa sehemu kupitia Uungu wake kwa nje, na hutupa nafsi wakati
mwingine njia moja, na wakati mwingine njia nyingine na kwa sehemu kupitia
uzoefu wetu na Roho wake hupendezwa sana kufanya kazi ndani yetu.
Katika wakati huo
huo, kwa hakika na kuhitimisha jumla, wote ambao huugua kwa ajili ya
wokovu wa Mungu ni hili nafsi inapotokea, tumia njia zote ambazo Mungu aliweka
wakfu, kwani ni nani ajuaye ni kupitia njia ipi katika njia za Mungu ametupa,
atakutana na wewe kwa neema iletayo wokovu?
Kumngoja Mungu
“Kwamba
kwa Bwana …. Miaka elfu ni kama siku moja”
2 Petro 3: 8
Kama tutashikilia
kwa bidii; “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka… Yesu Kristo” na
“Nimehesabiwa haki bure kwa neema”, bado shetani anahoji, “Lakini mti
hutambulikana kwa matunda yake; je, una matunda ya haki? Je, nia uliyonayo
ndivyo ilivyokuwa ndani ya Yesu Kristo? Je, umekufa kwa habari
ya dhambi na kwamba uko hai katika haki?
Na kisha,
tukilinganisha matunda madogo tunayoyaishi ndani ya nafsi zetu pamoja na
utimilifu wa ahadi: tutakuwa tayari kuhitimisha, “Hakika Mungu hajasema kwamba
dhambi zangu zimesamehewa. Hakika, sijapokea msamaha wa
dhambi zangu, je, nina fungu gani miongoni mwa hao waliotakaswa?
Lakini fugnu hili
katika shingo yako; uziandike juu ya moyo wako; “Nimekubaliwa mbele za Mungu,
kwa haki ya Mungu kwa imani; uwe na shauku zaidi ya neema ya Mungu kama alivyofanya
yeye katika kumtoa mwanae wa pekee, kwa ulimwengu, ili kila amwaminiye asipotee
bali awe na uzima wa milele (angalia Yohana 3:16). Ndipo amani ya Mungu
itakapoanza kutiririka, licha ya milima uovu. Itakuwa tambarare wakati wa
mchana bwana atakapokuja kuchukua nafsi na kutawa moyo wako. Bwana hawezi
kukosa muda wa kutimiza kazi ambayo ilipaswa kutimizwa ndani ya nafsi
yako. Muda-wakati wake ni wakati sahihi zaidi. Kwa hiyo, mwambie na umtumaini
yeye, kwa sababu huwezi kuzuia chochote kwako ambacho ni chema.
Kazi ya wito wako
“Msikitendee kazi chakula
chenye kuharibika”
Yohana 6:27
Je, ni kwa kusudi
gani unafanya na kufuata kazi au shughuli za kidunia? “Ili kupata mambo au
mahitaji muhimu kwa ajili yako na familia pia”. Jibu lenye utoshelevu “kwa kadri
linavyoendelea, lakini haliwezi kufika mbali hasa kwa mkristo lazima twende
zaidi ya hapo tena. Kusudi letu katika mambo yote ni kumpendeza Mungu,
kutofanya mapenzi yetu bali kufanya mapenzi ya Mungu
hapa duniani kama malaika wa navyofanya mbinguni. Tunafanyia kazi kile
kinachodumu hata milele.
Tena, ni kwa jinsi
gani tunafanya shughuli zetu za kidunia (ki maisha)? Ninaimani
kwa bidii yote, kwa nguvu zako zote. Na kwa haki: tukiyafanya yote kwa wakati
wake katika kila mazingira. Na katika rehema; tukifanya kila mmoja, kama
ipasavyo na ndivyo watakavyotufanyia. Lakini wakristo wameitwa kwenda zaidi ya
hapo: kuongoza huruma katika haki; kuchanganya
na maombi – maombi ya moyo –
katika kazi zote za mkono yao. Pasipo hii juhudi yote na haki inawaonyesha kuwa
waaminifu. Lazima tutembee “katika njia iliyo bora zaidi” - kuliko waaminifu wapagani.
Ni “roho” gani
ambayo unatenda kazi kwayo? Je, ni katika roho ya dunia au Roho wa Kristo? Kama
unatenda katika roho wa Kristo; unafanya yote katika roho ya dhabihu, ukitoa mapenzi
yako katika mapenzi ya Mungu. Utaendelea kukusudia,
bila ya kusita, au kutaka fahari; au kuwa tajiri wa
chochote zaidi ya utukufu wa Mungu. Hii ni njia iliyo bora zaidi ya
kufuatilia shughuli zetu za kila siku hapa duniani.
Kuulilia wema wa Mungu
“Tuzidi
katika dhambi ili neema izidi, La hasha!”
Warumi 6: 1-2.
Inaweza kuwa baadhi
hawapendi kuzungumzia rehema za Mungu zinazo okoa na kutuhesabia haki bure kwa
imani kwa sababu wanaamini kwamba zinatia watu moyo kuendelea katika dhambi:
kweli, inawezekana pengine! Wengi wataendelea
kutenda dhambi ili neema izidi, lakini damu yao iko juu ya vichwa vyao wenyewe.
Wema wa Mungu unapaswa kuwaongoza katika toba, na hivyo huwa
kwa wale walio na moyo mnyoofu. Wale wamtafutao Bwana kwa bidii wanajua kwamba
kuna msamaha kwa Mungu, hulia kwa sauti ili dhambi zao ziweze kusamehewa pia,
kupitia imani iliyo katika Yesu.
Kama watalia kwa
bidii pasipo kuzimia, ikiwa watamtafuta kwa njia zote alizoziweka, ikiwa
watakataa kufarijiwa, mpaka amekuja, atakuja, na hata kaa (Waebrania 10:37). Na
ataweza kufanya kazi kubwa kwa muda mfupi, Matendo ya mitume imerekodi mifano
mingi ya utendaji wa ki Mungu kwa imani ndani ya
wanadamu, kama mwangaza kutoka mbinguni. Wakati huo huo Paulo na Sila
walipoanza kuhubiri, askari alitubu, aliamini, na akabatizwa. Ndivyo ilivyo
tokea kwa watu elfu tatu katika siku ya Pentecoste ambapo walitubu na kuamini,
wakati Petro, Mtume akihubiri kwa mara kwanza. Na, abarikiwe Mungu, kuna
uthibitisho wa kutosha kuwa Mungu, “hodari katika kuokoa”.
Kumtafuta Bwana na utii
“Angalia,
kutii ni bora kuliko dhabihu”
1Samweli 15: 22
Kifungu kingine
ambamo maelezo, “simama imara” yameonekana yakisomeka: “wakaja watu
waliomwambia Yehoshaphati, wanakuja jamii kubwa juu yako watokeao Shamu,
ng’ambo ya Bahari … Yehoshaphati akaogopa, akauelekeza uso wake amtatute Bwana;
akatangaza mbiu ya watu kufunga katika Yuda yote, Yuda wakakusanyika wote ili
wamtafute Bwana; hata kutoka miji yote ya Yuda wakaja kumtafuta Bwana. Yehoshaphati
akasimama katika kusanyiko … nyumbani mwa Bwana… ndipo Roho ya Bwana akaja juu
ya Yahazaeli, … akasema, Sikieni ... hivi ndivyo
asemavyo Bwana kwenu, 2 Nyakati 20:2-23.
Huo ndiyo wokovu
ambao wana wa Yuda waliuona. Walitii,
Waliimba na walimsifu Bwana. Ni kwa namna gani yote haya yanathibitisha kwamba
hatupaswi kuongoja neema ya Mungu katika njia ambayo ameiweka.
Kuutunza (kuujali) mwili
“Basi, mlapo, au mnywapo, au
mtendapo neno lolote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu”
1 Wakoritho 10: 31
Hizi “nyumba za udongo” ambazo huhifadhi roho zetu
zinahitaji fidia au utunzaji, au
vinginevyo itatoweka mapema kabla ya wakati wake. Chakula cha kila siku ni
muhimu kuzuia vifo vya ghafla au vya mapema. Kabla ya wakati ili kurekebisha uharibifu wa mwili. Ilikuwa ni
desturi katika ulimwengu wa kipagani; walipokaribia kila chakula, wangemwaga
kiasi kidogo cha kinywaji kama ishara ya heshima kwa Mungu wao (ijapokuwa mungu wa kipagani alikuwa ni shetani – 1
Wakorintho 10:19 – 21). Ilikuwa ni jambo la kawaida – kidesturi katika nchi
hii. Je, isingekuwa ni njia iliyo bora zaidi kama kila kiongozi wa familia
angeomba Baraka kutoka kwa Mungu juu kila ambacho walitaka kukila na kurudisha shukurani
kwa mtoaji wa Baraka?
Kama ilivyo kwa
wingi vyakula, baadhi ya watu hawali kupita kiasi; ili wasije wakajiletea
madhara kupitia vyakula. Kama ilivyo desturi ya ulaji, wakati wote hakina
tatizo, kuchanganya na vinywaji ambavyo inasemekana kwamba
husaidia uyeyushaji wa chakula. Maadamu itakuwa ni kiasi kidogo, ubora wa
chakula ambao husaidia kuleta afya ya mwili na akili. Inasemekana kwamba, njaa
ni kichocheo cha hamu ya chakula lakini pia njaa inayotosheleza huleta au
kisababisho cha uchangamfu wenye shukurani, na chakula kinacholiwa au
kupatikana na wakati wake kunafaa.
Uimbe upendo wake
“….
Asema Bwana. Nitawapa sheria zangu katika nia zao, na katika mioyo yao
nitaziandika; … na dhambi zao sitazikumbuka tena”
Waebrania 8: 10,
12
Baada ya kutumia
miongoni mwa njia hizi za neema, uwe mwangalifu na jinsi unavyojitathimini
mwenyewe, jinsi unavyojipongeza baada ya kufanya mambo makuu. Hii ni kugeuza
yote kuwa sumu. Sababu ya ukombozi wetu siyo matendo yetu au haki yetu lakini
ni wema na upendo wa Mungu mwokozi wetu ….
Sawa sawa na rehema zake … ili tuwe warithi wa uzima wa
milele (angalia Tito 3:4-7) kwa muda Fulani, fikiri, kama Mungu
hakuwepo, kutumia njia hizi kuna faida gani? Je, siongezi dhambi juu ya dhambi?
Ee, Bwana, niokoe,
vinginevyo nitaangamia! Usinihesabie dhambi hizi!
“Kama Mungu alikuwepo pale, kama upendo wake uliingia ndani ya moyo wako,
tayari umekwisha sahau matendo ya nje. Unaona, unajua, unahisi, Mungu ni yote
katika yote. Shuka mbele zake, mpe sifa zote. Mungu atukuzwe katika mambo yote,
kupitia Kristo Yesu. Lia kutokea ndani ya moyo wako, “fadhili
za Bwana nitaziimba milele, kwa kinywa changu nitavijulisha
vizuri nyote uaminifu wako” - (Angalia Zaburi 89:1 na Zaburi
100:5).
Kuomba Neema
“Ee
Bwana unifundishe njia yako, na kuniongoza
katika njia iliyonyoka”
Zaburi 27: 11
Kwa kuangalia
utaratibu ambao Mungu huutumia ili kumwongoza mwenye dhambi, tunaweza kujifunza
ni njia ipi tunaweza kupendekeza kwa mtu yeyote. Kama kitu chochote kinaweza
kumfikia mwenye dhambi asiyejali, inaweza kuwa kusikiliza au kuwasiliana, kama
aliwahi kuwa na wazo kuhusu wokovu. Kwa mwingine ambaye huanza kuhisi uzito wa
dhambi: siyo, kwa kusikiliza neno la Mungu tu bali kwa kusoma pia, na pengine
vitabu Fulani, inaweza kuwa njia ya kuonyesha jinsi alivyoshawishiwa na Roho
Mtakatifu. Anaweza kushauriwa kutafakari alichosoma ili kiweze kuwa na uzito
katika moyo wake. Tukisema ukweli, hasa kwa wale ambao wako katika hali hiyo
hiyo. Wakati shida na uzito unapomshika, anapaswa kuumimina moyo wake kwa bidii
mbele za Bwana, na hasa hasa kuomba bila kukata tamaaa. Na ikiwa
hatajisikia hali ya kutoona uthamani wa maombi yake, mkumbushe.
Aende katika nyumba
ya Bwana ili aombe pamoja na wale wamchao Bwana. Lakini anafanya hivi ili neno
la Bwana wake litakumbushiwa kushiriki meza ya Bwana.
Tunapaswa kuendelea zaidi kwa Roho wa Baraka, anayeongozwa na hatua kwa
hatua, kupitia njia zote ambazo Mungu aliziweka (aliziandaa) - si sawa sawa na mapenzi yetu, lakini kama Mungu na Roho wa Mungu
anavyotangulia na kufungua njia.
Kutunza hali ya kuzaliwa
kiroho
“Kadhalika
aliyezaliwa kwa Roho”
Yohana 3: 8
Mtu anapozaliwa na
Mungu, huzaliwa na Roho, ndiyo hata namna
ya kuishi kwake inabadilika! Utu wake wa ndani unaanza kuwasiliana na
Mungu, na anaweza kusema kwa hakika katika ujuzi “uko kando ya kutenda, na
kando ya njia yangu”. Roho au pumzi ya Mungu inaivuvia nafsi ya mtu na kuifanya
kuwa kiumbe kipya. Na pumzi hiyo hiyo ambayo hutoka kwa Mungu, hurudi kwa Mungu
tena. Kama jinsi inavyopokelewa njia ya imani, vivyo hivyo hurejeshwa kwa njia
ya upendo, maombi, sifa na shukurani. Upendo, maombi, na sifa ni pumzi ya kila nafsi
ambayo imezaliwa kweli kweli. Kwa kupitia hivyo, maisha ya kiroho hayahuishwi
tu, bali hongezeka siku kwa siku.
Macho ya moyo wake yako wazi sasa, kumwona yeye ambaye haonekani.
Anaweza kutambua upendo wa msamaha wa Mungu. Kumwelekea yeye na ahadi zake
zilizo kuu na za thamani. Masikio yake sasa yako wazi, sauti ya Mungu haiiti
bure. Anajua sauti ya Mchungaji wake – anasikia na kutiii wito wa mbinguni.
Hisia zake za kiroho zimeamshwa, (He has
the clear
communication with the
invisible world). Sasa anajua jinsi ambavyo amani ya Mungu ilivyo: furaha
katika Roho Mtakatifu na upendo wa Mungu unaomiminwa ndani ya mioyo yao waaminio. Utaji umeondolewa;
hakuna chochote katika nafsi isipokuwa nuru, maarifa na upendo wa Mungu.
Kwa ujumla Mkristo: Ni upendo
wa Mungu
“Mpende
Bwana Mungu wako kwa moyo wote”
Mathayo 22: 37
Kwa mara nyingine
tunakuja katika suala linalomwelezea mkristo kwa ujumla. Kwanza, upendo wa
Mungu. Neno lake linasema: ”utampenda Bwana Mungu wako
kwa moyo wako wote, Kwa akili zako zote, kwa roho yako yote, kwa
nguvu zako zote.” (Marko 12:30) Upendo huu hujaa ndani ya moyo wote, na hutawala hisia
za moyo wote, hujaza uwezo wote wa nafsi, na maeneo mengine yote ya binadamu.
Yeye apendaye
huendelea kufurahia upendo katika Mungu, furaha yake iko katika Mungu, Bwana wake
na yote yanayohusiana na Mungu, kwa huyu hutoa shukurani katika kila Jambo.
Shauku zake zote ni za kumwelekea Mungu na kwa kumbukumbu jina lake. Moyo wake
hulia; “Nani aliye katika mbingu ila wewe”
na hakuna duniani nimwoneae shauku zaidi yako”.
Hakika, ni nini
aweza kukionea shauku ila Mungu? Siyo ulimwengu,
kwa mambo ya ulimwengu na ulimwengu umesulubiwa kuhusu yeye. Amesulubiwa katika
shauku za mambo ya mwilini, shauku (tamaaa) za macho, na kiburi cha uzima.
Amekufa na kila aina ya kiburi: kwa kuwa “Upendo haujivumi”
Akaaye katika pendo, hukaa katika Mungu, na Mungu hukaa
ndani yake, na yeye si kitu machoni pake mwenyewe, kwa kuwa upendo wa Mungu ni
alama ya jumla ya mkristo.
Hesabu ya maombi.
“Si
kila aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa Mbinguni”
Mathayo 7: 21
Maelezo ya Bwana
wetu katika kifungu hiki yanamaanisha (kuanzia katika hali ya chini) maneno
yote mazuri, matendo yote ya kidini. Inajumlisha imani yoyote tuikiriyo, ukiri
wa imani tuipokeayo, idadi ya maombi tuyarudiayo, shukurani tunazozisoma au
kumwambia Mungu.
Tunaweza kulitaja
au kulitamka vema jina lake na kutangaza wema wake kwa watu wote. Tunaweza
kutamka (kuzungumza) matendo yake makuu ya kuwaeleza wokovu wake siku kwa siku.
Tukiyafasiri mambo
ya rohoni kwa maneno ya rohoni, tunaweza kuonyesha maana ya neno la Mungu.
Tunaweza kuelezea siri ya ufalme ambao ulifichwa tangu mwanzo wa ulimwengu.
Tunaweza kunena kwa
lugha za malaika kuliko za wanadamu kuhusu mafumbo ya Mungu.
Tunaweza kutangaza kwa wenye dhambi, “Tazama, mwana kondoo wa Mungu,
aichukuaye dhambi ya ulimwengu!” - (Yohana 1:29).
Ndiyo, na tunaweza
kufanya hili kwa kadiri ya nguvu za Mungu na udhihirisho wa Roho
Mtakatifu, ili kuweza kuokoa nafsi nyingi katika mauti na kusitiri wingi wa
dhambi.
Hata hivy
inawezekana, yote haya yasiwepo zaidi ya kusema, “Bwana, Bwana,” Ninaweza
nikahubiri kwa mafanikio makubwa na kunyakua nafsi nyingi katika moto, na bado
nikadondokea hapo baada ya kufanya yote. Mungu na aturehemu sote.
Kuomba kwa ajili ya wokovu
“Maagizo
ya Bwana ni ya adili, hufurahisha moyo”
Zaburi 19: 8
Kuna aina Fulani ya
utaratibu ambao Mungu mwenywe hupendezwa kuutumia ili kumleta mwenye dhambi
katika kupata wokovu. Mtu anaweza kuenenda katika hali ya kutokujua katika
njia. Na Mungu huja kwake bila yeye kuelewa – kwa kutumia ujumbe wa kumwamsha
au mazugumzo, na hali Fulani ya ki Mungu au kushawishiwa na Roho
wake bila njia yoyote ya kawaida. Kisha huanza kuwa na shauku ya kukimbia
ghadhabu ya Mungu, kwa kusudi kuendelea kusikiliza jinsi itakavyofanyika. Akipata
mhubiri ambaye anongea na moyo wake, anastaajabu na anaanza kuchunguza
maandiko.
Kwa kadiri
anavyosikia na kusoma, ndivyo anavyozidi kushawishiwa, ndiyo anavyozidi
kutafakari mchana na usiku. Kwa njia hizi, mishale ya ushawishi na Roho mtakatifu
inazidi kuzama ndani ya nafsi yake. Huanza kuongea vitu kuhusu Mungu
na kuomwomba Mungu kwa hakika akijua anachopaswa kusema.
Labda ni katika “kuugua kusikoweza kutamkwa’, labda kuwa na shaka kama Mungu
aliye juu atamsikia kama alivyo. Anakwenda kuomba pamoja na hao wanaomjua
Mungu, katika kusanyiko. Anawaona wengine wakishiriki meza ya Bwana. Anafikiri
“Kristo amesema, fanyeni hivi”. Inakuaje, Mimi siombi? Mimi ni mwenye dhambi
nyingi wala sistahili.
Anahangaika kidogo,
na hatimaye anapata upenyo, na hivyo anaendelea katika njia ya Mungu; katika
kusikia, kusoma, kutafakari, kuomba na kushiriki meza ya Bwana; katika jinsi
ambavyo atampendeza Bwana, Mungu anasema, “imani yako imekuokoa. Nenda kwa
amani”.
Kuwa na mfano wa utauwa
“Wenye
mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake”
2 Timetheo 3: 5
Wale wenye mfano wa
utauwa hawajitengi tu kwa kawaida na uovu unaoonekana kwa nje, katika kufanya
mema yanayowezekana. Pia wanatumia njia ya neema katika nafsi zote, hasa katika
kuhudhuria nyumba ya Mungu mara kwa mara kwa kadiri iwezekanavyo. Hawaendi
wakiwa wamefumbwa macho pamoja na tofauti zisizo na maana. Pia huwatendi kana
kwamba mungu amelala, kuzungumza mmoja na mwenzake au kwa kawaida wakiona
kutumia kumwomba Mungu kutumia kwa ajili ya Baraka zao.
Hapana, wanaendelea
kwa umakini na kwa macho katika kila huduma muhimu, hasa hasa katika ushirika
wa meza ya Bwana. Kwao si tabia ya mazoea, lakini ni idara ambayo inasema tu,
“Mungu anirehemu mimi mwenye dhambi.”
Kama ni viognozi wa
familia, hufanya maombi ya pamoja na familia na huweka muda maalum kwa ajili ya
kuongea na Mungu. Wale wenye mfano wa utauwa, wakiwa wakristo, wakiwa hasa na
kanuni za kidini ndani yao, unyenyekevu, ambapo haya matando
ya nje hudhihirika.
Hakika
bila unynyekevu hakuna anayeweza kuwa mwaminifu, kwa kuwa, hata wapagani
hufanya tofauti kati ya wale ambao huepuka dhambi kwa kuogopa adhabu na wale
ambao hutenda, na ndiyo inavyokuwa. Kwa watauwa ambao hujiepusha na dhambi ili
kuwa na upendo wa nguvu zake. Pasipo kanuni za ndani za uaminifu,
hakuna hata mmoja anayeweza kuwa mkristo. Anaweza tu kuwa mnafiki.
Kulinda kwa njia ya maombi
“Vaeni
silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzishinda siku za uovu, mkiisha kuyatimiza yote, kusimama”
Waefeso 6: 11-13
Jilinde
dhidi ya roho ambazo hushinda dhidi yetu ili kuweka hali ya kutokuamini,
kiburi, ibada ya sanamu, wivu, hasira, chuki: katika ulimwengu wa roho, ambapo palikuwa ni makao yao hapo awali na
ambapo wanapotamaani ikiwa wataruhusiwa. Kwa hiyo tunahitaji silaha zote za
Mungu.
Siku ya uovu,
(Mstari 13) - vita ni endelevu, lakini wakati mwingine vita
yetu inaweza kuwa si ya muda mrefu, na nyingine ni zaidi ya siku, yenye vurugu
nyingi. Siku ya uovu – inaweza kuwa inayoelekea mauti, au uzima. Hiyo vita
inaweza kuwa ndefu au fupi, na isiyokuwa na idadi ya siku sahihi za mapambano.
Ili uendelee kuvaa
silaha za Mungu na kisha kusimama, lazima ukeshe na kuomba. Hivyo,
utawezeshwa kustahimili mpaka mwisho na kisha
kusimama kwa furaha kabla ya kukutana na mwana wa Adamu, “katika siku ya mwisho”.
Ili uweze kuwa
tayari kwa kila hatua, vaa kweli kiunoni, siyo tu kwa kweli ya Injili, bali
kwa, “Kwa kweli katika utu wa ndani” - (zaburi 51:6) Vivyo
hivyo Bwana wetu anaelezwa (Isaya 11;5) Pasipo kweli katika utu wetu ndani,
maarifa yetu yote ya kweli na ki ungu yatathibitisha lakini kujifunga ki
udhaifu katiak siku ya uovu. Na kwa kadiri mwamume na mwanamke
aliyejifunga huwa tayari kusonga mbele, kwa hiyo hii inaonyesha moyo wa uasi
(kutotii), na utashi uliotayari, na marafiki wasiotengana - (Imani na upendo).
Huwazuia mbali na uovu
“Maana
mbali ya uovu yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi”
Waebrania 12: 6
Tunaweza kufanya
nini ili kwamba nyumba zetu ziweze kumtumkia Bwana? Je, hatupaswi kujitahidi;
kwanza, kuwazuia dhidi ya dhamba zote za nje-kulichukua JINA la Bwana bure na
kufanya yasiyostahili kutendwa katika siku ya Bwana? Wale wanawakodi wanaweza
kuzuiwa kwa mazungumzo ya mabishano au ushawishi, lakini klama watakuwa tayari;
wanapaswa kuondolewa.
Mwenzi wako hawezi
kuondolewa, isipokuwa uzinzi. Katika masuala mengine, nini kifanyike hasa
wakati dhambi ni mazoea? Yote yanayofanyika, hufanyika kwa mifano, kwa sehemu, kupitia malumbano au ushawishi; kama yanayoweza kuelekezwa na mkristo
mwenye busara. Kama uovu unaweza ukashindwa, lazima iwe kwa wema. Hatuwezi
kumpinga shetani kwa silaha zake mwenyewe. Ikiwa uovu huu hauwezi kushindwa kwa
wema, tumeitwa kuteswa katiak kupitia huo. Ikiwa Mungu auona wema mbele yake,
na kuuondoa. Kwa sasa, endelea katika maombi ya kung’ang’ania kwa wakati
sahihi. Anaweza kuliondoa jaribu na hulifnaya jaribu kuwa Baraka katika nafsi
yako.
Wakati watoto wako
wana umri mdogo, unaweza kuwazuia kufanya uovu kwa kuwashauri; kuwashawishi na
kuwaonya, na kuwasahihisha pia. Pia kumbuka, njia hii inapswa kutumika kwa
kuendelea - baada njia nyingine kuwa zimekwishafanyiwa kazi na kuabaini kuwa hazina matunda
yaliyotarajiwa. Yote yafanyike kwa upole na kwa ukarimu. Vinginevyo, roho yako
hupata hasara na mtoto hupata matokeo au faida kidogo. Usifikirie
mwenyewe kuwa na busara kuliko Mungu. Anasema, mradi mwanao … liko
tumaini; wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake” (mithali 19:18).
Kristo ni yote
“Bali
Kristo ni yote, na katika yote”
Wakolosai 3: 11
Tunajua kwamba
Mungu ana uwezo wa kutoa neema ingawa hakuna njia katika uso nchi. Kwa maana
hii tunaweza thibitisha, sambamba na Mungu, hakuna kitu
kama hicho, njia tuiangaliayo, kuwa ana uwezo
wa kutenda chochote kama apendavyo, kwa njia yoyote, au pasipo njia yoyote
kabisa.
Tunajua zaidi,
kwamba matumizi ya njia zote ambazo huweza kutupatanisha kwa sababu ya dhambi
zetu. Ni damu ya kristo pekee ambayo kwa hiyo mwenye dhambi yeyote hupatanishwa
na Mungu. Hakuna upatanisho mwingine kwa ajili ya dhambi zetu, au chemchemi kwa
ajili ya dhambi; uchafu.
Kila mwamini katika
kristo anashawishika kwa undani kwamba hakuna faida isipokuwa ndani yake.
Hakuna faida yoyote katika matendo yao:
si katika kuomba, au kuchunguza maandiko, au kusikiliza neno la Mungu, au kula
mkate ana kukinywea kile kikombe cha meza ya Bwana. Kama
wale wanaosema.” Kristo ni njia pekee ya kupata neema”, Inamaanisha kwamba yeye
ndiye pekee wa kusababisha neema, haiwezekani kushinda, ni kwa yeyote ambaye
hujua neema ya Mungu. Kwa “Kristo”, kama Mtume aliyvyosema,”Ni yote katika
yote”.
Siyo tu kusema maombi ya mtu
“Wengi
wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jila lako?
Mathayo 7: 22
Bwana wetu alisema
mara kadhaa kwamba, hakuna mtu ambaye hana ufalme wa Mungu ndani yake watakayeingia katika ufalme wa mbinguni.
Hata hivyo, alijua vema kwamba wengi wasingeupokea usemi huu. Kwa hiyo
anathibitisha: “Wengi (siyo mmoja, siyo wachache tu; siyo kitu cha
juu juu) wataniambia katika siku hiyo”, siyo tu kwa kuomba sana; tumekusifu;
hatujafanya uovu; lakini nini cha zaidi: “Tumefanya unabii kwa jina lako”.
Tumesema mapenzi yako kwa wanaume na wanawake, tumewaonyesha wenye dhambi njia
ya amani na utukufu. Na tunapofanya hivi “Kwa jina lako”, kwa
mujibu wa kweli ya Injili yako. Katika au kwa jina lako, “Kwa nguvu
ya neno lako na Roho wako” hatukutoa
pepo; na kwa jina lako (kwa nguvu zako, siyo zetu) hatukufanya miujiza mingi?
Lakini Yesu
alisema, “na kisha nitawaambia kamwe sikuwajua ninyi”, sikuwajua ninyi kuwa
watu wangu, kwa kuwa mioyo haikuwa sawa/ kukamilika kumwelekea Mungu. Hamkuwa
wapole na wanyenyekevu; hamkuwa na upendo wa mungu; na watu wote. Hamkufanya
upya katika sura ya Mungu; hamkuwa watakatifu kama jinsi nilivyo mtakatifu.
“Ondokeni kwangu, ninyi” ambayo licha ya yote sheria yangu ni takatifu na pendo
langu ni kamilifu. Umejenga juu ya mchanga.
Wema wangu wote, moyo wangu
wote
“Fanyeni
yote kwa utukufu wa Mungu”
1 Wakorintho 10: 31
Kujiwekea hazina
duniani kunakatazwa kabisa na Bwana wetu na kufananishwa na
muuaji au mwasherati. Kwa kufanya hivyo, utakuwa unajiwekea hasira katika siku
ya hasira (ghadhabu) na kufunulia kwa wenye haki siku ya hukumu ya Mungu.
Lakini, jaribu
kufikiri kwamba isingekuwa inakatazwa? Je,
waweza kwa sababu za msingi, kutumia pesa kwa namna ambayo Mungu anaweza
kukusamehe, badala ya kutumia katika namna ambayo hatukupa thawabu? Hatukuwa na
thawabu mbinguni kwa kile ulichoweka; lakini pia utapata thawabu
kwa kile ulichoweka mbinguni. Kila kiasi cha pesa unchoweka katika benki ya
kidunia kinapotea, hakileti faida yoyote. Lakini kila kiasi cha pesa unachompa
masikini kinawekwa katika akauni yako, katika benki ya mbinguni. Na italeta
faida yenye utukufu, ikikusanywa katika umilele wote.
Ni nani aliye na
ufahamu na hekima kwenu? Na akusaidie leo hii, akichagua katika mambo yote, “njia
iliyo bora zaidi.” Kwa uthabiti
akitunza maamuzi sawasawa na kupumzika (kulala), sala, kazi, chakula,
mazungumzo. Lakini vivyo hivyo katika kutumia kipawa muhimu na pesa. Moyo wako
na uitikie katika wito wa Mungu, “kuanzia sasa, Mungu
awe msaada wangu, sitaweka hazina tena hapa duniani”.
Nitaweka hazina mbinguni nitampa Mungu vitu vyake vyote, vyote vilivyo vyema na
moyo wangu wote.
Kutimiza kusudi la Mungu
“Nimekuchagua
katika tanuru ya mateso”
Isaya 44:10
Unapokuwa na uwezo
juu ya moyo wa mwanadamu, Mungu hutiririsha chemchemi za moyo
kama apendavyo. Kwa namna Fulani, huwasababisha wale awapendao kwenda nguvu
hadi nguvu hata watakapofikia “utimilifu wa utakatifu”, kwa shida na kwa hali
ya uzito. Lakini mambo kama haya hutokea kwa nadra sana. Kwa ujumla, Mungu
huona mema ili kuwajaribu wanaume na wanawake waliokubaliwa
ndani ya tanuru ya mateso.
Kwa hiyo, wingi wa
majaribu na uzito huwapata wengi au wachache miongoni mwa watoto
awapendao sana. Hakika, karibu watoto wote wa Mungu hupitia hii hatua, kwa
kiwango cha juu au cha chini.
Bila mashaka,
tunapaswa kukesha na kuomba na kujitahidi kwa kadiri
tuwezavyo kuepuka kuanguka katika giza. Lakini hatuhitaji sana kujua namna ya
kuepuka uzito kama namna ya kuboresha maisha yetu. Hiyo hali inapotokea tunapaswa
kuwa waangalifu tunapomngoja Bwana ili uzito uweze kukamilisha kile
kilichoruhusiwa - ili imani yetu iweze kuongozeka tumaini letu
linapothibitika, hasira ya kibinadamu itakapoondolewa, na
pendo lote hukamilika.
Tufanye kazi pamoja
naye, kwa namna ambayo Bwana ameendelea kumkirimia, katika “kujitakasa katika
uchafu, wa kimwili na kiroho”. Na kukua katika neema ya
Bwana wetu yesu Kristo, mpaka tutakapopelekwa katika ufalme wake
wa milele.
Ukristo halisi
“Lakini
pasipo imani haiwezekani kumpendeza”
Waebrania 11: 6
Baadhi ya wanaume
na wanawake hujenga tumaini la wokovu wao katika hali ya kutokuwa na hatia.
Je, wewe ni mmoja wao? Je, umejenga katika hali ya
kuona kwamba hauna uhasama au ugomvi na mtu yeyote – hujamkosea mtu yeyote?
Unajitaabisha tu! Unafanya mambo ambayo hayaongezi lolote kwako, kwani ndiyo
sote tunavyopaswa kufanya. Husemi uongo, na unaishi
vema. Na unadhamiri kumwelekea Mungu; wala haishi katika dhambi yoyote.
Yote ni mema pia,
lakini hayo yote siyo wokovu. Unaweza kwenda au kufanya zaidi ya hapo na
usiende mbinguni. Ikiwa hali hii inatoka katika kanuni sahihi, ni
sehemu ndogo ya dini na kikristo. Lakini kama haitokani na kanuni sahihi, basi
siyo sehemu ya dini kabisa. Kwa hiyo kuweka wokovu juu ya sehemu hiyo peke
yake, bado utakuwa unajenga juu ya mchanga. Je, bado unaendelea zaidi? Je,
unaongeza katika mtendo yako? Unaangalia njia zote za neema? Katika fursa zote
angalia meza ya Bwana, fanya maombi ya mkusanyiko na ya faragha,
fanya mara kwa mara kwa kadiri uwezavyo, unavyosikia, na chunguza maandiko na
tafakari maandiko hayo?
Kweli, mambo haya
yanapaswa kuwa yamefanyika. Hata hivyo, haya pia ni bure ikiwa yatafanyika bila
imani, rehema na upendo wa Mungu, utakatifu wa moyo;
mbingu kufunguka ndani ya nafsi kama kuna hivi, bado utakuwa umejenga juu ya
mchanga.
Omba kabla migogoro
“Na
ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye wewe na yeye peke yenu”.
Mathayo 18:
Njia kuu ya kawaida
ya kufuata kanuni ya kwanza hapo juu ni bora kama wewe
mwneyewe umeona au kusikia mkristo mwanamke ametenda dhambi
isiyoweza kukanwa (Undeniable sin) - kiasi kwamba ni
ngumu wewe kuwa na shaka juu ya ukweli wake hivyo sehemu yako
ni dhahiri. Chukua nafsi ya kwanza kumwendea na kumwambia kosa lake kati yenu.
Lazima kuwa na umakini mkubwa ili jambo lifanyike katika roho
sahihi na katika namna sahihi. Maonyo yenye mafanikio hasa hutegemeana na roho
ambayo maonyo hayo yametolewa. Omba kwa bidii ili kwamba
yafanyike katika roho ya upole na unyenyekevu. Kwani mtu hawezi kurejeshwa
pasipo roho ya upole (angalia Wagalatia 6; 1)
Angalia pia namna
unavyoongea iwe sawasawa na injili ya Kristo. Epuka namna
Fulani ya kutazama, ishara, sauti yenye kiburi au kutokuwa mnyenyekevu, kuwa na
msimamo au majivuno, pamoja na kujali kwa usawa, epuka mshikano wa wenye
hasira; kushutumu; au dalili ya kuumizwa, uchungu, au uchungu
katika maelezo. Tumia pumzi na lugha tamu na upole pia, ambavyo vinatokana na
upendo katika moyo. Hata hivyo utamu huu hauhitaji kukuzuia kusema kwa kumaanisha
… Mungu kwa kadri ianvyobidi, tumia maneno matakatifu ya Mungu, kama jicho lake
yeye ajaye kuwahukumu walio hai na wafu.
Kuomba katika Roho ya upole
“Mrejezeni mtu kama huyo kwa
roho ya upole”
Wagalatia 6: 1
Kama wema umefanyika kwa kile kilichosemwa,
ni Mungu anayefanya. Omba ili aulinde moyo wako, aongeze ufahamu wako, na
auelekeze mwili wako katika maneno kama apendavyo katika kubariki. Kama
akipinga kweli, hataweza kuletwe katika kuijua kweli hiyo, isipokuwa kwa upole.
Hata hivyo ongea katika roho ya
upendo wa dhati”, ambao maji mengi hayawezi kuuzimisha”. Kama upendo hauwezi
kushindwa, unaweza kushinda vitu vyote, nani aweza kuelezea nguvu ya upendo?
Upendo unaweza kuinamisha shingo shupavu,
jiwe kuwa nyama laini, lainisha, na kuchoma, na kuvunja moyo wa mtu mkaidi.
Kama huna fursa ya kuongea na mtu; unaweza kufanya hivyo kwa kutumia mjumbe,
rafiki wa karibu na mwenye busara na mnyofu ambaye hawezi kumficha. Kuongea
wewe mwenyewe ni bora zaidi,
lakini njia hii ni bora pia kuliko kutoongea kabisa (yaani kutumia rafiki wa karibu) kama huwezi kusema mwenyewe au kupata mjumbe mwaminifu
(wakili wa siri), kilichobaki ni kuweka ujumbe huo katika maandishi. Kuna
baadhi ya mazingira ambayo hufanya
njia kuwa ndiyo hasa inayoweza kutumika katika kufikisha ujumbe.
Ikiwa mtu mwenyewe ni mwenye hasira
ukamfikia kwa lugha laini (maandishi rahisi) katiak namna ambayo ataweza
kuvumilia. Wengi huweza kusoma
maneno yale yale ambayo wasingeweza
kusikia moja kwa moja. Kwa kuongeza jina lako, ni karibu sawa na kuongea na mtu.
Kuongea (KUZUNGUMZA) na Bwana”
“Maana yote yawezekana kwa Mungu”
Marko 10: 32
Ni namna Fulani ya
ujuzi wa jumla kwa wana wa Mungu kwamba bila
kujali kutofautiana katika masuala Fulani. Fulani,
hukubaliana na ujumla katika hili: ijapokuwa tunaweza” kwa Roho, kufisha matendo ya mwili” na
kumdhoofisha adui yetu siku kwa siku, hata hivyo hatuwezi kumwondoa. Kwa neema
tuliyopewa siku ya wokovu hatuwezi kuviondoa. Ingawa tunaomba na kukesha
kwa kadiri tuwezavyo, hatuwezi hata kujitakasa mioyo yetu na mioyo yetu na
mikono yetu.
Kwa hakika kabisa,
hatuwezi, mpaka inapompendeza Bwana wetu kusema / kuzungumza na mioyo yetu. Tena, kuzungumza kwa mara ya
pili, “uwe safi!” hivyo ni ukoma tu uliotakasika kisha ni shida ovu, nia ya
mwili, imeharibiwa, na dhambi ya asili hauwezi kustahimili.
Katika hali hii,
tunapokuwa tumetubu, hivyo tunaitwa “kuamini injili” na hili nalo linapaswa
kueleweka kwa upekee, tofautiana ambapo tuliamini ili kuhesabiwa haki. Tunapaswa
kuamini habari njema ya wokovu mkuu na mkamilifu ambao Mungu ameondoa.
Amini kwamba yeye ambaye ni mng’ao wa utukufu wa baba yake, ana uwezo wa
kuwaokoa wote wamjiao katika yeye. Ana uwezo wa kuokoa katika
dhambi zote ambazo zimebaki ndani ya moyo, wako – na kukupa chochote
unachopungukiwa. Hili haliwezekani kwa mwanadamu, lakini kwa Mungu yote
yanawezekana.
Endelea kukesha na kuomba
“Na
masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema …. Njia ni hii, ifuateni”
Isaya 3: 21
Unaona mabadiliko
na maendeleo au mabadiliko yasiyoweza kuhojiwa kutoka neema hadi dhambi. Hiyo
huendelea, kutoka hatua hadi hatua: (1) Mbegu
ya uepndo ya ki-ungu, imani ishindayo hubaki ndani ya aliyezaliwa
na Mungu. “Hujilinda mwenyewe”
kwa neema ya Mungu na hawezi kutenda dhambi”. (2) Jaribu linapoinuka; kama ni kutokea ulimwenguni,
katika mwili au kwa shetani, haijalishi (3) Roho mtakatifu humpa tahadhari kuwa
kwamba dhambi iko karibu na anapaswa kukesha katika sala. (4) Hukupa
njia, kwa kiasi Fulani katika jaribu, ambalo sana limeanza
kufuata mapenzi ya Mungu (yaani kilichoruhusiwa (5) Roho mtakatifu
amehuzunishwa; imani yake imedhoofishwa na upendo wa Mungu umepoa
(6) Roho mtakatifu anamwonya kwa bidii akisema, “Hii ndiyo njia; tembea katika
hiyo” (7) Anageuka mbali na sauti ya Mungu na kusikiliza sauti
ya kupendeza ya majaribu (8) shauku huanza na kuenea ndani ya nafsi
yake mpaka imani na upendo unapotoweka.
Hatimaye huanza
kutenda dhambi kwa dhahiri na nguvu inaondoka katika maisha yake. Ni ukweli
usiohojiwa, kwamba aliyezaliwa na Mungu, hujilinda,
huwa haishi au kutenda dhambi. Hata kama hata
“Jilinda mwenyewe” anaweza kutenda dhambi za kila aina kwa uchu.
Amri mbili zilizo kuu
“Utampenda”
Marko 12: 30.
Kumpenda Bwana
Mungu wako kwa moyo wako, akili nafsi nguvu ni tawi la kwanza la hakiya
mkristo. Utajifurahisha katika Bwana Mungu, ukitafuta na
kupata furaha timilifu katika yeye. Utasikia
na kutimiza neno lake, “Mungu nipe moyo wako”. Na baada ya kumpa mtu wa ndani
ili kutawala hapo bila ya kuvutana, unaweza kulia katika utimilifu wa
moyo wako”, Nitakupenda, ee Bwana wangu, nguvu zangu. Bwana
ni wangu ndio imara; mwokozi wangu; Mungu wangu, ambaye ninamtegemea.
Amri ya pili, tawi
kuu la pili katika hali ya kikristo, ni kwa
karibu na isiyotengana kabisa na ile ya kwanza”. Mpende jirani yako kama nafsi
yako.”
“upendo” –
ukumbatie kwa mapenzi mema, kwa bidii na pendo
la dhati, shauku inayowaka ndani kuzuia au kukufunga na uovu na kuleta kila
mema unapobidi. “Jirani yako” – siyo tu rafiki zako, washirika wenzako tu, au
watu mnaofahamiana; siyo tu wenye nguvu (Neema) wanaokuheshimu, wanaokutendea
mema, au kurudisha wema lakini kila mtu, siyo kuwatenga watu
ambao hajawahi kuwaona au kuwajua kwa majina; siyo kwa
kuwatenga watu unaowajua ka ubaya au wasio na shukurani, na wale ambao licha ya
kukutumia.
Hata wale ambao
utawapenda kama unavyo jipenda mwenyewe kwa kiu na furaha ile ile. Tumia
umakini ule ule usiochoka kuhakikisha kwamba unawaponya na mambo ambayo yaweza
kuwaumiza au kumjeruhi nafsi au miili yao. Huu ni upendo.
Kuthibitishwa katika milele yote
“Aidhihirishe bidii ile ile
kwa utimilifu wa matumaini hata mwisho”
Waebrania 6: 11
Tunathibitisha kipawa cha Mungu ndani yetu kwa hisia za ndani, kwa kile ambacho ametuonyesha – hisia za
pendo kuu na uwezo wa hali ya juu wa kuhisi (kutambua). Sasa
tunaishi katika furaha na siyo katika hofu. Tunatazama mambo yenye kuleta furaha, hali, sifa, mambo yote
ya dunia, kama yasiyokuwa na thamani, wa dhahiri, yasiyo kuwa na mfano wa vitu vya milele.
Je, unaweza kusema, ”wewe, Bwana
na rehema katika hali yangu yakutokuwa na haki; makosa yangu hukuyakumbuka
daima?” kisha, kwa muda ujao, tazama kwamba unaruka dhambi kama kutoka katika
uso wa nyoka! Kwa jinsi gani jambo hilo huonekana ni dhambi iliyozidi
mbele zako sasa!
Kwa upendo
mwingine, kwa jinsi gani katika nuru unaweza kuona mapenzi ya Mungu yaliyo
matakatifu na makamilifu! Sasa, kwa hiyo,
fanya kazi ili yaweze kutimia katika maisha yako, kwa kupitia wewe, au kwa kuwa
juu yako! Sasa kaza na uombe ili usijetenda dhambi
tena, kwamba uone na kujiepusha na hata dhambi ndogo katika amri zake.
Jua linapoangaza katika giza, utaona vitu ambavyo hukuweza kuviona, kuanzia sasa jua
la haki linawaka ndani ya moyo wako, na sasa unaweza kuona dhambi ambazo
usingeweza kuziona hapo kwanza. Hivyo uwe
na shauku zaidi ya kupokea nuru zaidi kila siku, zaidi ya maarifa na pendo la
Mungu, zaidi ya Roho wa Kristo, zaidi
ya uhai wake na zaidi ya nguvu za ufufuo. Sasa tumia vyote unavyopata. Kwa hiyo
utazidi kuongezeka katika upendo mtakatifu mpaka imani itakapomezwa katika upeo
na sheria ya upendo itakapothibitishwa katika umilele wote!
Kinyume na pendo la Mungu
“Wote
niwapendao Mimi nawakemea… basi uwe na bidii, ukatubu”.
Ufunuo 3: 19
Mara au baada ya kuhesabiwa
haki, mwamini anajisikia (utashi) – kufanya ambayo si kinyume
na mapenzi ya Mungu. Sasa - (matakwa)
ni sehemu muhimu sana ya siri katika mwili wa binadamu mwenye akili,
hata ya Bwana wetu mwenyewe. Lakini ni mapenzi ya kibinadamu yalitiishwa katika mapenzi ya baba
yake.
Suala ambalo hata
waminio wa kweli katika Kristo ni kwamba kuyafuata
mapenzi yao zaidi au kuyainua kiasi Fulani kuliko ya Mungu. Wanapamba dhidi
utashi wa mapenzi yao. Kwa nguvu zao zote na kisha huendelea katika imani.
Lakini (utashi –
ubinafsi) kama kilivyo kiburi ni vionyo vya sanamu. Yote yako tofauti na upendo
wa Mungu, kama ilivyo kwa katika kupenda ulimwengu. Ni kweli mtu kutoka mautini
na kuingia uzimani, hana shauku ya Mugnu zaidi. Hakika
unaweza kusema, “Hakuna kingine katika ninacho tamam,
zaidi yako”.
Lakini mara zote si
hivyo. Kama hataendelea kukesha na kuomba, atajisikia tu kuependa ulimwengu,
lakini tamaa huanza kuinuaka na kushambulia pendo la Mungu ndani yake.
Hujisikia pambano la juu katika kupenda viumbe (ulimwengu) kuliko muumba –
aliye viumba vitu vyote- iwe ni mme, wazazi, watoto, mke, rafiki wa karibu.
kiasi kwamba
hujitoa kwenye shauku / tamaa za mambo ya
kidunia na starehe zake, huelekea kumsahau Mungu. Na katika hili, hata wakristo
wa kweli katika Kristo wanahitaji kutubu.
Kuwa mkrito kwa pamoja
“…pendo
la Mugnu liemiminwa ndani ya mioyo yetu kwa njia ya Roho
mtakatifu tuliyopewa”
Warumi 5: 6
Haitoshi tu
kujitenga na uovu na kutenda mema katika fursa zote, pia haitoshi kutumia njia
zote za neema kwa unyofu na shauku ya kumpenda Mungu.
Swali kubwa hubaki
kwa kila mmoja wetu: Je, moyo wangu hulia kwamba yeye ni yote kwangu? Je, ninafuraha
katika Mungu? Je, yeye (Mungu) ni shangwe yangu? Je haikuandikwa
ndani ya moyo wangu kwamba wale wampendao Mungu
huwapenda majirani zao?
Endelea mbele
zaidi: Je, ninaamini kwamba Kristo alinipenda na akajitoa
mwenyewe kwa ajili yangu? Je, nina imani katika damu yake? Je, ninaamini kwamba
mwana kondoo ameniondoa dhambi zangu zote na kuzitupa
kama jiwe katika kina cha bahari, na kunipa ukombozi kupitia
damu yake, na hata ondole la dhambi? Je, Roho
wake
huishuhudia roho yangu kwamba Mimi ni mwana wa mungu?
Mtu asikushawishi
kuacha dhawabu ya mwito mkuu. Lia mchana na usiku mbele zake ambaye, mlipokuwa
hamna nguvu akafu kwa ajili ya waovu; mpaka utakapomjua unayemwamini kumfahamu
kwamba mko pamoja kama wakaristo.
Kisha, kuhesabiwa haki bure kwa neema. Kwa ukombozi ulio katika Yesu, utakuwa
na ujuzi wa Baraka ya Kristo
na kujua pendo la Mungu lililomiminwa katika moyo kwa Roho tuliyopewa.
Kuzaliwa kutoka juu
“Mmezaliwa mara ya pili, si
kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye
uzima, lidumulo hata milele”
1 Petro 1: 23.
Haijalishi kama hukuishi maisha ya
kujidhili na hukuishi maisha ya dhambi ya kudhamiria. Lazima uende mbele ya
zaidi, au vinginevyo huwezi kuokolewa. Hata kama unafanya mema kwa kadiri
uwezavyo na umefanikiwa kutumia nafsi ulizopata kutenda mema, hata hivyo hayo
mema hayafuti au kubatili suala
(kuzaliwa mara ya pili). Bado, unahitaji kuzaliwa mara ya pili.
Pasipo kuzaliwa mara ya pili, hakuna
utakachofanya katika hali ya umaskini, ya dhambi na nafsi iliyochafuka. Unaweza
kuhudhuria ibada kwa uaminifu na kushiriki meza ya Bwana, na kuomba sana kwa
faragha; na kusikia jumbe nyingi za Neno la Mungu; unaweza kuwa umewahi kusoma
vitabu vingi sana. Bado; “unapaswa
kuzaliwa mara ya pili” Hakuna hata kimoja kati ya hivi kinachoweza (chini ya
jua) kukuokoa na Jehanamu, isipokuwa umezaliwa mara ya pili.
Kama bado hujapata badiliko hili ni ndani
kupitia kazi ya Mungu; “haya yawe maombi ya kuendelea katika maisha yako”,
Bwana, ongeza hili katika Baraka zako zote – Nizaliwe mara ya pili.
Usininyime hili; nizaliwe kutoka juu, ondoa
kila kisichokupendeza - tabia mbaya, bahati, mbaya, marafiki wabaya, Afya mbaya – unipe hiki tu – kuzaliwa mara ya pili,
kupokelewa miongoni mwa watoto wa Mungu. Nizaliwe na mbegu isiyoharibika kwa
Neno la Mungu. Nikue kila siku katika neema, na katika maarifa ya Bwana na
Mwokozi Yesu Kristo.
Swali la kushangaza
“Lakini kila na mmoja
hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanyanywa”
Yakobo 1: 14
Wengi wenye mioyo minyoofu wamekuwa
wakishangazwa na maswali. ”Je, dhambi hutangulia au hufuata baada ya
kupoteza imani? Je, mtoto wa Mungu lazima atende dhambi kwanza ndipo apoteze imani? Au hupoteza imani yake
kwanza, kabla ya kutenda dhambi?”
Ninajibu: baadhi ya
dhambi za kutotenda tuliyopewa kutenda, lazima hutangulia kupoteza imani-dhambi
ya ndani. Lakini kupoteza imani lazima kutanguliwe na kutenda dhambi. Kwa
kadiri mwamini anavyozidi kuchunguza moyo wake, ndivyo anavyoshuhudiwa
hili. Kutenda kwa upendo huondoa dhambi ya ndani ya nje katika nafsi ya mtu
anayekesha katika sala. Hata ikiwa tukiwa katika hali ya majaribu, hasa
tunapokuwa katika dhambi ituzingayo kwa upesi.
Ikiwa jicho la
upendo la nafsi linamtazama Mungu, jaribu hutoweka mara
moja. Lakini kama sivyo tuko, kama mtume Yakobo asemavyo (Mstari wa 14),
tunaondoshwa mbali na Mungu kwa tamaaa zetu na kukamatwa
na kipawa cha starehe za muda tulizoahidiwa. Kisha hiyo tamaaa,
hutunga mimba ndani yetu, huzaa dhambi, (Mstari 15). Kwa kuwa ni dhambi hiyo ndani,
hudhoofisha na kisha kuharibu imani, tunakuwa tumekamatwa katika mtego wa
Ibilisi, ili tuweze kutenda dhambi yoyote iliyo dhahiri. Kwa hiyo, kisha
wakati wote, ili uweze kusikia na kutii sauti ya Mungu wakati wote.
Tiba: mimina moyo wako katika
sala
“Jijaribuni wenyewe…
jithibitisheni wenyewe”
2Wakorintho 13: 5
Je, umemlazimisha Mungu kuondoka katika
maisha yako kwa kuruhusu hasira? Je, umewahi kuvunjika moyo kwa sababu ya maisha ya
waovu? Au Umewahi kuwaonea wivu watenda mabaya? Je, umewahi kukwazwa na Kaka au
Dada katika Bwana, ukiangalia uhalisi wa dhambi ya kufikirika - ili kutenda dhambi dhidi ya sheria na upendo, kwa kuugeuza moyo wako
mbali mno? Mwangalie Bwana ili moyo wako uweze kufanywa upya -
na kwamba ubaridi na ukatili huo uondoke, ili upendo, amani na furaha irejee,
kwa moyo mkunjufu na roho ya msamaha.
Je, umejitoa katika tamaa za upumbavu? Katika aina yoyote au kwa kiasi Fulani cha kutokuwa mwadilifu,ufedhuli, pendo lisilo na uadilifu? Je, inawezekanaje upendo wa Mungu kuwa na nafsi ndani ya moyo wako mpaka utakapoweka vinyago mbali nawe? Haiwezekani kupona au kupata nuru ya Bwana ndani yako mpaka, “umeling’oa jicho lako la kuume,” na kulitupa mbali nawe. Ondoa vinyago vyote katika patakatifu pake, na mara utukufu wa Bwana utaonekana mara.
Labda ni kutokana
na bidii, uvivu wa kiroho ambao umeiweka roho yako katika giza. Unandelea
katika hali hiyo hiyo, katika shughuli za kawaida, na giza hilo limekuwa sehemu
ya maisha yako.
Je, unastaajabu
kwamba roho yako imekufa? Oo, jichochee mwenyewe mbele za Bwana.
Jikung’ute mavumbi: pigana mieleka na Bwana ili upate Baraka kuu za ki-Mungu.
Mimina moyo wako katika maombi! Endelea kwa uvumilivu wote! Kesha! Uamke kutoka katika usingizi na
uwe macho, ili usiwe tena na tena mateka mbali na nuru na uzima wa Mungu.
Ushikilie sana ujasiri wako
“Bali
neno la Bwana huduma hata milele”
1 Petro 1: 25
Ni vigumu kujua
kuliko kuelezea mapambano “vita” (mawazo) ambayo kwayo Shetani huleta majaribu
kwa wale ambao wana njaa na kiu ya haki. Wanaona vema, kwa uwazi zaidi kwa
upande mmoja, uovu uliokithiri wa mioyo yao. Kwa upande mwingine ni utakatifu
usio na doa lolote ambao kwa huo waliitiwa.
Mara nyingi,
wanaona hakuna roho iliyobaki ndnai yao. Wanaona uharibifu na jinsi
walivyofungwa na Mungu, na jinsi walivyokuwa mbali na utukufu wa Mtakatifu, na
wako tayari kuacha vyote, imani na tumaini. Hukaribia kutupa ujasiri ambapo
“wanaweza mambo yote katika kristo awatiaye nguvu”. Hata hivyo kupitia kristo
wanaweza kupokea ahadi.
Wakati shambulio
hili lina ghafla linapokuja, shikilia sana, “najua mkombozi wangu yu hai, na
nitasismama siku ya mwisho juu ya nchi”. Na sasa nina ukombozi katika damu
yake, na ondoleo la dhambi”.
Hivyo, kujazwa na amani na fuzaha timilifu katika kumwamini, songa mbele
katika imani ya kuwa na amani; na furaha katika kufanywa upya kwa nafsi katika
sura yake aliyekuumba. Kwa sasa, mlilie Mungu ili upate thawabu ya mwito mkuu,
na siyo kama shetani anavyowakilisha, lakini katika uzuri wa asili yake. Siyo
kama kitu ambacho lazima, au utakwenda Jehanamu lakini kama kitu ambacho
kinaweza kukuonyesha kuelekea mbinguni.
U-lazima wenye kudiriki
“Tukiangusha
… kila kitu kilichoinuka… tukiteka nyara kila fikra… ipate kumtii Kristo”
2 Wakorintho 10: 5
Usahihi wa mtazamo
wa asili ya toba na imani kwa waaminio unahitajika ili kuepuka madhara ya wazi
ambayo hatuhitaji kuwa na badiliko lingine zaidi. Kwa kuwa wenye afya
hawahitaji tabibu. Kama ndani tumefanywa wazima tayari,
hakuna nafasi ya kutafuta uponyaji tena.
Vinginevyo, ule
ushawishi wa Roho mtakatifu unaotuonyesha kwamba bado hatuja - kamilika, badohatushurutishi kupata ukombozi mkamilifu kwake aliye na
uwezo wa kuokoa-kuishi kwamba anaweza kutusaidia:
Vunja nira za
dhambi za mawazo na uiweke roho yangu huru ki ukamilifu! Siwezi kupumzika mpaka
usafi uwemo moyoni, mpaka nimekaa ndani yako kabisa.
Usahihi wa mtazamo
wa hii toba na hii imani, huenda sambamba na ushawishi wa Roho
Mtakatifu kuhusu udhaifu wetu na hatia, ni lazima kabisa ili tuweze kuona uthamani
wa kweli wa upatanisho katika damu. Tunahitaji ulazima wa kuona kushawishiwa au
kushurutishwa na roho mtakatifu ili kujua au kufahamu
kwamba tunahitaji hali hiyo ndani yetu mara baada ya kuhesabiwa haki
kama ilivyokuwa hapo kwanza wakati tunashurutishwa na roho mtakatifu ili
kuokoka ili kujua kuomba;
Anaishi (Mungu) juu
ili tuweze kufanya maombezi, pendo lake la upatanisho na damu yake ya thamani,
kusihi.
Hatimahe usahihi wa
mtazamo wa toba na imani ya waaminio huleta ushawishi wa Roho Mtakatifu
unaodhihirisha udhaifu wa kutoweza kuhifadhi cochote tulicopokea, ambao kwa huo
tumeletwa kumhimidi Mungu il kila hali ya kuhamaki, mawazo, neno na tendo
viletwe katika kumtii kristo.
Imani ilivyoongezwa kama njia
“Bwana
Mungu akamwita Ibrahimu”
Mwanzo 3: 9
Ni hakika kwamba
imani; hata katika ujumla wa neno lenyewe haikuwa na sehemu katika pepo
(Paradiso). Ni uwezekano wa hali ya juu, kutoka katika kitabu cha Mwanzo,
kwamba Adamu (kabla hajamwasi Mungu) alitembea na Mungu kwa hisia na siyo kwa
imani.
“Kwa sababu hiyo
macho yake yalikuwa yana nguvu na uwezo, Na (kama Tai awezavyo kutazama juu)
aliweza kutazama uso wa Muumba kwa karibu kama jinsi malaika
walivyoweza kufanya. Alikuwa anauwezo wa kuongea na Mungu uso kwa uso, yeye
ambaye uso wake hatuwezi kuuona na kuishi naye katika hali ya ki-mwili;
hivyoAdamu hakuhitaji imani ambayo kazi ni kutusaidia vema.
Kwa upande
mwingine, hiyo ni hakika kwamba imani katika uhalisi wake haikuwa na nafsi
kwao. Kwa mantiki hiyo, ni lazima kufikiria dhambi na ghadhabu ya Mungu dhidi
ya wenye dhambi. Pasipo haya hakuna haja ya upatansiho kati ya mwenye dhambi na
Mungu.
Kama kusingekuwa na
haja ya upatanisho kabla ya anguko, hivyo kusingekuwa na nafsi ya imani katika
upatanisho huo. Kwa sababu mwnadamu alikuwa safi mbali na doa la dhambi; yaani
Mtakatifu kama Mungu alivyo Mtakatifu.
Na Upendo, mpaka
hapo ulikuwa umejaa moyo wake, na kutawala hapa pasipo uasi. Lakini upendo
ulikupokuwa umepotezwa na dhambi, imani iliongezwa, siyo kwa jinsi yake, lakini
kama njia ya kuimarisha au kuthibitisha sheria ya upendo.
Ushirika na Mungu katika
kuzaliwa upya
“Tuliumbwa katika Kristo”
Waefeso 2: 10
Tunapokuwa tumezaliwa
mara ya pili ki-ungu, sasa tunaweza kusema tunaishi maisha sahihi. Mungu
anakuwa ametuhuisha maisha ambayo ulimwengu hauyaelewi-na uhai wake umefichwa
katika Kristo. Katika Mungu “Mungu anaendelea kupulizia pumzi yake
katika nafsi yake, kama aina Fulani ya upumuaji wa
kiroho, na nafsi nayo inapumua kumwelekea Mungu”.
Neema hushuka
katika moyo wake, maombi na sifa hupanda kuelekea juu
mbinguni: kwa ushiirika huu kati ya mtu na Mungu mwenyewe, kwa ushirika huu,
kati ya Baba na mwana, uhai wa Mungu ndani ya mtu huendelea kuwepo. Mtoto wa
Mungu hakua, mpaka atakapofikia utimilifu wa cheo cha kristo (Aghalia Waefeso
4:13).
Tunaona ya kuwa
asili ya kuzaliwa upya ni kwamba badiliko kubwa ambalo hutokea wakati Mungu
anatenda kazi ndnai ya nafsi, wakati Mungu
analeta uhai ndani yake, akiinua nafsi kutoka katika wafu (mauti) na kuileta
katika uhai wa haki. Ni badiliko ambalo huleta ndani ya nafsi na Roho Mtakatifu
wakati nafsi ikiumbwa upya ili kufanana na Mungu katika haki na utakatifu wa
kweli (Angalia Waefeso 4:24).
Kuupenda ulimwengu
kunabadilishwa na kumpenda Mungu; kiburi kuwa unyoofu, ukatili kuwa
unyenyekevu; chuki, wivu, tamaaa za kidunia, nia ya kishetani hugeuzwa na kuwa
nia iliyokuwa katika kristo Yesu. Hii ni asili ya kuzaliwa upya: “ kadhalika
kwa mtu aliyezaliwa kwa Roho”.
Kuitwa na Mungu
“Usijivune,
bali Uogope”
Warumi 11:20
Mungu huenda mbele
yetu na Baraka za wema wake. Kwanza kabisa, anatupenda na kujidhihirisha ndani
yetu. Tulipokuwa tungali mbali na neema yake alituita na kutuangazia nuru yake
katika mioyo yetu. Lakini kama hatutampenda aliyetenda kwanza na kuisikia sauti
yake, na kuyageuza macho yetu mbali naye, na kutokuruhusu nuru kuingia ndani
yetu, na Roho wake wakati wote hushindana (Angalia Mwanzo 6:3). Kwa taratibu,
huanza kuondoka na kutia giza ndan iyetu, isipokuwa roho zetu tuwasiliane naye
tena; isipokuwa tumerudisha pendo, sifa
na maombi yasiyokoma, mawazo ya mioyo yetu, maneno yetu, na matendo yetu:
mwili, nafsi na roho katika hali ya dhabihu takatifu na iliyokubalika (Angalia
Warumi 12:1).
Tujifunze kufuata
maelekezo hayo ya Mtume Mkuu, “Usinie makuu, lakini
uogope”. Tuogope dhambi, kuliko mauti au Jehanamu. Na tuwe na hofu nyenye wivu,
(japokuwa si kwa maumivu), ili tusije tukategemea moyo uliodanganyika. “yeye
aliyesimama, aangalie asije akaanguka”. Hata yeye ambaye amesiamama imara
katika neema ya Mungu, katika imani ishindayo ulimwngu anaweza kuangukia katika
dhambi ya kutenda asiyopaswa kutenda na kuleta uharibifu wa imani”.
Kwa jinsi gani
dhambi ya nje (inayoonekana) anavyopatanguvu ya kutawala maisha yako! Kesheni,
kwamba mwombe bila kukoma wakati wote na kila
mahali, huku ukiumimina moyo mbele ya Mungu! Hivyo unapaswa kuamini wkati wote,
kupenda wakati wote, na kamwe kutotenda dhambi tena.
Uhai wa Mungu ndani ya roho
“Basi,
kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika hayo
yatakayotokea”
Luka 21 : 36
Kwa mara moja na
kwa ulazima Fulani, uhai wa Mungu unamaanisha mwendelezo wa tendo la Mungu juu
ya roho kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu na mwitikio wa roho ya mtu kwa Mungu
kurudisha pendo, maombi na sifa zisizokoma.
Kuanzisha hapa,
inaonekana kwa uwazi kwamba Mungu hataendelea kutenda lolote ndani ya roho,
mpaka roho ya mtu inapoendelea kuwa na mawasiliano na Mungu. Ni rahisi kuelewa
jinsi hawa watoto wa Mungu, Daudi, Barnabas, na Petro, wanaweza kufanya kitu kutokana
na uimara wao, na hata hivyo kweli kuu ya Mungu, ilinenwa na Mtume Yohana, ibaki
imara na bila kutikiswa. Hawakujilinda wenyewe, bali kwa neema ya Mungu.
Hawakujilinda wenyewe, bali kwa neema ya Mungu, ambayo inatosha kwa kila mmoja.
Kila mmoja huanguka, hatua kwa hatua, kwanza katika mambo ya kinyume, ndani ya
moyo wa mtu, “bila kuchochea karama ya Mungu iliyo ndani yake,” bila “kukesha
na kuomba”, bila “kukaza mwendo ili kupata thawabu ya mwito mkuu”.
Uzito wa nafsi
“Uko
katika uzito”
1Petro 1: 6
Kuna uhusiano wa
karibu katika ya giza katika ufahamu, na hali ya ukame na
uzito wa nafsi, ambo ni wa kawaida miongoni mwa waaminio. Kufanana kwake ni kwa
hali ya juu kiasi kwamba hali hizi hushikamana pamoja. Lakini haya si maneno
yanayofanana; siyo mbali, tofauti yake ni kubwa na ya
muhimu sana, kama jinsi ambavyo watoto wa Mungu wanahitaji kuelewa ili kuwazuia
wasiteleze katika uzito ndani ya giza.
Aina ya watu ambao
mtume petro alwaandikia walikuwa ni waaminio wakati huo anasema kwa uwezi
(mstari 5) nanyi mnalindwa na nguvu za mungu kwa njia ya imani hata mpate
wokovu tena (mstari 7) ametaja ili kwamba kujaribiwa kwa imani yetu na hivyo
tena (mstari 9) anaongelea kupokea mwisho wa imani yenu yaani ya wakovu wa roho
kwa hiyo ingawa walikuwa katika hali ya uzito lakini waliokuwa na imani iliyo
hai.
Uzito wao haukuweza
kuharibu imani. Hauwezi kuharibu amani ambayo haiwezi
kutengwa na imani ya kweli na iliyo hai. Mtume anaomba (Mstari 2) siyo kuomba
neema na amani iliyo tolewa, lakini iweze kuongozwa. Pia walikuwa wamejaa
tumaini lililo hai. Kwa sababu, anasema, (Mstari 3) …. Baba wa Bwana wetu Yesu
Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini
lenye uzima kwa kufukuka kwake Yesu kristo katika wafu; licha ya uzito wao,
bado wana tumaini timilifu. Na wakafurahi (Mstari 8) kwa furaha isiyo neneka,
yenye utukufu. Pamoja na uzito wao, huendelea na tumaini lililo hai furaha
isiyoneneka!.
Changamoto ya mwisho
“Ili
ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiye uliyenituma”
Yohana 17: 21
Oo,
ili kwamba wote wanaolichukua jina la Kiristo waweze kuweka ouvu mbali nawe
– kwa kuongea, kunong’ona usiruhusu hata kimoja kati ya hivi kutoka kinywani
mwako! Angalia, usiseme neno ovu dhidi ya mwenzako, usiseme lolote isipokuwa
lililo jema. Kama ungeweza kutofautishwa au kuwa mtu mashuhuri, na iwe kwa
alama hii: “Hawamsengenyi mtu anapokuwa hayupo”. Kwa jinsi gani matokeo ya
kujina mwenyewe, hata tukajaza haraka ndani ya mioyo yetu? Jinsi amani yetu
inavyoweza kutiririka kama mto! Jinsi upendo wa Mungu unavyoweza kujaa tele
ndani ya nafsi zetu huku tukithibitisha upendo wetu kwa Kaka na Dada zetu! Ni
matokeo gani tutapata kwa hayo yote kwa umoja katika jina la Yesu Kristo! Jinsi
upendo wa ndugu unaweza kuendelea kuongezeka ambapo kizuizi chake
kilikwishatolewa.
Wala hii siyo yote. Ni matokeo gani haya
yanaweza kuwa Jangwa, ulimwingu usiofikiria! Hivi karibuni wataona ndani yetu
kile ambacho wasingeweza kukipata katika maelfu yao yote, na kulia, “Ona jinsi
hawa wakristo wanavyopendana wao kwa wao”,
Kwa hii, Mungu atazidi kuishawishi dunia na
kuwaandaa wao pia kwa ajili ya ufalme wake (Mungu). Kwa kuwa tunaweza kujifunza
kutoka katika maneno hayo na ajabu ya ibada ya mwisho ya maombi ya Mungu wetu;
“Nawaombea wale ambao wataniamini mimi, ambao wanaweza kuwa na umoja… ili
kwamba ulimwengu upate kujua wewe ndiwe uliyenituma”.
Mungu, fanya hima muda ambao tunapendana
kwa kweli na kwa ukweli, kama Yesu Kristo atupendavyo!