Niko Duniani kwa Kusudi Gani?
Maisha yanayotegemea vitu ni
maisha mfu, kama kisiki; maisha
yanayomtegemea Mungu ni mti
unaostawi sana.
Mithali 11:28 (Msg)
Wamebarikiwa wanaomtumaini Bwana…
Ni kama miti iliyopandwa
kandokando ya mto,
Yenye mizizi ifikayo chini kwenye
maji. Miti kama hiyo
Haisumbuliwi na joto wala miezi ya
ukame. Majani yake
Hukaa mabichi na hudumu kuzaa
matunda mazuri.
Yeremia 17:7-8 (NLT)
Siku ya Kwanza
Yote
Huanza Na Mungu
Kwa kila jambo, hakika kwa kila kitu,
kiicho juu na kiicho
chini, kinachoonekana na
kisichoonekana,….
Kila kitu kilianza katika yeye na
hupata
Kusudi lake katika yeye.
Wakolosai 1:16 (Mag)
Bila kukubali kuwa kuna Mungu,
swali kuhusu
Kusudi la maisha halina maana.
Bertrand Russel, mpagani asiyeamini kuwa kuna Mungu
Siyo kuhusu Wewe.
Kusudi la maisha yako liko juu Zaidi ya utoshelevu wako binafsi, Amani
yako, au hata furaha yako. Ni kubwa Zaidi ya jamaa yako, kazi yako, hata kuliko
ndoto na matazamio ya mbele uliyo nayo. Kama unataka kujua kwa nini uliwekwa
hapa duiani, lazima uanze na Mungu. Ulizaliwa na kusudi lake na kwa kusudi
lake.
Kutafuta maana ya maisha kumewatatiza watu wengi kwa maelfu ya
miaka. Hivi ni kwa sababu tunaanza na mwanzo mbaya – sisi wenyewe. Tunauliza
maswali ya ubinaafsi kama, Je, nataka kuwa nani? Je, nifanye nini na maisha yangu? Je malengo yangu ni yapi,
matarajio yangu, na ndoto zangu kwa
ajili ya siku zijazo? Lakini kule kutafuta majibu ya maswali haya kutoka ndani
yetu hakutatudhihirishia kusudi la maisha yetu. Biblia husema, “Mungu
ndiye huongoza maisha ya viumbe yake; maisha ya kila mtu yako katika uwezo
wake.” Ayubu 12:10 (TEV)
Tofauti na mafundisho ya vitabu
vingi vya siku hizi, sinema, na semina huwezi kugundua kusudi la maisha yako
kwa kujichunguza ndani yako. Labda umekwisha kujaribu hivyo. Hukujiumba
mwenyewe, hivyo hakuna njia yoyote unaweza kujieleza kwa nini uliumbwa. Kama
nikikupatia chombo kilichovumbuliwa na hujawahi kukiona kabla huwezi kujua
kusudi lake, na hata chombo hicho chenyewe hakiwezi kukueleza.
Wakati fulani nilipotea mlimani. Niliposimama kuuliza njia iendayo
kwenye kituo, nilielezwa, “Huwezi kufika huko kutokea hapa. Ni lazima uanzie upande mwingine wa mlima.” Vivyo hivyo, huwezi
kufika kwenye kusudi la maisha yako kwa kuanzia kujitazama mwenyewe. Ni lazima
uanze na Mungu, Muumba wako. Unaishi kwa sababu tu Mungu anapenda uishi. Wewe
uliumbwa na Mungu – na kwa ajili ya Mungu – na mpaka ufahamu hivyo, maisha
hayatakuwa na maana yoyote. Ni katika Mungu peke yake nidipo tunaweza kuvumbua
asili yetu, utambullisho wetu, umuhimu wetu, kusudi letu, umaana wetu, na
mwisho wa maisha yetu kwa ujumla. Njia nyingine yoyote hugonga ukuta.
Watu Wengi hujaribu kumtumikia Mungu katika kujithibitishia nafsi
zao wenyewe, lakini hivyo ni kinyume cha asili na mwisho wake ni kushindwa.
Uliumbwa kwa ajili ya Mungu, na siyo kinyume, na maana ya maisha ni kumruhusu
Mungu, akutumie kwa malengo yake, siyo wewe umtumie Mungu kwa malengo yako.
Biblia husema, “kuendekeza nafsi yako katika mambo haya,
huleta mauti, lakini kumtazama Mungu hutuongoza mahali pa uwazi na maisha buru.” Warumi 8:6 (Msg)
Nimesoma vitabu vingi ambavyo hupendekeza njia za kugundua kusudi
la maisha yangu. Vyote naweza kuviweka katika kundi la “jisaidie-mwenyewe” kwa
sababu vinalishughulikia somo hili katika mtazamo wa ubinafsi (kujitazama
mwenyewe). Vitabu vya jisaidie-mwenyewe, hata vile vya Kikristo, mara nyingi
vinatoa hatua zile zile zinazoweza kutabirika katika kutafuta kusudi la maisha
yako: Angalia ndoto zako. Changanua mambo unayoyathamini (values). Weka
malengo. Tambua kipawa chako. Uwe na malengo ya juu. Shughulikia hayo. Jiweke
wakfu. Amini unaweza kuyatimiza malengo yako. Wahusishe wengine. Usikate tamaa.
Kwa hakika, maelezo haya huleta mafanikio makubwa mara kwa mara.
Mara nyingi utafanikiwa kufikia lengo lako unapoweka moyo wako hapo. Lakini
kuwa na mafanikio na kutosheleza kusudi la maisha yako siyo kitu kimoja kabisa!
Unaweza kufikia malengo yako yote binafsi, ukawa na mafanikio makubwa kwa jinsi
ya viwango vya dunia hii, na bado ukakosa kusudi zima alilokuumbia Mungu.
Unahitaji Zaidi ya ushauri wa jisaidie-mwenyewe. Biblia inasema, “kujisaidia
mwenyewe si msaada kabisa. Kujitoa nafsi yako ndiyo njia, njia yangu, katika
kuipata nafsi yako, nafsi yako halisi.
Mathayo 16:25 (Msg)
Hiki siyo kitabu cha jisaidie-mwenyewe. Siyo kuhusu namna ya
kupata kazi sahihi, kufanikiwa ndoto zako, au kupanga kuhusu maisha yako. Siyo
kuhusu namna ya kuongeza shughuli katika ratiba yako iliyojaa. Hakika
kitakufundisha namna ya kufanya mambo machache – kwa kuangalia mambo yaliyo ya
muhimu zaidi. Kitabu hiki kinaeleza namna ya kuwa vile Mungu alivyokuumba uwe.
Sasa je, ni kwa jinsi gani unaweza
kuvumbua kusudi uliloumbiwa? Una njia mbili tu. Njia ya kwanza ni kukisia. Hii ndiyo njia ambayo watu wengi huichagua. Hubahatisha,
kukisia, wakaandika nadharia. Watu wnaposema, “Mara nyingi nimedhania maisha ni….,”
wana maana kwamba “Hili ndilo kisio bora ninaloweza kulifanya.”
Kwa maelfu ya miaka, wanafalsafa wenye akili wamejadili kuhusu
maana ya maisha. Falsafa ni somo muhimu na lina umuhimu wake; lakini habari ya
kutambua kusudi la maisha, hata wanafalsafa wenye hekima kuu hubahatisha tu.
Dr. Hugh Moorhead, mwalimu wa falsafa katika Chua kikuu cha
Northeastern Illinois, aliwaandikia wanafalsafa maarufu, wanasayansi,
waandishi, na wenye akili ulimwenguni, wapatao 250, akawauliza swali, “Nini
maana ya maisha?” Kisha alichapisha majibu hayo katika kitabu.Baadhi yao
walitoa makisio yao bora, wengine walikubali Kwamba walijitengenezea lengo la
maisha, na baadhi yao walikuwa waungwana wakakubali kuwa hawakufahamu chochote.
Kwa hakika, baadhi ya watu hawa maarufu wenye akili walimwandikia Profesa
Moorhead kuwaandikia tena na kuwaarifu kama alivumbua kusudi la maisha!
(Chicago: Chicago review Press, 1988)
Kwa bahati nzuri, kuna njia
nyingine Zaidi ya ile ya kukisia kuhusu maana na kusudi la maisha. Njia hii ni ufunuo.
Tunaweza kupata kile Mungu
alichokifunua kuhusu maisha katika neno lake. Njia rahisi ya kugundua kusudi la
chombo chochote kipya ni kuuliza aliyekitengeneza. Ukweli huu unawiana na
kugundua kusudi la maisha yako: Muulize Mungu. Mungu hajatuacha tutangetange
katika giza na kubahatisha. Amefunua wazi makusudi yake matano kwa ajili ya
maisha yetu katika Biblia. Hiki ni kitabu cha maelezo kwetu, kutueleza kwa nini
tuko hai, maisha huendaje, nini cha kuepuka, na kitu gani kitatokea hapo siku
za usoni. Biblia hutuelezea mambo ambayo kitabu cha jisaidie-mwenyewe au
falsafa hakiwezi kuyajua. Biblia husema, “Hekima ya Mungu…
huenda ndani sana katika makusudi yake… siyo ujumbe mpya, lakini ni wa zamani –
kile ambacho Mungu alikusudia kuwa njia ya kuleta mema ndani yetu.” 1Wakorintho 2L7 (Msg)
Mungu siyo tu mwanzo wa maisha yako, Yeye ni asili yake. Ili
kugundua kusudi la maisha yako lazima ugeukie neno la Mungu, siyo hekima ya
ulimwengu. Unapaswa kujenga maisha yako kwenye msingi wa kweli wa milele, siyo
katika saikolojia, hamasa ya mafanikio, au hadithi za kuhamasisha. Biblia
inasema, “Katika Kristo tunatambua sisi ni nani na
tunaishi kwa ajili gani. Mwanzoni tulipokuwa hatujasikia habari za Kristo na
kutupa matumaini, Yeye aliweka jicho laske kwetu, alikuwa na mipango juu yetu
ya maisha ya utukufu, ambayo ni sehemu ya mpango uliokamilika anaotekeleza
katika kila kitu na kila mtu.” Waefeso 1:11 (Msg) Kifungu hiki
hutupatia utambuzi wa aina tatu kuhusu kusudi lake:
1.
Unavumbua wewe ni nani na kusudi
lako kwa kuwa na uhusiano na Yesu Kristo. Kama huna uhusiano kama huo, baadaye
nitaeleza namna ya kuuanzisha.
2.
Mungu alikuwa akifikiri juu yako
tangu zamani kabla hujawaza chochote juu yake. Kusudi lake kwa maisha yako
limekuwepo kabla ya kutungwa mimba yako. Alipanga kabla hujakuwepo, bila
mchango wako! Unaweza kuchagua aina ya kazi,
mwenzi wa ndoa, mambo uyapendayo na mengine mengi kuhusu maisha yako, lakini
huchagua kusudi lako.
3.
Kusudi la maisha yako linawiana na
kusudi kubwa la uumbaji wa Mungu ambalo Mungu ameliweka kwa umilele. Kitabu
hiki kipo kwa ajili yako.
Andrei Bitov, mwandishi wa Kirusi wa vitabu vya hadithi, alikulia
katika mazingira ya utawala wa Kikomunisti ambayo hayakubali kuwa kuna Mungu. Lakini
Mungu alipata usikivu wa mtu huyu siku moja ya huzuni. Anakumbuka, “Katika
mwaka wangu wa ishirini na saba, nilipokuwa katika treni linalopita chini ya
ardhi katika mji wa Leningrad (sasa St. Petersburg) nililemewa na kukata tamaa
kiasi kwamba maisha yalionekana kukoma mara moja, yakiwa bila matumaini yoyote
ya mbele wala maana yoyote kabisa. Ghafla, bila mtu yeyote kuhusika, maneno
haya yalionekana: Bila Mungu maisha hayana maana. Nikayarudia kwa mshangao, nilitoka katika treni huyo na kutembea
katika nuru ya Mungu. (Boston: Little, Brown, 1991)
Unaweza kuwa
umejisikia uko gizani kuhusu kusudi la maisha yako. Hongera, uko karibu kuingia
nuruni.
Siku ya pili
Wewe
Si Bahati Mbaya
Mimi ni Muumba wako. Ulikuwa
katika uangalizi
Wangu hata kabla hujazaliwa
Isaya 44:2a (CEV)
Mungu hachezi bahati nasibu.
Albert Einstein
Wewe si bahati mbaya.
Kuzaliwa kwako hakukutrokana na makossa wala bahati mbaya, na
maisha yako si matokeo ya bahati tu ya asili. Wazazi wako wanaweza kuwa
hawakupanga kukuzaa lakini Mungu alipanga.Hajashangazwa hata kidogo na kuzaliwa
kwako. Kwa kweli alitegemea uzaliwe.
Hapo zamani kabla hujatungwa mimba na wazazi wako, ulitungwa
katika mawazo ya Mungu. Alikufikiri kwanza. Si jambo baya, wala bahati au tukio
la bila kutegemewa kwamba wewe unapumua kwa wakati huu. Uko hai kwa sababu
Mungu alitaka kukuumba! Biblia inasema. “Bwana atatimiza
kusudi lake kwangu.” Zaburi 138:8
Mungu alitoa maagizo ya kila kipengele cha mwili wako. Kwa kusudi
kabisa alichagua taifa lako, rangi ya ngozi na nywele zako na kila kiungo
chako. Alilitengeneza umbile lako kama alivyopenda. Pia alikupangia vipawa vya
kuzaliwa navyo na namna ya hulka yako binafsi. Biblia inasema, “Unanijua
ndani nan je, unajua kila mfupa katika mwili wangu; unajua jinsi
nilivyotengenezwa, kidgo kidogo, nilivyotokana na vitu visivyokuwepo nilikuwa
mtu halisi.” Zaburi 139:15 (Msg)
Kwa kuwa Mungu alikuumba akiwa na sababu, pia aliamua ni lini
uzaliwe na uishi kwa muda gani. Alipanga siku za maisha yako kabla, akachagua
muda maalum wa kuzaliwa na kufa kwako. Biblia inasema, “Uliniona
kabla sijazaliwa na ukapanga kila siku ya maisha yangu kabla sijaanza kupumua.
Kila siku iliandikwa katika kitabu chako.”
Zaburi 139:16 (LB)
Mungu pia alipanga wapi uzaliwe na wapi uishi kwa ajili ya kusudi
lake. Rangi na utaifa wako si wa bahati mbaya. Mungu hakuacha kipengele
chochote cha maisha yako kitokee kwa bahati. Alipanga yote kwa ajili ya kusudi
lake. Biblia inasema, “Kutoka katika mtu mmoja alifanya kila
taifa … na aliwapangia nyakati na mipaka ya makazi yao.” Matendo 17:26 (NIV) Hakuna chochote katika maisha yako
kinachoamriwa tu. Kuna kusudi katika yote.
Cha kustaajabisha Zaidi, Mungu aliamua utakavyozaliwa. Bila kujali
mazingira uliyozaliwa au wazazi wako ni nani, Mungu alikuwa na mpango
alipokuumba. Haijalishi kama wazazi wako walikuwa wema au wabaya au wasiojali.
Mungu alijua kwamba watu hao wawili walikuwa na viini sahihi vya uzazi kuweza
kutengeneza kama wewe mwenye sura aliyokuwa nayo akilini mwake. Walikuwa na
viini vya uzazi (DNA) Mungu alivyovitaka ili kukutengeneza wewe.
Ingawa kuna wazazi haramu, hakuna
watoto haramu. Watoto wengi hawakuwa katika mpango wa wazazi wao lakini si
kwamba hawakupangwa na Mungu. Kusudi la Mungu lilipitia katika kosa au hata
dhambi ya watu.
Mungu kamwe hafanyi jambo lolote kwa kubahatisha na wala hafanyi makossa.
Analo kusudi kwa kila anachokiumba. Kila mmea na kila mnyama alikusudiwa na
Mungu, na kila mtu alibuniwa kwa malengo maalum. Nia ya Mungu kukuumba ilikuwa
ni upendo wake. Biblia inasema, “Hapo zamani kabla Mungu hajaweka
misingi ya ulimwengu alitujua, na kutuweka kuwa washiriki wakuu wa pendo lake.” Waefeso 1:4a (Msg)
Mungu alikuwa anakufikiri hata kabla hajiaumba ulimwengu. Bila shaka
ndiyo maana aliuumba ulimwengu. Mungu alibuni mazingira ya sayari hii dunia,
yafae kwa sisi kuishi. Sisi ndio kitovu cha mwelekeo wa upendo wake na wa
thamani kuliko viumbe vyake vyote. Biblia inasema, “Mungu aliamua
kutupa uzima kwa njia ya neno la kweli ili tuwe wa muhimu sana kuliko vitu
vyote alivyoviumba.” Yakobo 1:18 (NCV) Hivi ndivyo
Mungu anavyokupenda na kukuthamini.
Mungu habahatishi; alipanga kwa usahihi mkubwa. Kadri wanasayansi
wanavyojifunza kuhusu ulimwengu, ndivyo tunatambua jinsi ulivyotengenezwa kwa
namna ya pekee utufae kuishi; ukawekewa utaratibu na mipango halisi ambayo
humwezesha binadamu kuishi.
Dr. Michael Denton mtaalam maarufu katika utafiti wa kibaiolojia
(molecular genetics) katika chuo kikuu cha Otango huko New Zealand, amehitimisha
akisema, “Ushahidi wote uliokwishapatikana katika sayansi za kibaiolojia
unaunga mkono … kwamba ulimwengu umebuniwa kwa ujumla ukiwa na lengo na kusudi
kuu la kuhifadhi uhai na binadamu, kila kitu kina maana na maelezo yanayolenga
ukweli huu. (New York, Free Press, 1998) Biblia ilisema jambo hilo hilo maelfu
ya miaka iliyopita. “Mungu aliumba nchi … Hakuiumba ikae
ukiwa lakini aliiumba ikaliwe. Isaya 45:18 (GWT)
Kwa nini Mungu alifanya haya yote? Kwa nini alijisumbua kuumba
ulimwengu kwa ajili yetu? Kwa sababu yeye ni Mungu wa upendo. Upendo wa namna
hii ni vigumu kuufahamu, lakini ni wa hakika na wa kuaminika. Uliumbwa kama
kiumbe maalum cha kupokea upendo wa Mungu! Mungu alikuumba ili akupende. Huu ni
ukweli wa kuimarisha maisha yako.
Biblia hutuambia, “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Haisemi kuwa Mungu ana upendo. Yeye ni upendo!
Upendo ndio kiini cha tabia ya Mungu. Kuna upendo
mkamilifu katika ushirika wa Utatu
wa Mungu, hivyo Mungu hakuhitaji akuumbe wewe. Hakuwa mpweke. Lakini alitaka
kukuumba ili aonyeshe upendo wake. Mungu anasema, “Nimekushika
mikononi tangu ulipozaliwa; nimekutunza tangu siku ile ulipozaliwa. Hata ukiwa
mzee, mimi nitakuwa yule yule. Hata nywele zako zikigeuka na kuwa nyeupe,
nitakutunza. Nilikuumba na nitakutunza.
Isaya 46:3-4 (NCV)
Kama Mungu asingekuwepo, sisi sote tungekuwa tumetokea kwa bahati
tu, matokeo ya mwendo wa viumbe vya angani. Ungeweza kuacha kusoma kitabu kiki
kwa sababu maisha hayangekuwa na maana yoyote. Kusingekuwa na mema wala mabaya,
wala matumaini baada ya miaka michache ya kuishi hapa duniani.
Lakini kuna Mungu aliyekuumba kwa kusudi, na maisha yako yana
umuhimu mkubwa! Tunavumbua maana na kusudi hilo tunapomfanya Mungu kuwa kiini
cha maisha yetu. Ujumbe wa Warumi 12:3 unasema, “Njia pekee sahihi
ya sisi kujitambua ni kwa vile Mungu alivyo na kwa yale Mungu anayotutendea.”
Ushairi wa Russell Kelfer unatoa muhtasari wa ukweli huu:
Wewe
ni wewe kwa kusudi.
Wewe
ni sehemu ya mpango wa ajabu.
Wewe
ni wa thamani na chombo maalum kikamilifu.
Unaitwa mtu mwanamume au mwanamke maalum wa Mungu.
Unaonekana
kama unatafuta sababu.
Mungu
wetu hakukosea.
Alikufinyanga
vizuri tumboni,
Wewe uko vile alivyopenda kukuumba.
Wazazi
ulionao ndio aliowachagua,
Na
haijalishi unajisikiaje,
Waliumbwa
kwa kusudi la Mungu,
Na wanao muhuri wa Bwana.
Hapana,
ile taabu uliyoipata haikuwa rahisi.
Na
Mungu alilia kwa kuwa ili kuufinyanga moyo wako.
Ili kwamba ukue katika sura yake.
Wewe
ni wewe kwa kusudi,
Umetengenezwa
kwa fimbo ya Bwana.
Wewe
ni wewe, mpendwa,
Kwa sababu kuna Mungu! (Russell Kelfer, Kimetumiwa kwa ruhusa)
Siku ya Tatu: Je, Nini Huongoza Maisha Yako?
Nilichunguza
na kuona kuwa nia kubwa ya mafanikio
ni
ule msukumo wa husuda na wivu!
Mhubiri 4:4 ( LB)
Mtu
asiye na lengo ni kama meli bila
usukani
– mtu aliyepotea, mtu bure, kabwela.
Thomas Carlyle
Maisha ya kila mtu yanaongozwa na kitu fulani.
Kamusi nyingi hugaganua neno ongoza (drive) kama “Kuongoza, kutawala, kuelekeza.” Unapokuwa unaongoza
gari, msumari, au mpira wa gofu, unachokifanya ni kuongoza, kutawala na
kuelekeza kwa wakati hua. Je, ni nguvu gani inayoongoza maisha yako?
Sasa hivi unaweza kuongozwa na tatizo, msukumo fulani, au tarehe
ya mwisho kwa kitu fulani. Unaweza kuongozwa na kumbukumbu ya jambo fulani
linaloumiza, hofu mbaya, au Imani ya ndani. Kuna mamia ya hali mbalimbali,
mambo muhimu, na hisia ambavyo vyaweza kukuongoza. Hapa kuna mambo matano
ambayo ni ya kawaida kwa wengi.
Watu
wengi huongozwa na hatia. Watu hawa hutumia muda wa maisha
yote wakiepuka lawama na kuficha aibu. Watu wanaoongozwa na hatia wanaonewa
sana na kumbukumbu. Wanaruhusu mambo yaliyopita kutawala mambo yao ya usoni.
Wanajiadhibu bila kujua kwa kuharibu mafanikio yao. Kaini
alipotenda dhambi, hatia yake ilimtenga na Mungu, na Mungu akasema, “Utakuwa
mtangatangaji asiyetulia katika nchi.”
Mwanzo 4:12 (NIV) Hii inawaeleza jinsi watu wengi walivyo siku hizi –
wanatagatanga katika maisha bila lengo.
Sisi ni matokeo ya muda uliopita lakini hatupaswi kuwa wafungwa wa
muda hua. Kusudi la Mungu halifungwi na muda wako uliopita. Alimbadilisha
muuaji Musa na kuwa kiongozi mzuri: akambadilisha Gidioni aliyekuwa mwoga akawa
shujaa na hodari; anaweza kufanya mambo ya ajabu na maisha yako yaliyobaki.
Mungu ni mtaalam wa kuwapa watu mwanzo mpya. Biblia inasema,”Wana
furaha kubwa wale waliosamehewa hatia yao! ….. Wana Amani wale waliotuby dhambi
zao na Mungu amefuta mashtaka yako.” Zaburi
32:1 (LB)
Watu
wengi wanaongozwa na chuki na hasira. Wanashikilia
maumivu (machungu) bila kuyaacha. Badala ya kutoka katika maumivu kwa kusamehe,
wanaendelea kuyakumbuka katika mawazo yao tena na tena. Baadhi ya watu
wanaoongozwa na chuki hutunza ndani uchungu wao, na wengine huwalipukia watu
wengine. Hali zoe hizi si nzuri na hazisaidii maishani.
Chuki mara nyingi huleta maumivu kwako kuliko yule unayemchukia.
Mtu aliyekukosea anaweza kuwa amesahau lile kosa na anaendelea na maisha yake
vizuri, wewe unaendelea kuumia na kuhangaika na yaliyopita.
Sikiza: Wale waliokuumiza wakati uliopita hawawezi huendelea
kufanya hivyo sasa isipokuwa
kama utaendelea kutunza uchungu. Yaliyopita yamepita! Hakuna
kitakachoyabadilisha. Unajiumiza tu na uchungu wako. Kwa ajili yako, jifunze
kutokana na hilo na kisha achana nalo. Biblia inasema, “Kuwa
na hofu kiasi cha kufa kwa sababu ya uchungu ni upumbavu, ni kitu cha kipumbavu
kukifanya.” Ayubu 5:2 (TEV).
Watu
wengi wanaongozwa na woga. Woga wao unaweza kutokana na
jambo baya sana lililowapata, matarajio yasiyotekelezeka, kukulia katika jamaa
isiyo na uhuru, au hata maumbile ya asili. Bila kujali sababu, watu
wanaoongozwa na woga mara nyingi hupitwa na nafasi kubwa kwa sababu wanaogopa
kuchukua hatua. Badala yake wanajitahidi kuwa salama, wakiepuka kupata hasara
na hivyo hujaribu kulinda hadhi yao.
Woga ni kifungo ambacho mtu hujifunga mwenyewe na chaweza kukuzuia
kuwa mtu yule ambaye Mungu anapenda uwe. Unatakiwa kutoka humo kwa silaha ya Imani
na upendo. Biblia inasema, “Upendo halisi huiondoa hofu kwa kuwa
hofu hulemaza, maisha ya hofu – hofu ya kifo, hofu ya hukumu – ni maisha ambayo
hayajakamilika katika upendo.” 1 Yohana 4:18 (Msg)
Watu
wengi wanaongozwa na mali. Tamaa yao ya kupata vitu linakuwa
ndilo lengo la maisha yao yote. Msukumo huu wa kutaka Zaidi kila siku una
misingi yako katika udanganyifu wa kuwa nikiwa na vingi nitakuwa na furaha Zaidi,
nitakuwa wa muhimu, na nitakuwa salama; lakini mawazo yote haya matatu si ya
kweli. Mali huleta furaha ya muda mfupi.
Kwa kuwa vitu havibadiliki, hivyo vinatuchosha na tunataka vipya, vikubwa, na
bora Zaidi.
Kuna Imani pia kwamba kama nitapata mali nyingi nitakuwa wa
muhimu. Umuhimu wako na umuhimu unaotegemea ulivyo navyo ni vitu viwili
tofauti. Thamani yako haitegemei mali zako, Mungu anasema kitu cha muhimu
maishani mwako si vitu!
Imani ya watu wengi kuhusu fedha
ni kwamba kuwa nazo nyingi kutanipa usalama. Haziwezi. Utajiri unaweza
kupotezwa mara moja kwa sababu zisizozuilika. Usalama halisi unaweza kupatikana
katika kile ambacho huwezi kunyang’anywa yaaani uhusiano wako na Mungu.
Watu
wengi wanaongozwa na kutaka sifa. Wanaruhusu
matarajio ya wazazi, waume au wake, watoto, waalimu au rafiki zao kutawala
maisha yao. Watu wazima wengi bado wanajaribu kupata sfa kwa wazazi wao ambao
hawajafurahi kamwe. Wengine wanasukumwa na vikundi vya marafiki, wanahofu
wenzao watawafikiriaje. Kwa bahati mbaya, wale wafuatao kundi hupotelea ndani
yake.
Sijui funguo zote za mafanikio, lakini ufunguo mmoja wa kushindwa
ni kujaribu kumpendeza kila mtu. Kutawaliwa na maoni ya watu wengine ni nijia
wazi ya kukosa makusudi ya Mungu katika maisha yako. Yesu alisema, “Hakuna
mtu awezaye kutumikia mabwana wawili.”
Mathayo 6:24 (NLT)
Kuna nguvu nyingine zinazoweza kuongoza maisha yako lakini zote
mwisho wako ni mfu: kutotumia vipawa ulivyo navyo, mahangaiko ya moyo, na
maisha yasiyo ya utoshelevu.
Safari hii siku 40 itakuonyesha jinsi ya kuishi maisha yanayoongozwa
na malengo – maisha yanaoongozwa, kutawaliwa , na kuelekezwa na makusudi ya
Mungu. Hakuna kitu cha muhimu Zaidi kama kujua malengo ya Mungu kwa maisha
yako, na hakuna mbadala kwa hilo – siyo mafanikio, utajiri, kujulikana, au
anasa. Bila malengo, maisha ni mwendo usio na maana, shughuli bila mwelekeo, na
matukio bila sababu. Bila malengo, Maisha ni kitu duni, kidogo sana, kisicho na
umuhimu wowote.
FAIDA
ZA KUISHI KWA MALENGO
Kuna faida kuu tano za kuishi misha yenye kuongozwa na malengo:
Kujua
lengo lako hukupa maana ya maisha yako.
Tuliumbwa tuwe na maana. Ndio maana watu hujaribu njia za udanganyifu kama
unajimu na mazingaombwe ili kuigundua. Maisha yanapokuwa na maana unaweza
kuchukuliana na chochote; bila hiyo hakuna kinachobebeka.
Kijana mmoja katika umri wa miaka 20 hivi aliandika, “najisikia
kama mtu aliyeshindwa kwa sababu najaribu kuwa kitu fulani, na hata sijui kitu
hicho ni nini. Ninachojua ni kuendelea tu. Siku fulani kama nitagundua lengo
langu, nitajisikia sasa naanza kuishi.
Bila Mungu maisha hayana lengo, na
bila lengo maisha hayana maana. Bila maana maisha hayana umuhimu wala thamani
au matumaini. Katika Biblia, watu wengi walionyesha hali hii ya kukosa
matumaini. Isaya alinung’unika akisema. “Nimefanya kazi
bila malengo; nimetumia nguvu zangu bure kabisa.”
Isaya 49:4 (NIV) Ayubu alisema, “Maisha yangu yamejikongoja – siku
baada ya siku bila matumaini.” Ayubu 7:6 (LB) na “Nakata
tamaa; nimechoka na kuishi. Niacheni. Maisha yangu hayana maana yoyote. Ayubu 7:16 (TEV) Jambo baya kuliko yote siyo kifo, lakini maisha
yasiyo na malengo.
Kuwa na tumaini ni muhimu kwa maisha yako kama vile hewa na maji.
Unahitaji tumaini ili kukabili mambo ya maisha. Dr. Bernie Siegel aligundua
kuwa angeweza kutabiri ni mgonjwa gani kati ya wagonjwa wake wa kansa angeweza
kufa kwa kuulize; “Je, unapenda kuishi mpaka miaka mia
moja?” Wale wenye hali ya kina ya malengo katika masha walijibu ndiyo
na hao ndio walioishi. Tumaini hutokana na kuwa na malengo.
Kama umewahi kujisikia kutokuwa na tumaini, tulia, mabadiliko
makubwa yatatokea maishani maishani mwako mara utakapoanza kuishi maisha yenye
malengo. Mungu anasema, “Najua yale ninayoyapanga kwa ajili
yenu … nina mipango mizuri kwa ajili yenu, sio mipango ya kuwaumiza.
Nitawapatia tumaini na mustakabali wa maana.”
Yeremia 29:11 (NCV) Unajihisi unakabiliana na hali isiyowezekana, lakini Biblia
inasema, “Mungu … anaweza kufanya Zaidi ya yale
tunayoweza kuyaomba au kuyaota – anafanya mambo ya juu Zaidi kuliko sala zetu,
nia zetu, mawazo yetu, au matumaini.”
Waefeso 3:20 (LB)
Kujua
lengo lako hurahisisha maisha yako. Hii
hukuwezesha kuelewa ni nini ufanye na nini usifanye. Lengo lako linakuwa ndicho
kigezo cha kutathmini kazi gani ni muhimu na zipi siyo. Unajiuliza, “Je, kazi
hii inanisaidia kutimiza moja ya malengo ya Mungu kwa maisha yangu?”
Bila kuwa na malengo Dhahiri huna msingi wa kufanyia maamuzi,
kupanga muda, na kutumia rasilimali zako. Utajaribu kuganya maamuzi kwa
kuzingatia mazingira, msukumo, na hali yako kimawazo wakati huo. Watu wasiojua
lengo lao hujaribu kufanya mambo mengi – na hiyo husababisha msongo (stress),
uchovu, na migongano.
Haiwezekani kufanya kila kitu watu wanachotaka ufanye. Una muda wa
kutosha tu kufanya mapenzi ya Mungu. Kama huwezi kufanya Zaidi ya Mungu
alivyokukusudia kufanya (au labda, unatumia muda wako mwingi kutazama runinga).
Kuishi kwa kuongozwa na malengo hutuwezesha kuishi maisha rahisi na yenye
ratiba iliyopangwa kwa busara. Biblia inasema, “Maisha ya kuigiza
na kujionyesha ni maisha ya ubatili; maisha ya uwazi na yaliyo rahisi ni maisha
ya utoshelevu.” Mithali 13:7 (Msg) Maisha yanayoongozwa
na malengo pia huleta Amani moyoni. “Wewe BWANA
unawapa Amani kamili wale wanaotunza malengo yao kwa uthabiti na kuweka tumaini
lao kwako.” Isaya 26:3 (TEV)
Kujua
lengo lako hukupa mwelekeo wa maisha yako.
Hukuwezesha kukusanya pamoja juhudi na nguvu zako kufanya kilicho cha muhimu.
Unakuwa na ufanisi katika kuchagua kilicho cha muhimu.
Ni hali ya binadamu kukanganywa na mambo madogo madogo. Tunacheza
mchezo wa Trivial Pursuit
katika maisha yetu. Henry David Thoreau alisema kuwa watu huishi maisha ya “kukata
tama sana,” lakini siku hizi maelezo mazuri yaweza kuwa ni kutokuwa
na mwelekeo. Watu wengi wako kama gurudumu
lizungukalo upesi (gyroscope) bila kwenda popote.
Bila kuwa na malengo Dhahiri, utadumu katika kubadili mwelekeo,
kazi, mahusiano, makanisa, na mengineyo – ukitegemea kuwa kila badiliko
litajaza utupu ulio moyoni mwako, unafikiri, Labda sasa mambo
yatakuwa tofauti, lakini tatizo lako halisi linabaki – kutokuwa na
mwelekeo na malengo.
Biblia inasema, “Msiishi pasipo uangalifu, bila
kufikiri. Hakikisheni Bwana wenu anapenda nini.”
Waefeso 5:17 (Msg)
Nguvu ya kuwa na mwelekeo inaweza kuonekana kwenye nuru. Nuru
hafifu ina nguvu kidogo, lakini unaweza kuifanya nuru hivyo kuwa na nguvu kwa
kukusanya pamoja mwanga huo. Kwa kutumia kipande cha kioo kikuzacho, mionzi ya
jua yaweza kukusanywa na kuchoma moto nyasi au karatasi. Mwanga huo
unapokusanywa pamoja kwa namna fulani unaweza kukata hata chuma.
Hakuna kitu chenye nguvu kama maisha yenye mwelekeo, ukiyaishi kwa
malengo. Wanaume na wanawake waliofanya tofauti kubwa katika historia ni watu
waliokuwa na mwelekeo. Mathalani, Mtume Paulo kwa sehemu kubwa alieneza Ukristo
katika Himaya ya Rumi. Siri yake ilikuwa maisha yenye mwelekeo. Alisema, “Ninaelekeza
nguvu zangu zote katika kitu kimoja: Nikiyasahau yaliyopita na ninatazama yale
valiyo mbele yangu.” Wafilipi 3:13 (NLT)
Kama unataka maisha yako yawe na mvuto mbubwa, yape
mwelekeo! Acha kufanya mambo juu juu tu. Acha kufanya mambo yote. Fanya
machache. Ondo ahata zile shughuli nzuri na ufanye kile cha muhimu Zaidi.
Usichanganye shughuli na ufanisi wa kuzalisha. Unaweza kuwa na shughuli nyingi
bila malengo, lakini kuna faida gani? Paulo anasema, “Na
tudumu kuwa na mwelekeo wa lengo hilo, sisi ambao tunataka kila kitu alichonacho
Mungu kwa ajili yetu.” Wafilipi 3:15 (Msg)
Kujua
lengo lako huhamasisha maisha yako. Lengo
wakati wote huzaa bidi ya moyo. Hakuna kinachotia nguvu kama lengo Dhahiri. Kwa
upande mwingine, shauku hupungua unapokuwa huna malengo. Kuamka toka kitandani
tu inakuwa mzigo. Mara nyingi hatuchoshwi na kufanya kazi za ziada, bali kazi
isiyokuwa na maana ndiyo hutuchosha sana na kutuchukulia furaha yetu yote.
George Bernard Shaw aliandika, “Hii ndiyo furaha ya kweli ya
maisha: kutumiwa kwa ajili ya lengo unalolifahamu kuwa ni kubwa; ikiwa ni nguvu
ya asili badala ya pupa za maumivu madogo madogo na manung’uniko, ukilalamika
kuwa ulimwengu hauwezi kujitoa na kukupa furaha.”
Kujua lengo lako hukuandaa kwa ajili ya maisha ya milele. Watu wengi wanatumia nguvu nyingi katika kujaribu kufanya
historia duniani. Wanapenda wakumbukwe watakapokuwa wametoka duniani. Lakini
cha muhimu Zaidi si kile watu watacholsema juu yako, bali kile Mungu anasema.
Kitu kile Mungu anasema. Kitu ambacho watu hushindwa kufahamu ni kwamba
mafanikio yote mwishowe hupitwa, na rekodi huvunjwa, heshima hufifia, na sifa za
watu husahaulika. Katika chuo, malengo ya James Dobson yalikuwa awe bingwa wa
shule yao katika mpira wa tenesi. Alijisikia vizuri sana pale kombe la ushindi
wake lilipowekwa katika schemu ya makombe ya shule ya ushindi. Miaka kadhaa
baada ya mtu mmoja alimtumia lile kombe. Walikuwa wameliokota kwenye pipa la
takataka wakati shule ilipofanyiwa matengezo. James akasema, “kadiri
muda wa kutosha unapopita vikombe vyako vya ushindi vitatupwa na mtu mwingine!” Wafilipi 3:15 (MSg)
Kuishi ukitengeneza historia ya kuacha duniani ni lengo la mtu
asiyeona mbali. BMatumizi ya busara ya muda ni kujenga urithi wa milele.
Hukuwekwa duniani ili ukumbukwe. Uliwekwa hapa kujiandaa kwa ajili ya umilele
Siku moja utasimama mbele za Mungu na atakagua maisha yako,
mtihani wa mwisho, kabla ya kuingia katika umilele. Biblia inasema, “Kumbuka
kila mmoja wetu binafsi atasimama mbele za kiti cha hukumu cha Mungu … ndiyo,
kila mmoja atapaswa kutoa hesabu binafsi kwa Mungu.”
Warumi 14: 10b, 12 (NLT) Kwa bahati, Mungu anatutaka tushinde jaribio hilo,
hivyo ametupa maswali mapema kabisa. Kutoka katika Biblia tunaweza kuona kuwa
Mungu atatuuliza maswali muhimu mawili:
Kwanza, “Je, ulifanya nini kuhusu mwanangu Yesu Kristo?”Mungu
hatauliza kuhusu maisha yako ya nyuma ya kidini au maoni kuhusu mafundisho ya Imani
Jambo la pekee ambalo litakuwa la muhimuni, Je, ulipokea kile Yesu alikufanyia
, na je, ulijifunza kumpenda na kumtumaini? Yesu alisema “Mimi
ndimi njia na ukweli wa uzima. Hakuna mtu awezaye kuja kwa Baba isipokuwa kwa
njia ya mimi.” Yohana 14:6 (NIV)
Pili, “Je, ulifanya nini na kile nilichokupa?” ulifanya nini na
vipawa vyote, nafasi mbalimbali, nguvu, mahusiano, na raslimali alizokupa
Mungu? Je, ulivitumia mwenyewe tu, au ulivitumia kwa malengo Mungu
aliyokuumbia? Kukuandaa kwa ajili ya maswali haya mawili ndilo kusudi la kitabu
hiki. Swali la kwanza litaamua ni wapi utaishi milele. Swali la pili litaamua
utafanya nini katika umilele. Mwisho wa kitabu hiki utakuwa tayari kujibu
maswali yote mawili.
Siku ya Nne: Umeumbwa Kuishi Milele
Mungu…
amepanda umilele ndani ya moyo wa mwanadamu.
Mhubiri 3:11 (NLT)
Hakika
Mungu asingeweza kuumba kiumbe kama binadamu na aishi kwa siku moja! Hash ahata
kidogo, mtu aliumbwa aishi milele.
Abraham Lincoln
Maisha haya si mwisho wa kila kitu.
Maisha duniani ni kama vazi la mazoezi tu kabla ya kitu halisi.
Utatumia muda mwingi Zaidi katika ule upande mwingine baada ya kifo – yaani
katika umilele kuliko hapa duniani. Duniani ni jukwaa la maonyesho yako ya
milele. Ni kazi ya mazoezi kabla ya mchezo halisi; matayarisho kabla ya
shindano halisi la mbio. Maisha haya ni maandalizi ya yale yajayo.
Kwa kiwango cha juu sana, unaweza kuishi miaka mia moja duniani,
lakini utaishi siku zote katika umilele. Maisha yako duniani ni, kama bwana
Thomas browne alivyosema, “ni alama ndogo sana katika umilele.” Uliumbwa ili
uishi milele.
Biblia inasema, “Mungu… amepanda umilele katika moyo wa
binadamu.” (NLT) Mhubiri 3:11Ndani yako kuna hali ya kuzaliwa nayo ambayo
inatamani kuishi tu bila kufa. Hii ni kwa sababu Mungu alikubuni katika sura
yake, uishi milele. Ingawa tunajua kwamba kila mtu mwishowe hufa kifo wakati
wote huonekana si cha kawaida na ni kibaya Sababu inayotufanya tujisikie kuishi
milele ni kwamba Mungu amefungamanisha hali hiyo na ubongo wetu!
Siku
moja moyo wako utaacha kupiga. Huo utakuwa mwisho wa mwili wako na wakati wako
hapa duniani. Mwili wako wa duniani ni makazi ya muda ya roho yako. Biblia
huita mwili wako wa duniani “hema,” lakini inauita mwili wako wa baadaye “nyumba”.
Biblia inasema, “wakati hemahili tunaloishi – mwili
wetu hapa duniani – likiharibiwa, Mungu anayo nyumba mbinguni ya sisi kuishi,
makazi ambayo Yeye mwenyewe ameandaa, yadumuyo milele”. 2 Wakorintho 5:1 (TEV)
Wakati
maisha duniani yana uchaguzi mwingi, umilele hutoa mambo mawili tu: mbingu au
kuzimu. Mahusiano yako na Mungu duniani yataamua uhusiano wako naye katika
umilele. Ukijifunza kumpenda na kumtumikia Mwana wa Mungu, Yesu, utakaribishwa
kuishi naye milele. Vinginevyo, kama utakataa upendo wake, msamaha, na wokovu
wake, basi utatengwa milele kutoka uso wa Mungu.
C.S
Lewis alisema, “Kuna aina mbili za watu: wale wasemao Mungu ‘mapenzi
yako yafanyike’ na wale ambao Mungu huwaambia ‘haya
basi, fanyeni mjuavyo wenyewe.’” Inasikitisha sana, watu wengi watalazimika kuishi katika hali
ya kutengwa na Mungu milele yote kwa kuwa walichangua kuishi bila Mungu hapa
duniani.
Utakapotambua bayana kwamba kuna Zaidi
katika maisha kuliko maisha haya katika dunia, na kufahamu kuwa maisha ni
maandaalizi tu ya umilele, utaanza kuishi kitofauti. Utaanza
kuishi katika nuru ya umilele na hiyo itaonekana katika jinsi
unavyohusiana na watu wengine, unavyofanya kazi, na unavyokuwa katika mazingira
mbalimbali. Ghafla, shughuli nyingi, malengo n ahata matatizo mengi yaliyokuwa
yakionekana ya muhimu yataanza kuonekana mambo madogo madogo yasiyohitaji
uyashughulikie. Kadiri unavyoishi karibu na Mungu, Ndivyo kila kitu huonekana
kidogo.
Unatumia
muda na pesa zako kwa busara. Unaweka umuhimu wa juu katika mahusiano na tabia
badala ya kutafuta kujulikana na utajiri au mambo makuu au hata michezo.
Mpangilio wa mambo yako muhimu unabadilika. Kufuatisha mambo ya kisasa kama
mitindo na mengineyo hayana maana tena. Paulo alisema, “Hapo
nyuma nilidhani mambo haya yote yalikuwa ya muhimu, lakini sasa nayaona kuwa
bure kwa sababu ya kile Kristo amefanya.”
Wafilipi 3:7 (NLT)
Iwapo muda wako duniani ungekuwa
ndiyo kila kitu kwa maisha yako, basi ningekushauri uanze kuutumia ipasavyo
mara moja. Ungeweza kusahau kuwa mwema wala mwadilifu, na wala usingehofu
chochote kama matokeo ya matendo yako. Ungeweza kuzama katika mambo ya
kuifurahisha nafsi yako kwa sababu matendo yako yasingekuwa na madhara ya
kudumu. Lakini – hii inafanya tofauti – kifo siyo mwisho wako! Kifo ni hali ya mpito kuelekea katika
umilele, hivyo kuna matokeo ya kila unachokifanya duniani. Kila tendo la
maishani mwetu hugusa nyuzi ambaxo hutikisa katika umilele.
Jambo
baya kabisa katika maisha ya siku hizi ni kuwa na mtazamo mfupi kimawazo. Ili
kutumia vizuri maisha yako unapaswa kuwa na maono ya umilele katika akili zako
na kutunza uthamani wako moyoni mwako. Kuna mengi Zaidi katika maisha kuliko ya
hapa na ya sasa tu! Leo ni kama ncha ndogo ya mwamba wa barafu ichomozayo
baharini. Umilele ni kama ile sehemu nyingine isiyooneka iliyo ndani ya bahari.
Je,
itakuwaje katika umilele na Mungu? Kusema wazi, uwezo wa ubongo wetu hauwezi
kuelewa ajabu na ukuu wa tovuti (internet) kwa sisimizi. Ni upuuzi.
Hayajagunduliwa maneno ambayo labda yangeweza kueleza hali ilivyo katika
umilele. Biblia inasema, “Hakuna mtu was kawaida amewahi kuona,
kusikia n ahata kufikiri mambo ya ajabu Mungu aliyowaandalia wale wampendeo.” 1 Korintho 2:9 (LB)
Lakini, Mungu ametudokeza kuhusu
mambo ya milele katika Neno lake. Tunajua kwamba sasa hivi Mungu anatuandalia
makao ya milele. Mbinguni tutakutana na wapendwa ambao ni waamini, tutakutana
na wapendwa ambao ni waamini, mateso, tutapewa tuzo kwa uaminifu hapa duniani,
na tutapewa kazi nyingine ambayo tutaifurahia kuifanya kwetu. Hatutalala
mawinguni tukizingirwa na nuru kichwani huku tukicheza vinubi! Tutafurahia
ushirika wa kudumu pamoja na Mungu, na atatufurahia milele. Siku moja Yeu
atasema, “Njooni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini
ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa kwa ulimwengu.” Mathayo 25:34 (NIV)
C.S.
Lewis aliliweka wazo la umilele katika ukurasa wa mwisho wa kitabu chake
dkiitwacho Chronicles of Narnia, ambayo ni sehemu ya vitabu vyake saba vyenye mfululizo wa
hadithi za watoto: “Kwetu huu ni mwisho wa hadithi zote… Lakini kwao ulikuwa ni
mwanzo wa hadithi ya kweli. Maisha yao yote hapa duniani … yalikuwa ni ukurasa
wa jalada na jina la kitabu; sasa hatimaye walikuwa wanaanza Sura ya kwanza ya
ile Hadithi Kuu, ambayo hakuna mtu hapa duniani amewahi kuisoma, ambayo
inaendelea milele na ambayo kila sura ni bora Zaidi kuliko iliyotangulia.” C.S.
lewis, Vita ya Mwisho (New York: Collier Books, 1970), 184.
Mungu
ana malengo kwa maisha yako duniani, lakini hayakomei hapa. Mpango wake unahusisha
Zaidi ya miongo michache ya miaka utakayoishi katika sayari hii. Ni Zaidi ya “nafasi
njema sana maishani;” Mungu hukupatia nafasi iliyo juu Zaidi kuliko maisha yako
ya hapa. Biblia inasema “Mipango yake (Mungu) yadumu milele;
makusudi yake niya milele.” Zaburi 33:11 (TEV)
Muda
pekee ambao watu hufikiri juu ya umilele ni ule wakati wa msiba, na hata hivyo
hufikiri juu juu tu bila ufahamu wa kutosha. Unaweza kudhani kuwa ni jambo baya
kuongelea mambo ya kifo, kwa kweli, si vema kuishi kwa kukikana kifo, kitu
ambacho ni lazima kitokee. Mhubiri 7:2 (CEV) Ni mpumbavu tu ndiye aweza kuishi
pasipo maandalizi kwa ajili ya kile sisi tunajua hatimaye kitatokea. Unahitaji
kufikiri Zaidi kuhusu umilele, na siyo kidogo.
Kama
ilivyokuwa katika ile miezi tisa uliyoitumia katika tumbo la mama yako kwamba
haikuwa mwisho wa yote, lakini maandalizi kwa ajili ya maisha, hivyo maisha
haya ni maandalizi kwa yajayo. Kama una uhusiano na Mungu kwa njia ya Yesu,
huhitaji kuogopa kifo. Ni mlango wa kuingia umilele. Hivyo itakuwa saa yako ya
mwisho wako. Badala ya kuwa mwisho wa maisha yako, itakuwa siku ya kuzaliwa
katika maisha ya umilele. Biblia inasema, “ulimwengu huu si
nyumbani, tunatazamia makao yetu ya kudumu mbinguni.”
Hebrews 13:14 (LB)
Maisha
yetu hapa duniani, yakilinganishwa na yale ya milele, ni kama kufumba na
kufumbua jicho, na matokeo yake yatadumu milele. Matendo ya maisha haya ni
mwamuzi wa maisha yajayo. Tunatakiwa “kufahamu kwamba
muda tuishipo katika miili hii ya duniani ni muda wa kukaa mbali na makao yetu
ya milele huko mbinguni na Yesu.” 2
Wakorintho 5:6 (LB) Miaka iliyopita kulikuwa na msemo uliopendwa na uliwahimiza
watu kuishi kila siku kama “siku ya kwanza ya maisha yako yote.” Hakika,
ingekuwa busara kuishi kila siku kama vile ilikuwa siku ya mwisho wa maisha
yako. Matthew Henry alisema, “Yapasa iwe wajibu wa kila siku kujiandaa kwa
ajili ya sku ya mwisho.”
Siku ya Tano:
Kuyaona Maisha Katika Mtazamo Wa Mungu
Maisha yako ni
kitu gani?
Yakobo
4:14 (NIV)
Hatuoni vitu kama
vilivyo, tunaviona kama tulivyo.
Anais
Nin
Jinsi
uyaonavyo
maisha yako huumba
maisha yako.
Jinsi
unavyoelewa maana ya maisha huamua juu ya hatima yako. Mtazamo wako utakuwa na
mvuto juu ya matumizi ya muda wako, pesa zako, vipawa na jinsi unavyothamini
mahusiano.
Njia
mojawapo ya kuwaelewa watu wengine ni kuwauliza, “Unayaonaje maisha
yako?” Utagundua kwamba kuna majibu mengi kwa swali hilo sawa na watu
uliowauliza. Nimeshaelezwa kuwa maisha ni tamasha, machimbo ya madini, reli
ndogo ya michezo, fumbo, wimbo, safari, na mchezo wa dansi. Watu wamesema, “maisha
ni karamu au ulevi: mara unaanguka, wakati mwingine unazunguka tu” au “maisha
ni baiskeli yenye mwendo mkali tusiyoweza kutumia gia zake” au “maisha ni kama
mchezo wa karata.”
Kama
ningekuuliza unayaoonaje maisha, je, picha gani ingekujia akilini mwako? Hiyo
sura ndiyo mfano wako wa maisha. Ni mtazamo wa maisha ulio nao, kwa kufahamu au
kutokufahamu, akilini mwako. Ni maelezo yako jinsi maisha yanavyofanya kazi ya yale
unayotazamia kuyapata. Mara nyingi watu hudhihirisha mfano wa maisha yao kwa
njia ya mavazi, mapambo, magari, nywele, maandishi makubwa, au hata mikwaruzo
katika miili yao.
Mfano
wa maisha yako ambao hautamkwi kwa maneno una mvuto kwa maisha yako kuliko
unavyofahamu. Huwa na mvuto kwa matarajio yako, mambo yako ya muhimu (values),
mahusiano yako, malengo na vipaumbele vyako. Mathalani kama unadhani maisha ni
sherehe, jambo muhimu maishani mwako litakuwa kujifurahisha. Kama unafikiri maisha ni mbio, utathamini mwendo
mkali na labda utakuwa mtu mwenye haraka wakati wote. Kama unaona
maisha kuwa riadha, utathamini uvumilivu.
Kama utaona maisha kuwa vita au mashindano, basi ushindi litakuwa jambo la muhimu kwako.
Je, mtazamo wako wa maisha ni upi?
Unaweza kuwa umejenga maisha yako kwenye mfano wa maisha usio sahihi. Ili
kutimiza malengo aliyokuumbia Mungu, basi utapaswa kuipa changamoto hekima yako
ya kawaida na badala yake utumie kielezo cha kibiblia kuhusu maisha. Biblia
inasema, “Msijifananishe na kanuni za ulimwengu huu,
lakini mpeni Mungu nafasi awabadilishe utu wa ndani kwa kuwabadilisha kabisa
nia zenu. Kisha mtaweza kuyajua mapenzi ya Mungu.”
Warumi 12:2 (TEV)
Biblia
hutoa mifano mitatu ambayo hutufundisha mtazamo wa Mungu wa maisha ni jaribu, maisha ni dhamana,
na maisha ni jukumu la muda mfupi. Mawazo haya ni ya msingi kwa maisha yanayoongozwa na malengo.
Tutayatazama mawazo mawili katika sura hii na lile la tatu katika sura
inayofuata.
Maisha duniani ni Jaribu.
Kielelezo hiki cha maisha kinaonekana ktika hadithi ya Biblia yote. Wakati wote
Mungu huijaribu tabia ya watu, Imani yao, utii, upendo, ukamilifu na uaminifu
wao. Maneno kama majaribu, kusafisha, na kujaribu hupatikana mara 200 katika Biblia. Mungu alimjaribu Ibrahimu kwa
kumwambia amtoe sadaka mwanae Isaka. Mungu alimjaribu Yakobo alipopaswa kufanya
kazi miaka ya ziada ili kumpata Raheli kama mkewe.
Adamu
na Hawa walishindwa jaribio lao katika Bustani va Edeni, na Daudi alishindwa
majaribu yake kutoka kwa Mungu mara kadhaa. Lakini Biblia pia hutupa mifano mingi
ya watu walioshinda majaribu makubwa mfano Yusufu, Ruthu, Esta na Daniel.
Majaribu
hukuza tabia na kuiweka wazi, na maisha yote ni majaribu. Siku zote unajaribiwa.
Mungu siku zote anatazama unavyoenenda kwa watu, matatizo, mafanikio,
migongano, magonjwa, mambo ya kukatisha tamaa, hata hali ya hewa! Mungu
anaangalia hata matendo rahisi sana kama vile unapowafungulia mlango wengine,
unapookota kipande cha takataka, au unapoonyesha upole kwa karani au mhudumu.
Hatuyajui majaribu yote ambayo
Mungu anatupa lakini tunaweza kutabiri baadhi yake, kwa kuzingatia Biblia.
Utajaribiwa kwa mabadiliko makubwa, kucheleweshwa ahadi, matatizo magumu, sala
zisizojibiwa, lawama zisizostahili, na hata mikasa isiyo na sababu. Katika
maisha yangu nimetambua kwa Mungu anajaribu Imani yangu kupitia matatizo,
anajaribu tumaini langu kwa njia ya mali, na anajaribu upendo wangu kwa njia ya
watu.
Jaribu
la muhimu sana ni jinsi unavyotenda unapoacha kuhisi uwepo wa Mungu katika
maisha yako. Wakati mwingine Mungu hujiondoa kwa makusudi, na hatuoni uwepo
wake. Mfalme aitwaye Hezekia alipatwa na jaribu hili. Biblia inasema, “Mungu
alimwacha Hezekia ili kumjaribu na aweze kuona kile kilichokuwa ndani ya moyo
wake hasa.” 2 Mambo ya Nyakati 32:31 (NLT) Hezekia alikuwa amefaidi
ushirika wa karibu na Mungu, lakini kwa wakati wa muhimu sana Mungu alimwasha
peke yake ili ampime tabia yake, adhihirishe udhaifu wake, na amwandae kwa
majukumu Zaidi.
Ukielewa
kuwa maisha ni jaribu, unatambua kuwa hakuna kitu kidogo katika maisha yako.
Hata tukioa dogo sana lina maana kubwa katika kukuza tabia yako. Kila siku ni
siku ya muhimu, na kila dakika ni wasaa wa kukua kitabia, kuonyesha upendo, au
kumtegemea Mungu. Majaribu mengine hata huyatambui. Lakini yote yana matokeo ya
milele.
Habari
njema ni kwamba Mungu anakutaka ushinde mtihani huo wa maisha, kwa hiyo
haruhusu majaribu unayoyapata kuwa makubwa kuliko neema anayokupatia katika
kukabili majaribu hayo. Biblia inasema, “Mungu hutunza
abadi yako, na hatawaacha mjaribiwe kupita uwezo wenu wa kutahimili; mnapokuwa
katika majaribu, atawapa nguvu za kuvumilia na mlango wa kutokea.” 1 Wakorintho 10:13 (TEV)
Kila
unaposhinda jaribu, Mungu hutambua na kupanga kukupa tuzo la milele. Yakobo
anasema, “Heri wanaostahimili wanapojaribiwa. Wakishinda
jaribu hilo, watapokea taji ya uzima ambayo Mungu ameawaahidi wampendao.” Yakobo 1:12 (GWT)
Maisha duniani ni dhamana. Huu
ni mfano wa pili wa kibiblia kuhusu maisha. Muda wetu duniani na nguvu zetu,
akili, nafsi, mahusiano, na mali zetu zote ni zawadi toka kwa Mungu ambazo
ametukabidhi tuvitunze na kuvitumia vizuri. Sisi ni mawakili wa yale Mungu anasema,
“Ulimwengu na vyote vilivyomo ni mali ya BWANA;
dunia na wote waishio humo ni mali yake.”
Zaburi 24:1 (TEV)
Hakika
hatumiliki
chochote kwa wakati wetu mfupi wa kuishi duniani. Mungu hutukopesha dunia tunapoishi hapa. Ilikuwa mali ya Mungu kabla hujaja, na
Mungu atamkopesha mtu mwingine ukifa. Unaifurahia kwa muda mfupi tu.
Mungu
alipowaumba Adamu na Hawa, aliwakabidhi uangalizi wa uumbaji wake na akawaweka
kuwa wadhamini wa uumbaji wamali yake. Biblia inasema, “Mungu
aliwabariki akasema, ‘mkawe na watoto wengi,
iliwazaliwa wenu waishi duniani kote na kuitawala. Nawaweka kuwa waangalizi.’”
Mwanzo 1:28 (TEV)
Kazi
ya kwanza ambayo Mungu aliwapa wanadamu ni kuangalia na kutunza “vitu” vya
Mungu duniani. Wajibu huu haujaondolewa kamwe. Ni sehemu ya malengo yetu leo.
Kila kitu tunachokifurahia yapasa tukione kama dhamana ambayo Mungu ameiweka
mikononi mwetu. Biblia inasema, “Mna kitu gani ambacho Mungu hakuwapa”
Na iwapo kila mlicho nacho kinatoka kwa Mungu kwa nini basi mjivune kama vile
mmefanikiwa kwa nguvu zenu wenyewe?”
1 Wakorintho 4:7b (NLT)
Miaka
mingi iliyopita, jamaa moja walituruhusu kutumia nyumba yao nzuri mbele ya
pwani kule Hawaii kwa ajili ya mapumziko. Ilikuwa ni jambo ambalo tusingemudu
gharama zake, lakini tulifurahia kweli. Tuliambiwa, “Itumieni kama vile ni yenu,”
Hivyo ndivyo tulivyofanya! Tuliogelea katika bwawa, tukala chakula kilichokuwa
jokofuni, tukatumia vitambaa vya kuogea na vyombo, n ahata tukarukia vitandani
kucheza! Lakini tulifahamu wazi kwamba nyumba hii haikuwa yetu, hivyo tulikuwa
waangalifu kwa kila kitu. Tulifaidi kutumia nyumba ambayo haikuwa yetu.
Mila
zetu husema, “Kama si mali yako, huhitaji kuitunza.” Lakini Wakristo wanaishi
kwa maadili ya kiwango cha juu: “Kwa kuwa ni mali ya Mungu, ni lazima niitunze kwa uangalifu wa hali ya juu.” Biblia
inasema, “Wale ambao wameaminiwa kwa kitu cha thamani
waonyeshe kweli wanastahili heshima hiyo’”
yo.”
1 Korintho 4:2 (NCV) Yesu mara kwa mara alionyesha kuwa maisha ni dhamana na
alitoa mifano mingi kufundisha wajibu huu kwa Mungu. Katika ule mfano wa
talanta, Mathayo 25:14-19 nfanya biashara aliposafiri. Aliporudi alitathmini
kazi ya kila mtumishi na kumpa ujira sawasawa na kazi yake. Yule tajiri
anasema, “Vema, mtumishi mwema na mwaminifu! Umekuwa
mwaminifu katika vichache; nitakuweka uwe mwangalizi wa vitu vingi. Njoo
ushiriki hatika furaha ya bwana wako.”
Mathayo 25:21 (NIV)
Mwisho
wa maisha yako duniani utatathminiwa kulingana na ulivyotumia yale Mungu
aliyokukabidhi. Hii ina maana mambo yote unayoyafanya, hata yale mambo madogo
madogo ya kila siku, yana matokeo ya umilele. Kama utaona mambo yote kuwa
dhamana, Mungu anaahidi zawadi tatu katika maisha ya milele. Kwanza, utapewa uthibitisho. Atasema, “kazi nzuri! Umefanya vema!” Kisha utapandishwa daraja na utapewa jukumu kubwa katika umilele: “Nitakuweka uwe
mwangalizi wa vitu vingi.” Na mwisho utakaribishwa katika karamu: “Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako.”
Watu
wengi wanashindwa kufahamu kuwa pesa ni jaribu na dhamana toka kwa Mungu. Mungu
anatumia pesa kutufundisha kumtegemea; na kwa watu wengi fedha ni jaribu kuu
kupita yote. Mungu anaagalia jinsi tunavyotumia pesa ili kupima jinsi gani
tunaaminika. Biblia inasema, “Kama hamuaminiki kwa utajiri wa
duniani, je, ni nani atakayewaamini kwa utajiri wa kweli mbinguni?” Luka 16: 11 (NLT)
Huu
ni ukweli wa muhimu sana. Mungu anasema kuna uhusiano wa moja kwa moja baina ya
ninavyotumia pesa zangu na hali yangu ya kiroho. Jinsi ninavyotawala pesa zangu
(“utajiri wa dunia”)
ni kigezo cha kiasi gani Mungu anaweza kunikabidhi Baraka za rohoni, (“utajiri
wa kweli”). Hebu Nikuulize: je, namna unavyotumia fedha zako yaweza
kumzuia Mungu kufanya mambo zaidi maishani mwako? Je, unaweza kuaminiwa katika
utajiri wa kirobo?
Yesu
alisema, “kutoka kila mtu aliyepewa vingi, vitatakiwa
vingi; na kutoka aliyekabidhiwa Zaidi; ataulizwa vingi Zaidi.” Luka 12:48b (NIV) Maisha ni jaribu na dhamana. Na kadiri Mungu
anavyokupa Zaidi, ndivyo anakutaka uwajibike Zaidi.
Siku ya Sita:
Maisha ni Jukumu La Muda Mfupi
Bwana nikumbushe
jinsi muda wangu wa kukaa hapa duniani ulivyo mfupi. Nikumbushe kuwa siku zangu
zimehesabiwa, na kwamba maisha yangu yanatoweka kwa haraka.
Zaburi
39:4 (NLT)
Niko duniani kwa
muda mfupi tu.
Zaburi
119:19 (TEV)
Maisha
duniani ni jukumu la muda mfupi.
Bfiblia
imejaa mifano ambayo hutufundisha kuhusu maisha yetu duniani yalivyo mafupi na
yasiyodumu. Maisha yanaelezwa kama ukungu, mkimbiaji, pumzi, na mvuke. Biblia
husema, “Kwa kuwa tulizaliwa jana tu … Maisha yetu
duniani yanapita kama kivuli.” Ayubu 8:9 (NLT)
Ili
kutumia vizuri maisha yako hupaswi kusahau ukweli wa aina mbili: Kwanza,
yakilinganishwa na umilele, maisha ni mafupi sana. Pili, dunia ni makazi ya
muda tu. Huwezi kukaa hapa kwa muda mrefu, hivyo usijishikamanishe sana nayo.
Mwombe Mungu akusaidie kuyaona maisha ya duniani kama anavyoyaona yeye
mwenyewe. Daudi aliomba, “Bwana nisaidie nitambue jinsi muda
wangu wa kukaa duniani utakavyokuwa mfupi. Nisaidie kujua kwamba niko hapa kwa
muda tu.” Zaburi 39:4 (LB)
Biblia
imerudia sana kulinganisha maisha hapa duniani kama kuishi nchi ya ugenini.
Haya si makazi yako ya kudumu, au hatima yako ya mwisho. Unapita tu, unatembea
tu duniani. Biblia inatumia maneno kama vile mgeni, msafiri, na mtoka nchi ya mbali, katika kueleza ufupi wa maisha yetu duniani. Daudi alisema, “Mimi
ni mgeni hapa duniani.” Zaburi 119:19 (NLT) na Petro
akasema, “Kama mnamwita Mungu Baba yenu, muishi kama
wakazi wa muda mfupi hapa duniani.” 1 Petro
1:17 (GWT)
Kule
California, ambako runaishi, watu wengi wamehamia toka schemu nyingine za dunia
ili kupata kazi hapa, lakini wanatunza uraia wao wa nchi zao. Hapa wanatakiwa
kuwa na kitambulisho cha mgeni (kiitwacho “kadi ya kijani”), ambacho huwaruhusu
kufanya kazi hapa hata kama si raia wa hapa. Wakristo lazima wachukue kadi za
kijani za kiroho ili kutambulisha kwamba uraia wetu uko mbinguni. Mungu anasema
watoto wake wanapaswa kufikiri tofauti na wasioamini kuhusu maisha. “Wao
wanachokifikiri ni maisha haya duniani. Lakini sisi ni raia wa mbinguni, ambako
Bwana Yesu Kristo anaishi.” Wafilipi 3:19-20 (NLT) Waamini
wa kweli wanafahamu wazi kwamba kuna mambo mengi ya maisha kuliko hii miaka michache
tunayoishi hapa duniani.
Kitambulisho chako kiko katika
umilele, na nchi yako ni mbinguni. Unapofahamu ukweli huu, utaacha kuwa na
wasiwasi wa “kupata kila kitu “hapa duniani. Mungu yuko wazi kabisa kuhusu
habari za kuishi kwa ajili ya hapa
na sasa
tu huku ukijifananisha na watu wa dunia hii katika kipaumbele na mtindo wa
maisha. Tunapochezacheza na majaribu ya dunia hii, Mungu anaita hali hivyo
uzinzi wa kiroho. Biblia inasema, “Mnajidanganya mbele za Mungu. Iwapa mnachotaka
ni mambo yenu tu, kuchezacheza na ulimwengu kwa kila nafasi mnayopata mwisho
wenu ni kuwa maadui wa Mungu na njia yake.”
Yokobo 4:4 (Msg)
Hebu
fikiri kama ungeombwa na nchi yako uwe balozi katika taifa adui yenu. Labda
ungelazimika kujifunza lugha mpya na mila na desturi zao uweze kukubalika na
kukamilisha huduma yako. Kama balozi hungeweza kuitenga na adui zako. Ili
kukamilisha kazi yako, ungelazimika kuwa na mawasiliano na uhusiano nao.
Lakini
fikiri kama ungefurahia maisha katika nchi hii ya ugeni, ukaipenda kuliko nchi yako.
Uaminifu na kujitoa kwako bingeweza kubadilika. Wajibu wako kama balozi
ungeingia dosari. Badala ya kuiwakilisha nchi yako, ungeanza kufanya mambo kama
adui. Ungekuwa msaliti.
Biblia inasema, “Sisi ni mabalozi
wa Kristo.” 2 Korintho 5:20 (NLT) Cha kusikitisha, Wakristo wengi wamemsaliti
mfalme wao na ufalme wake. Katika hali ya upumbavu wameamua kwamba, kwa sababu
wanaishi duniani, basi hapa ndiko nyumbani kwao. Biblia iko wazi: “Rafiki,
hii dunia si nyumbani kwenu, hivyo msidanganywe na dunia. Msifuate tamaa zenu
na kuleta hasara kwa nafsi zenu.” 1 petro
2:11 (Msg) Mungu anatuonya tusijishikamanishe sana na vitu vinavyotuzunguka kwa
kuwa si vya kudumu. Tunaambiwa, “Wale wanaowasiliana mara kwa mara na vitu
vya dunia hii wavitumie vizuri bila kujishikamanisha navyo, kwa kuwa ulimwengu
huu na vyote vilivyomo vitapita.” 1
Wakorintho 7:31 (NLT)
Ikilinganishwa
na karne zingine, maisha yamekuwa si mepesi kwa sehemu kubwa ya ulimwengu wa
magharibi. Wakati wote tunafurahishwa na tunapewa huduma. Kwa mivuto ya hali ya
juu, na vyombo vy mawasiliano vyenye kutia upofu, na mambo mengi ya anasa
yaliyopo siku hizi, ni rahisi kusahau kwamba maisha si kutafuta raha tu. Ni
pale tu tunapokumbuka kuwa maisha ni majaribu, dhamana, na jukumu la muda mfupi
ndipo mvuto wa mambo ya anasa utakapokosa nguvu maishani mwetu. Tunajiandaa kwa
jambo jingine ambalo ni bora Zaidi. “Mambo tunayoyaona
sasa yapo leo, na kutoweka kesho. Lakini mambo tusiyoyaona sasa yatadumu milele.” 2 Wakorintho 4:18b (Msg)
Ukweli
kwamba dunia si makazi yetu ya kudumu huelezea kwa nini, kama wafuasi wa
Kristo, tunapatwa na magumu, huzuni, na kukataliwa duniani. (Yahana 16:33;
16:20; 15:18-19) Ukweli huu pia hueleza kwa nini baadhi ya ahadi za Mungu
huonekana kutotimizwa, baadhi ya sala hazijajibiwa, na baadhi ya mazingira
kuonekana kutokuwa ya haki. Huu si mwisho wa mambo.
Ili kutufanya tusijifungamanishe
na ulimwengu sana, Mungu hurubusu tusikie hali fulani ya kutokuridhirisha na
kutosheka katika maisha – hitaji ambalo haliwezi kutoshelezwa kamwe hapa
duniani. Hatuna furaha kabisa hapa kwa sababu hatutakiwi! Dunia si makazi yetu
ya milele, tuliumbwa kwa ajili ya kitu bora zaidi.
Samaki
hawezi kuwa na furaha kuishi nchi kavu, kwa sababu ameumbwa kwa ajili ya kuishi
majini. Tai asingefurahi kama hangeruhusiwa kupaa angani. Hatuwezi kamwe
kujisikia kutosheka kabisa hapa duniani, kwa sababu uliumbwa kwa ajili ya mambo
mengine Zaidi. Utakuwa na vipindi vya furaha hapa, lakini hakuna cha kufanana
na kile Mungu amepanga kwa ajili yako.
Kwa
kutambua kwamba maisha duniani ni jukumu la muda mfupi tu ni lazima kubadili
kabisa mambo unayoyaona ya muhimu maishani mwako. Mambo ya milele, yasiyo ya
muda mfupi, yapasa yawe vigezo vya maamuzi yako. Kama C.S. Lewis alivyosema, “Kila
kisicho cha milele hakifai milele.” Biblia inasema, “Tunakaza
macho yetu si kwa kile kinachoonekana, lakini kwa kisichoonekana. Kwa kuwa kila
kinachoonekana ni cha muda, na kisichoonekana ni cha milele.” 2 Korintho 4:18 (NIV)
Ni
kosa kubwa kudhani kuwa mpango wa Mungu kwa ajili ya maisha yako ni mafanikio
ya mali au mafanikio ya siku hizi, kama ulimwengu unavyoyaona. Maisha tele
hayana uhusiano na mali tele, na uaminifu kwa Mungu hautuhakikishii kuwa na
mafanikio ya kazi au huduma, usitazamie taji zisizodumu. 1 Petro 2:11 (GWT)
Paulo
alikuwa mwaminifu lakini alijikuta gerezani. Yohana Mbatizaji alikuwa mwaminifu
lakini alikatwa kichwa. Mamilioni ya watu waaminifu wameuawa, wamepoteza kila
walichokuwa nacho, au maisha yao yamekoma wakiwa hawana kitu. Lakini
mwisho wa maisha haya si mwisho!
Katika
macho ya Mungu, mashujaa wa Imani sio wale waliopata mali, wenye mafanikio na
nguvu katika maisha haya, lakini ni wale wanaoyaona maisha kama jukumu la muda
mfupi na kutumika kwa uaminifu, wakitumaini kupokea thawabu yao katika umilele.
Biblia husema kuhusu jambo hili, “Watu hawa wote wakafa katika Imani.
Hawakupata vitu vile Mungu alivyowaahidi watu wake, lakini waliviona kwa mbali
vikija wakashangilia. Walisema walikuwa kama wangeni na wapitaji hapa duniani …
Walisubiri nchi bora- nchi ya mbinguni. Hivyo Mungu haoni hayakuitwa Mungu wao,
kwa sababu amewatayarishia mji.” Waebrania
11:13, 16 (NCV) Maisha yako duniani si historia timilifu ya maisha yako.
Unahitaji kusubiri mpaka mbinguni kwa ajili ya utimilifu wa maisha yako yote.
Unahitaji Imani kuishi duniani kama mgeni.
Hadithi
ya zamani inayosemwa mara nyingi ya mmishonari aliyekuwa anamaliza kazi yake na
kurudi nyumbani Marekani alikuwa katika meli moja na Rais wa Marekani. Kundi
kubwa la watu lililokuwa linashangilia, bendi ya jeshi, zuria jekundu, bendera
na watangazaji walimkaribisha Rais nyumbani, lakini mmishonari alitoka polepole
katika meli na kwenda zake bila Mungu. Kisha Mungu kwa upole alimkumbusha, “Lakini
mwanangu, hujafika nyumbani bado.”
Hutakuwa
mbinguni nukta mbili kabla hujapiga kelele ukisema, “Kwa nini niliweka umuhimu
mkubwa kwa vitu ambavyo vilikuwa vya muda mfupi sana? Nilikuwa nafikiri nini? Kwa nini nilipoteza muda mwingi sana,
nguvu nyingi, na kujali sana vitu ambavyo si vya kudumu?”
Maisha
yanapokuwa magumu, unapokuwa umelemewa na mashaka, au unapojiuliza kama
kumwishia Kristo kweli kunahitajika, kumbuka kuwa hujafika nyumbani bado.
Wakati wa kufa hutatoka nyumbani bali utakwenda nyumbani.
Siku ya Saba:
Sababu Ya Kila Kitu
Kila
kitu kimetoka kwa Mungu tu.
Ila
kitu huishi kwa nguvu zake,
na
kila kitu kipo kwa ajili ya utukufu wake.
Warumi
11:36 (LB)
BWANA
amefanya kila kitu kwa ajili ya utukufu wake.
Mithali
16:4 (NLTo)
Kila
kitu ni kwa ajili yake.
Lengo
la ulimwengu mzima ni kuonyesha utukufu wa Mungu. Ni sababu ya kila kitu
kilichopo, hii ni pamoja na wewe. Mungu aliumba vyote kwa ajili ya utukufu
wake. Bila utukufu wa Mungu, kusingekuwepo chochote.
Utukufu
wa Mungu ni nini? Ni Mungu alivyo. Ni kiini cha hali yake, uzito wa umuhimu
wake,mng’ao wa ukuu wake, udhihirisho wa nguvu zake, na hali ya uwepo wake.
Utukufu wa Mungu ni udhihirisho wa wema wake na sifa zake zote za milele.
Utukufu
wa Mungu uko wapi? Tazama kuzunguka pande zote. Kila alichokiumba
kinadhihirisha utukufu wake kwa namna fulani. Tunauona kila
mahali, kuanzia viumbe vidogo vyenye uhai hadi mfumo mkubwa wa nyota, tangu
kutua kwa jua na nyota hadi tufani na majira. Uumbaji unafunua utukufu wa
muumba wetu. Kwa uumbaji wa asili tunajifunza kuwa Mungu ni mwenye nguvu,
kwamba anafurahia vitu viwe tofauti tofauti, anapenda uzuri, ni wa mipango, na
ana hekima na ubunifu. Biblia inasema, “Mbingu zinatangaza
utukufu wa Mungu.” Zaburi 19:1 (NIV)
Katika
historia yote, Mungu amedhihirisha utukufu wake kwa watu katika mazingira mbali
mbali. Alijjifunua kwanza katika Bustani ya Edeni, kisha kwa Musa,
na halafu katika Hema ya Kukutania
na hekaluni, na kisha kwa njia ya Yesu, na sasa kupitia Kanisa. (Mwanzo 3:8;
Kutoka 33:18-23; 40:33-38; 1 Wafalme 7:51; 8:10-13; Yohana 1:14; Waefeso
2:21-22; 2 Wakorintho 4:6-7) Utukufu wake ulionekana kama moto ulao, wingu,
ngurumo, moshi, namwanga mkali. (Kutoka 24:17; 40:33-38, Zaburi 29:1; Isaya
6:3-4; 60:1; Luka 2:9) Mbinguni, utukufu wa Mungu hutoa mwanga wote
unaohitajika. Biblia inasema, “Ule mji hauhitaji jua wala mwezi ili
kutoa mwanga kwa kuwa utukufu wa Mungu huuangazia.”
Ufunuo 21:23 (NIV)
Utukufu
wa Mungu unaonekana vizuri Zaidi katika Yesu Kristo. Yeye, nuru ya ulimwengu,
hudhihirisha hali ya Mungu. Kwa sababu ya Yesu, hatuko tena gizani kuhusu jinsi
Mungu alivyo. Biblia inasema, “Mwana ni mng’ao wa utukufu wa Mungu.” Waebrania 1:3 (NIV), 2 Korintho 4:6 (LB) Yesu alikuja duniani
ili tumfahamu Mungu vyema. “Neno akawa mwanadamu na akaishi
katikati yetu. Tuliuona utukufu wake … utukufu uliojaa neema na kweli.” Yohan 1:14 (GWT)
Utukufu
wa asili wa Mungu ni ule alionao kwa sababu yeye ni Mungu. Ni hali yake ya
asili. Hatuwezi kuongeza chochote Kwenye utukufu huu, kama ambavyo haiwezekani
kwetu kulifanya jua ling’ae Zaidi. Lakini tumeamriwa kuutambua utukufu wa
Mungu, kuuheshimu utukufu wake, kuutangaza, kuusifu, kuuonyesha, na kuishi kwa
utukufu wake. (Mambo ya Nyakati 16:24; Zaburi 29:1; 66:2; 96:7; 2 Wakorintho
3;18) Kwa nini? Kwa sababu Mungu anastahili. Tunawiwa kila namna ya heshima
tunayoweza kumpa. Kwa kuwa Mungu aliumba vitu vyote, anastahili utukufu wote.
Biblia inasema, “Unastahili, Ee Bwana Mungu wetu,
kupokea utukufu, heshima na nguvu. Kwa kuwa uliumba kila kitu.” Ufunuo 4:11a (NLT)
Katika
ulimwengu mzima, ni viumbe viwili tu, katika viumbe vyake vyote, waliishashindwa
kuleta utukufu kwake: malaika walioanguka (mapepo) na sisi (Watu).
Dhambi
yote, katika mzizi wake, ni kushindwa kumpa Mungu utukufu. Ni kupenda kitu
kingine Zaidi ya Mungu. Kukataa kuleta utukufu kwa Mungu ni uasi wenye
majivuno, na ni dhambi iliyomsababisha Shetani kuanguka na kuanguka kwetu pia.
Kwa njia mbalimbali sisi sote tumeishi kwa ajili ya utukufu wetu, siyo utukufu
wa Mungu. Biblia inasema, “Wote wefanya dhambi na kupungukiwa na
utukufu wa Mungu.” Warumi 3:23 (NIV)
Hakuna
hata mmoja wetu ambaye amempa Mungu utukufu wote anaostahili katika maisha
yetu. Hii ndiyo dhambi mbaya na kosa kubwa kufanya. Kwa upande mwingine, kuishi
kwa ajili ya Mungu ni jambo kubwa tunaloweza kufanya katika maisha yetu Mungu
anasema, “Wao ni watu wangu, na niliwaumba waniletee utukufu,” Isaya 43:7 (TEV)
kwa hiyo ni lazima liwe lengo letu kuu maishani.
JE, NAWEZAJE KULETA UTUKUFU KWA MUNGU
Yesu alimwambia Baba yake, “Nimeleta
utukufu kwa jina lako hapa duniani kwa kufanya kila kitu ulichoniambia nifanye.” Yohana 17:4 (NLT) Yesu alimheshimu Mungu kwa kutimiza lengo
lake hapa duniani.
Tunamheshimu
Mungu kwa njia hiyo hiyo. Kila kitu katika uumbaji kinapotimiza lengo lake,
huleta utukufu wa Mungu. Ndege huleta utukufu kwa Mungu kwa kuruka juu, kwa
kuimba, kutengeneza viota, na kufanya kazi nyingine ambazo Mungu aliwapangia.
Hata sisimizi wadogo huleta utukufu kwa Mungu pale wanapotimiza lengo la
kuumbwa kwao. Mungu aliumba sisimizi ili wawe sisimizi, na alikuumba wewe uwe
wewe. Mtakatifu Irenaeus alisema, “Utukufu wa Mungu ni binadamu mkamilifu aliye
hai!”
Kuna
njia nyingi za kuleta utukufu kwa Mungu, lakini zaweza kuwekwa katika muhtasari
wa malengo matano ya Mungu kwa ajili ya maisha yako. Tunatumia sehemu iliyobaki
ya kitabu hiki kuyaangalia kwa kina, lakini hapa tunatoa kwa ufupi:
Tunamletea Mungu utukufu kwa kumwabudu. Kuabudu ni wajibu wetu wa kwanza kwa Mungu. Tunamwabudu kwa
kumfurahia C. W. Lewis alisema, “Katika kutuamuru tumwabudu, Mungu anatualika
tumfurahie,” Mungu anapenda kuabudu kwetu kuchochewe na upendo, shukrani, na
kufurahia, na siyo wajibu.
John
Piper anasema, Mungu anatukuzwa Zaidi ndani yetu tunapokuwa tumetoshelezwa sana
katika Yeye.”
Kuabudu
ni Zaidi ya kusifu, kuimba na kumwomba Mungu. Kuabudu ni mtindo wa maisha wa kumfurahia Mungu, kumpenda,
na kujitoa
tutumiwe kwa ajili ya malengo yake. Unapotumia maisha yako kwa ajili ya utukufu
wa Mungu, Kila unachokifanya chaweza kuwa tendo la ibada. Biblia inasema, “Tumia
mwili wote kama chombo cha kufanya yaliyo sahihi kwa ajili ya utukufu wa Mungu.” Warumi 6:13b (NLT)
Tunaleta utukufu kwa Mungu kwa kuwapenda waamini wengine. Ulipozaliwa mara ya pili, ulikuwa sehemu ya jamii ya Mungu.
Kumfuata Kristo siyo tu kuamini, ni pamoja na kuwa sehemu ya jamii ya Mungu, na
kuipenda. Yohana aliandika, “Upendo wetu kwa ndugu unathibitisha
kwamba tumetoka mautini na kwenda uzimani.”
1 Yohana 3:14 (CEB) Paulo alisema, “Pokeaneni kila mmoja na mwenzake kama
vile Kristo alivyowapokea; ndipo Mungu atatukuzwa.”
Warumi 15:7 (NLT)
Ni
wajibu wako kujifunza kupenda kama Mungu apendavyo, kwa sababu Mungu ni upendo,
na hii humletea heshima. Yesu alisema, “Kama
nilivyowapenda, pendaneni vivyo hiyo. Kwa njia hii watu wote watajua kwamba
ninyi ni wanafunzi wangu, kama mkipendana.”
Yohana 13:34-35 (NIV)
Tunaleta utukufu kwa Mungu kwa kuwa kama Kristo. Mara tunapozaliwa katika jamii ya Mungu, anatutaka tukue kiroho.
Hiyo inaonekanaje? Kukua kiroho ni kuwa kama Kristo katika namna tunavyofikiri,
tunavyohisi, na kutenda. Kadiri unavyokua katika tabia ya Kristo, ndivyo
unamletea utukufu Zaidi. Biblia inasema, “Kadiri Roho wa
Bwana anavyotenda kazi ndani yetu, tufanane naye zaidi na Zaidi na tunaonyesha
utukufu wake Zaidi.” 2 Wakorintho 3:18 (NLT)
Mungu
alikupa maisha mapya na asili mpya ulipompokea Kristo. Sasa, kwa maisha yako
yaliyobaki hapa duniani, Mungu anapenda kuendeleza kazi ya kukubadili tabia.
Biblia inasema, “Mjazwe siku zote na tunda la wokovu
wenu – yale mambo mazuri yanayotolewa maishani mwenu na Yesu Kristo – Kwa kuwa
hili litaleta utukufu mwingi na sifa kwa Mungu.”
Wafilip 1:11 (NLT); Yohana 15:8 (GWT)
Tunaleta utukufu kwa Mungu kwa kuwatumikia wengine kwa vipawa
vyetu. Kila mmoja wetu alibuniwa kwa namna ya pekee na Mungu. Jinsi
ulivyosokotwa si bahati mbaya. Mungu hakukupa uwezo ulio nao kwa ajili ya
matumizi ya kichoyo. Ulipewa ili kuwafaidi wengine, kama vile wengine
walivyopewa uwezo mbalimbali ili kukufaidi wewe. Bibla inasema, “Mungu
amewapa karama kila mmoja wenu kutoka katika karama zake mbalimbali. Zitumieni
vizuri ili ukarimu wa Mungu ububujike kupitia ninyi … Je, umeitwa kusaidia
wengine? Fanya hivyo kwa nguvu zote unazojaliwa na Mungu. Kisha Mungu atapewa
utukufu.” 1 Petro 4:10-11 (NLT); 2 Wakorintho 8;19 (NLT)
Tunaleta utukufu kwa Mungu kwa kuwaelezea wengine habari zake. Mungu hapendi upendo wake na malengo yake yawe siri. Mara
tunapofahamu ukweli, anategemea tuwashirikishe wengine. Hii ni heshima kubwa –
kuwatambulisha wengine kwa Yesu, kuwasaidia wagundue lengo lao, na kuwaandaa
kwa ajili ya hatima yao ya millele. Biblia inasema, “Kadiri
neema ya Mungu inavyoleta watu wengi Zaidi kwa Kristo, … Mungu atapokea utukufu
Zaidi na Zaidi.” 2 Korintho 4:15
JE,
TUNAISHI KWA AJILI YA NINI?
Ili
kuishi maisha yako yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu unahitaji kubadili
vipaumbele vyako, ratiba yako, mahusiano yako, na kila kitu. Wakati mwingine
itamaanisha kuchagua njia ngumu badala ya ile nyepesi. Hata Yesu alihangaika na
jambo hili. Akijua alikuwa karibu kusulubiwa, alilia akisema, “Nafsi
yangu inahangaika; na nisemeje, ‘Baba uniokoe kutika saa hii’? Lakini kwa ajili
ya lengo hili nimefika saa hii. Baba, litukuze jina lako.” Yohana 12:27-28 (NASB)
Yesu
alisimama katika njia panda barabarani. Je, atatimiza lengo lake na kuleta
utukufu kwa Mungu, au atanyong’onyea na kuishi maisha ya raha yenye ubinafsi?
Unakabiliwa na uchaguzi wa aina hiyo. Je, utaishi kwa ajili ya malengo yako
mwenyewe, ya kujifurahisha, au utaishi maisha yako yaliyosalia kwa ajili ya
utukufu wa Mungu, ukijua kwamba ameahidi zawadi na milele? Biblia inasema, “Yeyote
anayeyashika maisha kama yalivyo huyaharibu maisha hayo. Lakini ukiyaacha, … utayapata
milele, ya kweli nay a milele.” Yohana 12:25 (Msg)
Ni
wakati wa kutengeneza jambo hili. Utaishi kwaajili ya nani – nafsi yako au
Mungu? Unaweza kusita au kushangaa kama utakuwa na nguvu za kuishi kwa ajili ya
Mungu. Usihofu. Mungu atakupa unachohitaji kama utafanya uchaguzi wa kuishi
kwaajili yake. Biblia inasema, “Kila kitu kinachoenda katika maisha ya
kumpendeza Mungu kimepewa kwetu kimiujiza kwa kumjua binafsi na kwa ukaribu,
yeye aliyetukaribisha kwa Mungu.” 2Petro
1:3 (Msg)
Sasa
hivi, Mungu anakukaribisha uishi kwa ajili ya utukufu wake kwa kutimiza kusudi
alilokuumbia. Ndiyo njia ya pekee ya kweli kuishi. Vingine ni kuwepo tu. Maisha
ya kweli huanza kwa kujiweka wakfu kikamilifu kwa Yesu Kristo. Kama huna hakika
umefanya hivi unachohitaji kufanya ni kupokea na kuamini. Biblia inaahidi, “Kwa
wote waliompokea, wale walioliamini jina lake, aliwapa haki ya kuwa watoto wa
Mungu.” Yohana 1:12 (NIV) Je, unaweza kupokea zawadi ya Mungu?
Kwanza, uamini. Amini Mungu anakupenda na alikuumba kwa lengo au
malengo yake. Amini wewe si bahati mbaya. Amini uliumbwa kuishi milele. Amini
Mungu amekuchagua uwe na uhusiano na Yesu, aliyekufia msalabani. Amini kwamba
haijalishi umeshafanya nini, Mungu anapenda kukusamehe.
Pili,
pokea. Mpokee Yesu maishani mwako kama Bwana na mwokozi wako. Pokea msamaha wa
dhambi zako. Pokea Roho wake Mtakatifu, ambaye atakupa nguvu za kutimiza lengo
la maisha yako. Biblia inasema, “Yeyote ampokeaye na kumwamini Mwana hupata
yote, uzima mtimilifu na wa milele.” Yohana
3:36 (Msg) Popote unaposoma maneno haya nakualika uinamishe kichwa chako, na
taratibu Sali sala hii itakayobadili umilele wako: “Yesu nakuamini, na
ninakupokea.” Endelea.
Kama
kweli ulimaanisha sala hiyo kutoka moyoni, hongera! Karibu katika jamii ya
Mungu! Sasa uko tayari kugundua na kuanza kuishi malengo ya Mungu kwa ajili ya
maisha yako. Nakushauri umweleze mtu mwingine juu ya jambo hili. Utahitaji
msaada. Kama utanitumia barua pepe (Nyongeza ya 2), nitakutumia kijitabu kidogo
nilichoandika kiitwacho Hatua za Mwanzo Katika Kukua Kiroho.
Lengo La I
ULIKUSUDIWA KWA
AJILI YA FURAHA YA MUNGU
Kwa kuwa Mungu amewapanda kama mti
imara wenye
kuneemeka kwa ajili ya utukufu wake
Isaya 61: 3 (LB)
Siku ya Nane:
Ulikusudiwa Kwa Ajili Ya Furaha Ya Mungu
Uliumba Kila kitu, na ni kwa furaha yako
kwanba vipo na viliumbwa.
Ufunuo 4:11 (NLT)
Bwana huwafurahia watu wake
Zaburi 149:4a (TEV)
Ulikusudiwa
kwa furaha ya Mungu.
Wakati
ulipozaliwa duniani, Mungu alikuwepo hapa kama shahidi asiyeonekana, akifurahia
kuzaliwa kwako. Alikutaka uwe hai, na kufika kwako kulimpa furaha kubwa. Mungu
hakuhitaji kukuumba, lakini alichagua kukuumba kwa ajili ya furaha yake
mwenyewe. Upo kwa sababu ya faida yake, utukufu wake, na furaha yake. Kuleta
furaha kwa Mungu na kumburudisha, ni lengo la kwanza kwa maisha yako.
Unapoelewa kikamilifu ukweli huu hutakuwa na tatizo kamwe la kujisikia hufai.
Ni uthibitisho wa uthamani wako. Kama wewe ni wa muhimu hivyo kwa Mungu, na
anakuthamini kiasi cha kukutunza ukae naye milele, ni uthamani gani mkubwa
ungekuwa nao? Wewe ni mtoto wa Mungu, na unaleta furaha kwa Mungu kuliko chochote
kingine alichokiumba. Biblia inasema, “kwa sababu ya
upendo wake Mungu ameamua kwamba kupitia Yesu Kristo atatufanya watoto wake – hii
ilikuwa furaha yake na kusudi lake.” Waefeso 1:5 (TEV)
Moja ya zawadi kubwa
Mungu aliyokupatia ni uwezo wa kufurahia.
Alikuunganisha
kwa milango mitano ya fahamu na hisia ili uweze kupata furaha hiyo. Anapenda
ufurahie maisha, siyo tu kuyavumilia. Sababu ya wewe kuweza kufurahia ni kwamba
Mungu alikuumba kwa mfano wake.
Mara
nyingi tunasahau kwamba Mungu ana hisia pia. Huhisi mambo kwa kina. Biblia
inatuambia kwamba Mungu huhuzunika, hupata wevu na hasira, na husikia huruma,
sikitiko, pia furaha, shangwe, na utoshelevu. Mungu hupenda, kufurahia, hupata
burudiko, hushangilia, na hata kucheka! Mwanzo 6:6; Kutoka 20:5; Kumbukumbu
32:36; Waamuzi 2:20; 1 Wafalme 10:9; 1 Mambo ya Nyakati 16:27; Zaburi 2:4; 5:5;
18:19; 35:27; 37:23; 103:13; 104:31; Ezekiel 5:13; 1 Yohana 4:16.
Kuleta furaha kwa Mungu huitwa “kuabudu.” Biblia inasema, “Mungu anapenezwa na wale tu
wanaomwabudu na kutumaini pendo lake.” Zaburi
147:11 (CEV)
Chochote
ufanyacho kinacholeta furaha kwa Mungu ni tendo la ibada. Kama almasi, kuabudu
kuna nyuso nyingi, lakini katika sehemu hii tutaangalia mambo ya msingi kuhusu
kuabudu.
Wataalamu
wa mambo ya wanadamu na mila zao wamegundua kwamba kuabudu ni jambo lililo
ndani ya wanadamu wote, Mungu amelifunga ndani ya utu wetu wa ndani – hitaji
lililojengwa ndani yetu kutuunganisha na Mungu.Kuabudu ni hali ya asili yetu kama
vile kula na kupumua. Tukishindwa kuabudu, mara nyingi tunatafuta njia mbadala,
hata ikibidi sisi wenyewe. Sababu ya Mungu kutuumba na hamu hii ni kwamba
anapenda wamwabuduo! Yesu alisema, “Baba anatafuta waabuduo.” Isaya 29:13 (NIV)
Kutegemeana na mazingira ya nyuma
ya kidini, unaweza kuhitaji kupanua ufahamu wako kuhusu “kuabudu.” Unaweza
kufikiri ibada za kanisani zenye nyimbo, sala, na kusikiliza mahubiri. Au
unaweza kufikiri desturi mbalimbali, mishumaa, na meza ya Bwana. Au unaweza
kufikiri uponyaji, miujiza, na hali ya kuwa katika msisimko wa kiroho. Kuabudu
kunaweza kuhusisha mambo yote haya, lakini kubudu ni zaidi sana kuliko mambo
haya. Kuabudu ni maisha.
Kuabudu ni Zaidi sana kuliko
kuimba. Kwa watu wengi, kuabudu ni sawa na uimbaji. Wanasema, “Kanisani
kwetu tunaabudu kwanza, kisha mafundisho. “ Huku ni kutokujua ukubwa. Kila
tendo la huduma ya kanisa ni ibada: sala, kusoma maandiko, kuimba, toba,
ukimya, kutulia, kusikiliza mahubiri, kuandika mahubiri, sadaka, ubatizo, meza
ya Bwana, ahadi mbalimbali, na hata kuwasalimu waabuduo wengine.
Kwa
hakika, kuabudu hutangulia uimbaji. Adamu aliabudu katika Bustani ya Edeni,
lakini uimbaji haujatajwa mpaka Mwanzo 4:21 kwa kuzaliwa kwa Yubali. Kama
kuabudu kungekua uimbaji tu, basi wale wote wasio na kipawa cha kuimba
wasingeabudu. Kuabudu ni Zaidi sana kuliko uimbaji.
Kibaya
Zaidi, kuabudu mara nyingi kumefananishwa na mtindo fulani wa uimbaji: “Kwanza tuliimba utenzi, kisha wimbo wa sifa
na kuabudu.” Au “Napenda nyimbo za haraka za sifa lakini nafurahia Zaidi
nyimbo za pole pole za kuabudu.” Kwa matumizi haya, kama wimbo unaimbwa kwa
haraka au kwa sauti ya juu, au unatumia zana za shaba, basi unadhaniwa ni wa “sifa.”
Lakini ukiwa wa pole pole na wa taratibu wenye mguso wa karibu, labda
ukifuatana na gitaa, huo ni wa kuabudu. Hayo ni matumizi mabaya ya neno “kuabudu.”
Kuabudu
hakuhusiani na namna (mtindo) au sauti au mwendo wa wimbo. Mungu anapenda aina
zote za uimbaji kwa kuwa zote alizibuni yeye – za haraka na polepole, za juu na
za chini, za kale na mpya. Labda wewe huzipendi kabisa, lakini Mungu
anazipenda! Kama zinatolewa kwa ajili ya Mungu katika roho na kweli, ni tendo la kuabudu.
Wakristo
mara nyingi hawakubaliani kuhusu mtindo wa uimbaji unaotumiwa katika kuabudu,
wakitetea mtindo wanaoupendelea wao kuwa ndio wa kibiblia au unaomheshimu
Mungu. Lakini hakuna mtindo wa kibiblia! Hakuna nota za muziki katika Biblia;
wala siku hizi hatuna zana za uimbaji zilizotumika wakati wa Biblia.
Kusema
kweli, mtindo wa uimbaji unaoupenda Zaidi unasema sana kuhusu wewe – mazingira yako na hali ya utu wako – kuliko kuhusu Mungu. Aina
fulani ya uimbaji wa jamii fulani ya watu yaweza kusikika kama kelele kwa watu
wa jamii nyingine. Lakini Mungu anapenda aina mbalimbali na anazifurahia zote.
Hakuna kitu kama muziki wa “Kikristo,”
kuna mashairi tu ya Kikristo. Maneno ndiyo hufanya wimbo kuwa mtakatifu, siyo
sauti. Hakuna sauti za kiroho kama ningeimba wimbo bila maneno, huna jinsi ya kujua
kama ni wimbo wa “Kikristo”.
Kuabudu si kwa ajili ya faida yako. Kama
mchungaji, napokea ujumbe usemao “Nilipenda ibada ya leo. Nimepata mengi.” Huku
ni kutokuelewa tena maana ya neno kuabudu. Si kwa ajili yetu! Tunaabudu kwa
ajili ya faida ya Mungu. Tunapoabudu, lengo letu ni kuleta furaha kwa Mungu, si
kwetu wenyewe. Nia yetu ni kuleta utukufu na furaha kwa Muumba wetu.
Kama
ukisema, “sikupata chochote katika kuabudu leo” Uliabudu na sababu zisizo za
haki. Kuabudu sio kwako wewe. Ni kwa Mungu. Kwa kweli, Ibada za “Kuabudu”
kwingi pia huwa na aina za ushirika, mafundisho mema, na uinjilisti na pia kuna
faida za kuabudu, lakini hatuabudu kwa kujifurahisha wenyewe. Nia yetu ni
kuleta utukufu na raha kwa Muumba wetu.
Katika
Isaya 29 Mungu analalamika juu ya ibada ambayo ni nusu nusu na ya kinafiki.
Watu walikuwa wakitoa sala za ovyo ovyo, sifa zisizotoka moyoni, maneno matupu,
na mapokeo ya ibada yaliyotungwa na watu bila hata kufikiri maana yake. Moyo wa
Mungu hauguswi na desturi katika ibada, lakini kwa nia ya ndani na kwa moyo wote.
Biblia inasema, “Watu hawa huja karibu yangu kwa vinywa
vyao na huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Kuniabudu
kwao ni sheria zinazofundishwa na wanadamu tu.”
Zaburi 105:4 (TEV)
Kuabudu siyo sehemu ya maisha yako tu; ni maisha yako. Kuabudu si tu huduma
za kanisani. Tunaagizwa “kumwabudu kila wakati.” Zaburi 113:3 (LB) na “kumsifu tangu maawio
hadi machweo.” Zaburi 119:147; 5:3; 63:6;
119:62 Katika Biblia watu walimtukuza Mungu kazini, nyumbani, vitani, gerezani,
hata vitandani. Sifa iwe ni kazi yako ya kwanza unapofumbua macho asuhuhi na
iwe kazi unapofumba macho usiku. Zaburi 34:1 (GWT) Daudi alisema, “Nitamshukuru
Bwana wakati wote. Kinywa change kitamtukuza daima.”
1 Wakorintho 10:31 (NIV)
Kila
shughuli yaweza kugeuzwa na kuwa tendo la ibada unapoifanya kwa ajili ya sifa,
utukufu, na furaha ya Mungu. Biblia inasema, “Hivyo mlapo au
mnywapo au chochote mkifanyacho, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.” Wakolosai 3:21 (NIV) Martin Luther alisema, “Mfanyakazi wa
nyumbani anaweza kukamua ng’ombe wa maziwa kwa utukufu wa Mungu.”
Je,
yawezekanaje kufanya kila kitu kwa utukufu wa Mungu? Kwa kufanya kila kitu kana
kwamba unamfanyia Yesu na huku ukifanya mazungumzo naye unapoendelea na kazi
hiyo. Biblia inasema, “Kila mkifanyacho, kifanyeni kwa moyo
wenu wote, kama kumtumikia Bwana, siyo watu.”
Warumi 12:1 (Msg)
Hii
ndiyo siri ya maisha ya kuabudu, kufanya kila kitu kana kwamba unamfanyia Yesu.
Tafsiri ya ujumbe inasema, “Yachukueni maisha yenu ya kawaida, ya
kila siku, kulala kwenu, kula, kwenda kazini, na mizunguko yenu ya maisha - na
myaweke mbele za Mungu kama sadaka.” Warumi
12:1 (Msg) Kazi inakuwa ibada unapoiweka wakfu kwa Mungu na ukaifanya na
utambuzi wa uwepo wake.
Nilipompenda
kwa mara ya kwanza mke wangu, nilimfikiria daima: nilipokua kifungua kinywa,
nilipoendesha kwenda shuleni, nilipokuwa darasani, nilipokuwa kwenye msitari
sokoni – sikuacha kumfikiria mwanamke huyu! Mara nyingi nilijisemea peke yangu
kuhusu huyu mwanamke na nikafikiri mambo yote niliyoyapenda kwake. Hii ilinisaidia
kujisikia kuwa karibu na Kay ingawa tuliishi maili mamia kadhaa mbali na
tulikuwa katika vyuo tofauti. Kwa kumfikiria daima, nilidumu katika
pendo lake. Hivi ndivyo kuabudu halisi kulivyo – kumpenda Yesu.
Siku ya Tisa: Nini
Humfanya Mungu Kutabasamu?
BWANA anatabasamu
kwa ajili yako…
Hesabu
6:25 (NLT)
Tabasamu kwa
ajili ya yangu, mtumishi wako,
nifundishe njia
sahili ya kusihi.
Zaburi
119:135 (Msg)
Tabasamu la Mungu ni lengo la maisha yako.
Kwa kuwa kumfurahisha Mungu ndilo lengo lako la kwanza la maisha
yako, kazi yako ya muhimu Zaidi ni kugundua namna ya kutekeleza jambo hilo.
Biblia inasema, “Tafuteni ni nini kinachompendeza
Kristo, na kisha fanyeni hicho” Waefeso
5:10 (Msg) Kwa bahati nzuri, Biblia hutupa mfano Dhahiri wa maisha yampendezayo
Mungu. Jina la mtu huyo alikuwa Nuhu.
Wakati wa Nuhu, ulimwengu wote ulikuwa umeharibika kwa kukosa
uadilifu. Kila mtu aliishi kwa kujifurahisha mwenyewe na siyo Mungu. Mungu
hakuweza kupata mtu yeyote duniani aliyetafuta kumpendeza, hivyo alihuzunika na
akajilaumu kwa nini alimuumba mwanadamu. Mungu alikasirishwa sana na binadamu
kiasi cha kufikiri kumfutilia mbali kabisa. Lakini kulikuwa na mtu mmoja
aliyemfanya Mungu kutabasamu. Biblia inasema, “Nuhu
alimfurahisha Bwana.” Mwanzo 6:8 (LB)
Mungu alisema, “Mtu huyu ananiletea furaha. Hunifanya nitabasamu.
Nitaanza upya na jamaa yake.” Kwa sababu Nuhu alileta furaha kwa Mungu, ndiyo
maana mimi na wewe tupo leo. Kutokana na maisha yake tunajifunza matendo ya
ibada yanayomfanaya Mungu atabasamu.
Mungu
hutabasamu tunapompenda kuliko vyote. Nuhu
alimpenda Mungu kuliko kitu chochote duniani, hata kama hapakuwa na mwingine
yeyote aliyefanya hivyo! Biblia inatuambia kwamba kwa maisha yake yote, “Nuhu siku zote alifuata mapenzi ya Mungu na kufurahia uhusiano wa
karibu naye.” Mwanzo 6:9 (NLT)
Hiki ndicho Mungu anachokitaka kwako kuliko vyote: Uhusiano! Ni
ukweli wa ajabu duniani – kwamba Muumba wetu anapenda kuwa na ushirika na sisi.
Mungu alikuumba ili akupende, na anatamani na wewe umpende. Anasema, “Sitaki dhabihu zenu – nataka upendo wenu; Sitaki sadaka zenu –
nataka mnifahamu.” Hosea 6:6 (LB)
Je unaweza kuona nia ya Mungu katika kifungu hiki? Mungu anakupenda
kwa kina na anatamani umpende. Anatamani umjue na utumie muda pamoja naye.
Ndigyo maana kujifunza kumpenda Mungu na kupendwa naye linapaswa liwe lengo
lako kubwa la maisha. Hakuna kinachokaribia lengo hili katika umuhimu. Yesu aliliita
amri kuu kupita zote. Alisema, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako
wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri kuu naya
kwanza.” Mathayo 22:37-38 (NIV)
Mungu hutabasamu tunapomwamini kabisa.
Sababu ya pili Nuhu alimpendeza Mungu ni kwamba alimtumaini Mungu, hata pale
ambapo hapakuleta maana yoyote. Biblia inasema, “Kwa imani, Nuhu alijenga
meli katikati ya nchi kavu. Alionywa juu ya jambo ambalo hakuliona, na akatenda
kama alivyoagizwa …. Matokeo yake, Nuhu akawa karibu sana na Mungu.” Waebrania 11:6 (NIV)
Jaribu kukisia tukio hili: siku moja Mungu anakuja kwa Nuhu
kumwambia, “Nimekatishwa tamaa na wandamu. Dunia nzima, isipokuwa wewe, hakuna
anayenifikiria. Lakini Nuhu, ninapokuangalia, naanza kutabasamu. Nimefurahishwa
na maisha yako, hivyo nakwenda kuugharikisha ulimwengu mzima na kuanza upya na
jamaa yako. Nakutaka ujenge meli kubwa ambayo itawaokoa ninyi pamoja na
wanyama.”
Kulikuwa na matatizo matatu ambayo yangemfanya Nuhu kuwa na
mashaka. Kwanza, Nuhu alikuwa hajaona mvua, kwa sababu kabla ya gharika, Mungu
alinyeshea ardhi kutoka chini kwenda juu. Mwanzo 2: 5-6 Pili, Nuhu aliishi
mamia ya maili kutoka bahari ya karibu. Hata kama angejifunza kutengeneza meli,
angeipelekaje majini? Tatu kulikuwa na tatizo la kuwapata wanyama wote hao na
kuwatunza. Lakini Nuhu hakulalamika wala kutoa udhuru. Alimtumaini Mungu
kabisa, na hicho kilimfanya Mungu kutabasamu.
Kumwamini Mungu kabisa maana yake ni kuwa na Imani kwamba yeye
anajua kilicho bora kwa maisha yako. Unamtengemea kuwa atatimiza ahadi zake,
atakusaidia katika matatizo, na afanye yasiyowezekana inapobidi. Biblia
inasema, “Anawafurahisha wale wanaomheshimu; wale
wanaoamini upendo wake wa daima.” Zaburi
147:11 (TEV)
Iimchukua Nuhu miaka 120 kujenga safina. Nahisi alikabiliwa na
siku nyingi za kukatisha tamaa. Bila dalili yoyote ya mvua mwaka hadi mwaka,
alichekwa na kudharauliwa kama “Mtu punguani anayefikiri Mungu anasema naye.”
Nafikiri watoto wa Nuhu waliudhiwa mara nyingi na lile meli kubwa lilipojengwa
uwanjani mwao. Lakini Nuhu alidumu kumwamini Mungu.
Je, ni eneo gani la maisha yako unahitaji kumwamini Mungu kabisa?
Kuamini ni tendo la kuabudu. Kama vile wazazi wanavyofurahi watoto wao wanapoamini
pendo na hekima yao, Imani yako humfanya Mungu afurahi. Biblia inasema, “Pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu.” Waebrania 11:6 (NIV)
Mungu
hutabasamu tunapomtii kwa moyo wote.
Ili kuokoa wanyama wa aina zote duniani kutoka kwenye gharika la dunia nzima
kulihitaji uangalifu mkubwa katika utekelezfaji na maelekezo ya kina. Kila kitu
kilipaswa kifanywe kama Mungu alivyoagiza. Mungu hakusema, “Nuhu jenga safina
yoyote unayopenda.” Alitoa maelekezo ya kina kuhusu ukubwa, umbo, na vifaa vya
kujengea safina pamoja na idadi mbalimbali ya wanyama wa kuletwa ndani ya
safina. Biblia hutuelezea juu ya mwitikio wa Nuhu: “Hivyo Nuhu
alifanya kila kitu kama Mungu alivyomwagiza.”
Mwanzo 6:22 (NLT); Waebrania 11:7b (NCV)
Angalia ambavyo Nuhu alitii kabisa (Hakuacha agizo hata moja), na alitii kama alivyoagizwa (kwa namna na wakati Mungu
alivyotaka ifanyike). Hii ni kwa moyo wote. Haishangazi kwamba Mungu
alitabasamu kwa Nuhu.
Kama Mungu angekueleza ujenge meli kubwa, hufikiri kwamba ungekuwa
na mswali kadhaa, upinzani, au kusita? Nuhu hakuwa hivyo. Alimtii Mungu kwa
moyo wote. Hii ina maana kufanya yale yote Mungu anavyosema bila kusubiri au
kusita. Hupaswi kuahirisha kwa kusema, “nitaliombea jambo hili”. Fanya bila
kuchelewa. Kila mzazi anafahamu kwamba kuchelewa kutii ni kutokuwa na utii
(uasi kamili).
Mungu hahitaji kutoa sababu au kujieleza
kwako kwa alivyokuagiza kufanya. Kufahamu kunawezi kusubiri, lakini huwezi
kungoja kutii. Utii wa mara moja unakufundisha kuhusu Mungu kuliko majadiliano
ya Biblia kwa maisha yako yote. Hakika huwezi kuelewa baadhi ya maagizo mpaka
uyatii kwanza. Utii hufungua ufahamu.
Mara nyingi tunajaribu kumpa Mungu nusu utii. Tunataka kuchagua maagizo ya kutii tuna fanya orodha ya
maagizo tunayopenda kutii na tunayaacha yale tunayodhani hayafai, magumu, ya
gharama, au hayakubaliki na wengi. Nitahudhuria kanisani lakini sitatoa fungu
la kumi. Nitasoma Biblia yangu lakini sitamsamehe mtu aliyenikosea. Lakini
kutii nusu ni kutotii.
Kutii kwa moyo wote kunafanywa kwa furaha, na moyo wa kupenda.
Biblia inasema, “Mtii BWANA kwa furaha.” Zaburi 100:2 (LB) Hii ndiyo ilikuwa nia ya Daudi: “Niambie cha kufanya nami nitatenda, Bwana. Kwa siku zote
nitakazoishi nitakutii kwa moyo wote.”
Zaburi 119:33 (LB)
Yakobo, akiwaeleza Wakristo, alisema, “Tunampendeza
Mungu kwa yale tuyafanyayo na siyo tu kwa yale tuyaaminiyo.” Yakobo 2:24 (CEV) Neno la Mungu liko wazi kwamba mtu huwezi
kupata wokovu kwa nguva zako. Hupatikana tu kwa neema, si nguvu zako. Lakini
kama mtoto wa Mungu unavyoweza kuleta furaha kwa Baba yako wa mbinguni kwa
kutii.
Tendo lolote la utii ni tendi la kuabudu pia. Kwa nini utii ni
jambo linalopendeza sana kwa Mungu? Kwa sababu hii huthibitisha kweli unampenda
Mungu. Yesu alisema, “Kama mnanipenda, mtatii amri zangu.” Yohana 14:15 (TEV)
Mungu
hutabasamu tunapomsifu na kumshukuru daima.
Ni vitu vichache hufurahisha kuliko kupokea sifa na shukrani toka kwa mtu
mwingine. Mungu hupenda jambo hili pia. Yeye hutabasamu tunapoonyesha ibada na
shukrani kwake.
Maisha ya Nuhu yalileta furaha kwa Mungu kwa sababu aliishi na
moyo wa sifa na shukrani. Tendo la kwanza la Nuhu baada ya gharika lilikuwa
kuonyesha shukrani kwa Mungu kwa kutoa dhabihu. Biblia inasema, “Kisha Nuhu alijenga madhabahu kwa ajili ya BWAMA ….. na akatoa
sadaka ya kuteketezwa juu yake.” Zaburi
116:17 (KJV)
Kwa sababu ya sadaka ya Yesu, hatutoi sadaka za wanyama kama
alivyofanya Nuhu. Badala yake tunaambiwa kumtolea Mungu “dhabihuza sifa” Waebrania 13:15 (KJV) na “dhabihu za shukrani.” Zaburi
116:17 (KJV)
Tunamsifu Mungu kwa vile alivyo, na tunamshukuru kwa yale anayoyafanya. Daudi alisema, “Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na
kumtukuza kwa shukrani. Hili litampendeza Bwana.”
Zaburi 69:30-31 (NIV)
Jambo la ajabu hutokea tunapotoa sifa na shukrani kwa Mungu.
Tunapompa Mungu furaha, mioyo yetu inajawa na furaha!
Mama yangu alipenda kunipikia. Hata baada ya kumwoa Kay,
tulipowatembelea wazazi, mama alituandalia karamu safi sana. Moja ya mambo
yaliyomfurahisha maishani ilikuwa ni kutuona sisi watoto wake tukila na
kufurahia chakula alichokiandaa. Kadiri tulivyofurahia, ndivyo furaha yake
ilivyoongezeka.
Lakini sisi pia tulifurahia kumpendeza mama kwa kuonyesha
kukifurahia chakula chake. Ilifanyika kwa pande zote mbili. Nilipokula ule mlo
safi, nilikisifia na kumsifu mama pia. Nilikusudia si kukifurahia chakula tu,
lakini kumfurahisha mama pia. Kila mmoja alikuwa na furaha.
Kuabudu kunahusisha pande mbili pia. Tunafurahia kile Mungu
ametutendea, na tunapoonyesha furaha hiyo kwa Mungu, humletea furaha – lakini
pia huongeza furaha yetu. Kitabu cha Zaburi kinasema, “Wenye haki wanafuraha, na wanashangilia katika uwepo wake;
wanafuraha na wanapiga kelele za shangwe.”
Zaburi 68:3(TEV)
Mungu
hutabasamu tunapotumia uwezo wetu. Baada ya
gharika, Mungu alimpa Nuhu maagizo rahisi: “Zaeni
mkaongezeke na mkaijaze nchi …. Kila kilicho hai na kiendacho katika nchi
kitakuwa chakula chenu. Kama nilivyowapa mimea, sasa nawapa kila kitu.” Mwanzo 9:1-3 (NIV)
Mungu alisema, “Ni wakati wa kuendelea na maisha yenu! Fanyeni
mambo niliyowaambia wanadamu kufanya. Lala na mwenzi wa ndoa. Zaeni watoto.
Mtunze jamaa. Pandeni mazao na kula chakula. Iweni wanadamu! Ndivyo nilivyowaumba
muwe!”
Unaweza kuhisi kwamba muda pekee anaokufurahia Mungu ni pale
unapofanya mambo ya “kiroho” – kama kusoma Biblia, kwenda kanisani, kusali, au
kuwaeleza watu wengine Imani yako. Na unaweza kufikiri kwamba Mungu hahusiki na
mambo mengine ya maisha yako. Hakika, Mungu anafurahi kuona
kila jambo katika maisha yako, iwe
kazini, kucheza, kupumzika, au kula. Hakosi kuhusika na chochote kile
unachokifanya. Biblia inatuambia, “Hatua za wenye haki zinaongozwa na
BWANA. Hupendezwa kila jambo katika maisha yao.”
Zaburi 37:23 (NLT)
Kila kazi ya binadamu, isipokuwa dhambi, yaweza kufanywa kwa ajili
ya furaha ya Mungu hasa kama kukuona ukitumia karama na uwezo aliokupa. Unaweza
kuosha vyombo, kurekebisha mtambo, uza kitu, andika ratiba ya kompyuta, kuuza
zao, na lea jamaa kwa utukufu wa Mungu.
Kama mzazi aonaye furaha kwa mwanae, Mungu hufurahia sana akikuona
ukivitumia vipawa na uwezo aliokupa. Kwa makusudi alitupa vipawa mbalimbali kwa
ajili ya furaha yake. Wengine amewafanya wakimbiaji na wengine watafiti.
Unaweza kuwa umepewa kipawa cha ufundi au hisabati au muziki au maelfu ya
vipawa vingine. Vipawa vyote hivi vinaweza kuleta tabasamu kwenye uso wa Mungu.
Biblia inasema, “Amemuumba kila mtu kwa zamu; sasa
anaangalia kila kitu tunachokifanya.”
Zaburi 33:15 (Msg)
Mtu huwezi kuleta furaha au
utukufu kwa Mungu kwa kuficha vipawa vyako au kwa kujaribu kuwa mwingine.
Unamletea furaha pale tu unapokuwa wewe. Wakati wowote unapokataa sehemu yoyote
uliyonayo, unakataa hekima ya Mungu na utawala wake katika kukuumba. Mungu
anasema, “Huna haki ya kubishana na Muumba wako. Wewe ni
chombo cha udongo wa mfinyanzi kilichotengenezwa na mfinyanzi. Udongo hauulizi,
‘Kwa nini umenitengeneza namna hii?’”
Isaya 45:9 (CEV)
Katika filamu iitwayo Chariots of Fire, mkimbiaji wa Olimpiki aitwaye Eric Liddell anasema, “Mungu
aliniumba kwa malengo, lakini aliniumba mwepesi na ninapokimbia, nahisi furaha
ya Mungu.” Baadaye anasema, “kuacha kukimbia ingekuwa kumsaiti.” Hakuna vipawa
visivyo vya kiroho, labda vinavyotumiwa vibaya. Anza kutumia vipawa ulivyo
navyo kwa ajili ya furaha ya Mungu.
Mungu pia hufurahi anapokuona unafurahia uumbaji wake. Alikupa
macho ili ufurahie uzuri, masikio ufurahie sauti, pua yako na ulimi uweze
kufurahia harufu na kuonja, na mishipa ya fahamu chini ya ngozi yako ili
ufurahie mguso. Kila tendo la kufurahia huwa tendo la kuabudu unapomshukuru
Mungu kwa ajili yake. Kwa kweli, Biblia inasema, “Mungu … Kwa
ukarimu hutupatia kila kitu ili tufurahie.”
1 Timotheo 6:17 (TEV)
Mungu anafurahia hata kukuona umelala! Watoto wangu walipokuwa
wadogo, nakumbuka utoshelevu wa kina nilioupata kwa kuona wamelala. Wakati
mwingine siku hiyo ilikuwa imejaa matatizo na kutotii, lakini wakiwa wamelala
walionekana wametosheka, salama, na wenye amani, na nilikumbushwa kiasi gani
ninavyowapenda.
Watoto wangu hawakuhitaji kufanya chochote ili niwapende. Nilikuwa
na furaha ile kuwaona tu wakipumua, kwa sababu niliwapenda sana. Kadiri vifua
vyao vidogo vilivyopanda na kutelemka, nilitabasamu, na wakati mwingine machozi
ya furaha yalijaza macho yangu. Unapokuwa umelala, Mungu hukutazama kwa upendo kwasababu
ulitokana na mawazo yake. Anakupenda kama vile ni wewe peke yako dunia nzima
hakuna mtu.
Wazazi hawahitaji watoto wao kuwa wakamilifu, au kupevuka, ili
kuwafurahia. Wanawafurahia katika kila hatua ya kukua kwao. Vivyo hivyo, Mungu
hasubiri wewe ufikie kupevuka kabla ya kuanza kukupenda. Anakupenda na
anakufurahia katika kila hatua ya kukua kwako kiroho.
Inawezekana umewahi kuwa na walimu au wazazi wasiofurahia katika
kukua kwako. Tafadhali usifikiri Mungu naye yuko hivyo juu yako. Anajua huna
uwezo wa kuwa mkamilifu au bila dhambi. Biblia inasema, “Anajua bila shaka sisi tumetengenezwa na nini. Anajua moyoni mwake
kuwa sisis tu mavumbi.” Zaburi 103:14 (GWT)
Mungu anachokitazama ni nia ya moyo wako: Je, kumpendeza yeye
ndiyo nia yako kubwa? Hili ndilo lilikuwa lengo la Paulo maishani: “Zaidi ya chochote kile, walakini, tunataka kumpendeza Yeye, iwe
katika maskani yetu hapa au kule.” 2 Wakorintho 5:9 (TEV) Unapoishi
katika nuru ya umilele, mtazamo wako unabadilika kutoka “Ni kiasi gani cha
furaha ninakipata maishani?” kwenda “Je, Mungu anapata kiasi gani cha furaha
kutoka maishani mwangu?”
Mungu anatafuta watu kama Nuhu katika karne hii ya ishirini na
moja – watu walio tayari kuishi kwa ajili ya furaha ya Mungu. Biblia inasema, “Mungu anatazama chini kutoka mbinguni ili aone kama kuna watu
wenye hekima, wanaotaka kumpendeza Mungu.”
Zaburi 14:2 (LB)
Je, utafanya kumpendeza Mungu liwe lengo lako la maisha? Hakuna
chochote ambacho Mungu hawezi kumfanyia mtu ambaye amejitosheleza kabisa
kutimiza lengo hili.
Siku ya Kumi: Kiini Cha Kuabudu
Jikabidhini kwa Mungu …
Jisalimisheni utu wenu kwake ili mpate kutumiwa kwa malengo ya
haki.
Warumi 6:13 (NLT)
Kiini cha kuabudu ni kujisalimisha.
Ni neno lisilotumiwa sana, halipendwi kama vile neno kunyenyekea.
Lina maana ya kupoteza, na hakuna mtu yeyote anapenda kupoteza. Kujisalimisha
kunaonyesha picha isiyopendeza ya kukubalika kushindwa katika vita, kupoteza
katika michezo, au kukubali kushindwa na mpinzani mwenye nguvu zaidi. Neno hili
linatumiwa mara nyingi katika hali isiyokubalika. Wahalifu waliotekwa
hujisalimisha kwa mamlaka.
Katika mila ya leo ya ushindani tunafundishwa kutokuacha au
kutokukubali tu – hivyo hatusikii sana kuhusu kujisalimisha. Kama kushinda
ndiyo kila kitu, basi kujisalimisha hakupo. Labda tuongelee kushinda,
kufanikiwa, kuzidi nguvu na kushinda vita kuliko kujitoa, kunyenyekea, kutii,
na kujisalimisha. Lakini kujisalimisha ni kiini cha kuabudu. Ni mwitikio wa
asili wa huruma na upendo wa ajabu wa Mungu.Tunajitoa nafsis zetu kwake, si kwa
hofu au kwa kuwa ni wajibu, lakini kwa upendo, “kwa sababu
alitupenda kwanza.”
1 Yohana 4:9-10, 19
Baada ya kutumia sura kumi na moja za kitabu cha Warumi kuelezea
neema kuu ya Mungu wetu, Paulo anatusihi tujisalimishe maisha yetu yote kwa
Mungu kwa kuabudu. “Hivyo basi ,ndugu zangu, kwa sababu ya
rehema kuu ya Mungu Kwetu … Jitoeni nafsi zenu kama dhabihu hai kwa Mungu,
ilivyowekwa wakfu kwa utumishi wake na yenye kumpendeza. Hii ndiyo ibada ya
kweli mnayopaswa kutoa.” Warumi 12:1 (TEV)
Ibada ya kweli yenye kuleta furaha kwa Mungu hutokea unapojitoa
kikamilifu kwa Mungu. Angalia neno la kwanza na la mwisho katika kifungu hicho
yanafanana: kutoa.
Kujitoa kwa Mungu ndiyo kuabudu hasa.
Kujitoa
nafsi yako kwa Mungu ndiyo kuabudu hasa
|
Tendo hili la kujisalimisha binafsi linaitwa kwa majina mengi: kujiweka
wakfu, kumfanya Yesu Bwana wako, kuchukua msalaba wako, kuifisha nafsi, kujitoa
kwa Roho mtakatifu. Cha muhimu hapa ni kwamba ulitende, siyo linaitwaje. Mungu
anapenda maisha yako – yote kabisa. Asilimia tisini na tano haitoshi.
Kuna vizuizi vitatu ambavyo huzuia kujisalimisha kwetu kikamilifu
kwa Mungu. Hatuelewi kiasi gani Mungu anatupenda, tunataka kutawala maisha yetu
wenyewe, na tunashindwa kuelewa maana ya kujisalimisha.
Je,
naweza kumwamini Mungu? Imani ni jambo muhimu katika
kujisalimisha. Huwezi kujisalimisha kwa Mungu mpaka uwe unamwamini, lakini
huwezi kumwamini Mungu mpaka umfahamu vyema. Hofu hutuzuia kujisalimisha, lakini
upendo huondoa hofu yote.
Kadiri unavyotambua jinsi Mungu anavyokupenda, ndivyo kujisalimisha kunavyokuwa
rahisi.
Je unajuaje Mungu anakupenda? Anakupa ushahidi mwingi: Mungu
anasema anakupenda; hautoki kwenye uangalizi wake kamwe; Zaburi 145:9 hautoki
kwenye uangalizi wake kamwe; Zaburi 139:3 yeye anayaangalia mambo yote ya
maisha yako; Mathayo 10:30 alikupa uwezo wa kufurahia aina zote za viburudisho;
1 Timotheo 6:17b ana mpango mzuri kwa ajili ya maisha yako; Yeremia 29:11 yeye
hukusamehe; Zaburi 86:5 na kwa upendo anakuvumilia; Zaburi 145:8 Mungu
anakupenda kiasi kisichopimika kuliko unavyoweza kufikiri.
Uthibitisho wa ukweli huu ni dhabihu ya mwana wa Mungu kwa ajili
yako. “Mungu aliuthibitisha upendo wake kwetu kwa
vile tulipokuwa tungali wenye dhambi Kristo alitufia.” Warumi 5:8 (NRSV) Kama unataka
kufahamu uthamani wako mbele za Mungu, mwangalie Yesu Kristo na mikono yake
iliyowambwa msalabani, akisema“nakupenda sana! Bora nife kuliko kukukosa.”
Mungu siyo kiongozi katili wa msafara wa watumwa au mchokozi
anayetumia mabavu kutulazimisha tumtii. Hajaribu kuvunja utashi wetu, lakini
hutusihi ili tujitoe wenyewe kwake kwa kupenda. Mungu ni mpendwa na mkombozi,
na kujisalimisha kwake huleta uhuru, siyo utumwa. Tunapojisalimisha kwa Yesu
kikamilifu, tunagundua kwamba yeye si mtawala wa imla, lakini ni mwokozi; siyo
bwana mkubwa, lakini ndugu; si mtawala wa imla, lakini rafiki.
Kukubali
mipaka yetu. Kikwazo kingine cha kujisalimisha
kikamilifu ni majivuno yetu. Hatukubali kwamba sisi ni viumbe tu na kwamba
hatuna utawala na kwamba hatuna utawala juu ya kila kitu. Hili ni jaribu kila
zamani; mtakuwa
kama Mungu, Mwanzo 3:5 tamaa hiyo ya kuwa na utawala juu ya kila kitu ni
chanzo cha matatizo mengi katika maisha yetu. Maisha ni mapambano, lakini jambo
ambalo watu wengi hawaelewi ni kwamba mapambano yetu kama yale ya Yakobo hakika
ni mapambano na Mungu! Tunataka kuwa sawa na Mungu, na haitawezena sisi
kushinda pambano hilo.
SIKU
YA KUMI:
MOYO WA KUABUDU
|
A.W. Tower alisema, “Sababu kwa nini watu wengi bado wanasumbuka,
bado wanatafuta, bado wanafanya maendeleo kidogo ni kwa vile bado hawajafikia
mwisho wao wenyewe. Bado tunajaribu kuamuru na kuingilia kazi ya Mungu ndani
yetu.”
Sisi sio Mungu na hatutakuwa kamwe. Sisi ni wanadamu. Ni pale
tunapojaribu kuwa Mungu ndipo tunaishia kuwa kama Shetani kabisa, ambaye
alitamani jambo hilo hilo.
Tunakubali ubinadamu wetu kiakili lakini siyo kihisia. Tunapokabiliwa
na mapungufu yetu, ndipo tunaonyesha uchungu, hasira na chuki. Tunataka kuwa
warefu (au wafupi), wenye akili, wenye nguvu, wenye vipawa, warembo, na
matajiri. Tunataka kuwa na kila kitu na kufanya kila kitu na tunakata tamaa
inaposhindikana. Kisha tunatambua kwamba Mungu aliwapa watu wengine vipawa
ambavyo sisi hatuna, na hivyo tunapatwa husuda, wivu, na kujisikitikia.
Maana
ya kujisalimisha. Kujisalimisha kwa Mungu si
kujiuzulu na kukaa tu kusubiri, au kuamini kuwa yote yameandikwa binadamu hana
hiari, au kuwa na udhuru na wivu. Siyo kukubali hali hiyo hiyo uliyo nayo.
Inaweza kumaanisha kinyume cha haya; kujitoa sadaka maisha yako au kuteseka ili
kubadilisha yanayohitajika kubadilishwa. Mara nyingi Mungu huwaita watu waliojisalimisha
kwake kupiga vita kwa jina lake. Kujisalimisha sio kwa uoga au mazulia. Vivyo
hivyo haimaanishi kuacha kutumia akili katika kufikiri. Mungu asingependaa
kupoteza akili alizokupa! Mungu hapendi watu wawe kama mitambo (robots) ili
kumtumikia. Kujisalimisha siyo kukomesha utu wako. Badala ya kukomesha utu
wako, kujisalimisha hutia nguvu. C. S. Lewis alisema, “Kadiri tunavyomruhusu
Mungu atutawale ndivyo tunavyozidi kuwa sisi wenyewe – kwa sababu yeye ndiye
aliyetuumba. Alibuni namna mbalimbali za watu wote tofauti ambao mimi na wewe
tulikusudiwa kuwa .… Ni pale ninapomgeukia Kristo, ninapojikabidhi nafsi yangu
kwake, ndipo ninapokuwa na ule utu wangu halisi.”
Kujisalimisha kunadhihirika vyema katika utii. Unasema “ndivyo,
Bwana” Kwa chochote anachokueleza. Kusema “hapana, Bwana” ni kutamka kinyume. Hatuwezi kumwita Yesu Bwana na wakati huo
huo hatutaki kumtii. Baada ya usiku kucha bila kupata samaki, Simioni
alionyesha kujisalimisha pale Yesu alipomwambia kujaribu tena: “Bwana
tumefanya kazi kwa bidi usiku wote na hatujakamata samaki yeyote. Lakini kwa
sababu umesema, nitatia nyavu majini.”
Luka 5:5 (NIV) Watu waliojisalimisha hutii neno la Mungu hata kama linaonekana
kutokuwa na maana.
Jambo jingine katika kujisalimisha ni Imani. Ibrahimu alifuata
maelekezo ya Mungu bila kujua alikokuwa akienda. Hana alisubiri wakati wa Mungu
bila kujua ni lini. Mariamu alitarajia muujiza bila kufahamu utatendekaje. Yusufu
aliamini lengo la Mungu bila kujua kwa nini mazingira yalikuwa hivyo. Kila mmoja
wa watu hawa alikuwa amejisalimisha kwa Mungu kwelikweli.
Utafahamu umejisalimisha kwa Mungu unapomtegemea Mungu
akutengenezee mambo yako badala ya kujaribu kuwafanyia hila wengine, ukapitisha
jambo lako, na mwisho ukatawala mazingira hayo. Unamwachia Mungu afanye, huhitaji
wakati wote kuwa “mwangalizi”. Biblia inasema, “Jisalimishe nafsi
yako kwa Bwana, na umsubiri kwa uvumilivu.”
Zaburi 37:7a (GWT) baada ya kujaribu sana, umwamini zaidi. Pia unafahamu kwamba
unajisalimisha unapokua huchukizwi na lawama na kukimbilia kujitetea. Mioyo
iliyojisalimisha huonyesha mahusiano mazuri na wengine. Huwatupilii mbali
wengine, hudai haki zako, na hutumikii nafsi yako kama umejisalimisha.
Eneo gumusana kwa watu wengi kujisalimisha ni pesa zao. Wengi
wamefikiri, “Nataka kuishi kwa ajili ya Mungu lakini pia nataka kupata pesa
nyingi ili niishi kwa raha baadaye nipumzike.” Kupumzika siyo lengo la maisha
ya kujisalimisha, kwa sababu huku ni kushindana na Mungu kwa sababu ya kuweka
mkazo kwanza kwa maisha yetu. Yesu alisema, “Huwezi kutumikia
Mungu na pesa” Mathayo 6:24 na kwamba “Popote
hazina yako ilipo ndipo na moyo wako uko.” Mathayo 6:21
Kielelezo kikubwa cha kujisalimisha ni Yesu. Usiku ule kabla ya
mateso Yesu alijisalimisha kwa mpango wa mpango wa Mungu. Alisali, “Baba
Kila kitu kinawezekana kwako. Tafadhali niondolee kikombe hiki cha mateso.
Lakini nataka mapenzi yako, siyo yangu.”
Marko 14:36 (NLT)
Kujisalimisha kunadhihirika vyema katika utii na
Imani.
|
Yesu hakuomba, “Baba, kama unaweza kuniondolea maumivu haya, tafadhali fanya hivyo.” Alikuwa tayari
amethibitisha kuwa Mungu ana uwezo kufanya lolote! Badala yake aliomba, “Mungu,
kama inapendeza kwako
kuniondolea mateso haya, tafadhali fanya hivyo. Lakini kama
yanatimiza kusudi lako,
ndivyo ninavyotaka pia.”
Kujisalimisha halisi husema, “Baba, kama tatizo hili, maumivu,
ugonjwa, au hali yoyote inahitajika kutimiza lengo lako na utukufu kwako katika
maisha yangu au ya mwingine, tafadhali usiliondoe.”
Kiwango hiki cha ukomavu hakiji kwa urahisi. Kwa upande wa Yesu, aliugua sana
kuhusu mpango wa Mungu kiasi cha kutoa jasho la damu. Kwa upande wetu, ni vita
kali dhidi ya asili yetu ya ubinafsi.
Baraka
za kujisalimisha. Biblia iko wazi kabisa kuhusu
unavyoweza kufaidika unapojisalimisha kikamilifu kwa Mungu. Kwanza, unapata
amani: “Acha kugombana na Mungu! Ukikubaliana naye,
utapata amani hatimaye, na mambo yatakunyookea.”
Ayubu 22:21 (NLT) Pili, unapata uhuru: “Jitoeni nafsi zenu
kuzifuata njia za Mungu na uhuru hautatoka kamwe … Amri zake zinawaweka huru
kuishi kwa uwazi katika uhuru wake!”
Warumi 6:17 (Msg) Tatu, unapata nguvu za Mungu katika maisha yako. Majaribu
makali na matatizo mazito yanaweza kushindwa na Kristo kama atakabidhiwa.
Joshua alipoviendea vita vile vikubwa maishani mwake, Yoshua
5:13-15 alikutana na Mungu, akamsujudia, na akasalimisha mipango yake.
Kujisalimisha huko kulileta ushindi mkubwa pale Yeriko. Hiki ni kitendawili:
Ushindi huja kwa kujisalimisha, kujisalimisha hakukudhoofishi wewe; kunakutia
nguvu. Jisalimishe kwa Mungu, hauhitaji kuogopa au kujisalimisha kwa chochote
kile. William Booth, mwanzilishi wa Jeshi la wokovu, alisema, “ukuu wa nguvu za
ubinadamu unapimwa kwa kiwango chake cha kujisalimisha.”
Watu waliojisalimisha ndio Mungu anaowatumia. Mungu alimchagua Mariamu
kuwa mama wa Yesu, siyo kwa sababu alikuwa na kipawa, utajiri au uzuri wa
umbile, lakini kwa sababu alikuwa amejitoa kikamilifu kwake. Malaika wa Bwana
alipomwelezea mpango mgumu wa Mungu, alijibu kwa upole, “Mimi
ni mjakazi wa Bwana, na niko tayari kupokea chochote anachotaka.” Luka 1:38 (NLT) Hakuna kitu kikubwa kama maisha ya kujisalimisha
katika mikono ya Mungu. “Hivyo zikabidhini nafsi zenu
kikamilifu katika mikono ya mungu.” Yakobo 4:7a (NCV)
Kujisalimisha sio njia bora ya kuishi. Ndiyo njia ya
pekee ya kuishi. Hakuna nyingine inayoleta ufanisi.
|
Njia
bora ya kuishi. Kila mtu hatimaye hujisalimisha
kwa mtu au kitu Fulani. Kama sio kwa Mungu, utajisalimisha kwa matarajio au
maoni ya watu wengine, au pesa, chuki, hofu, au kwa kiburi chako au tamaa
mbaya, au ubinafsi. Ulibuniwa kumwabudu Mungu – na kama utashindwa kumwabudu,
utatengeneza vitu vingine (sanamu) ili uvipe maisha yako. Unao uhuru wa
kuchagua usalimishe maisha yako, lakini hauko huru na mtokeo ya uchuguzi huo.
E. Stanly Jones alisema, “kama hutajisalimisha kwa Kristo, utajisalimisha kwa
machafuko.”
Kujisalimisha si nijia bora ya kuishi; ni njia pekee ya kuishi.
Hakuna kitu kingine cha kukufanikisha. Njia nyingine zote hukuongoza kwenye
kukukatisha tamaa, na kuiangamiza nafsi. Tafsiri ya King James huita
kujisalimisha “ ibada yenu yenye maana.” Warumi 12:1 (KJV) Tafsiri nyingine
inasema, njia yenye maana zaidi ya kumtumikia Mungu.” Warumi 12:1 (CEV)
Kusalimisha maisha yako si hisia za kipumbavu lakini nitendola akili na busara
ambalo unaweza kulifanya kwa ajili ya maisha yako. Ndiyo maana Paulo alisema, “Ni
lengo letu kwamba tumpendeze yeye.” 2 Korintho
5:9 (NIV) Nyakati zako za busara zitakuwa zile ambazo unasema ndiyo kwa Mungu.
Wakati mwingine huchukua miaka, lakini hatimaye unagundua kwamba
kizuizi kikubwa kwa baraka zaMungu maishani mwako sio watu wengine, ni wewe
mwenyewe – matakwa yako binafsi, kiburi cha hali ya juu, na matarajio yako.
Huwezi kutimiza lengo la Mungu kwa maisha yako huku ukikazania malengo yako
binafsi.
Kama Mungu ataenda kufanya kazi ya kina ndani yako, itaanza hivyo.
Kwa hiyo mpe yote Mungu: kushindwa kwako hapo nyuma, matatizo yako ya sasa,
matarajio yako ya mbele, hofu zako, ndoto, udhaifu, tabia, maumivu, na madhara
yoyote uliyo nayo. Mweke Yesu katika kiti cha dereva wa maisha yako na uondoe
mikono yako toka kwenye usukani. Usiopope; hakuna chochote katika uongozi wake
kinaweza kupoteza dira. Chini ya uongozi kwa Kristo unaweza kumudu chochote.
Utakuwa kama Paulo, “Niko tayari kwa lolote na kuwa sawa na
chochote kwa njia yayeye anayetia nguvu ndani yangu, yaani, ninajitosheleza
katika utoshelevu wa Kristo.” Wafilipi 4:13 (Amp)
Kujisalimisha kwa Paulo kulitokea katika njia ya Dameski
alipoangushuwa chini na mwanga mkali uliompofusha. Kwa watu wengine, Mungu
anapata mwitikio wetu bila kutumia njia ya ajabu sana. Pamoja na hayo,
kujisalimisha siyo tukio la wakati mmoja tu. Paulo alisema, “Nakufa
kila siku.”1 Wakorintho
15:31 Kuna wakati wa kujisalimisha, na kuna tendo la kujisalimisha, ambalo ni
la muda-hadi-muda na maisha zote. Tatizo la sadaka iliyo hai
ni kwamba inaweza kutambaa na kutoka madhabahuni, hivyo unaweza kutakiwa
kujisalimisha hata mara hamsini kwa siku. Ni lazima ufanye jambo hili kuwa
tabia yako ya kila siku. Yesu alisema, “Kama watu
wanapenda kunifuata ni lazima waache mambo wanayoyapenda. Lazima wawe tayari
kuacha maisha yao kila siku na kunifuata.” Luka 9:23 (NCV)
Ngoja nikuonye: unapoamua kuishi maisha ya kujisalimisha
kikamilifu, uamuzi huo utapimwa. Wakati mwingine itamaanisha kufanya mambo
yasiyostahili, ya gharama, au yanayoonekana hayawezekani. Mara nyingi
itamaanisha kufanya kinyume cha unavyojisikia kufanya.
Mmoja wa viongozi wakuu wa Kikristo wa karne ya ishirini alikuwa
Bill Bright, mwanzilishi wa Campus Crusade for Christ. Kwa kupitia watumishi wa
shirika hili duniani pote, kipeperushi cha sheria nne za kiroho, na filamu ya
Yesu (iliyoonwa na watu zaidi ya billioni nne), zaidi ya watu milioni 150
wamekuja kwa Yesu na watatumia umilele mbinguni.
Siku moja nilimuuliza Bill, “Kwa nini Mungu anakutumia na kubariki
maisha yako kiasi kikubwa hivyo? Alisema, “Nilipokuwa kijana mdogo, nilifanya
mkataba na Mungu. Niliandika na kutia sahihi ya jina langu chini yake.
Mkatabahuo ulisema, ‘Tangu siku ya leo na kuendelea, mimi ni mtumwa wa Kristo.’”
Je, umewahi kusaini mkataba kama huo na Mungu? Au bado unabishana
na kupambana na Mungu juu ya haki yake kufanya lolote apendalo kwa maisha yako?
Sasa ni wakati wako kujisalimisha – kwa neema ya Mungu, upendo na hekima yake.
SIKU YAKUMI
KUFIKIRIA JUU YA LENGO LANGU
Jambo la kutafakari: Kiini cha kuabudu ni
kujisalimisha.
Kifungu cha Kukumbuka: “Jisalimisheni
utu wenu wote kwake ili mpate kutumiwa kwa malengo ya haki.” Warumi 6:13b (TEV)
Swali la Kujiuliza: Je, ni eneo gani la maisha yangu
bado sijamkabidhi Mungu?
|
Siku ya Kumi na
moja: Kuwa Marafiki Wakubwa Na Mungu
Kwa
kuwa tulirejeshwa tena katika urafiki na Mungu kwa kifo cha
Mwana
wake tulipokuwa tungali adui zake, bila shaka tutaokolewa
Kutoka
hukumu ya milele kwa uzima wake.
Warumi 5:10 (NLT)
Mungu anapenda kuwa rafiki yako mkubwa. Uhusiano wako na Mungu una
vipengele vingi mbalimbali: Mungu ni Muumbaji na Mtengenezaji wako, Bwana na
Mtawala, Hakimu, Mkombozi, Baba, Mwokozi, na zaidi. (Zaburi 95:6; 136:3; Yohana
13:13; Yuda 1:4; 1 Yohana 3:1; Isaya 33:22; 47:4; Zaburi 89:26). Lakini ukweli
wa kushtua ni huu: Mungu mwenyewe anatamani kuwa rafiki yako!
Katika Edeni tunaona uhusiano halisi aliotaka kuwa nao nasi: Adamu
na Hawa walifurahia uhusiano wa karibu na Mungu.. Hapakuwa na desturi za ibada
wala dini – ulikuwa ni uhusiano rahisi wa upendo kati ya Mungu na watu
aliowaumba. Haukuwa na kizuizi cha hatia wala hofu, Adamu na Hawa walipendezwa
na Mungu, naye aliwafurahia.
Tuliumbwa ili kuishi katika uwepo wa Mungu daima, lakini baada ya
anguko, uhusiano huo mkamilifu ulipotea. Watu wachache tu katika Agano la kale
walikuwa na upendeleo wa urafiki na Mungu. Musa na Ibrahimu waliitwa “marafiki
wa Mungu” Daudi aliitwa “mtu aliyeupendeza moyo wa Mungu”, na Ayubu, Henoko, na
Nuhu walikuwa na urafiki wa karibu na Mungu. (Kutoka 33:11, 17 2Mambo ya
Nyakati 20:7; Isaya 33:22; 47:4; Zaburi 89:26). Lakini hofu ya Mungu, siyo
urafiki, lilikuwa ni jambo la kawaida katika Agano la Kale.
SIKU YA KUMI NA MOJA
KUWA RAFIKI WAKUBWA WA MUNGU
|
Kisha Yesu alibadilisha mambo. Alipolipa kwa ajili ya dhambi zetu
msalabani,pazia la hekaluni ambalo lilionyesha kutengwa kwetu na Mungu
lilipasuka toka juu hadi chini, hii ikiwa ni kuonyesha kwamba sasa haki ya
kumwendea Mungu moja kwa moja ilikuwa tena imepatikana.
Tofauti na makuhani wa Agano la Kale ambao walipaswa kutumia masaa
kujiandaa kukutana naye, sisi sasa tunaweza kumwendea Mungu saa yoyote. Biblia
inasema, “Sasa tunaweza kushangilia katika uhusiano wetu
wa ajabu mpya na Mungu – yote hii ikiwa ni kwa sababu yayale aliyofanya Bwana
wetu Yesu Kristo kwa ajili yetu kwa kutufanya rafiki wa Mungu.” Warumi 5:11 (NLT)
Urafiki na Mungu unawezekana tu kwa sababu ya neema ya Mungu na
sadaka ya Yesu. “Yote haya yamefanywa na Mungu ambaye
kwa njia ya Yesus Kristo alitubadilisha kutoka maadui na kuwa marafiki zake.” 2 Wakorintho 5:18a (TEV). Wimbo
wa zamani unasema, “Yesu kwetu ni rafiki,” lakini kwa kweli Mungu anatualika
tufurahie urafiki na uhusiano na nafsi zotetatu za utatu: Baba(1 Yohana 1:3),
Mwana (1Wakorintho 1:9), na Roho Mtakatifu (2Korintho 13:14).
Yesu alisema, “Siwaiti tena watumwa, kwa sababu
mtumwa hajui kazi za Bwana wake. Badala yake, ninawaita rafiki, kwa kuwa kila
nilichojifunza kwa Baba yangu nimewajulisha.” Yohana 15:15(NIV) Nenorafiki, katika kifungu hikihalimaanishi urafiki wa juu juu lakini ule wa
karibu sana, uhusiano wa kuaminika. Neno hilo hilo linatumika kumaanisha
msimamizi wa ndoa katika harusi (Yohana 3:29) na watu wa karibu sana na mfalme,
rafiki wa kuaminika. Katika nyua za kifalme, watumishi lazima wawe mbali na
mfalme, lakini wale marafiki wa karibu yake huwa na ukaribu, humwendea moja kwa
moja, na kufahamu taarifa nyeti.
Kwamba Mungu angependa niwe rafiki yake wa karibu ni vigumu
kuelewa, lakini Biblia inasema, “Yeye
ni Mungu ambaye anatamani uhusiano wake na ninyi.”
Kutoka 34:14 (NLT)
Mungu anatamani sana kwamba tumjue kwa ukaribu sana. Kwa hakika,
Mungu aliubuni ulimwengu na kuipanga historia, ikiwa ni pamoja na maisha yetu,
ili kwamba tuweze kuwa marafiki zake. Biblia inasema, “Aliumba
wanadamu wote na akaifanya nchi iweze kukalika, akaweka muda na nafasi vya
kutosha kwa kuishi ili tumtafute Mungu, na sio tu tutangatanga gizani lakini
tupate kumwona hakika.” Matendo 17:26-27 (Msg)
Kumjua na kumpenda Mungu ni upendeleo mkubwa kwetu, na kujulikana
na kupendwa na Mungu ni furaha kubwa kwa Mungu. Mungu anasema, “Kama
kuna watu wanaotaka kujisifu, basi wajisifu kwamba wananijua na kunifahamu ….
Haya ndio mambo yanifurahishayo.”Yeremia 9:24
(TEV)
Si rahisi kuelewa jinsi uhusiano wa karibu unawezekana kati ya
Mungu muweza wa yote, asiyeonekana, mkamilifu na mwanadamu ambaye ni kiumbe
kidogo na tena mwenye dhambi. Ni rahisi kuelewa uhusiano wa Bwana na mtumishi
au muumba na kiumbe au hata uhusiano wa Baba na mtoto. Lakini ina maana gani
Mungu anaponitaka niwe rafiki zake? Kwa kuyachunguza maisha ya marafiki za
Mungu katika Biblia, tunajifunza siri sita za urafiki na Mungu. Katika surahii,
utaona sura mbili na zile nne tutaziangalia katika sura ifuatayo.
KUWA RAFIKI MKUBWA WA MUGU
Kwa
njia ya mazungumzo ya daima. Huwezi kamwe kuwa na
uhusiano wa karibu na Mungu kwa kuhudhuria Kanisani mara moja tu kwa wiki au
hata kwa kuwa na muda wa kutulia mbele za Mungu kila siku. Urafiki unajengeka
kwa kumshirikisha mambo yako yote ya maisha.
Kumjua na kumpenda Mungu ni upendeleo mkubwa kwetu,
na kujulikana na kupendwa na Mungu ni furaha kubwa kwa Mungu.
|
Kwa kweli, ni muhimu kuwa na muda kila siku wa kujitoa mbele
za Mungu, (Angalia, “Jinsi ya kuwa na wakati wa kimya Wenye Manufaa” ndani ya kanuni za kujisomea Biblia Binafsi, Rick Warren, 1981,
kutoka www.pastors.com)
Lakini unahitaji zaidi ya muda huo wa kwenye ratiba yako. Anahitaji kuhusishwa
katika kila kazi, kila mazungumzo, kila tatizo, na hata kila wazo. Unaweza kuwa
na mazungumzo ya moja kwa moja naye kwa siku nzima, ukiongea naye kuhusu kila
unachofanya au kufikiri kwa muda huo. “Kuomba bila kukoma” (1 Wathesalonike
5:17) maana yake ni kuzungumza na Mungu wakati ukiwa dukani, unaendesha gari,
au unafanya kazi yoyote ya kila siku.
Watu wengi hudhani “kuwa na mudana Mungu” humaanisha kuwa peke yako na
Mungu. Ni kweli, kama Yesu alivyotoa kielelezo, unahitaji muda peke yako na
Mungu, lakini huo ni sehemu tu ya masaa yako ya kukesha. Kila kitu
unachofanya chaweza kuwa “muda pamoja na Mungu” kama akikaribishwa kushiriki na
wewe ukautambua uwepo wake.
Kitabu cha kisasa kinachohusu kujifunza kukuza mazungumzo ya
daima na Mungu kinaitwa “Kujizoeza Uwepo wa
Mungu”. Kiliandikwa katika karne ya kumi na saba na Brother
Lawrence, mpishi katika nyumba ya watawa Ufaransa. Brother Lawrence aliweza
kugeuza hata maeneo ya kawaida na shughuli ndogo ndogo, kama vile kupika na
kuosha vyombo, kuwa matendo ya sifa na ushirika na Mungu. Ufunguo wa urafiki na
Mungu, alisema, siyo kubadili unachofanya, lakini kubadili nia ya ndani kuhusu
unachofanya, kili unachofanya kwa ajili yako sasa unakifanya kwa ajili ya Mungu,
iwe ni kula, kuoga, kufanya kazi, kupumzika, au kutupa taka.
Siku hizi tunajisikia lazima “tutoke” katika kazi zetu za
kila siku ili kumwabudu Mungu, lakini hiyo ni kwa sababu hatujajifunza
kujizoeza uwepo wake wakati wote. Brother Lawrence aliona jambo hili kwa rahisi
la kumwabudu Mungu kwa kazi za kawaida maishani; hakuhitaji kwenda mahali maalum
kwa ajili ya mambo ya kiroho.
Hili ndilo kusudi la Mungu. Kule Edeni, kuabudu halikuwa
tukio la kuhudhuria, lakini hali ya daima; Adamu na hawa walikuwa na ushirika
wa daima na Mungu. Kwa sababu Mungu yu pamoja nawe wakati wote, hakuna sehemu
iliyo karibu naye kuliko hapo ulipo sasa hivi. Biblia ina sema, “Anatawala kila kitu na yuko kila mahali na yuko ndani
katika kila kitu.” Waefeso 4:6b (NCV)
Wazo jingine la msaada toka kwa Brother Lawrence lilikuwa
kusali sala fupi za kimazungumzo daima mara kwa mara katika siku badala ya
kujaribu kusali kwa muda mrefu sala ngumu. Ili kuwa na mwelekeo mmoja na
kuepuka mawazo mbali mbali, alisema, “sikushauri kutumia maneno mengi katika
sala, kwa kuwa maneno mengi mara nyingi ni chanzo cha kutangatanga.” Brother
Lawrence, Mazoezi ya uwepo wa Mungu (Grand Rapids: Revell/Spire Books, 1967), Barua ya Nane.
Katika kipindi hiki ambacho hakuna muda wa kutulia, ushauri huu uliotolewa
miaka 450 unaonekana kuwa wa muhimu na wa kufaa sana.
Kila kitu
unachofanya chaweza kuwa “muda na Mungu” kama akikaribishwa kushiriki na
wewe ukatambua uwepowake.
|
Biblia inatuambia, “kusali
bila kukoma.” 1 Wathesalonike 5:17
(Msg) Je, inawezekana vipi kufanya hivi? Njia moja wapo ni kutumia “sala za
pumzi” katika siku nzima, kama wakristo wengi wamefanya kwa karne nyingi. Unachagua
sentensi fupi au maneno machache yanayoweza kurudiwa mbele za Yesu kwa pumzi
moja: “Uko nami.”“Napokea neema yako.”“Nakutegemea.”“Kwangu kuishi ni Kristo.”“Hutaniacha
kamwe.”“Wewe ni Mungu wangu.” Sali sentensi hii fupi mara kwa mara ikae moyoni
mwako. Hakikisha kwamba nia yako ni kumheshimu Mungu na siyo kumtawala.
Kujizoeza uwepo wa Mungu ni ujuzi, tabia ambayo unaweza
kuijenga. Kama vile wanamuziki wanavyofanya mazoezi kila siku ili waimbe muziki
mzuri kwa wepesi, ni lazima ujilazimishe kufikiri juu ya Mungu kwa Nyakati
mbali mbali katika siku nzima. Ni lazima ufundishe akili yako kumkumbuka Mungu.
Mwanzoni itakubidi utengeneze vitu vya kukukumbusha daima
kwamba Mungu yupo pamoja nawe kwa wakati huo. Anza kwa kuweka vitu
vinavyoonekana ili kukukumbusha. Unaweza kuweka ukutani maandishi yanayosema, “Mungu yuko nami na yupo kwa ajili yangu sasa hivi.”
Watawa wabenedictine hutumia kengele ya saa kuwakumbusha kutulia na kusali “sala
ya kila saa.” Kama una saa au simu ya mkononi yenye kengele, unaweza kufanya
hivyo hivyo. Mara nyingine unahisi uwepo wa Mungu; wakati mwingine hutaweza.
Kama unatafuta kuhisi uwepo wake kwa kupitia haya yote, basi
umekosa maana halisi. Hatumsifu Mungu ili tujisikie vizuri, lakini tutende mema. Lengo lako siyo
hisia, lakini ufahamu wa wakati wote wa ukweli kwamba Mungu yupo wakati wote.
Haya ndiyo maisha ya kuabudu.
Kwa
njia ya kutafakari daima. Njia ya pili ya kujenga
urafiki na Mungu ni kwa kufikiri juu ya neno lake siku nzima. Hii huitwa
kutafakari, na Biblia hutushauri kutafakari kuhusu Mungu ni nani, amefanya
nini, na amesema nini. (Zaburi 23:4; 143:5; 145:5; Yoshua 1:8; Zaburi 1:2).
Haiwezekani kuwa rafikiwa Mungubila kufahamu asemayo. Huwezi
kumpenda Mungu mpaka umjue, na huwezi kumjua bila kujua neno lake. Biblia
inasema Mungu “Alijifunua kwa Samueli kwa kupitia
neno lake.” (1 Samueli 3:21) Mungu bado anatumia njia hiyo siku hizi.
Ingawa huwezi ukatumia siku nzima kusoma Biblia, unaweza
kufikiri juu yake siku nzima, ukikumbuka vifungu ulivyosoma au kukariri na
kuanza kuvitafakari akilini mwako.
Kutafakari ni jambo ambalo watu wengi hawalielewi na kudhani
kuwa ni jambo fulani la kiibada lililo gumu na la siri fulani ambalo hufanywa
na watawa wajitengao wa watu. Lakini kutafakari ni kufikiri kwa mwelekeo mmoja –
ujuzi ambao mtu yeyote anaweza kujifunza na kuutumia popote.
Unapofikiri juu ya tatizo tena na tena katika akili yako,
hiyo ni hofu. Unapofikiri juu ya neno la Mungu tena na tena, huko ni
kutafakari. Kama unajua namna ya kuhofu, tayari unajua namna ya kutafakari!
Unatakiwa kubadili mwelekeo wako kutoka kwenye matatizo yako na kwenda kwenye
vifungu vya Biblia. Kadiri unapotafakari neno la Mungu, ndivyo na hofu yako
inavyopungua.
Sababu iliyomfanya Mungu awaone Ayubu na Daudi kuwa rafiki
zake wa karibu ni kwamba walithamini neno la Mungu kuliko chochote kile, na
walilitafakari daima siku nzima. Ayubu alikiri, “Nimeyatunza
maneno ya kinywa chake kuliko mkate wangu wa kila siku.” Ayubu 23:12 (NIV) Daudi alisema, “Jinsi gani ninavyoipenda sheria yako! Naitafakari mchana
kutwa.” Zaburi 119:27 (NIV) “Nayatafakari
daima. Siwezi kuacha kuyafikiri.”
Zaburi 77:12 (NLT)
Marafiki hushirikishana siri, na Mungu atakushirikisha siri
zake kama utajenga tabia ya kutafakari neno la lake siku nzima. Mungu
alimwambia Ibrahimu siri zake, na alifanya hivyo pia kwa Daudi, Paulo,
wanafunzi wake, na marafiki wengine. (Mwanzo 18:17; Danieli 2:19; 1 Wakorintho
2:7-10).
Unaposoma Biblia yako au ukasikiliza mahubiri au kanda,
usisahau na kuondoka. Jenga tabia ya kutathmini ukweli akilini mwako, ufikiri
tena na tena. Kadiri unapotumia muda mwingi kutathmini Mungu alichosema, ndipo
utakapoelewa zaidi “siri” za maisha haya ambazo watu wengi hawana. Biblia
inasema, “Urafiki na Mungu ni kwa ajili ya
wale wanaomheshimu. Ni hao tu ndio anaowashirikisha siri za ahadi zake.” Zaburi 25:14 (LB)
Siku
ya Kumi naMbili: Kukuza Urafiki Wako Na Mungu
Yeye
hufanya urafiki na watauwa
Mithali 3:32 (NLT)
Mkaribieni
Mungu, naye Mungu atawakaribia ninyi.
Yakobo
4:8 (NLT)
Unakuwa karibu na Mungu kulingana na unavyochagua kuwa.
Kama urafiki mwingine wowote, ni lazima ujitahidi kuukuza
urafiki wako na Mungu. Haiwezi kutokea tu kwa bahati, inahitaji nia, muda na
nguvu. Kama unataka uhusiano wa kina na Mungu lazima ujifunze kumshirikisha
wazi hisia zako, kumwamini anapokutaka ufanye kitu fulani, jifunze kujali mambo
anayoyajali, na utamani urafiki wake kuliko kitu kinginecho.
Lazima
nichague kuwa mwaminifu kwa Mungu.
Tofali la kwanza la kujenga urafiki wa kina na Mungu ni uaminifu wa kweli
kuhusu makosa na hisia zako. Mungu hakutegemei wewe kuwa mkamilifu, lakini
anasisitiza uaminifu wa kweli. Hakuna rafiki yoyote wa Mungu katika Biblia
aliyekuwa mkamilifu. Kama ukamilifu kingekuwa kigezo cha kuwa rafiki wa Mungu,
haingewezekana kwetu kuwa rafiki zake, lakini kwa sababu ya neema ya Mungu,
Yesu bado ni “rafiki wa wenye dhambi.” Mathayo 11:19
Katika Biblia marafiki wa Mungu walikuwa waaminifu kuhusu
hisia zao, mara nyingi walilalamika, walikisia, walilaumu, na kubishana na
Mungu wao. Mungu hata hivyo hakuonekana kuudhiwa na uwazi huu, badala yake
alichochea hali hiyo.
Mungu alimruhusu Ibrahimu kuuliza kutoa changamoto kuhusu
maangamizi ya mji wa Sodoma, Ibrahimu alijadili na Mungu kuhusu kilichotakiwa
ili kutokuangamiza mji, akajadili na Mungu toka watu hamsini mpaka watu kumi.
Mungu pia alimsikiliza kwa uvumilivu Daudi katika lawama zake nyingi za
kumnyima haki, kusalitiwa na kuachwa. Mungu hakumuua Yeremia alipodai kuwa
Mungu amemfanyia ujanja. Ayubu aliruhusiwa kutoa uchungu wake katika mateso na
hatimaye Mungu alimtetea kwa kuwa mwaminifu, na akawakemea rafiki za Ayubu kwa
kutokuwa wakweli. Mungu aliwaambia, “Hamkuwa
waaminifu kwangu wala juu yangu – sivyo rafiki yangu alivyofanya … Rafiki yangu
Ayubu sasa atawaombea na nitapokea maombi yake.”
Ayubu 42:7 (Msg)
Katika mfano mmoja wa ajabu wa urafiki ulio wazi (Kutoka
33:1-17), Mungu alionyesha kuchukizwa kwake kabisa na uasi wa Israeli.
Alimwmbia Musa kwamba angeitunza ahadi yake ya kuwapatia Israeli nchi ya ahadi,
lakini asingeweza kuendelea nao zaidi jangwani! Mungu alikuwa amechoshwa, na
alimjulisha wazi Musa alivyokuwa anajisikia.
Mungu hategemei wewe kuwa mkamilifu lakini
anasisitiza uaminifu wa kweli.
|
Musa akizungumza kama “rafiki” wa Mungu alijibu: “Tazama unaniambia
kuongoza watu hawa lakini hunijulishi nani utamtuma kwenda nami … kama mimi ni
wa muhimu kwako, basi nijulishe mipango yako … kama uwepo wako hautatuongoza,
basi simamisha safari hii sasa hivi! Je nitajuaje uko pamoja na mimi katika
hili, mimi pomoja wa watu wako? Je utaenda nasi au la? … Mungu akamwambia Musa,
‘Vyema. Kama unavyosema; hili pia nitalifanya, kwa kuwa nakujua vyema na wewe
ni mtu wa muhimusana kwangu.’”Kutoka 33:12-17 (Msg)
Je, Mungu anaweza kuchukuliana na uaminifu wako wa kina na
wa wazi? Bila shaka! Urafiki wa kweli umejengwa kwenye uwazi. Kile kinachoweza
kuonekana kama ufidhuli Mungu anauona kuwa ukweli. Mungu husikiliza maneno ya
uwazi ya rafiki zake; anachoshwa na maneno yale yale ya kiunyenyekevu ya
kidini. Kuwa rafiki wa Mungu ni lazima uwe mwaminifu kwa Mungu, ukimshirikisha
hisia zako kikweli, siyo unavyodhani unapaswa kuhisi au kusema.
Uchungu ni kikwazo kikubwa cha urafiki na Mungu.
|
Wakati mwingine inabidi kutubu hasira na chuki vilivyofichika
dhidi ya Mungu kwa maeneo fulani ya maisha yako uliyofikiri umedanganywa au
kukatishwa tamaa. Mpaka tutakapopevuka kufikia kuelewa vile Mungu hutumia kila kitu kutupa mema maishani mwetu,
tutaendelea kutunza chuki dhidi ya Mungu kuhusu sura zetu, mazingira yetu ya
nyuma, maombi ambayo hayakujibiwa, maumivu ya nyuma, na mambo mengine ambayo
tungeyabadilisha kama tungekuwa Mungu. Watu mara nyingi humlaumu Mungu kwa
maumivu yanayosababishwa na watu wengine. Hii inatengeneza kile William Backus
anaita “ufa uliofichika kati yako na Mungu.”
Uchungu ni kikwazo kikubwa cha urafiki na Mungu: kwa nini
nitamani kuwa rafiki wa Mungu kama aliruhusu jambo hili? Dawa, kwa kweli, ni kuelewa kwamba Mungu siku zote hutenda
yote ili kukupa mema. Hata kama inaumiza na huelewi jambo hilo. Lakini
kuachilia chuki na kudhihirisha hisia zako ni hatua ya kwanza kuelekea
uponyaji. Kama watu wengi wa Biblia walivyofanya, mwambie Mungu wazi
unavyojisikia. Fikiria Ayubu (Ayubu 7:17-21), Asafu (Zaburi 83:13), Yeremia
(Yeremia 20:7), Naomi (Ruth 1:20).
Ili kutupa mwongozo dhahiri kuhusu uaminifu, Mungu alitupa
kitabu cha zaburi – kitabu cha ibada, kilichojaa makelele, kupayukapayuka,
mashaka, hofu, chuki, shauku zenye kujaa shukrani, sifa na kauli za imani. Kila
aina ya hisia imo katika Zaburi. Unaposoma toba za Daudi na wengine, elewa
kwamba hivi ndivyo Mungu anapenda umwabudu – usizuie chochote unavyojihisi.
Unaweza kusali kama Daudi, “Natoa manung’uniko
yangu mbele zake na kumwambia mateso yangu yote. Kwa kuwa mimezidiwa.”
Zaburi 142:2 (NLT)
Inatia moyo kwamba marafiki wote wa Mungu – Musa, Daudi,
Ibrahimu, Ayubu na wengine – walikabiliwa na mashaka. Lakini badala ya kuigiza
kwa namna ya kidini tu, walisema wazi na hadharani. Kuelezea mashaka yako
wakati mwingine ni hatua ya kwanza kuelekea kiwango kingine cha uhusiano na
Mungu.
Ni
lazima nichague kumtii Mungu katika Imani.
Kila wakati unapoamini hekima ya Mungu na kufanya kila analosema, hata pale
unapokuwa huelewi, unakuza urafiki wako na Mungu. Mara nyingi hatufikiri utii
kama sifa ya urafiki; huo ni kwa ajili ya uhusiano na mzazi, mkubwa wa kazi,
siyo kwa rafiki. Lakini, Yesu aliweka wazi kwamba utii ni kigezo cha uhusiano
na Mungu. Alisema, “Ninyi ni rafiki zangu kama mtafanya ninayowaamuru.” Yohana
15:14 (NIV)
SIKU
YA KUMI NA MBILI:
KUKUZA URAFIKI NA MUNGU
|
Katika sura iliyopita nilisema kwamba neno alilolitumia Yesu
alipotuita “rafiki” laweza kumaanisha “marafiki wa mfalme,” katika baraza la
kifalme. Wakati hawa marafiki wana upendeleo maalum, walikuwa bado chini ya
mfalme na walipaswa kutii amri zake. Sisi ni marafiki na Mungu, lakini sisi
siyo sawa na Yeye. Yeye ni kiongozi wetu atupendaye, na tunamfuata.
Tunamtii Mungu, si kama wajibu au kwa hofu au kwa
kushurutishwa, lakini kwa sababu tunampenda na tunaamini kwamba anajua kile
kilicho bora kwetu. Tunataka kumfuata Kristo kwa shukrani kwa yote
aliyotufanyia, na tunapomfuata kwa karibu, ndipo urafiki wetu naye unakuwa wa
kina zaidi.
Wasioamini mara niyingi hudhani kwamba Wakristo hutii kwa
sababu ni wajibu, au kuogopa lawama, au kuogopa hukumu, lakini ukweli ni kinyume
cha hayo. Kwa sababu tumesamehewa na kuwekwa huru, tunatii kwa upendo – na utii
wetu hutuletea furaha kubwa! Yesu alisema, “Nimewapenda
kama vile Baba alivyonipenda. Kaeni katika pendo langu. Mnaponitii mnakaa
katika pendo langu, kama ninavyomtii Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
Nimewaambia haya ili mjazwe na furaha yangu. Ndiyo, furaha yenu itafurika!” Yohana 15:9-11 (NLT)
Angalia jinsi ambavyo Yesu anatutazamia kufanya yale tu
aliyoteda kwa Baba yake. Uhusiano wake na Baba yake ni Kielelezo kwa uhusiano
wetu naye. Yesu alifanya chochote Baba alichomwagiza kufanya – kwa upendo.
Urafiki wa kweli si wa kukaa tu ni wa vitendo. Yesu
anapotuagiza kuwapenda wengine, kusaidia wahitaji, kuwagawia wengine mali zetu,
kuwa na maisha safi, kusamehe, na kuleta wengine kwake, upendo hutuchochea
kutii mara moja.
Mara nyingi tunapewa changamoto la kumfanyia Mungu “mambo makubwa.”
Ni bayana kwamba Mungu anafurahishwa zaidi tunapotenda mambo madogo madogo kwa
ajili yake kutokana na utii wa upendo. Yawezekana kuwa hayonekani kwa wengine,
lakini Mungu anayaona na kuyahesabu kuwa matendo ya kuabudu.
Nafasi kubwa inaweza kutokea mara moja katika maisha, lakini
nafasi ndogo ndogo zinatuzunguka kila siku. Hata katika matendo madogo kama
vile kusema kweli, kuonyesha wema, kuwatia moyo wengine, tunaleta tabasamu
katika uso wa Mungu. Mungu anathamini matendo rahisi tu ya utii kuliko sala
zetu, sifa na sadaka. Biblia inatuambia, “Kinachompendeza
Mungu zaidi ni nini? Je, ni dhabihu za kutekezwa na sadaka au kutii sauti yake?
Nibora kutii kuliko sadaka.” 1 Samweli 15:22 (NCV)
Yesu alianza huduma yake ya hadharani katika umri wa miaka
thelathini kwa kubatizwa na Yohana. Katika tukio hilo Mungu alizungumza kutoka
mbinguni, “Huyu ni mwanangu mpendwa na
ninapendezwa naye.” Mathayo 3:17 (NLT) Je,
Yesu alikuwa anafanya nini kwa miaka thelathini ambacho kilimfurahisha Mungu?
Bablia haisemi kitu huhusu miaka hiyo iliyofichika, isipokuwa kwa maneno
machache katika Luka 2:51: “Alirudi Nazareti nao
na akaishi kwa kuwatii” (Msg). Miaka thelathini
ya kumpendeza Mungu ilijumuishwa katika maneno: “Akaishi
kwa kuwatii.”
Ni
lazima nichague kuthamini mambo Mungu anayoyathamini. Hivyo ndivyo marafiki hufanya – wanajali kile ambacho ni cha
muhimu kwa mwenzake. Unapozidi kuwa rafiki wa Mungu, ndivyo utakavyozidi kujali
mambo anayoyajali, kusikitika kwa mambo anayosikitikia, na kufurahia mambo
yanayomletea furaha.
Paulo ni mfano wa hili. Mjadala wa Mungu ndio ulikuwa
mjadala wake, na shauku ya Mungu ilikuwa shauku yake; “Jambo linalonilemea moyo ni kwamba ninawajali ninyi sana
– hii ni shauku ya Mungu ikiwaka ndani yangu!”
2 Wakorintho 11:2 (Msg) Daudi alijisikia namna hiyo hiyo: “Shauku ya nyumba yako inawaka ndani yangu, hivyo
wanaokutukana wananitukana na mimi pia.”
Zaburi 69:9 (NLT)
Je, Mungu anajali nini zaidi? Ukombozi wa watu wake.
Anapenda watoto wake wote waliopotea warudi! Hiyo ndiyo sababu kuu ya Yesu kuja
duniani. Jambo la thamani sana kwenye moyo wa Mungu ni kifo cha mwanae. Jambo
la pili la thamani ni pale watoto wake wanaposhirikisha wengine habari hizo.
Kuwa rafiki wa Mungu ni lazima uwajali watu wote wanaokuzunguka ambao Mungu
anawajali. Marafiki wa Mungu wanawaeleza rafiki zao kuhusu Mungu.
Unapozidi kuwa fafiki wa Mungu nidivyo utakavyozidi
kujali mambo anayoyajali.
|
Ni
lazima nitamani urafiki na Mungu kuliko kitu chochote. Zaburi zimejaa mifano mingi ya shauku hii. Daudi alikuwa na
shauku kubwa ya kumjua Mungu kuliko vitu vyote; alitumia maneno kama vile
kutamani, kuwa na shauku, kuwa na kiu, kuwa na njaa. Alimhitaji Mungu. Alisema,
“Jambo ninalolitafuta zaidi ni ule upendeleo wa kutafakari
hekaluni mwake, kuishi katika uwepo wake siku zote za maisha yangu. Niufurahie
ukamilifu na utukufu wake usiopimika.” Zaburi 63:3 (LB)Katika zaburi nyingine alisema, “Upendo wako wamaanisha zaidi ya uzima kwangu.”
Zaburi 63:3 (CEV)
Shauku ya Yakobo kwa ajili ya baraka za Mungu katika maisha
yake ilikuwa kubwa sana kiasi kwamba alipigana na Mungu usiku kucha, “Sitakuachaia uende mpaka unibariki.”
Mwanzo 32:26 (NIV) Sehemu ya kushangaza ya hadithi hiyo ni kwamba, Mungu mweza
yote alimruhusu Yakobo ashinde! Mungu haudhiwi tunaposhindana naye, kwa sababu
pambano hilo huhitaji kugusana ana kwa ana na hutuleta karibu naye. Pia ni kazi
yenye shauku, na Mungu anapenda hivyo tunapokuwa na shauku naye.
Paulo ni mtu mwingine aliyekuwa na shauku ya kuwa na urafiki
na Mungu. Hakuna kilichokuwa na maana kwake; Hili ndilo lilikuwa jambo la
kwanza kwake, mwelekeo mzima, na lengo kuu la maisha yake. Ndiyo maana Mungu
alimtumia Paulo kwa kiwango kikubwa sana. Tafsiri ya Biblia iitwayo Amplified
huueleza vizuri msukumo wa shauku ya Paulo, “Lengo
langu kubwa ni kwamba nimjue yeye – ili hatua kwa hatua nimjue kwa kina na kwa
karibu sana, nikitambua na kuelewa na kufahamu maajabu yanafsi yake kwa kina na
kwa uwazi.” Filipi 3:10 (Amp)
Ukweli ni kwamba – unakuwa karibu na Mungu kulingaza
unavyochagua. Urafiki wa karibu na Mungu ni uchaguzi, si bahati tu. Ni lazima
uutafute kwa makusudi. Je, kweli unauhitaji urafiki huu – kuliko chochote kile?
Je, kuna faida gani kwako? Je, kuna faida kuacha mengine? Je, unastahili kutia
bidii kujenga tabia na ujuzi unaohitajika?
Yawezekana ulikuwa na shauku ya Mungu siku zilizopita lakini
umepoteza haja hiyo. Hilo lilikua tatizo la Wakristo kule Efeso – walikuwa
wameacha upendo wao wa kwanza. Walifanya mambo yote sahihi, kwa kutimizawajibu,
na siyo kwa upendo. Kama umekuwa katika hali ya hisia tu kiroho, usishangae
Mungu akiruhusu maumivu katika maisha yako.
Maumivu ni kichocheo cha shauku – hututia nguvu kwa
kuchochea badiliko ambalo kwa kawaida hatunalo. C.S. Lewis alisema, “Maumivu ni
kipaza sauti cha Mungu.” Ni njia ya Mungu ya kutuamsha katika usingizi wa
kiroho. Matatizo yako si adhabu; ni miito ya kukuamsha kutoka kwa Mungu wa upendo.
Mungu hajakukasirikia; anasumbuka kwa ajili yako, atafanya kila awezalo ili
kukurudisha katika ushirika naye. Lakini kuna njia rahisi ya kuwasha upya
shauku yako kwa ajili ya Mungu: Anza kumwomba Mungu akupatie, na endelea
kumwomba mpaka umepata. Omba hivi kwa siku nzima: “Mpendwa Yesu, zaidi ya
chochote kile, nataka kukujua wewe kwa ukaribu sana. “Mungu aliwaambia mateka
wa babeli, “Mtanitafuta kwa bidii na mtamani
jambo hilo kuliko chochote kile, nitahakikisha hamkatishwi tamaa.” Yeremia 29:13 (Msg)
UHUSIANO
MUHIMU ZAIDI KWAKO
SIKU YA KUMI NA MBILI
KUFIKIA JUU YA LENGO LANGU
Jambo la Kutafakari: Ninakuwa karibu na Mungu kulingana
na ninavyochagua.
Kaifungu cha Kumbukumbu:“Mkaribieni
Mungu na Munguatawakaribieni.”
Yakobu 4:8a (NLT)
Swali la kujiuliza: Je, ni mambo gani ninayoweza
kuchagua kuyafanya leo ili niweze kuwa karibu na Mungu?
|
Hakuna chochote – hakuna kabisa – kilicho cha muhimu kuliko
kukuza uhusiano na Mungu. Ni uhusiano utakaodumu milele. Paulo alimwambia
Timotheo, “baadhi ya watu hawa wanakikosa
kitu cha muhimu sana katika maisha – hawamjui Mungu.”
1Timotheo 6:21a (LB) Je, umekuwa ukikosa kitu cha muhimu zaidi maishani?
Unaweza kufanya kitu fulani kuanzia sasa. Kumbuka ni uchaguzi wako. Unakuwa
pamoja na Mungu kulingana na unavyochagua.
SIKU YA
KUMI NA MOJA
KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU
Jambo la kutafakari: Mungu aapenda kuwa rafiki yangu
mkubwa.
Kifungu cha Kukumbuka:“Urafiki
na Mungu ni kwa ajili ya wale wanaomheshimu.” Zaburi 25:14a (LB)
Swali la Kujiuliza: Je, naweza kufanya nini ili
kujikumbusha kuhusu Mungu na kusema naye mara kwa mara siku nzima?
Siku
ya Kumi naMbili: Kukuza Urafiki Wako Na Mungu |
Yeye
hufanya urafiki na watauwa
Mithali 3:32 (NLT)
Mkaribieni
Mungu, naye Mungu atawakaribia ninyi.
Yakobo
4:8 (NLT)
Unakuwa karibu na Mungu kulingana na unavyochagua kuwa.
Kama urafiki mwingine wowote, ni lazima ujitahidi kuukuza
urafiki wako na Mungu. Haiwezi kutokea tu kwa bahati, inahitaji nia, muda na
nguvu. Kama unataka uhusiano wa kina na Mungu lazima ujifunze kumshirikisha
wazi hisia zako, kumwamini anapokutaka ufanye kitu fulani, jifunze kujali mambo
anayoyajali, na utamani urafiki wake kuliko kitu kinginecho.
Lazima
nichague kuwa mwaminifu kwa Mungu.
Tofali la kwanza la kujenga urafiki wa kina na Mungu ni uaminifu wa kweli
kuhusu makosa na hisia zako. Mungu hakutegemei wewe kuwa mkamilifu, lakini
anasisitiza uaminifu wa kweli. Hakuna rafiki yoyote wa Mungu katika Biblia
aliyekuwa mkamilifu. Kama ukamilifu kingekuwa kigezo cha kuwa rafiki wa Mungu,
haingewezekana kwetu kuwa rafiki zake, lakini kwa sababu ya neema ya Mungu,
Yesu bado ni “rafiki wa wenye dhambi.” Mathayo 11:19
Katika Biblia marafiki wa Mungu walikuwa waaminifu kuhusu
hisia zao, mara nyingi walilalamika, walikisia, walilaumu, na kubishana na
Mungu wao. Mungu hata hivyo hakuonekana kuudhiwa na uwazi huu, badala yake
alichochea hali hiyo.
Mungu alimruhusu Ibrahimu kuuliza kutoa changamoto kuhusu
maangamizi ya mji wa Sodoma, Ibrahimu alijadili na Mungu kuhusu kilichotakiwa
ili kutokuangamiza mji, akajadili na Mungu toka watu hamsini mpaka watu kumi.
Mungu pia alimsikiliza kwa uvumilivu Daudi katika lawama zake nyingi za
kumnyima haki, kusalitiwa na kuachwa. Mungu hakumuua Yeremia alipodai kuwa
Mungu amemfanyia ujanja. Ayubu aliruhusiwa kutoa uchungu wake katika mateso na
hatimaye Mungu alimtetea kwa kuwa mwaminifu, na akawakemea rafiki za Ayubu kwa
kutokuwa wakweli. Mungu aliwaambia, “Hamkuwa
waaminifu kwangu wala juu yangu – sivyo rafiki yangu alivyofanya … Rafiki yangu
Ayubu sasa atawaombea na nitapokea maombi yake.”
Ayubu 42:7 (Msg)
Katika mfano mmoja wa ajabu wa urafiki ulio wazi (Kutoka
33:1-17), Mungu alionyesha kuchukizwa kwake kabisa na uasi wa Israeli.
Alimwmbia Musa kwamba angeitunza ahadi yake ya kuwapatia Israeli nchi ya ahadi,
lakini asingeweza kuendelea nao zaidi jangwani! Mungu alikuwa amechoshwa, na
alimjulisha wazi Musa alivyokuwa anajisikia.
Mungu hategemei wewe kuwa mkamilifu lakini
anasisitiza uaminifu wa kweli.
|
Musa akizungumza kama “rafiki” wa Mungu alijibu: “Tazama unaniambia
kuongoza watu hawa lakini hunijulishi nani utamtuma kwenda nami … kama mimi ni
wa muhimu kwako, basi nijulishe mipango yako … kama uwepo wako hautatuongoza,
basi simamisha safari hii sasa hivi! Je nitajuaje uko pamoja na mimi katika
hili, mimi pomoja wa watu wako? Je utaenda nasi au la? … Mungu akamwambia Musa,
‘Vyema. Kama unavyosema; hili pia nitalifanya, kwa kuwa nakujua vyema na wewe
ni mtu wa muhimusana kwangu.’”Kutoka 33:12-17 (Msg)
Je, Mungu anaweza kuchukuliana na uaminifu wako wa kina na
wa wazi? Bila shaka! Urafiki wa kweli umejengwa kwenye uwazi. Kile kinachoweza
kuonekana kama ufidhuli Mungu anauona kuwa ukweli. Mungu husikiliza maneno ya
uwazi ya rafiki zake; anachoshwa na maneno yale yale ya kiunyenyekevu ya
kidini. Kuwa rafiki wa Mungu ni lazima uwe mwaminifu kwa Mungu, ukimshirikisha
hisia zako kikweli, siyo unavyodhani unapaswa kuhisi au kusema.
Uchungu ni kikwazo kikubwa cha urafiki na Mungu.
|
Wakati mwingine inabidi kutubu hasira na chuki vilivyofichika
dhidi ya Mungu kwa maeneo fulani ya maisha yako uliyofikiri umedanganywa au
kukatishwa tamaa. Mpaka tutakapopevuka kufikia kuelewa vile Mungu hutumia kila kitu kutupa mema maishani mwetu,
tutaendelea kutunza chuki dhidi ya Mungu kuhusu sura zetu, mazingira yetu ya
nyuma, maombi ambayo hayakujibiwa, maumivu ya nyuma, na mambo mengine ambayo
tungeyabadilisha kama tungekuwa Mungu. Watu mara nyingi humlaumu Mungu kwa
maumivu yanayosababishwa na watu wengine. Hii inatengeneza kile William Backus
anaita “ufa uliofichika kati yako na Mungu.”
Uchungu ni kikwazo kikubwa cha urafiki na Mungu: kwa nini
nitamani kuwa rafiki wa Mungu kama aliruhusu jambo hili? Dawa, kwa kweli, ni kuelewa kwamba Mungu siku zote hutenda
yote ili kukupa mema. Hata kama inaumiza na huelewi jambo hilo. Lakini
kuachilia chuki na kudhihirisha hisia zako ni hatua ya kwanza kuelekea
uponyaji. Kama watu wengi wa Biblia walivyofanya, mwambie Mungu wazi
unavyojisikia. Fikiria Ayubu (Ayubu 7:17-21), Asafu (Zaburi 83:13), Yeremia
(Yeremia 20:7), Naomi (Ruth 1:20).
Ili kutupa mwongozo dhahiri kuhusu uaminifu, Mungu alitupa
kitabu cha zaburi – kitabu cha ibada, kilichojaa makelele, kupayukapayuka,
mashaka, hofu, chuki, shauku zenye kujaa shukrani, sifa na kauli za imani. Kila
aina ya hisia imo katika Zaburi. Unaposoma toba za Daudi na wengine, elewa
kwamba hivi ndivyo Mungu anapenda umwabudu – usizuie chochote unavyojihisi.
Unaweza kusali kama Daudi, “Natoa manung’uniko
yangu mbele zake na kumwambia mateso yangu yote. Kwa kuwa mimezidiwa.”
Zaburi 142:2 (NLT)
Inatia moyo kwamba marafiki wote wa Mungu – Musa, Daudi,
Ibrahimu, Ayubu na wengine – walikabiliwa na mashaka. Lakini badala ya kuigiza
kwa namna ya kidini tu, walisema wazi na hadharani. Kuelezea mashaka yako
wakati mwingine ni hatua ya kwanza kuelekea kiwango kingine cha uhusiano na
Mungu.
Ni
lazima nichague kumtii Mungu katika Imani.
Kila wakati unapoamini hekima ya Mungu na kufanya kila analosema, hata pale
unapokuwa huelewi, unakuza urafiki wako na Mungu. Mara nyingi hatufikiri utii
kama sifa ya urafiki; huo ni kwa ajili ya uhusiano na mzazi, mkubwa wa kazi,
siyo kwa rafiki. Lakini, Yesu aliweka wazi kwamba utii ni kigezo cha uhusiano
na Mungu. Alisema, “Ninyi ni rafiki zangu kama mtafanya ninayowaamuru.” Yohana
15:14 (NIV)
SIKU
YA KUMI NA MBILI:
KUKUZA URAFIKI NA MUNGU
|
Katika sura iliyopita nilisema kwamba neno alilolitumia Yesu
alipotuita “rafiki” laweza kumaanisha “marafiki wa mfalme,” katika baraza la
kifalme. Wakati hawa marafiki wana upendeleo maalum, walikuwa bado chini ya
mfalme na walipaswa kutii amri zake. Sisi ni marafiki na Mungu, lakini sisi
siyo sawa na Yeye. Yeye ni kiongozi wetu atupendaye, na tunamfuata.
Tunamtii Mungu, si kama wajibu au kwa hofu au kwa
kushurutishwa, lakini kwa sababu tunampenda na tunaamini kwamba anajua kile
kilicho bora kwetu. Tunataka kumfuata Kristo kwa shukrani kwa yote
aliyotufanyia, na tunapomfuata kwa karibu, ndipo urafiki wetu naye unakuwa wa
kina zaidi.
Wasioamini mara niyingi hudhani kwamba Wakristo hutii kwa
sababu ni wajibu, au kuogopa lawama, au kuogopa hukumu, lakini ukweli ni kinyume
cha hayo. Kwa sababu tumesamehewa na kuwekwa huru, tunatii kwa upendo – na utii
wetu hutuletea furaha kubwa! Yesu alisema, “Nimewapenda
kama vile Baba alivyonipenda. Kaeni katika pendo langu. Mnaponitii mnakaa
katika pendo langu, kama ninavyomtii Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
Nimewaambia haya ili mjazwe na furaha yangu. Ndiyo, furaha yenu itafurika!” Yohana 15:9-11 (NLT)
Angalia jinsi ambavyo Yesu anatutazamia kufanya yale tu
aliyoteda kwa Baba yake. Uhusiano wake na Baba yake ni Kielelezo kwa uhusiano
wetu naye. Yesu alifanya chochote Baba alichomwagiza kufanya – kwa upendo.
Urafiki wa kweli si wa kukaa tu ni wa vitendo. Yesu
anapotuagiza kuwapenda wengine, kusaidia wahitaji, kuwagawia wengine mali zetu,
kuwa na maisha safi, kusamehe, na kuleta wengine kwake, upendo hutuchochea
kutii mara moja.
Mara nyingi tunapewa changamoto la kumfanyia Mungu “mambo makubwa.”
Ni bayana kwamba Mungu anafurahishwa zaidi tunapotenda mambo madogo madogo kwa
ajili yake kutokana na utii wa upendo. Yawezekana kuwa hayonekani kwa wengine,
lakini Mungu anayaona na kuyahesabu kuwa matendo ya kuabudu.
Nafasi kubwa inaweza kutokea mara moja katika maisha, lakini
nafasi ndogo ndogo zinatuzunguka kila siku. Hata katika matendo madogo kama
vile kusema kweli, kuonyesha wema, kuwatia moyo wengine, tunaleta tabasamu
katika uso wa Mungu. Mungu anathamini matendo rahisi tu ya utii kuliko sala
zetu, sifa na sadaka. Biblia inatuambia, “Kinachompendeza
Mungu zaidi ni nini? Je, ni dhabihu za kutekezwa na sadaka au kutii sauti yake?
Nibora kutii kuliko sadaka.” 1 Samweli 15:22 (NCV)
Yesu alianza huduma yake ya hadharani katika umri wa miaka
thelathini kwa kubatizwa na Yohana. Katika tukio hilo Mungu alizungumza kutoka
mbinguni, “Huyu ni mwanangu mpendwa na
ninapendezwa naye.” Mathayo 3:17 (NLT) Je,
Yesu alikuwa anafanya nini kwa miaka thelathini ambacho kilimfurahisha Mungu?
Bablia haisemi kitu huhusu miaka hiyo iliyofichika, isipokuwa kwa maneno
machache katika Luka 2:51: “Alirudi Nazareti nao
na akaishi kwa kuwatii” (Msg). Miaka thelathini
ya kumpendeza Mungu ilijumuishwa katika maneno: “Akaishi
kwa kuwatii.”
Ni
lazima nichague kuthamini mambo Mungu anayoyathamini. Hivyo ndivyo marafiki hufanya – wanajali kile ambacho ni cha
muhimu kwa mwenzake. Unapozidi kuwa rafiki wa Mungu, ndivyo utakavyozidi kujali
mambo anayoyajali, kusikitika kwa mambo anayosikitikia, na kufurahia mambo
yanayomletea furaha.
Paulo ni mfano wa hili. Mjadala wa Mungu ndio ulikuwa
mjadala wake, na shauku ya Mungu ilikuwa shauku yake; “Jambo linalonilemea moyo ni kwamba ninawajali ninyi sana
– hii ni shauku ya Mungu ikiwaka ndani yangu!”
2 Wakorintho 11:2 (Msg) Daudi alijisikia namna hiyo hiyo: “Shauku ya nyumba yako inawaka ndani yangu, hivyo
wanaokutukana wananitukana na mimi pia.”
Zaburi 69:9 (NLT)
Je, Mungu anajali nini zaidi? Ukombozi wa watu wake.
Anapenda watoto wake wote waliopotea warudi! Hiyo ndiyo sababu kuu ya Yesu kuja
duniani. Jambo la thamani sana kwenye moyo wa Mungu ni kifo cha mwanae. Jambo
la pili la thamani ni pale watoto wake wanaposhirikisha wengine habari hizo.
Kuwa rafiki wa Mungu ni lazima uwajali watu wote wanaokuzunguka ambao Mungu
anawajali. Marafiki wa Mungu wanawaeleza rafiki zao kuhusu Mungu.
Unapozidi kuwa fafiki wa Mungu nidivyo utakavyozidi
kujali mambo anayoyajali.
|
Ni
lazima nitamani urafiki na Mungu kuliko kitu chochote. Zaburi zimejaa mifano mingi ya shauku hii. Daudi alikuwa na
shauku kubwa ya kumjua Mungu kuliko vitu vyote; alitumia maneno kama vile
kutamani, kuwa na shauku, kuwa na kiu, kuwa na njaa. Alimhitaji Mungu. Alisema,
“Jambo ninalolitafuta zaidi ni ule upendeleo wa kutafakari
hekaluni mwake, kuishi katika uwepo wake siku zote za maisha yangu. Niufurahie
ukamilifu na utukufu wake usiopimika.” Zaburi 63:3 (LB)Katika zaburi nyingine alisema, “Upendo wako wamaanisha zaidi ya uzima kwangu.”
Zaburi 63:3 (CEV)
Shauku ya Yakobo kwa ajili ya baraka za Mungu katika maisha
yake ilikuwa kubwa sana kiasi kwamba alipigana na Mungu usiku kucha, “Sitakuachaia uende mpaka unibariki.”
Mwanzo 32:26 (NIV) Sehemu ya kushangaza ya hadithi hiyo ni kwamba, Mungu mweza
yote alimruhusu Yakobo ashinde! Mungu haudhiwi tunaposhindana naye, kwa sababu
pambano hilo huhitaji kugusana ana kwa ana na hutuleta karibu naye. Pia ni kazi
yenye shauku, na Mungu anapenda hivyo tunapokuwa na shauku naye.
Paulo ni mtu mwingine aliyekuwa na shauku ya kuwa na urafiki
na Mungu. Hakuna kilichokuwa na maana kwake; Hili ndilo lilikuwa jambo la
kwanza kwake, mwelekeo mzima, na lengo kuu la maisha yake. Ndiyo maana Mungu
alimtumia Paulo kwa kiwango kikubwa sana. Tafsiri ya Biblia iitwayo Amplified
huueleza vizuri msukumo wa shauku ya Paulo, “Lengo
langu kubwa ni kwamba nimjue yeye – ili hatua kwa hatua nimjue kwa kina na kwa
karibu sana, nikitambua na kuelewa na kufahamu maajabu yanafsi yake kwa kina na
kwa uwazi.” Filipi 3:10 (Amp)
Ukweli ni kwamba – unakuwa karibu na Mungu kulingaza
unavyochagua. Urafiki wa karibu na Mungu ni uchaguzi, si bahati tu. Ni lazima
uutafute kwa makusudi. Je, kweli unauhitaji urafiki huu – kuliko chochote kile?
Je, kuna faida gani kwako? Je, kuna faida kuacha mengine? Je, unastahili kutia
bidii kujenga tabia na ujuzi unaohitajika?
Yawezekana ulikuwa na shauku ya Mungu siku zilizopita lakini
umepoteza haja hiyo. Hilo lilikua tatizo la Wakristo kule Efeso – walikuwa
wameacha upendo wao wa kwanza. Walifanya mambo yote sahihi, kwa kutimizawajibu,
na siyo kwa upendo. Kama umekuwa katika hali ya hisia tu kiroho, usishangae
Mungu akiruhusu maumivu katika maisha yako.
Maumivu ni kichocheo cha shauku – hututia nguvu kwa
kuchochea badiliko ambalo kwa kawaida hatunalo. C.S. Lewis alisema, “Maumivu ni
kipaza sauti cha Mungu.” Ni njia ya Mungu ya kutuamsha katika usingizi wa
kiroho. Matatizo yako si adhabu; ni miito ya kukuamsha kutoka kwa Mungu wa upendo.
Mungu hajakukasirikia; anasumbuka kwa ajili yako, atafanya kila awezalo ili
kukurudisha katika ushirika naye. Lakini kuna njia rahisi ya kuwasha upya
shauku yako kwa ajili ya Mungu: Anza kumwomba Mungu akupatie, na endelea
kumwomba mpaka umepata. Omba hivi kwa siku nzima: “Mpendwa Yesu, zaidi ya
chochote kile, nataka kukujua wewe kwa ukaribu sana. “Mungu aliwaambia mateka
wa babeli, “Mtanitafuta kwa bidii na mtamani
jambo hilo kuliko chochote kile, nitahakikisha hamkatishwi tamaa.” Yeremia 29:13 (Msg)
UHUSIANO
MUHIMU ZAIDI KWAKO
SIKU YA KUMI NA MBILI
KUFIKIA JUU YA LENGO LANGU
Jambo la Kutafakari: Ninakuwa karibu na Mungu kulingana
na ninavyochagua.
Kaifungu cha Kumbukumbu:“Mkaribieni
Mungu na Munguatawakaribieni.”
Yakobu 4:8a (NLT)
Swali la kujiuliza: Je, ni mambo gani ninayoweza
kuchagua kuyafanya leo ili niweze kuwa karibu na Mungu?
|
Hakuna chochote – hakuna kabisa – kilicho cha muhimu kuliko
kukuza uhusiano na Mungu. Ni uhusiano utakaodumu milele. Paulo alimwambia
Timotheo, “baadhi ya watu hawa wanakikosa
kitu cha muhimu sana katika maisha – hawamjui Mungu.”
1Timotheo 6:21a (LB) Je, umekuwa ukikosa kitu cha muhimu zaidi maishani?
Unaweza kufanya kitu fulani kuanzia sasa. Kumbuka ni uchaguzi wako. Unakuwa
pamoja na Mungu kulingana na unavyochagua.
Katika sura inayofuata tutaona siri nyingine nne za kukuza
urafiki na Mungu, lakini usisubiri mpaka kesho. Anza leo kwa kujizoeza
kuzungumza na Mungu daima na kutafakari mara kwa mara Neno lake. Sala hukupa
nafsi ya kuzungumza kwa Mungu; kutafakari humpa Mungu kuzungumza kwako. Yote
mawili ni muhimu kwa wewe kuwa rafiki wa Mungu.





沒有留言:
張貼留言