LENGO LA 4
ULIUMBWA KUMTUMIKIA MUNGU
Sisi ni watumishi wa Mungu tu … kila –mmoja wetu anafanya
kazi
ile aliyopewa na Bwana kufanya. Mimi nilipanda mbegu,
Apolo akamwagilia maji, lakini Mungu ndiye aliyekuza
mmea.
1 Wakorintho 3:5-6 (TEV)
Siku ya Ishirini
na Tisa: Kupokea Jukumu Lako
Ni
Mungu mwenyewe aliyetufanya tuwe kama tulivyo na akatupatia
maisha
mapya kutoka kwa Yesu Kristo. Na tangu zamani sana
alipanga
kwamba tuyatumie maisha haya kwa kuwasaidia wengine.
Waefeso 2:10 (LB)
Nimekutukuza
ulimwenguni kwa kukamilisha kila kitu
cha
jukumu ulilonipa kufanya.
Yohana 17:4 (Msg)
Uliwekwa duniani kutoa mchango wako. Hukuumbwa ili kutumia
asilimali tu – kula, kupumua, na kuchukua nafasi. Mungu alikusanifu ili ufanye
tofauti kwa maisha yako. Wakati vitabu vingi vinavyonunuliwa sana vinatoa ushauri
juu ya “kupata”
zaidi kutokana na maisha yako, hiyo siyo sababu Mungu alikuumba. Uliumbwa uongeze katika maisha ya duniani, siyo tu kuchukua kutoka duniani. Mungu
anakutaka urudishe kitu fulani. Hili ndilo lengo la Mungu la nne kwa maisha
yako, na linaitwa “huduma” yako. Biblia inatupatia mambo kwa kina zaidi.
Uliumbwa
ili umtumikie Mungu. Biblia inasema, “Mungu
ametuumba kwa ajili ya maisha ya kazi njema, ambazo ameziandaa ili tuzifanye.” Waefeso 2:10b Hizi “kazi njema” ni huduma zako. Unapowahudumia
wengine katika njia yoyote, hakika unamtumikia Mungu (Wakolosai 3:23-24; Mathayo
25:34-45; Waefeso 6:7) na kutimiza moja ya malengo yako. Katika sura mbili
zifuatazo utaona jinsi Mungu alivyokuumba kwa uangalifu kwa kusudi hili. Mungu
alichomwambika Yeremia ni kweli kata kwako: “Kabla sijakuumba
katika tumbo la mama yako, nilikuchkagua. Kabla hujazaliwa, nilikutenga kwa
ajili ya kazi maalum.” Yeremia 1:5 (NCV) Uliwekwa
katika sayari hii kwa ajili ya jukumu maalum.
Uliokolewa
ili umtumikie Mungu. Biblia inasema, “Ni
Yeye aliyetuokoa na akatuchagua kwa ajili ya kazi yake takatifu, siyo kwa
sababu tunastahili lakini kwa sababu huo ulikuwa mpango wake.” 2 Timotheo 1:9 (LB) Mungu alikukomboa ili upate kufanya “kazi
yake takatifu.” Huokolewi kwa huduma, lakini umeokolewa ili uhudumu. Katika
ufalme wa Mungu, una sehemu, lengo, wajibu, na kazi ya kutimiza. Hii huyapa
maisha yako umuhimu na thamani kubwa.
SIKU
YA ISHIRINI NA TISA KUPOKEA JUKUMU LAKO |
Mtume Yohana alifundisha kwamba huduma yetu ya upendo kwa wengine
huonyesha kwamba kweli tumeokoka. Alisema, “Upendo wetu kwa wenzetu
huthibitisha kwamba tumevuka kutoka mautini na kuingia uzimani.” 1 Yohana 3:14 (CEV) Kama sina upendo kwa wengine, sina upendo wa
kuwatumika wengine, na ninajali tu mahitaji yangu, ni lazima nijiulize kama
kweli Kristo yuko maishani mwangu. Moyo uliookolewa ni ule unaotaka kutumika.
Neno jingine linalohusu kumtumikia Mungu ambalo linaeleweka vibaya
na watu wengi ni neno huduma
(ministry). Watu wengi wanaposikia “huduma” wanafikiri juu ya wachungaji,
mapadri, na watumishi wengine maalum makanisani, lakini Mungu anasema kila
mshirika wa jamii yake ni mhudumu. Katika Biblia, maneno mtumishi na mhudumu
yana maana moja, kama ilivyo kwa utumishi
(service) na huduma (ministry).
Kama wewe ni Mkristo, wewe ni mhudumu na unapotumika unahudumu.
Kama sina upendo kwa wengine, sina upendo wa
kuwatumikia wengine, ni lazima nijiulize kama kweli Kristo yuko maishani
mwangu. |
Je, umewahi kujiuliza kwa nini Mungu hatuchukui mbinguni mara tu
tunapookoka? Kwa nini anatuacha katika ulimwengu ulioanguka? Anatuacha hapa ili
kutimiza malengo yake. Unapookoka Mungu hukusudia kukutumia kwa malengo yake.
Mungu ana huduma kwa ajili yako katika kanisa lake na utume kwa ajili yako
duniani.
Umeitwa
kumtumikia Mungu. Wakati unakua, unaweza kuwa
umefikiri kwamba “kuitwa” na Mungu ni kitu ambacho kiliwapata tu wamishenari,
wachungaji, watawa, na watenda kazi wengine wa “kudumu” wa kanisa wenye uzoefu.
Lakini Biblia inasema kila Mkristo ameitw kutumika. (Waefeso 4:4-14; angalia
pia Warumi 1:6-7; 8:28-30; 1 Wakorintho 1:2, 9, 26; 7:17; Wafilipi 3:14; 1
Petro 2:9; 2Petro 1:3) Wito wako kwa wokovu ni pamoja na wito wako kwa huduma.
Ni jambo lilelile. Bila kujali kazi yako, umeitwa kwenye huduma ya Kikristo ya
kudumu. Mkristo “asiyetumika” yuko kinyume na wito wake.
Biblia inasema, “Alituokoa na kutuita ili tuwe watu
wake, si kwa sababu ya matendo tuliyofanya, lakini kwa sababu ya lengo lake.” 2 Timotheo 1:9 (TEV) Petro anaongeza, “Mliitwa
ili kuzitangaza sifa njema za Mungu aliyewaita.”
1 Petro 2:9 (GWT) Wakati wowote unapotumia uwezo uliopewa na Mungu kusaidia
wengine, unatimiza wito wako.
Biblia inasema, “Sasa ninyi ni watu wake … ili tuweze
kufaa katika utumishi wa Mungu.” Warumi 7:4
(TEV) Ni kwa muda gani wewe unafaa katika utumishi wa Mungu? Katika baadhi ya
makanisa kule China, wanakaribisha waamini wapya kwa kusema, “Sasa Yesu ana
macho mawili mapya ya kutazamia, masikio mapya ya kusikilizia, mikono mipya ya
kusaidia, na moyo mpya wa kupenda watu wengine.”
Sababu moja kwa nini unahitaji kuwajibika katika jamii ya kanisa
ni kutimiza wito wako wa kuhudumia waamini wengine kwa matendo. Biblia inasema,
“Ninyi nyote pamoja ni mwili wa Kristo, na kila
mmoja wenu ni kiungo pekee kinachohitajika katika mwili huo.” 1 Wakorintho 12:27 (NLT) Huduma yako inahitajika sana katika
mwili wa Kristo – uliza kanisa lolote la mahali. Kila mmoja wetu anao wajibu wa
kufanya, na kila wajibu ni wa muhimu. Hakuna huduma mdogo kwa Mungu; zote ni
muhimu.
Vivyo hivyo, hakuna huduma zisizofaa kanisani. Nyingine
zinaonekana na nyingine hazionekani, lakini zote ni za thamani. Huduma ndogo au
zilizofichika, mara nyingi zina matokeo makubwa. Nyumbani mwangu, nuru ya
muhimu sana siyo ile taa kubwa ya chumba cha kulia chakula lakini ni ile taa
ndogo ya usiku ambayo hunisaidia nisijigonge kidole cha mguu ninapoamka usiku.
Hakuna mlinganyo kati ya ukubwa na umuhimu. Kila huduma ni muhimu kwa sababu
tunategemeana ili tufanye kazi.
Kunatokea nini pale sehemu moja ya mwili wako inaposhindwa kufanya
kazi? Unaugua. Mwili wote unapata maumivu. Fikiri kama maini yako yangeamua
kuishi yenyewe: “Nimechoka! Sitaki kuhudumia mwili huu tena! Nahitaji kufanya
mambo yanayonifaa mimi! Viungo vingine vijaze nafasi yangu.” Kungetokea nini?
Mwili wako ungekufa. Siku hizi makanisa maelfu yanakufa kwa sabau ya Wakristo
ambao hawataki kutumika. Wanakaa kando kama watazamaji, na mwili unaugua.
Umeamriwa
kutumika. Yesu hakukosea: “Nia yenu iwe kama yangu, kwa kuwa mimi
Masihi, sikuja kutumikiwa kakini kutumika na kutoa uhai wangu.” Mathayo 20:28 (LB) Kwa Wakristo, utumishi si jambo la hiari,
kitu cha kuwekwa kwenye ratiba kama tuna muda wa ziada. Ni kiini cha maisha ya
Kikristo. Yesu alikuja “kutumika” na “kutoa” – na maneno haya mawili lazima
yawe kigezo cha maisha yako hapa duniani. Kutumika na kutoa pamoja hufanya
lengo la nne la Mungu kwa maisha yako. Mama Teresa alisema, “Kutoa kutakatifu
kunahusu kufanya kazi ya Mungu kwa tabasamu.”
Kukua kiroho si mwisho wa yote. Tunakua ili tutoe. |
Jambo la mwisho
waamini wanalohitaji siku hizi ni kuenda kwenye mafunzo mengine ya Biblia.
Wanajua mengi kuliko wanayotendea kazi. Wanachohitaji ni uzoefu wa kuhudumu
ambao utawapa mazoezi ya misuli yao ya kiroho.
Kutumika ni kinyume cha hali yetu ya asili. Mara nyingi tuna ile
hali ya “tutumikiwe”
na siyo kutumika.
Tunasema, “Natafuta kanisa linalohudumia mahitaji yangu na kunibariki,” siyo “Natafuta
mahali pa kutumika na niwe Baraka.” Tunategemea wengine watutumikie, na siyo
kinyume chake. Lakini tunapoendelea kukua katika Kristo, mwelekeo wa maisha
yetu lazima uwe kuishi maisha ya utumishi. Mfuasi wa Yesu aliyekomaa huacha
kuuliza, “Nani atatimiza mahitaji yangu?” na badala yake huanza kuuliza, “Nani
nimsaidie mahitaji yake?” Je, wewe unauliza swali kama hilo?
JIANDAE
KWA UMILELE
Mwishoni mwa maisha yako hapa duniani utasimama mbele za Mungu, na
atakuthamini namna ulivyowatumikia wengine na maisha yako. Biblia inasema, “Kila
mmoja wetu atatoa hesabu ya mambo yake binafsi mbele za Mungu.” Warumi 14:12 (NLT) Fikiri juu ya matokeo yake. Siku moja Mungu
atalinganisha nguvu na wakati tulivyotumia kwa maisha yetu binafsi na vile
tulivyotumia katika kuwatumikia wengine.
Kwa wakati huo, udhuru wetu wote kwa ajili ya ubinafsi wetu
utakuwa hauna maana: “Nilikuwa na shughuli nyingi” au “Nilikuwa na kazi” au “Nilikuwa
nafurahia, au nilikuwa najiandaa kustaafu.” Katika udhuru wote Mungu atajibu, “Pole,
siyo jibu sahihi. Nilikuumba, nikakuokoa, na kukuita na kukuagiza kuishi maisha
ya utumishi. Ni sehemu gani hukuelewa?” Biblia inawaonya wasioamini, “Atawamwagia
hasira na ghadhabu yake wale wanaoishi kwa ajili ya nafsi zao tu,” Warumi 2:8 (NLT) lakini kwa Wakristo itamaanisha kupoteza
thawabu za milele.
Tuko hai kabisa kama tunawasaidia wengine. Yesu alisema, “kama
utakazia kuokoa maisha yako, utayapoteza. Ni wale tu wanaopoteza maisha yao kwa
ajili yangu na Habaari Njema ndio wataelewa maana hasa ya kuishi.” Marko 8:35 (LB); angalia pia Mathayo 10:39; 16:25; Luka 9:24;
17:33 Ukweli huu ni wa muhimu sana kiasi cha kurudiwa mara tano katika Injili.
Kama hutumiki, wewe unaishi tu, kwa sababu maisha yapo ili kuhudumu. Mungu
anapenda ujifunze kupenda na kuwatumikia wengine na bila choyo.
HUDUMA NA UMUHIMU
Utumishi ni njia
ya kupata umuhimu wa kweli. |
Kama huhusiki na huduma yoyote, umekuwa na udhuru gani? Ibrahimu
alikuwa mzee, Yakobo hakuwa na usalama, lea hakuwa wa kukvutia, Yusufu
alidhalilishwa, Musa alikuwa na kigugumizi, Gidioni alikuwa maskini, Samsoni
alikuwa tegemezi, Rahabu alikuwa mzinzi, Daudi alizini na alikuwa na matatizo
mengi ya kijamaa, Eliya alitaka kujiua, Yeremia alivunjwa moyo, Yona hakuwa tayari,
Naomi alikukwa mjane, Yohana Mbatizaji hakuwa na matamshi mazuri, Petro alikuwa
mwepesi wa hasira, Martha alikuwa mwenye hofu sana, mwanamke Msamaria alikuwa
na ndoa kadhaa zilizovunjika Zakayo hakupendwa, Thomaso alikuwa mwenye mashaka,
Paulo alikuwa na afya mbovu, na Timotheo alikuwa mwoga. Hiyo ni mifano ya sifa
zisizofaa lakini Mungu aliwatumia kila mmoja katika huduma yake. Atakutumia
wewe pia, ukiacha kutoa udhuru.
SIKU YA
ISHIRINI NA TISA KUFIKIRI
JUU YA LENGO LANGU Jambo la Kutafakari: Huduma siyo hiari. Kifungu cha Kukumbuka: “Maana sisi ni
kazi ya mikono ya Mungu, tuliumbwa katika Kristo Yesu tutende matendo mema,
ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza tuyatende.” Waefeso 2:10 (NIV) Swali la Kujiuliza: Je, ni jambo gani linanizuia nisikubali
wito wa Mungu wa kumtumikia? |
Siku
ya Thelathini: Ulifinyangwa Kumtumikia Mungu
Mikono yako ilinifinyanga na kunitengeneza.
Ayubu 10:8 (NIV)
Watu
niliowafinyanga kwa ajili yangu watatangaza sifa zangu.
Isaya 43:21 (MJB)
Ulifinyangwa ili umtumikie Mungu.
Mungu aliumba kila kiumbe katika sayari hii kwa utaalamu maalum.
Wanyama wengine hukimbia, wengine huogelea, wengine huchimba mashimo na wengine
huruka angani. Kila mmoja ana wajibu wa kufanya, Ndivyo livyo kwa wanadamu.
Kila mmoja wetu alisanifiwa kipekee, au alifinyangwa ili kufanya vitu fulani.
Kabla wasanifu majengo hawajatoa michoro ya jengo jipya kwanza
huuliza, “Lengo lake nini? Litatumiwaje?” Matumizi yaliyokusudiwa mara nyingi
huwa kigezo cha sura ya jengo. Kabla Mungu hajakuumba aliamua wajibu
utakaotimiza hapa duniani. Alipanga kabisa alivyotaka wewe umtumikie, na kisha
akakufinyanga kwa ajili ya kazi hizo. Uko jinsi ulivyo kwa sababu ulifinyangwa
kwa ajili ya huduma maalum.
Biblia inasema, “Sisi ni kazi ya mikono ya Mungu,
tuliumbwa katika Kristo Yesu tutende matendo mema.”
Waefeso 2:10 (NIV) Neno letu la Kiingereza ushairi (poem) linataokana na neno la Kiyunani linalotafsiriwa “kazi ya
mikono.” Wewe ni kazi ya mikono ya ufundi wa Mungu. Wewe siyo matokeo ya vitu
vilivyokusanywa pamoja bila kufikiri. Wewe umetokana na usanifu wa hali ya juu,
wa asili.
Mungu hapotezi chochote. |
Mungu hakukufinyanga kabla ya kuzaliwa tu, alipanga kila siku ya
maisha yako kusaidia mchakato wake wa kukufinyanga. Daudi anaendelea, “Kila
siku ya maisha yangu iliandikwa kitabuni mwako. Kila wakat uliwekwa kabla hata
siku moja haijawepo.” Zaburi 139:16 (NLT) Hii
inamaanisha kwamba hakuna kdinachotokea maishani mwako bila kuwa na umuhimu.
Mungu hutumia yote
kukutengeneza kwa ajili ya huduma yako kwa wengine na pia kwa ajili ya huduma
yako kwake.
Mungu hapotezi chochote. Asingeweza kukupa uwezo, utashi, vipawa
karama, nafsi, uzoefu wa kimaisha, isipokuwa kwa makusudi ya utukufu wake. Kwa
kuamsha na kuelewa vipengele hivi unaweza kugundua mapenzi ya Mungu kwa maisha
yako.
Biblia inasema wewe ni “wa ajabu.” Wewe ni mchanganyiko wa
vipengele vingi tofauti. Ili kukusaidia ukumbuke vipengele vitano nimetengeneza
kielelezo rahisi – SHAPE. Katika sura hii na ile ifuatayo tutavitazama hivi
vipengele vitano, na baada ya hapo, nitaeleza jinsi ya kugundua na kutumia umbo
lako.
JINSI
MUNGU ANAVYOKUUMBA KWA AJILI YA HUDUMA YAKO
Mungu anpotupatia jukumu, daima hutupatia zana zinazohitajika
katika utekelezaji. Mchanganyiko huu unatiwa SHAPE yako:
Spiritual gifts (Karama za
kiroho)
Heart (Moyo)
Abilities (Akili)
Personality (Nafsi)
Ezperience (Uzoefu)
SHAPE:
KUDHIHIRISHA KARAMA ZAKO ZA KIROHO
Mungu humpa kila mwamini karama za kiroho. (Wstumi 12:4-8; 1
Wakorintho 12; Waefeso 4:8-15; 1 Wakorintho 7:7) Hizi ni uwezo maalum kutoka
kwa Mungu kwa ajili ya kumtumikia na hupewa kwa waamini tu. Biblia inasema, “Yeyote
asiyekuwa na Roho hawezi kupokea vipawa vinavyotoka kwa Roho wa Mungu.” 1 Wakorinthoo 2:14 (TEV)
SIKU YA THELATHINI: ULIFINYAN GWA UMTUMIKIE MUNGU |
Kwa sababu Mungu anapenda aina tofauti na anatutaka tuwe maalum,
hakuna kipawa kimoja kinachopewa kwa kila mtu. (1 Wakorintho 12:29-30) Pia
hakuna mtu mmoja anayepokea vipawa vyote. Kama ungekuwa navyo vyote,
usingemhitaji mtu mwingine yeyote, na hili lingekwamisha moja ya malengo ya
Mungu – kutufundisha kupendana na kutegemeana.
Vipawa vyako vya kiroho havikutolewa kwa ajili ya faida yako
binafsi lakini kwa kuwafaidia wengine, kama vile watu wengine walipewa vipawa
kwa ajili ya faida yako. Biblia inasema, “Kila mtu amepewa
karama ya kiroho kama njia ya kulisaidia kanisa.”
1 Wakorintho 12:7 (NLT) Munguu alipanga hivyo ili tuhitajiane. Tunapotumia
vipawa vyetu pamoja, sote tunafaidika. Kama wengine hawatumii karama zao,
unadanganyika, na usipotumia karama zako, wao hudanganyika. Ndiyo maana
tumeagizwa kugundua na kukuza vipawa vyetu vya rohoni. Je, umeshachukua muda
kugundua vipawa vyako vya kiroho? Kipawa ambacho hakijafunuliwa hakina faida.
Tunaposahau kweli hizi za msingi kuhusu vipawa mara nyingi huleta
matatizo kanisani. Matatizo mawili ya mara kwa mara ni “wivu
wa karama” na “kutukuza kipawa.” Tatizo la kwanza hutokea tunapojilinganisha kipawa chetu na
kile cha wengine, tunaacha kuridhika na kile Mungu alichotupa, na tunakuwa na
uchungu au wivu kwa jinsi Mungu alichotupa, na tunakuwa na uchungu au wivu kwa
jinsi Mungu anavyowatumia wengine. Tatizo la pili hutokea tunapotegemea kila
mtu awe na kipawa kama chetu, afanye tulichoitwa kufanya, na ajihisi kama
tunavyojihisi huu ya jambo hilo. Biblia inasema, “Kuna tofauti ya
huduma katika kanisa, lakini ni Bwana mmoja tunayemtumikia.”1 Wakorintho 12:5 (NLT)
Wakati mwingine karama za rohoni zinakazwa kupita kiasi na kuacha
vipengele vingine anavyotumia Mungu kukufinyanga kwa ajili ya huduma. Vipawa
vyko hudhihirisha ufunguo mmoja wa kugundua mapenzi ya Mungu kwa huduma yako. Mungu anakufinyanga kwa njia
nyingine nne.
SHAPE:
KUSIKIKIZA MOYO WAKO
Biblia hutumia neno moyo
kuelezea furushi la matakwa, matumaini, upendeleo, ndoto, na mapenzi uliyo
nayo. Moyo yako huwakilisha asili ya msukumo wa mambo yako yote – unayopenda
kufanya zaidi na unayoyajai zaidi. Hata siku hizi bado tunalitumia neno hili
kwa maana ile ile tunaposema, “Nakupenda kwa moyo wangu wote.”
Biblia inasema, “Kama uso unavyoonekana sura yake
katika maji, ndivyo moyo unavyomwonyesha mtu.”
Mithali 27:19 (NLT) Moyo wako hukufunua wewe halisi ulivyo kikwali, sivyo matu wengine wanavyofikiri juu yako au
jinsi mazingira yanavyokulazimisha uwe. Moyo wako huamua kwa nini useme mambo usemayo, kwa nini unahisi unavyohisi, na kwa nini unatenda unavyofanya.” (Mathayo 12:34; Mithali 4:23)
Kimaumbile kila mmoja wetu ana mapigo ya pekee ya moyo. Kama vile
kila mmoja wetu alivyo na alama za pekee za kidole, macho, sauti, mioyo yetu
pia hupiga kitofauti kidogo. Inashangaza kwamba katika mabilioni ya watu
waliowahi kuishi, hakuna aliyewahi kuwa na mapigo sawa kabisa na ya kwako.
Vivyo hivyo, Mungu ametupatia “mapigo ya moyo” ya hisia ya kipekee
ambayo hujitokeza tunapofikiri juu ya masomo, shughuli, na mazingira
yanayotuvutia. Kwa njia ya asili tunajali mambo fulani na mengine hapana. Hivi
ni vigezo kukuonyesha wapi unatakiwa utumike.
Neno jingine lenye maana ya moyo ni tamaa. Kuna mambo ambayo unakuwa na shauku kubwa nayo na mengine ambayo
usingejali kabisa. Uzoefu mwingine hukuteka n kuchukua msimamo wako wakati mambo
mengine hukufanya usiyatazame au hukuudhi kiasi cha kulia machozi. Haya hufunua
hali ya moyo wako.
Ulipokuwa unakua, inawezekana uligundua kwamba ulipendelea masomo
fulani ambayo hakuna mtu katika jamaa yenu aliyeyajali. Je, upendeleo huo
ulitoka wapi? Ulitoka kwa Mungu. Mungu alikuwa na lengo kukupatia upendeleo huu
wa kuzaliwa. Hisia zako ni ufunguo wa pili katika kuelewa kufinyangwa kwako kwa
ajili ya huduma. Usidharau mambo unayopendelea. Angalia yanavyoweza kutumiwa
kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Kuna sababu kwamba unapenda kufanya mambo haya.
Mara nyingi Biblia, inasema, “Kumtumikia Mungu
kwa moyo wako wote.” (Kumbukumbu 11:13; 1 Samweli
12:20; Warumi 1:9; Waefeso 6:6) Mungu anapenda umtumikie kwa shauku, si wajibu.
Mara chache watu hufanya vizuri katika kazi ambazo hawazifurahii au kuwa na
shauku nazo. Mungu anakutaka kutumia matakwa yako ya asili kumtumikia. Yeye na
wenzako. Sikiliza msukumo wa ndani kunaweza kukuongoza kwenye huduma Mungu anayokukusudia.
Unapofanya
kitu unachopenda kufanya hakuna mtu anayehitajika kukuchochea. |
Alama ya pili ya kumtumikia Mungu kutoka moyoni mwako ni ufanisi. Kila unapofanya kile Mungu alichokupangia upende kufanya, unakuwa na uwezo mkubwa nacho. Shauku huleta ukamilifu. Kama
hujali kazi fulani, siyo rahisi kuifanya kwa ubora. Badala yake, wale wanaofanikiwa
sana katika nyanja zote ni wale unaofanya kwa sababu ya shauku, siyo wajibu au
faida.
Sote tumeshasikia watu wakisema, “Nilichukua kazi ninayoichukia
ili nipate fedha nyingi, hivyo siku moja naweza kuiacha na kufanya kazi
niipendayo.” Hilo ni kosa kubwa. Usipoteze maisha yako katika kazi
isiyoshabihiana na moyo wako. Kumbuka, mambo makubwa maishani si vitu. Maana ni
muhimu zaidi kuliko fedha. Mtu mmoja tajiri sana ulimwenguni aliwahi kusema, “Kuwa
na mali chahe pamoja na kumcha Mungu ni bora kuliko maisha ya utajiri pamoja na
taabu.” Mithali 15:16 (Msg)
Usiangalie u kupata “maisha mazuri, “kwa sababu maisha mazuri
hayatoshi. Hakika hayatoshelezi. Unaweza kuwa na mali nyingi katika maisha na
bado ukawa huna kitu cha kukiishia. Badala yake lenga kupata “maisha
bora” – Kumtumikia Mungu katika njia ambayo inaonyesha moyo wako.
Tafuta kile upendacho kufanya – ile Mungu alichokupa kufanya – na kisha kifanye
kwa utukufu wake.
SIKU YA THELATHINI KUFIKIRI
JUU YA LENGO LANGU Jambo la Kutafakari: Nilifinyangwa ili kumtumikia Mungu. Kifungu cha Kukumbuka: Mungu hufanya
kazi kupitia watu mbalimbali, lakini ni Mungu yule yule anayekamilisha
malengo yake kwa kupitia hao wote.
1 Wakorintho 12:6 (Ph) Swali la Kujiuliza: Je, ni katika njia gani naweza kujiona
nikiwatumikia wengine kwa shauku na kupenda kufanya hivyo? |
Siku ya Thelathini na Moja: Kufahamu Umbo (SHAPE) Yako
Ulinumba
kwanza ndani, kisha nje; Uliniumba tumboni mwa mama yangu.
Zaburi 139:13 (Msg)
Unaweza kuwa wewe tu.
Mungu alitutengeneza kila mmoja wetu ili kwamba kusiwe na mtu
mwingine kama wewe duniani. Hakuna yeyote mwenye mchanganyiko wa viasili sawa
kabisa na wa kwako vinavyokufanya uwe wa pekee. Maana yako ni kwama hakuna
mwingine duniani anayeweza kutenda majukumu Mungu aliyokukusudia. Kama huwezi
kutoa mchango wako wa pekee katika mwili wa Kristo, hautafanywa kabisa. Biblia
inasema, “Kuna aina tofauti za karama za rohoni … njia
tofauti za kuhudumu … na uwezo tofauti wa kutoa huduma.” 1 Wakorintho 12:4-6 (TEV) Katika sura iliyopita tuliona zile
mbili za kwanza: karama zako za rohoni na moyo wako. Sasa tutaona sehemu
iliyobaki ya umbo (SHAPE) yako kwa kumtumikia Mungu.
SHAPE: KUTUMIA UWEZO WAKO
Uwezo wako ni vipawa vya asili ulivyozaliwa navyo. Baadhi ya watu
wana uwezo wa aili na maneno: walitoka tumboni wanaongea! Wengine wana uwezo wa
asili wa michezo, wanafanya vizuri sana katika mazoezi ya viungo. Wengine ni
wazuri katika hisabati, muziki, au ufundi.
Mungu alipotaka kutengeneza Hema ya Kukutania na vifaa vyote vya
ibada, alitoa wasanii na wachongaji waliokuwa wamepata “ujuzi,
uwezo, na maarifa katika aina zote za ufundi katika kufanya vifaa vya ufundi …
na kufanya kazi za kila aina za ufundi wa mikono.”
Kutoka 31:3-5 (NIV) Hata leo Mungu bado anatoa uwezo huu na zaidi ili watu
wamtumikie.
Uwezo
wetu wote hutoka kwa Mungu. Hata uwezo unaotumika kutenda
dhambi unatoka kwaa Mungu; unatumiwa tu vibaya. Biblia inasema, “Mungu
ametupatia kila mmoja wetu uwezo wa kutenda vyema.”
Warumi 12:6a (NLT) Kwa kuwa uwezo wa asili unatoka kwa Mungu, ni wa muhimu sawa
na karama zako za kiroho. Tofauti pekee ni kwamba uwezo wa asili ni wa
kuzaliwa.
Udhuru mmojawapo wa ule unatolewa na wengi kwa kutotumika ni “sina
uwezo wowote wa kutoa.” Hii inachekesha. Una makumi, labda mamia ya vipawa
ambavyo havijulikani, havijatumika, ambavyo vimelala ndani yako. Utafiti mwingi
umeonyesha kwamba mtu wa kawaida ana ujuzi wa vipawa tofauti vipatavyo 500 hadi
700 – kuliko unavyofahamu.
Kwa mfano, ubongo wako unaweza kutunza habari trilioni 100. Akili
yako inaweza kumudu maamuzi 1,500 kwa sekunde, kama ilivyo wakati mfumo wako wa
kuyeyusha chakula unafanya kazi. Pua yako inaweza kunusa kiasi cha 10,000
harufu tofauti. Mguso wako unaweza kutambua 1/25,000 ya unene wa inchi moja, na
ulimi wako unaweza kuonja sehemu moja ya kwinini katika sehemu milioni mbili za
maji. Wewe ni mkusanyiko wa vipawa mbali mbali vya maana. Ni kiumbe cha ajiabu
cha Mungu. Sehemu ya wajibu wa kanisa ni kutambua na kuruhusu uwezo wako ili
kumtumikia Mungu.
Kila
uwezo unaweza kutumia kwa utukufu wa Mungu.
Paulo alisema, “Kila mlifanyalo, fanyeni yote kwa utukufu wa
Mungu.” 1 Wakorintho 10:31 (NIV) Biblia imejaa mifano ya uwezo tofauti
ambao Mungu aliutumia kwa utukufu wake. Hapa kuna mfano wa vipawa vilivyotajwa
katika maandiko: Uwezo wa sanaa, uwezo wa ujenzi, uongozi, uokaji, kutengeneza
meli, utengenezaji wa vyakula vitamu, mdahalo, ubunifu, kutia dawa maiti,
kutarizi, kuchora kulima, uvuvi, bustani, kuongoza, kutawala, ufundi Uashi,
muziki, kutengeneza silaha, ufumaji, kutia rangi, kupanda mbegu, falsafa, uwezo
wa mitambo, uvumbuzi, useremala, ubaharia, uuzaji, uaskari, ushonaji,
kufundisha, kuandika fasihi na mashairi. Biblia inasema, “kuna
uwezo tofauti wa kutoa huduma, lakini Mungu yule mmoja hutoa uwezo kwa wote kwa
ajili ya huduma yao maalum.” 1 Wakorintho 12:6 (NIV) Mungu
ana nafasi katika kanisa lake ambapo kipawa chako chaweza kung’ara na unaweza
kufanya tofauti. Ni juu yako kutafuta nafasi hiyo.
Ninachoweza
kukifanya Mungu anapenda nifanye. |
Ninachoweza
kufanya, Mungu ananitaka nifanye. Wewe ni mtu
pekee duniani unayeweza kutumia uwezo wako. Hakuna mwingine awezaye kufanya
jukumu lako, kwa sababu hawana umbo la pekee ambalo Mungu amekupatia wewe.
Biblia inasema kwamba Mungu hukupatia “Vyote
unavyohitaji ili kufanya mapenzi yake.”
Waebrania 13:21 (LB) Ili kugundua mapenzi ya Mungu kwa maisha yako, huna budi
kuchunguza kwa makini una uwezo mkubwa katika kitu gani.
Kama Mungu hakukupa uwezo wa kuimba hataweza kukutegemea uwe
mwimbaji mashuhuri. Mungu kamwe hatakutaka utoe maisha yako kwa kazi ambayo
huna kipawa nayo.
Upande mwingine, uwezo
uli nao ni kigezo thabiti cha kile Mungu anachopenda ufanye na maisha yako. Ni
vigezo vya kutambua mapenzi ya Mungu kwako. Kama wewe una uwezo wa mitindo, au
kutayarisha watu, au kuchora, au kupanga mipango, ni vyema kudhani kwamba
mpango wa Mungu kwa maisha yako unahusisha kipawa hicho kwa namna fulani. Mungu
hapotezi vipawa; anaoanisha miito yetu na vipawa vyetu.
Uwezo wako haukutolewa ili kukuwezesha kuishi tu; Mungu alikupatia
kwa ajili ya huduma yako. Petro alisema, “Mungu amempa kila
mmoja wenuu uwezo wa pekee; hakikisheni mnautumia kuksaidiana, mkiwashirikisha
wengine aina mbalimbali za baraka za Mungu.”
1 petro 4:10 (LB)
Katika dakika hii ya kuandika, watu wapatao 7,000 wanatumia vipawa
vyao kwa huduma katika Kanisa la Saddleback, wakitoa huduma ya kila namna
unayoweza kuifikiri: kukarabati magari yaliyotolewa ili kuwapa wahitaji,
kutafuta bei nzuri kwa manunuzi ya kanisa; kusawazisha ardhi, kuweka sawa
mafaili, kusanifu sanaa, vipindi, majengo; kusaidia katika afya; kuandaa
chakula; kutunga nyimbo; kufundisha muziki; kuandika mapendekezo ya misaada,
kufundisha timu, kutafiti ujumbe au kuzitafsiri na mamia ya ujuzi mbalimbali.
Washirika wapya wanaelezwa, “kama una uwezo katika kitu chochote, unapaswa
kukifanya kwa kanisa lako.
SHAPE: KUTUMIA NAFSI YAKO
Hatuelewi jinsi kila – mmoja wetu alivyo wa pekee hasa. Viasili
vya DNA vinaweza kuungana kwa njia zisizohesabika. Kiasi hicho ni uwezo wa
sehemu 10 kwa 2,400,000,000. Kiwango hicho ni uthibitisho kwamba haiwezekani
kupata mtu mwingine aliye kama wewe kila hali. Kama kila sifuri ungeiondoa kwa
kuweka upana wa inchi moja, ungehitaji kipande cha karatasi cha urefu wa maili
37,000!
Ili kuweka jambo hili katika mwelekeo, wanasayansi wamebuni kwamba
viasili vyote (particles) katika ulimwengu labda viko chini ya 10 na sifuri 76
nyuma yake, chini ya uwezekano wa DNA yako. Upekee wako ni ukweli wa kisayansi
wa maisha. Mungu alipokuumba, alivunja kichongeo. Kwa hiyo hapakuwepo kamwe, na
hapatakuwa na mtu yeyote anayefanana na wewe kila kitu.
Ni wazi kwamba Mungu anapenda aina tofauti – angalia tu
kukuzunguka! Alituumba kila mmoja wetu kwa mchanganyiko pekee wa viasili
vinavyounda nafsi. Mungu aliumba watu wakimya na
wasemaji. Aliumba wanaopenda hali ya aina moja na wale wanaopenda hali
tofauti tofauti. Aliumba wengine kuwa watu wa kufikiri na wengine wa hisia.
Watu wengine hufanya kazi vizuri zaidi wanapopewa majukumu peke yao wakati
wengine hufanya vizuri katika kikundi. Biblia inasema, “Mungu
hufanya kazi kupitia watu tofauti kwa njia tofauti, lakini ni Mungu yule mmoja
anayetimiza lengo lake kupitia wote hao.”
1 Wakorintho 12:6 (Ph)
Biblia hutupa uthibitisho mwingi kwamba Mungu hutumia watu wa aina
zote. Petro alikuwa mcheshi
(sanguine). Paulo alikuwa mtu makali (choleric).
Yeremia alikuwa mwenye huzuni
(melancholy). Unapotazama tofauti za nafsi za watu katika wale wanafunzi kumi
na wawili ni rahisi kuona kwa nini wakati mwingine walikuwa na migongano baina
yao.
Hakuna hulka (temperament) inayofaa au isiyofaa
kwa huduma. Tunahitaji aina zote za nafsi ili kuliweka sawa kanisa na kulipatia
ladha. Ulimwengu ungekuwa wa kuchosha sana kama sisi sote tungekuwa vanila
tupu. Kwa bahati, watu huja na zaidi ya ladha thelathini na moja.
Hulka yako itakuwa na mvuto wa jinsi na wapi
utatumia tabia zako za rohoni na vipawa. Kwa mfano, watu wawili wanaweza kuwa
na kipawa cha aina moja cha uinjilisti, lakini kama mmoja ni mkimya na mwingine
ni msemaji, kipawa hicho kitadhihirishwa kwa njia tofauti.
Unahisi vizuri unapofanya kile Mungu alikuumba
ukifanye. |
Kama kioo chenye rangi, hulka zetu tofauti huonyesha mwana wa
Mungu katika rangi mbali mbali na mifumo tofauti. Hii huibariki jamii ya Mungu
kwa kina na kwa namna mbali mbali. Pia hutubariki sisi binafsi. Unapohudumu
kulingana na nafsi aliyokupa Mungu, unapata utoshelevu, kuridhika, na
mafanikio.
SHAPE:
KUTUMIA UZOEFU WAKO
Umefinyangwa na uzoefu mbalimbai katika maisha yako, uzoefu huo
mwingi ulikuwa zaidi ya uwezo wako. Mungu aliuruhusu kwa lengo lake la
kukufinyanga. (Warumi 8:28-29) Katika kutengeneza umbo lako la kumtumikia
Mungu, unahitaji kuchunguza walau aina sita za uzoefu kutoka maisha yako
yaliyopita.
l Uzoefu wa kijamaa:
ulijifunza nini ulipokuwa unakua katika jamaa yako?
l Uzoefu wa kielimu:
Ni masomo gani uliyapendelea ulipokuwa shuleni?
l Uzoefu wa kazi:
Ni kazi gani umefanya kwa ufanisi zaidi na kuzifurahia?
l Uzoefu wa kiroho:
Ni nyakati gani zimekuwa za maana sana na Mungu?
l Uzoefu wa kihuduma:
Umemtumikiaje Mungu siku za nyuma?
l Uzoefu wa maumivu:
Matatizo gani, maumivu, mwiba, na majaribu yamekupa mafundisho?
Ni kipengele hiki cha mwisho, uzoefu wa maumivu, ambacho Mungu hutumia zaidi katika kukuanda kwa huduma. Mungu kamwe
hapotezi maumivu yoyote! Hakika huduma yako kubwa itatoka kwenye maumivu yako makubwa. Nani angeweza kuhudumia
vyema, wazazi wa mtoto mwenye udhaifu wa upungufu wa kimaumbile kuliko jamaa
nyingine yenye mtoto aliye na tatizo kama hilo? Nani anaweza kumsaidia nyema
mlevi kuliko mtu aliyeshinda pepo la ulevi akapata uhuru? Nani anaweza
kumsaidia mwanamke aliyeachwa na mumewe kwa sababu ana mke nje kuliko mwanamke
aliyepitia tatizo la aina hiyo?
Ili
Mungu atumie uzoefu wako wa maumivu lazima uwe tayari kushirikisha wengine. |
Kama kweli unatamani kutumiwa na Mungu, lazima uelewe ukweli huu
muhimu: Uzoefu ule uliouchukia sana au hata kujilaumu katika maisha – ule
uliotaka kuficha na kusahau – ndio uzoefu Mungu anapenda kutumia kuwasaidia
wengine. Ndiyo huduma yako!
Ili Mungu atumie uzoefu wa maumivu uwe radhi kushirikisha wengine,
Acha kuficha, na lazima ukubali makosa yako, kushindwa, na hofu zako. Kufanya
hivi labda kutakuwa ni huduma yako kubwa zaidi. Watu daima hujengwa
tunapowashirikisha jinsi neema ya Mungu ilivyotusaidia katika udhaifu kuliko
tunapojisifia kufaulu kwetu.
Paulo alifahamu ukweli huu, hivyo alikuwa mwaminifu kuhusu
kupambana kwake na udhaifu. Alikiri wazi: “Nafikiri lazima
mafahamu, ndugu wapendwa kuhusu wakati mgumu tulioupata huko Asia. Kwa kweli
tulilemewa kupita kiasi; tukaogopa kwamba hatutaweza kuishi tena. Tulihisi
tulipangiwa kufa na tukaona jinsi tulivyokuwa hatuna nguvu za kujisaidia
wenyewe, lakini ilikuwa vyema, kwa kuwa tulimkabidhi Mungu kila kitu, ambaye
pekee angeweza kutuokoa, kwa kuwa anaweza kufufua hata wafu. Na kweli
alitusaidia na kutuokoa kutoka kwenye kifo kibaya; ndiyo, na tunamtegemea
afanye hivyo tena na tena.” 2 Wakorintho 1:8-10 (LB)
Kama Paulo angeficha uzoefu wake wa mashaka na udhaifu, mamilioni
ya watu wasingefaidika leo. Ni ule uzoefu unaoshirikisha ndio tu unaweza
kusaidia wengine. Aldous Huxley alisema, “Uzoefu si mambo yanayokupata, ni kile
unachofanya na yale yanayokupata.” Utafanya nini na yale uliyoyapitia?
Usipoteze maumivu yako; tumia hali hiyo kusaidia wengine.
Kama tulivyoona hizi njia tano Mungu anazotumia kukupa umbo la
utumishi, natumaini una shukrani za kina kwa mwenyezi Mungu na mawazo sahihi ya
jinsi alivyokuandaa kwa lengo la kumtumikia. Ukitumia SHAPE yako ni siri ya
mafanikio na utoshelevu katika huduma. (Kwa msaada zaidi unaweza kuagiza
kandaza Dalasa la 301, Kugundua Umbo Lako Kwa Ajili ya Huduma, ambazo hujumlisha nyezo ya kugundua Umbo.) Utakuwa na ufanisi
ukitumia karama
zako za rohoni na vipawa
katika eneo la upendeleo wa moyo
wako, na katika njia ambayo hudhihirisha vyema nafsi yako na uzoefu
wako. Ukifanya kinachokulingana, utafaulu sana.
SIKU YA THELATHINI NA MOJA KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU Jambo la Kutafakari: Hakuna mwingine yeyote anayeweza kuwa
mimi. Kifungu cha Kukumbuka: “Mungu
amempatia kila mmoja wenu uwezo wa pekee, hakikisheni mnautumia kusaidiana,
mkiwashirikisha wengine aina mbalimbali za baraka za Mungu.” 1 Petro 4:10 (LB) Swali la Kujiuliza: Je, ni uwezo gani niliopewa na Mungu au
uzoefu gani wa binafsi ninaweza kulipa kanisa langu? |
Siku ya
Thelathini na Mbile: Kutumia Alichokupa Mungu
Kwa
kuwa tuko katika ufumo wa viungo vya mwili wa Kristo vilivyotengenezwa vizuri
sana
na
kufanya kazi kiajabu, hebu tusonge mbele na tuwe tulivyoumbwa tuwe.
Warumi 12:5 (Msg)
Vile
ulivyo ni zawadi ya Mungu kwako; unachofanya na
nafsi
yako ni zawadi yako kwa Mungu.
Mithali ya Kidenishi.
Mungu anastahili kilicho bora toka kwako.
Alikufinyanga kwa lengo, na Mungu anakutegemea utumie vyema kile ulichopewa.
Hataki uwe na hofu au kuona wivu kwa ajili ya vipawa usivyo navyo. Badala yake
anapenda uviangalie kwa makini vipawa alivyokupatia kutumia.
Ukijaribu kumtumikia Mungu kwa njia ambazo kwanza hukuumbwa
kutumia kwazo, ni kama kulazimisha kipande cha mraba kuingiza katika tundu la mviringo.
Inavunja moyo na matokeo yake ni duni. Pia hupoteza muda wako, kipawa na nguvu
zako. Njia bora ya kutumia maisha yako ni kumtumikia Mungu kutokana na maumbile
yako. Ili kufanya hivyo lazima ugundue umbo lako, ujifunze kulikubali na kulifurahia
na kisha uliendeleze hadi kiwango chake cha juu.
GUNDUA
SHAPE YAKO
Biblia inasema, “Msifanye mambo bila kufikiri lakini
jaribuni kufahamu na kufanya lolote ambalo Bwana anawataka kufanya.” Waefeso 5:17 (LB) Usiache siku nyingine ipite. Anza kutafuta na
kubainisha Mungu anapenda uwe nani na utende nini.
Anza
kwa kutathmini karama na uwezo wako.
Chukua muda mrefu, kwa uaminifu angalia mambo unayofanya vizuri na yale
usiyofanya vizuri. Paulo alishauri, “Jaribuni kutumia
akili katika kupima uwezo wenu.” Warumi
12:3b (Ph) Fanya orodha. Waulize watu wengine kwa maoni yao ya kweli. Waambie
unatafuta ukweli, na wala sio kutafuta sifa. Karama za rohoni na vipawa vya
asili daima huthibitishwa na wengine. Kama unafikiri umepewa kipawa cha kuwa
mwalimu su mwimbaji na hakuna mwingine anayekubali, jiulize, kama unataka kujua
iwapo una kipawa cha uongozi, wewe angalia tu juu ya bega lako! Kama hakuna
anayekufuata basi wewe si kiongozi.
Jiulize maswali kama haya: Je, nimeona tunda gani maishani mwangu
ambalo watu wengine walilithibitisha? Ni wapi nimeshafanikiwa? Vipimo vya
karama za rohoni na rekodi za vipawa vyaweza kuwa na manufaa fulani, lakini
vina mipaka katika matumizi yake. Kwanza, vimewekwa katika viwango, hivyo
haviangalii upekee wako kama mtu. Pili hakuna ufafanuzi wa karamaa za rohoni
katika Biblia, hivyo ufafanuzi wowote ni maamuzi ya binafsi na mara nyingi
hutokana na msimamo wa kidhehebu. Tatizo jingine ni kwamba kadiri unavyokua
katika imani, ndivyo unavyoweza kudhihirisha tabia za karama kadha wa kadha.
Unaweza kuwa unatumika au unafundisha, au unatoa kwa ukarimu kutokana na kukua
kwako badala ya kwamba ni karama yako ya rohoni.
Hivyo njia bora ya kugundua karama na uwezo wako ni kufanyia
majaribio maeneo mbalimbali ya huduma. Ningeweza kuchukua vipimo vya karama na
uwezo mia moja nilipokuwa kijana na kamwe nisingegundua kwamba nina karama ya
kufundisha kwa sababu nilikuwa sijafanya kazi hiyo! Ni pale tu nilipoanza
kupokea nafasi za kuhutubu ndipo nilianza kuona matokeo, kupokea uthibitisho
toka kwa wengine, na nikaelewa “Mungu amenipa kipawa katika kazi hii!”
Hutaelewa kamwe una uwezo katika jambo gani mpaka
umejaribu. |
Una makumi ya vipawa vilivyofichika ambavyo hujui unavyo kwa
sababu hujavijaribu kamwe. Hivyo nakutia moyo ujaribu kufanya mambo ambayo
hujajaribu kabla. Usijali wewe una umri gani, nakusihi kamwe kufanya majaribio.
Nimekutana na waatu wengi waliogundua vipawa vyao wakiwa katika umri wa miaka
sabini hadi themanini. Namfahamu mwanamke mwenye umri wa miaka tisini na zaidi
ambaye hukimbia na kushinda mbio za kilomita 10 na hakugundua kwamba ana uwezo
kwenye mbio mpaka alipokuwa na umri wa miaka sabini na nane!
Usijaribu kutafuta kipawa chako kabla ya kujitoa kutumika mahali
fulani. Anza tu kutumika. Unagundua vipawa vyako kwa kuingia katika huduma.
Jaribu kufundisha, au kuongoza au kupanga mipango au kucheza chombo cha muziki
au kufanya kazi na vijana. Hutaelewa kamwe una uwezo katika kitu gani mpaka
umejaribu. Kama hupati matokeo mazuri, sema ni “jaribio” siyo kushindwa.
Hatimaye utaelewa una uwezo katika jambo gani.
Angalia
moyo wako na hulka yako. Paulo alishauri, “Fanyeni
uchunguzi makini wa ninyi ni nani na kazi mliyopewa, na kisha mzame katika hilo.” Wagalatia 6:4b (Msg) Tena, inasaidia kupata maelezo kutoka wale
wanaokufahamu zaidi. Jiulize maswali: Je, nafurahia kufanya nini zaidi? Ni lini
najisikia kuwa hai kabisa? Je, nafanya nini ninapokuwa nimepoteza muda? Je,
Napenda mambo ya kila siku au mambo tofauti? Je, napenda kufanya na wengine au
peke yangu? Je, mimi ni msemaji au mtu mkimya? Je, mimi ni mwenye kufikiri au
mwenye kufuata hisia? Je, nafurahia nini zaidi – ushindani au ushirika?
Chunguza
uzoefu wako na upate masomo uliyojifunza. Chunguza
maisha yako na ufikiri yalivyokufinyanga. Musa aliwaambia Waisraeli, “Kumbukeni
leo mliyojifunza kuhusu Bwana kwa uzoefu wenu naye.
“ Kumbukumbu 11:2 (TEV) Uzoefu ukisahaulika hauna faida; hili ni somo zuri la
kutunza kumbukumbu za kiroho. Paulo alipata wasiwasi kwamba waamini na Galatia
wangepoteza uzoefu wa maumivu waliyoyapata. Alisema, “Je
hayo yote yaliyowapata yamepotea? Sidhani!”
Wagalatia 3:4 (NCV)
Ni mara chache tunaona lengo zuri la Mungu katika maumivu au
kushindwa au maudhi yanapokuwa yanatokea. Yesu alipomwosha Petro miguu alisema,
“Nifanyalo sasa wewe huelewi, lakini baadaye
utaelewa.” Yohana 13:7 (NIV) Ni baada ya muda kupita ndipo tunaelewa jinsi
Mungu alivyoruhusu baya kwa ajili ya mema.
Kupata masomo kutoka katika uzoefu wako huchukua muda. Napendekeza
kwamba uchukue juma zima kwa ajili ya mapumziko ya kutathmini maisha yako,
ambapo utatulia na kuona vile Mungu amefanya kazi katika maeneo mbalimbali ya
maisha yako na kuangalia anavyotaka kutumia masomo hayo kusaidia wengine. Kuna
zana zinazoweza kukusaidia kufanya jambo hili. (Wasiliana na www.puposedrivenlife.com)
KUBALI
NA UFURAHIE SHAPE YAKO
Kwa kuwa Mungu anajua nini kinafaa kwako, ni vyema upokee kwa
shukrani jinsi alivyokutengeneza. Biblia inasema, “Una haki gani, wewe binadamu,
kumhoji Mungu? Chungu hakina haki ya kusema kwa mfinyanzi: Kwa nini
ulinifinyanga katika umbo hili? Hakika mfinyanzi anaweza kufanya apendavyo kwa
udongo.” Warumi 9:20-21 (JB)
SHAPE yako ilikusudiwa na Mungu kwa lengo lake, hivyo usilichukie
wala kulikataa. Badala ya kujaribu kujiumba upya na kuwa kama mtu mwingine,
unpaswa kushangilia kwa umbo Mungu alilokupa wewe tu. “Kristo
amempatia kila mmoja wetu uwezo wa aina fulani – chochote anachotaka tuwe nacho
kutoka stoo yake iliyojaa vipawa.” Waefeso
4:7 (LB)
Sehemu ya kukubali umbo lako ni kutambua mipaka yako. Hakuna aliye
na uwezo katika vyote, na hakuna aliyeitwa awe kila kitu. Sote tuna majukumu
maalam. Paulo alielewa kwamba wito wake haukuwa kufanya kila kitu au
kumfurahisha kila mtu lakini kukazania huduma maalum tu Mungu aliyomwandaa
kuifanya. (Wagalatia 2:7-8) Alisema, “Lengo letu ni
kukaa katika mipaka ya mpango wa Mungu kwa ajili yetu.” 2 Wakorintho 10:13 (NLT)
Neno mipaka
humaanisha ukweli kwamba Mungu ametupa kila mmoja wetu uwanja wa huduma. Umbo lako
huwa kigezo cha eneo la huduma yako. Tunapojaribu kupanua zaidi huduma yetu
kuvuka umbo la Mungu alilotuandalia, tunapata taabu. Kama ilivyo kwa kila
mkimbiaji anavyopewa mstari wa kufuata katika kukimbia, ni lazima sisi binafsi,
“Kukimbia kwa uvumilivu mbio ambazo Mungu
ameweka mbele yetu.” Waebrania 12:1 (LB) Usimwonee
wivu mkimbiaji mwingine katika mstari wa karibu nawe; wewe kazania kumaliza
mwendo wako.
Mungu anapenda ufurahie kutumia umbo alilokupatia. |
Biblia hutuonya tusijilinganishe kamwe na wengine: “Fanya
kazi yako vyema, na kisha utakuwa na kitu cha kujivunia. Lakini usijilinganishe
na wengine.” Wagalatia 6:4 (CEV) Kuna sababu mbili kwa nini usijilinganishe
umbo lako, huduma, au matokeo ya huduma yako na mtu mwingine. Kwanza, wakati
wote utampata mtu anayeonekana kufanya vizuri zaidi yako na utavunjika moyo. Au
wakati wote utapata mtu anayeonefana kutokufanya vizuri kama wewe na utajaa
majivuno. Tabia mojawapo itakuondoa katika huduma na kukuibia faraha yako.
Paulo alisema ni upumbavu kujilinganisha na watu wengine. Alisema, “Sisi hatujaribu kujifananisha au kujilinganisha nafsi zetu na wale wanaojipendekeza. Wanapojipima
SIKU YA THELATHINI NA MBILI: KUTUMIA ALICHOKUPA MUNGU |
Utakuta kwamba watu wasioelewa umbo lako la huduma watakulaumu na
kukutaka ufuatishe yale wanayofikiri unapaswa kufanya. Wapuuze. Paulo mara
nyingi alipambana na wapinzani ambao hawakuelewa huduma yake na hivyo kuipinga.
Jibu lake daima lilikuwa lile lile: Epuka kujilinganisha, pinga kukukza mambo,
natafuta tu kusifiwa na Mungu. (1 Wakorintho 10:12-18)
Moja ya sababu Paulo alitumiwa sana na Mungu ni kwamba alikataa
kugeuzwa na mwelekeo na lawama au kwa kulinganisha huduma yake na wengine au
kuvutwa na mijadala isiyo na faida kuhusu huduma yake. Kama John Bunyan
alivyosema, “Kama maisha yangu hayana matunda haijalishi nani ananisifu, na kama
maisha yangu yana matunda, haijalishi ni nani anayenilaumu.”
ENDELEZA UMBO LAKO
Mfano wa Yesu wa talanta ni kielelezo kwamba Mungu anatutazamia
tutumie vizuri anachotupatia. Tunatakiwa kukuza karama na vipawa vyetu,
kuipasha moto mioyo yetu, kukua katika tabia na nafsi zetu, na kupanua uzoefu
wetu ili tuweze kuongezeka kiufanisi katika huduma. Paulo aliwaambia Wafilipi “endeleeni
kukua katika maarifa na ufahamu wenu,
“ Wafilipi 1:9 (NLT) na alimkumbusha Timotheo, “Washa upya karama
ya Mungu iliyomo ndani yako.” 2 Timotheo 1:6 (NASB)
Kama hufanyi mazoezi ya misuli yako, hudhoofika na kupoteza nguvu.
Vivyo hivyo, kama hutumii uwezo na ujuzi Mungu aliokupatia, utaupoteza. Yesu
alifundisha mfano wa talanta ili kutoa kielelezo cha ukweli huu. Akimtaja yule
mtumishi ambaye alishindwa kutumia talanta yake moja, bwana alisema, “Mnyang’anyeni
ile talanta na mpatieni yule aliye na talanta kumi.”
Mathayo 25:28 (NIV) Ukishindwa kutumia ulichopewa utapoteza chote. Tumia uwezo
ulionao na Mungu atauongeza. Paulo alimwambia Timotheo, “Hakikisha
unatumia vipawa ulivyopewa na Mungu … Tumia vipawa hivi katika kazi.” 1 Timotheo 4:14-15 (LB)
Karama yoyote uliyo nayo yaweza kukuzwa na kuongezwa kwa kuifanyia
kazi. Kwa mfano, hakuna anayepata kipawa cha kufundisha kikiwa kimekamilika.
Lakini kwa kujifunza, kupata maoni ya wengine, na mazoezi, mwalimu “mzuri” anaweza
kuwa mwalimu bora,
na kadiri muda unavyopita, anakua na kufikia mwalimu aliyefuzu. Usikae na kipawa kilichoendelezwa nusu. Jitanue na ujifunze
kadiri uwezavyo. “Uwe na bidii kwa ajili ya Mungu, kazi
ambayo hutaionea aibu.” 2 Timotheo 2:15 (Msg) Tumia
vizuri kila nafasi ya mafunzo ili kuendeleza SHAPE yako na kunoa ujuzi wako wa
utumishi.
Mbinguni tutamtumikia Mungu milele. Sasa hivi, tunaweza kujiandaa
kwa ajili ya huduma hivyo ya milele kwa kufanya mazoezi hapa duniani. Kama wana
michezo wanapojiandaa kwa ajili ya olimpiki, tunadumu kujiandaa kwa ajili ya
siku ile kuu, “Wanafanya hivyo kwa ajili ya taji la dhahabu
ambalo hupata kutu na kuchakaa. Ninyi mnaitafuta taji ya dhahabu ambayo ni ya
milele.” 1 Wakorintho 9:25 (Msg)
Tunajiandaa kwa ajili ya majukumu na thawabu za milele.
SIKU YA THELATHINI NA MBILI KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU Jambo la Kutafakati: Mungu anastahili kilicho bora kutoka
kwangu. Kifungu cha Kukumbuka: “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na
Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, na anayetumia Neno la
kweli kwa halali.” 2 Timotheo 2:15 Swali la Kujiuliza: Je nawezaje kutumia kwa ufanisi zadi kile
Mungu alichonipa? |
Siku ya
Thelathini na Tatu: Jinsi Watumishi Halisi Wanavyotenda
Yeyote
anayetaka kuwa mkuu lazima awe mtumishi.
Marko 10:43 (Msg)
Unaweza
kusema wao ni nani kwa yale wayatendayo.
Mathayo 7:16 (CEV)
Tunamtumikia Mungu kwa kuwatumikia wengine.
Ulimwengu hufafanua ukuu kwa kuzingatia mamlaka, mali, heshima, na
nafasi. Kama unaweza kudai kutumikiwa na wengine, umefika. Katika mila yetu
watu wa magharibi ya kujitumikia binafsi na ule umimi kwanza, kutenda kama
utumishi si jambo la kawaida.
Yesu, lakini, aliupima ukuu kwa kigezo cha utumishi, na sio nafasi
uliyo nayo. Mungu anaona ukuu wako kwa watu wangapi unaowatumikia, na siyo watu
wangapi wanaokutumikia. Hii ni tofauti kabisa na kipimo cha kidunia na hivyo ni
vigumu kwetu kuelewa na kutenda. Wanafunzi wa Yesu walishindania juu ya nani
atachukua nafasi ya juu, na miaka 2,000 baadaye, viongozi wa kikristo bado
wanapigania nafasi na kujulikana katika kanisa, madhehebu na huduma shiriki za
kanisa.
Maelfu ya vitabu yameandikwa kuhusu uongozi, lakini vichache
kuhusu utumishi. Kila mtu anapenda kuongoza, hakuna yeyote anayetaka kuwa
mtumishi. Ni bora tuwe majenerali kuliko kuwa askari wa kawaida. Hata wakristo
wanapenda kuwa “viongozi – watumishi” siyo watumishi tu. Lakini kuwa kama Yesu ni kuwa mtumishi.
Ndivyo alivyojiita mwenyewe.
Wakati kujua umbo lako ni muhimu kwa kumtumikia Mungu, kuwa na
moyo wa utumishi ni muhimu zaidi. Kumbuka, Mungu alikufinyanga kwa ajili ya utumishi, siyo kwa ajili ya ubinafsi. Bila moyo wa utumishi utajaribiwa
kutumia umbo lako kwa mapato ya binafsi. Pia utajaribiwa kulitumia kama udhuru
wa kukwepa kutimiza mahitaji fulani.
Umbo lako hudhihirisha huduma yako lakini moyo wako
wa utumishi hudhihirisha kukomaa kwako. |
SHAPE yako hudhihirisha huduma yako, lakini moyo wako wa utumishi
hudhihirisha kukumaa kwako. Hakuna kipawa maalum kinachohitajika kubaki baada
ya mkutano na kuokota takataka au kupanga viti. Kila mtu anaweza kuwa mtumishi,
kinachohitajika ni tabia.
Kuna uwezekano wa kutumika kanisani kwa maisha yote bila kuwahi
kuwa mtumishi.
Lazima uwe na moyo wa utumishi. Je, unawezaje kujua kama una moyo wa utumishi?
Yesu alisema “Unaweza kusema wao ni nani kwa yale
wayatendayo.” Mathayo 7:16 (CEV)
Watumishi
halisi huwa tayari kutumika. Watumishi hawajazi nafasi zao na
mambo mengine yanayoweza kuzuia upatikanaji wao. Wanapenda kuwa tayari
wanapoitwa kutumika. Kama askari, mtumwa lazima awe tayari kuwajibika: “Hakuna
askari anayepigana vitu ajitiaye katika shughuli za maisha ya kila siku, ili
ampendeze yeye aliyempa kazi ya uaskari.”
2 Timotheo 2:4 (NASB) Kama unatumika pale tu inapokufaa, wewe si mtumishi
halisi. Watumishi halisi hufanya kinachohitajika, hata kwa wakati usiofaa.
Je, uko tayari kwa Mungu wakati wote? Je, unaweza kuvuruga mipango
yako bila wewe kukasirika? Kama mtumishi, hutakiwi kuchagua lini au wapi
utatumika. Kuwa mtumishi maana yake ni kuacha kutawala ratiba na kumruhusu
Mungu kuingilia kati anapohitaji.
Kama unajikumbusha kila mwanzoni mwa siku kwamba wewe ni mtumishi
wa Mungu, kuingilia ratiba yako hakutakuvunja moyo, kwa sababu agenda yako itakuwa
chochote Mungu anachotaka kuleta maishani mwako. Watumishi huona vurugu kama
hizo kuwa ni nafasi za kimungu za utumishi na wanafurahia kutoa huduma.
Watumishi
halisi hujali mahitaji. Watumishi wanatafuta njia za
kusaidia wengine wakati wote. Wanapoona hitaji, wanachukua nafasi hiyo
kulitimiza, kama tu Biblia inavyotuagiza: “Kila tunapokuwa
na nafasi, tutende mema kwa kila mtu, hasa kwa jamii ya wanaoamini.” Wagalatia 6:10 (GWT) Mungu anapomweka mtu mwenye mahitaji mbele
yako, anakupa nafasi ya kukua katika utumishi. Tambua kwamba Mungu anasema
mahitaji ya jamii ya kanisa lako yapewe kipaumbele, siyo kuyaweka chini katika
orodha ya “mambo ya kufanya.”
Tunapoteza nafasi nyingi za kutumika kwa sababu tunakosa hali ya
kujali na hiari. Nafasi kubwa za kutumika hazidumu kwa muda mrefu. Zinapita
kasi, wakati mwingine hazirudi tena. Unaweze kupata nafasi moja tu ya kumtumikia
mtu huyo, hivyo tumia nafasi hiyo, “Usiwaambie jirani zako kusubiri mpaka
kesho kama unaweza kuwasaidia sasa.” Mithali
3:28 (TEV)
John Wesley alikuwa mtumishi mzuri wa Mungu Msemo wake ulikuwa “Fanya
mema yote unayoweza, kwa njia zote unazoweza, katika sehemu zozote unazoweza,
ili mradi unaweza.” Huo ndio ukubwa. Unaweza kuanza kwa kutafuta kazi ndogo
ndogo ambazo hakuna mtu anapenda kufanya. Fanya vitu hivi vidogo kama vile
vikubwa, kwa sababu Mungu anatazama.
Watumishi
halisi hufanya vizuri zaidi na kile walichonacho.
Watumishi hawatoi udhuru, au kusubiri mazingira ya kufaa. Watumishi hawasemi, “Siku
fulani” au “Kwa wakati mwafaka.” Wao hufanya kile kinachohitajika kufanywa.
Biblia inasema, “Kama utasubiri hali kamilifu, kamwe
hutafanya chochote.” Mhubiri 11:4 (NLT) Mungu
anakutazamia ufanye unachoweza, na kile uliho nacho, popote ulipo. Huduma nusu
ni bora kuliko nia kamilifu.
Sababu moja kwa nini watu hawatumiki ni kwamba wanaogopa kwamba
wao si wema vya kutosha kutumika. Wameamini uongo kwamba Mungu anahitaji tu
wale mabingwa. Makanisa mengi yamechochea imani hii kwa kufanya “ubora” Mungu,
kitu ambacho huwafanya watu wenye kipawa cha kawaida kutokuwa tayari kushiriki.
Unaweza kuwa umesikia inasemwa, “Kama haiwezi kufanywa kwa ubora,
usifanye.” Yesu hakusema hivyo! Ukweli ni kwamba, karibu kila tunachofanya
hufanywa kwa kiwango cha chini – ndivyo tunavyojifunza. Katikka Kanisa la
Saddleback, tunayo kanuni ya “inatosha”: Haihitaji iwe kamilifu ili Mungu
aitumie na kuibariki. Ni bora tuwe na maelfu ya watu wa kawaida wakitumika
kuliko kuwa na kanisa kamilifu linaloongozwa na watu bora wachache.
Watumishi
halisi hufanya kazi zote kwa kujitoa sawa sawa.
Chochote wanachofanya, watumishi “hufanya kwa moyo wao wote.” (Wakolosai 3:23) Ukubwa wa kazi si kitu cha msingi. Jambo kuu,
ni je, inahitaji kufanyika?
Hutaweza kufikia hali katika maisha ambayo utakuwa wa muhimu sana
kabisa kiasi cha kutosaidia kazi ndogo ndogo. Mungu hawezi kukutenga kutoka
katika majukumu hayo. Ni sehemu muhimu ya mtaala wa tabia yako. Biblia inasema,
“Kama unadhani wewe ni wa muhimu sana huwezi
kumsaidia mtu mwenye mahitaji, unajidanganya mwenyewe tu. Wewe si kitu kabisa.” Wagalatia 6:3 (NLT) Ni katika huduma hizi ndogo ndogo ndipo
tunakua na kufanana na Kristo.
Yesu alichagua kufanya kazi za chini ambazo kila mtu aliziepuka:
kuosha miguu, kusaidia watoto, kuandaa chakula cha asubuhi, kutumikia wakoma,
hakuwa na kitu cha chini yake, kwa sababu alikuja kutumika. Haikuwa badala ya
ukuu wake kwamba alifanya haya, lakini kwa sababu yake, na anatutarajia tufuate
mfano wake. (Yohana 13:15)
Kazi ndogo ndogo mara nyingi huonyesha moyo mkubwa. Moyo wako wa
kitumishi unaonekana katika matendo madogo ambayo wengine hawafikiri kuyatenda,
kama vile Paulo alivyokusanya kuni kwa ajili ya moto wa kuwapa joto wote baada
ya kuvunjikiwa na meli. (Matendo 28:3) Alikuwa amechoka kama wengine, lakini
alifanya kile mtu alikihitaji. Hakuna kazi iliyo chini yako unapokuwa na moyo
ya kiutumishi.
Nafasi kubwa mara nyingi hujificha kwenye kazi ndogo. Mambo madogo
maishani huwa msingi wa ukubwa. Usitafute nafasi kubwa za kumtumikia Mungu.
Wewe fanya tu hizo kazi ndogo ndogo, na Mungu atakupangia chochote anachokutaka
ufanye. Lakini kabla ya kufanya mambo yasiyo ya kawaida, jaribu kufanya katika
njia za kawaida. (Luka 16:10-12)
Nafasi kubwa mara nyingi hujificha kwenye kazi ndogo. |
Watumishi
halisi ni waminifu kwa huduma yao. Watumishi
humaliza kazi yao, hutimiza majukumu yao, hutunza ahadi zao, na humaliza
wanachokifanya. Hawaachi kazi nusu, na hawaachi wanapovunjwa moyo. Ni wa
kuaminika na kutegemewa.
Uaminifu umekuwa sifa nadra. (Zaburi 12:1; Mithali 20:6; Wafilipi
2:19-22) Watu wengi hawajui maana ya ahadi. Wanaweka ahadi kienyeji tu,
wanazivunja kwa sababu ndogo tu bila kujali wala kuhuzunika. Kila wiki,
makanisa na mashirika mengine huwa na dharura kwa sababu watu waliojitolea
hwakuandaa, hawakuonekana, au hata hawakutoa taarifa kwamba hawangekuja.
Je, unaweza kuwajibishwa na wengine? Je, kuna ahadi unazotakiwa
kutunza, nadhiri unazohitaji kutimiza, au ahadi unazotakiwa kuziheshimu? Hiki
ni kipimo. Mungu anapima uaminifu wako. Kama utashinda mtihani huo, unakuwa
katika kundi zuri: Ibrahimu, Musa, Samweli, Daudi, Danieli, Timotheo, na Paulo
wote waliitwa watumishi waaminifu
wa Mungu. Bora zaidi, Mungu amekuahidi tuzo mbinguni kwa sababu ya uaminifu.
Hebu fikiri utakavyokuwa siku moja Mungu akikuambia, “Vyema, mtumishi wangu
mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika kiasi hiki kidogo, sasa nitakupa
majukumu makubwa zaidi. Hebu tusherehekee pamoja!” Mathayo 25:23 (NLT)
Hakika watumishi waaminifu hawastaafu. Hutumika kwa uaminifu
maadam wako hasi. Unaweza kustaafu kazini kwako, lakini hutastaafu kumtumikia
Mungu.
Watumishi
halisi hawatafuti kujilikana. Watumishi hawajitangazi wala
kutaka kujulikana. Badala ya kutenda kwa kujionyesha au kuvaa kuonyesha
mafanikio, wao, “huvaa vazi la unyenyekevu, ili
kutumikiana.” 1 Petro 5:5 (TEV) Wakishukuriwa
kwa huduma yao, huipokea kwa unyenyekevu lakini hawaruhusu sifa kupita kiasi
ziwaondoe kwenye utumishi wao.
Paulo aliweka wazi aina ya huduma inayoonekana ya kiroho lakini hakika ni maagizo na kujionyesha, tendo la
kutafuta kujulikana. Aliita “huduma ya jicho” Waefeso 6:6 (KJV); Wakolosai 3:22 (KJV) – kutumik ili tuwavvutie
watu wajue jinsi tulivyo wa kiroho. Hii ilikuwa dhamabi ya Mafarisayo.
Waligeuza kusaidia wengine, utoaji, hata sala kuwa kitu cha maonyesho kwa
wengine. Yesu alichukia tabia hii na akaonya, “unapofanya tendo
jema, usijaribu kujionyesha. Ukifanya hivyo, hutapata thawabu kutoka kwa Baba
yako wa mbinguni.” Mathayo 6:1 (CEV)
Kujitangaza na utumishi havichangamani. Watumishi halisi
hawatumiki ili wasifiwe na wengine. Wanaishi ili watazamwe na mmoja. Kama Paulo
alivyosema, “Kama ningelikuwa najaribu kufurahisha watu,
nisingekuwa mtumishi wa Kristo.” Wagalatia
1:10 (NIV)
Huwezi kuwapata watumishi wa kweli wakitafuta kujulikana, ni dhahiri
kabisa, wao huepuka hali hiyo inapowezekana. Wanaridhika na kutumika kimya
kimya katika vivuli. Yusufu ni mfano madhubuti. Hakutafuta kujulikana, lakini
alitumika kimya kwa Potifa, kifungoni, na kwa mwoka mikate na mnyweshaji wa
Farao. Na Mungu alibariki moyo huo. Farao alipomwinua katika nafasi ya juu,
Yusufu bado alidumu na moyo wa utumishi, hata kwa ndugu zake waliomsaliti.
Kwa bahati mbaya, viongozi wengi siku hizi huanza kama watumishi
lakini huishia kuwa watu maarufu sana. Huchukuliwa na sifa, hawajui kwamba kuwa
kwenye nuru kali hupofusha.
Unaweza kuwa unatumika kwenye mazingira ya kutojulikana katika
maeneo madogo, ukijihisi kutojulikana wala kupewa shukrani. Sikiliza: Mungu
alikuweka ulipo kwa malengo. Amezihesabu vywele zote za kichwa chako, na anafahamu
anwani yako. Ni vyema ukae hapo mpaka akuhamishe. Atakujulisha kama anakuhitaji
sehemu nyingine. Huduma yako ni ya muhimu katika ufalme wa Mungu. “Kristo
… anapoonekana tena katika dunia hii, utaonekana pia – wewe halisi, wewe
uliyetukuka, Kwa sasa, ridhika na hali yako ya unyonge.” Wakolosai 3:4 (Msg)
Kuna orodha za watu mashuhuri (Halls of Fame) 750 katika Marekani
na vitabu 450 vya “Nani ni Nani” lakini huwezi kupata watumishi halisi katika
haya. Kujulikana hakuna maana kwa watumishi kwa sababu wanajua tofauti na
umuhimu wa watu. Unavyo viungo kadhaa vyenye sifa mwilini mwako ambavyo
ungeishi hata bila kuwa navyo. Ni viungo vilivyofichika vya mwili wako ambavyo
ni muhimu sana. Ndivyo ulivyo hata kwa mwili wa Kristo. Huduma ya muhimu sana
ni ile isiyoonekana. 1 Wakorintho 15:58 (Msg)
SIKU YA
THELATHINI NA TATU: JINSI WATUMISHI HALISI WANAVYOTENDA |
Kwa kujua hili usivunjike moyo pale unapojua huduma yako
haijulikani au hupati shukrani yoyote. Endelea kumtumikia Mungu! “Jiingizeni
katika kazi ya Bwana mkiwe na hakika kwamba hakuna mnachotenda kwa ajili yake
ni kupoteza muda na nguvu.” 1 Wakorintho 15:58 (Msg) Hata
huduma ndogo inatambuliwa na Mungu na itatunzwa. Kumbuka maneno ya Yesu: “Iwapa
kama wawakilishi wangu, mtampatia hata kikombe cha maji ya baridi mtoto mdogo,
hakika mtapewa thawabu.” Mathayo 10:42 (LB)
SIKU YA
THELATHINI NA TATU KUFIKIRI
JUU YA LENGO LANGU Jambo la Kutafakari: Nametumikia Mungu kwa kuwatumikia watu
wengine. Kifungu cha Kukumbuka: “Kama mkimpatia kikombe cha maji ya
baridi mmoja wa wadogo hawa wa wafuasi wangu, hakika mtapata dhawabu:”
Mathayo 10:42 (NLT) Swali la Kujiuliza: Je, ni sifa gani kati ya zile sita za
mtumishi halisi inanipa changamoto kubwa? |
Siku ya
Thelathini na Nne: Kufikiri Kama Mtumishi
Mtumishi
wango Kalebu anafikiri tofauti na ananifuata kikamilifu.
Hesabu 14:24 (NCV)
Jifikirini
wenyewe kama vile Kristo Yesu alivyojifikiria mwenyewe.
Wafilipi 2:5 (Msg)
Huduma huanzia akilini.
Kuwa mtumishi kunahitaji badiliko la akili, kubadilika katika nia
yako. Mungu huchunguza sababu ya kufanya kitu Fulani, lakinsi siyo kitu
tunachofanya. Nia ni ya muhimu sana kulio mafanikio yetu. Mfalme Amazia
alipoteza kibali kwa Mungu kwa sababu “Alifanya
kilichokuwa sawa machoni pa Bwana, lakini si kwa moyo wa kweli.” 2 Nyakati 25:2 (NRSV) Watumishi wa Mungu humtumikia Mungu wakiwa
na mawazo yenye mwelekeo wa aina tano:
Watumishi
hufikiri zaidi kuhusu wengine na siyo wao wenyewe. Watumishi
huangalia watu wengine na siyo wao binafsi. Huu ni unyenyekevu wa kweli; siyo
kujifikiria kuwa thamani yetu ni ndogo, lakini kujifikiria juu ya nafsi zetu kidogo.
Wao hujisahau nafsi zao. Paulo alisema “Jisalimisheni
nafsi zenu vya kutosha kuweza kutoa msaada kwa wengine.” Wafilipi 2:4 (Msg) Hii ndiyo maana ya “kupoteza maisha yako” –
Kujisahau ili kutumikia wengine. Tunapoacha kukazia mahitaji yetu binafsi,
tunaanza kuyafahamu mahitaji yaliyopo katika mazingira yetu.
Yesu “alijitoa kwa kuchukua hali ya mtumwa” Wafilipi 2:7 (GWT). Ni lini kwa mara ya mwisho ulijitoa nafsi
yako kwa faida ya mtu mwingine? Huwezi kuwa mtumishi kama umejaa nafsi yako
mwenyewe. Ni pale tu tunapojisahau nafsi zetu ndipo tunafanya vitu
vinavyostahili kukumbukwa.
Watumishi halisi hawajaribu kumtumikia Mungu kwa
malengo yao. Wanamruhusu Mungu awatumie kwa malengo yake. |
Sifa ya kujisahau nafsi yako, kama uaminifu, ni nadra sana. Katika
watu wote Paulo alijua Timotheo alikuwa mfano pekee ambao angetaja. (Wafilipi
2:20-21) Kufikiri kama mtumishi ni vigumu kwa sababu hutoa changamoto kwa
tatizo la msingi la maisha yangu: kwa asili mimi ni mwenye ubinafsi. Najifikiri
zaidi ndiyo maana unyenyekevu ni pambano la kila siku, somo la kujifunza tena
na tena. Nafasi za kuwa mtumishi hunisonga mara kumi nyingi kwa siku, ambapo ninapewa
uchaguzi wa kuamua kutimiza mahihaji yangu au kutimiza mahitaji ya wengine.
Tunaweza kupima moyo wetu wa utumishi kwa namna tunapoitikia pale
wengine wanavyotutendea kama watumishi. Je, unajibuje watu wanapokutumia tu,
wakijifanya wakubwa wako, au wanakutendea kama mtu mdogo sana kwao? Biblia
inasema, “Kama mtu atataka kukutumia isivyo haki, basi
tumia nafasi hiyo kuonyesha maisha ya mtumishi.”
Mathayo 5:41 (Msg)
Watumishi
hufikiri kama mawakili na sio wamiliki. Watumishi
wanakumbuka kwamba Mungu anamiliki vyote. Katika Biblia, wakili alikuwa mtu
aliyeamini na kukabidhiwa kutunza mali. Yusufu alikuwa mtumishi wa aina hiyo
kama mfungwa huko Misri. Potifa alimkabidhi Yusufu nyumba yake. Mtunza gereza
alimkabidhi Yusufu gereza lake. Hatimaye Farao alimkabidhi taifa zima. Utumishi
na uwakili huenda pamoja. 1Wakorintho 4:1 (NJB) Kwa kuwa Mungu anatutegemea
kuwa waaminifu katika yote mawili. Biblia inasema, “Kitu kimoja
kinachotakiwa kwa watumishi kama hao ni kwamba wawe waaminifu kwa bwana wao.” 1 Wakorintho 4:2 (TEV) Je unatunzaje raslimali Mungu
aliyokukabidhi?
Ili uwe mtumishi halisi unatakiwa kutatua tatizo la fedha Katika
maisha yako. Yesu alisema “Hakuna mtumishi anayeweza kutumikia
mabwana wawili … Huwezi kutumikia Mungu na fedha.”
Luka 16:13 (NIV) Hakusema, “Hamtakiwi,”
lakini alisema “Hamuwezi.”
Haiwezekani. Kuishi kwa ajili ya huduma na kwa ajili ya fedha ni malengo mawili
tofauti kabisa. Je, ni lipi utachagua? Kama wewe ni mtumishi wa Mungu huwezi
kujipa kazi ya pili. Muda wako wote ni wa Mungu. Anakazia uaminifu mkamilifu,
siyo uaminifu nusu.
Fedha zina uwezo mkubwa wa kuchukua nafasi ya Mungu katika maisha
yako. Watu wengi wanapotoshwa njia ya utumishi kwa tamaa ya mali kuliko kitu
kingine chochote. Wanasema, “Baada ya kufanikiwa mipango yangu ya fedha,
nitamtumikia Mungu.” Huo ni uamuzi wa kipumbavu ambao utawapa majuto milele.
Yesu akiwa Bwana wako, fedha hukutumikia, lakini fedha zikiwa Bwana wako,
unakuwa mtumwa wa fedha. Utajiri kwa hakika si dhambi lakini kushindwa kuutumia
kwa utukufu wa Mungu ni dhambi. Watumishi wa Mungu mara nyingi wanajali zaidi
huduma kuliko fedha.
Biblia iko wazi: Mungu hutumia fedha kujaribu uaminifu wako kama
mtumishi. Ndiyo maana Yesu alizungumzia sana kuhusu fedha kuliko hata
alivyozungumzia mbingu au kuzimu alisema, “Kama hamjawa
waaminifu katika mali ya dunia, nani atawaamini na kuwakabidhi utajiri wa kweli? Luka 16:11 (NIV) Unavyotumia fedha zako huwa na matokeo makubwa
kwa kiasi ambacho Mungu anaweza kubariki maisha yako.
Katika sura ya 31, nilitaja aina mbili za watu: Wajenga Ufalme na
Wajenga Utajiri. Wote wana kipawa cha kufanya mradi wao kukua, kwa mikataba na
mauzo na kupata faida. Wajenga Utajiri huendelea kujirundikia mali hata wapate mali
nyingi kiasi gani, lakini Wajenga Ufalme hubadili kanuni hiyo. Bado hujaribu
kutengeneza fedha kwa kadiri ya uwezo wao, lakini wanafanya hayo ili wazitoe.
Wanatumia utajiri huo kufanya kazi ya kanisa, na huduma yake kwa ulimwengu.
Katika kanisa la Saddleback, tuna kikundi cha mameneja na wamiliki
wa miradi ya biashara ambao wanajitahidi kuzalisha kwa uwezo wao ili waweze
kutoa kwa kadiri ya uwezo wao katika kuendeleza ufalme wa Mungu. Nakutia moyo
uongee na Mchungaji wako ili kuanzisha kikundi cha kujenga ufalme kanisani
mwenu. Kwa msaada angalia nyongeza ya 2.
SIKU YA THELATHINI NA NNE: KUFIKIRI KAMA MTUMISHI |
Ushindani kati ya watumishi wa Mungu haufai kwa sababu nyingi:
Sote tuko timu moja; lengo letu ni kufanya Mungu aonekane mwema, siyo sisi
wenyewe; tumepewa majukumu tofauti; na sisi sote tumefinyagwa kipekee. Paulo
alisema, “Hatutajilinganisha sisi kwa sisi kana kwamba
wengine wetu ni wema na wengine ni wabaya. Tuna mambo mazuri ya kufanya katika
maisha yetu. Kila mmoja wetu ni wa asili.”
Wagalatia 5:26 (Msg)
Hakuna nafasi ya wivu kati ya watumishi. Unapokuwa unatumika kwa bidii,
huna muda muda wa kulaumu. Muda unaotumika kulaumu ungetumika vyema kwa
kuhudumu. Martha alipolalamika kwa Yesu kwamba Mariamu alikuwa hasaidii kazi,
alipoteza moyo wake wa utumishi. Watumishi halisi hawalalamiki dhidi ya
kutotendewa haki, hawajihurumii, wala hawawachukii wale wasiotumika. Wao
humwamini Mungu wakidumu katika kutumika.
Siyo kazi yetu kutathmini watumishi wengine wa Bwana. Biblia
inasema, “Wewe ni nani kumuhukumu mtumishi wa mtu
mwingine? Bwana ataamua iwapo mtumishi wake amefaulu.” Warumi 14:4 (GWT) Pia si kazi yetu kujitetea dhidi ya lawama,
Mwachie Bwana wako ashughulikie. Fuata mfano wa Musa, aliyeonyesha unyenyekevu
wa kweli alipokabiriwa na upinzani; kama alivyofanya Nehemia, ambaye aliwajibu
wapinzani wake kuwa, “Kazi yangu ni ya muhimu sana hivyo
siwezi kuacha sasa … niwatembelee.” Nehemia
6:3 (CEV)
Ukitumika kama Yesu, tegemea kulaumiwa. Ulimwengu, hata kanisa,
hawaelewi Mungu anathamini nini. Moja ya matendo mazuri ya upendo aliyotendewa
Yesu lililaumiwa na wanafunzi wake. Mariamu alichukua kitu cha thamani
alichokuwa nacho, manukato ya thamani, na akammiminia Yesu. Huduma yake kubwa
ilikuwa “Kupoteza”
kwa maoni ya wanafunzi, lakini Yesu aliita “tendo la maana.” Mathayo 26:10 (Msg) Na hilo ndilo lilitakiwa. Huduma yako kwa
Kristo haipotei kamwe hata kama watu wengine watasemaje.
Watumishi
huweka msingi wa utambulisho wao kwa Kristo. Kwa
sababu wanakumbuka kwamba wanapendwa na kukubaliwa kwa neema. Watumishi
hawahitaji kuthibitisha uthamani wao. Kwa moyo hukubali kazi ambazo watu wenye
hofu wangesema ni kazi zilizo “chini sana kwao”. Moja ya mifano madhubuti ya
kutumika kwa kujiamini ni tendo la Yesu kuosha miguu ya wafuasi wake. Kuosha
miguu ilikuwa sawa na kijana anayesafisha viatu mitaani, kazi isiyo na heshima.
Lakini Yesu alijua alikuwa nani, kwa hiyo kazi haikutishia utu wake. Biblia
inasema, “Yesu alijua kwamba Baba ameweka vitu vyote chini
ya uwezo wake, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu … hivyo aliinuka kutoka
kwenye chakula, akachukua vazi lake la juu, na akajifunga kitambaa kiunoni.” Yohana 13:3-4 (NIV)
Kama unataka kuwa mtumishi lazima upate kitambulisho cha utu wako
katika Kristo. Ni watu wenye amani ndio wanaweza kutumika. Watu wenye mashaka
daima wana hofu ya jinsi wanavyoonekana kwa wengine. Wanaogopa kuonekana
udhaifu wao na hivyo kujificha kwenye tabaka la majivuno na maigizo. Kadiri
ulivyo na mashaka, ndivyo utakavyotaka na watu wakutumikie, na ndivyo utahitaji
zaidi kukubalika kwao.
Henri Nouwen alisema, “Ili kuwaa na huduma kwa watu wengi lazima
tuwafie; yaani, tuache kupima umuhimu na thamani yetu kwa kipimo cha wengine …
Ndipo tunakuwa huru wa wenye huruma.” Unapoweka msingi wa uthamani na
utambulisho wako kwa uhusiano wako na Kristo, unawekwa huru mbali na matazamio ya
wengine, na hiyo hukupa uhuru wa kuwatumikia vyema zaidi.
Watumishi hawahitaji kufunika kuta zao kwa vyeti vyao kuthibitisha
kazi zao. Hawasisitizi kuitwa kwa vyeo vyao, na hawavai mavazi ya ukubwa.
Watumishi hawaoni umuhimu wa alama za wadhifa, na hawapimi uthamani wao
kulingana na walichofanya. Paulo alisema, “Unaweza kujisifia
mwenyewe, lakini kibali pekee ni kutoka kwa Bwana.”
2 Wakorintho 10:18 (CEV)
Kama kuna mtu yeyote aliyekuwa na nafasi ya maisha ya kujitukuza
ni Yakobo, ndugu yake na Yesu. Alikuwa na sifa ya kukaa pamoja na yesu kama
kaka yake. Lakini katika utangulizi wa waraka wake, anajitaja tu kama, “Mtumishi
wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo.” Yakobo 1:1
Kadiri unavyokuwa karibu na Yesu, ndivyo unavyopunguza kujitukuza.
Kadiri
unavyokuwa karibu na Yesu ndivyo unavyopunguza kujitukuza |
SIKU YA THELATHINI NA NNE KUFIKIRA
JUU YA LENGO LANGU Jambo la Kutafakari: Ili kuwa mtumishi lazima nifikiri kama
mtumishi. Kifungu cha kukumbuka: “Nia yenu iwe sawa ni ile ya Yesu Kristo.”
Wafilipi 2:5 (NIV) Swali la kujiuliza: Je, ninaangalia sana kutumikiwa au
kutafuta njia za kutumikia wengine? |
Siku ya
Thelathini na Tano: Nguvu Ya Mungu Katika Udhaifu Wako
Sisi
tu dhaifu … lackini kwa nguvu za Mungu tutaishi naye ili kuwatumikia.
2 Wakorintho 13:4 (NIV)
Mimi
niko pamoja nawe; hiyo inakutosha. Nguvu yangu
hudhihirika vyema katika watu dhaifu.
2 Wakorintho 12:9 a (LB)
Mungu hupenda kutumia watu dhaifu.
Kila mtu ana udhaifu. Kusema ukweli, una lundo la makosa na
mapungufu: ya kimwili, kihisia, kiakili, na kiroho. Unaweza pia kuwa na
mazingira yaliyo zaidi ya uwezo wako yanayokudhoofisha, kama vile mapungufu ya
kifedha au mahusiano. Jambo la muhimu ni kile unachokifanya na hali hizi. Mara
nyingi tunakana udhaifu wetu, tunatetea, tunatoa udhuru, tunaficha, na
kuchukia. Hii humzuia Mungu kutumia udhaifu huo kama upendavyo.
Mungu ana mtazamo tofauti kwa udhaifu wako. Anasema, “Mawazo
yangu na njia zangu ziko juu kuliko zenu.”
Isaya 55:9 (CEV) Hivyo mara nyingi yeye hutenda kinyume kabisa na mategemeo
yetu. Tunafikiri Mungu hupenda tu kutumia nguvu zetu, lakini pia anapenda
kutumia udhaifu wetu kwa ajili ya utukufu wake.
Biblia inasema, “Mungu kwa makusudi alichagua … kilicho
dhaifu machoni pa ulimwengu ili kuviaibisha vyeye nguvu.” 1 Wakorintho 1:27 (TEV) Madhaifu yako siyo bahati mbaya. Mungu
aliyaruhusu kwa makusudi kabisa, kwa lengo la kudhihirisha nguvu zake kupitia
wewe.
Mungu kamwe hajapendezwa na nguvu na utoshelevu wa binafsi.
Hakika, anavutwa na watu dhaifu, wenye kukubali hivyo. Yesu alihesabu utambuzi
wa uhitaji wetu kuwa kama, “mashini wa rohoni.” Huu ndio msimamo wa kwanza anaoubariki. (Mathayo 5:3)
Biblia imejaa mifano ya namna Mungu anavyopenda kutumia watu wa
kawaida wenye mapungufu kufanya mambo yasiyo ya kawaida bila kujali udhaifu
wao. Kama Mungu angetumia tu watu wakamilifu, hakuna ambacho kingetendeka, kwa
sababu hakuna mmoja wetu asiye na mapungufu. Kwamba Mungu anatumia watu wenye
mapungufu ni habari ya kututia moyo sisi sote.
Udhaifu, au “mwiba”
kama Paulo alivyouita, (2 Wakorintho 12:7) siyo dhambi au uovu au tabia mbaya
unayoweza kuibadili, mfano, ulafi, au kukosa uaminifu. Udhaifu ni upungufu
wowote uliorithi au huna uwezo wa kuubadili. Unaweza kuwa upungufu wa kimwili, kama ulemavu, ugonjwa usiopona au nguvu kidogo. Waweza kuwa
upungufu wa kihisia,
kama vile kovu la hofu kuu, tumbukumbu inayoumiza, udhaifu wa nafsi, au
mwelekeo wa kurithi. Au waweza kuwa upungufu wa kipawa au akili.
Sote si watu wenye akili nyingi au kipawa.
Kama Mungu angetumia tu watu wakamilifu hakuna
ambacho kingetendeka. |
Kiri
udhaifu wako. Ukikubali upungufu wako. Acha
kujifanya una kila kitu. Uwe mkweli kwako mwenyewe. Badala ya kuishi kwa kukana
na kutoa udhuru, chukua muda kuainisha udhaifu wako. Unaweza kufanya orodha
yake.
Ukiri mkubwa wa aina mbili katika Agano Jipya unaelezea
unachohitaji ili kuishi maisha ya utoshelevu. Ukiri wa kwanza ulitolewa na
Petro, alimwambia Yesu “Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu
aliye hai.” Mathayo 16:16 (NIV) Ukiri wa pili ni ule wa Paulo alipowaeleza
kundi lililotaka kumwabudu kama Mungu, “Sisi ni wanadamu
tu kama ninyi.” Matendo 14:15 (NCV) Kama
unataka Mungu akutumie, lazima ujue Mungu ni nani na ujue wewe ni nani.
Wakristo wengi, hasa viongozi, husahau ukweli huu wa pili: sisi ni binadamu tu!
Kama italazimu ufikwe na tatizo ili ukubali ukweli huu, Mungu hatasita
kuliruhusu, kwa sababu anakupenda.
Ridhika
na udhaifu wako. Paulo anasema, “Nafurahi
kujisifia udhaifu wangu, ili kwamba nguvu ya Kristo ifanye kazi kupitia mimi.
Kwa kuwa nafahamu yote ni kwa ajili ya Kristo. Nimeridhika kabisa na udhaifu
wangu.” 2 Korintho 12:9-10a (NLT) Mwanzoni hili halileti maana.
Tunataka kuwekwa huru kutoka udhaifu wetu. Haturidhiki nao! Lakini kuridhika ni
udhihirisho wa imani katika wema wa Mungu. Ni kusema, “Mungu naamini unanipenda
na unajua nini kinanifaa zaidi.”
Paulo anatupatia sababu kadhaa za kuridhika na udhaifu wetu wa
kuzaliwa nao. Kwanza, zinatufanya tumtegemee Mungu. Akirejea kwenye udhaifu
wake mwenyewe ambao Mungu alikataa kumwondolea, Paulo alisema, “Nina
furaha sana juu ya mwiba … kwa kuwa ninapokuwa dhaifu ndipo nina nguvu … nikiwa
na kidogo ndipo ninapomtegemea zaidi.”
2 Wakorintho 12:10 (LB) Unapojihisi dhaifu, Mungu anakukumbusha kumtegemea.
Udhaifu watu pia huzuia majivuno. Hutufanya wanyenyekevu. Paulo
anasema, “Ili nisiwe na kiburi, nilipewa zawadi ya
udhaifu. Ili kunifanya kila wakati nijue mipaka yangu.” 2 Wakorintho 12:7 (Msg) Mara nyingi Mungu huambatanisha udhaifu
mkubwa na uwezo mkubwa ili kudhibiti ubinafsi wetu. Upungufu unaweza kufanya
kazi kama kizuizi cha kutufanya tusiende kasi zaidi na kumtangulia Mungu.
Gidioni alipotayarisha jeshi la watu 32,000 ili kupigana na
Wamidiani Mungu alilipunguza mpaka watu 300 tu, akifanya maajabu ya watu 450
kwa mtu mmja walipoenda kupigana na jeshi la watu 135,000. Ilionekana kuwa
kujiletea janga kubwa, lakini Mungu alifanya hivyo ili Israel wajue kwamba
ilikuwa ni nguvu za Mungu, siyo nguvu zao wenyewe zilizowaokoa.
Huduma yako bora zaidi itatokana na maumivu yako ya
kina. |
Zaidi ya yote, udhaifu wetu huongeza uwezo wetu wa huruma na
huduma. Tunaweza kuwa na huruma zaidi na kujali udhaifu wa wengine. Mungu
anakutaka uwe na huduma kama ya yesu duniani. Maana yake watu wengine watapata
uponyaji katika vidonda vyako. Ujumbe wako mkubwa katika maisha na huduma yako
bora zaidi itatokana na maumivu yako ya kina. Mambo yanayokuudhi na kuyaonea
haya zaidi, na usiyapende kuyasema, ndiyo sana Mungu anazoweza kutumia kwa
nguvu sana kuponya wengine.
Mmishenari mkubwa Hudson Taylor alisema, “Watu maarufu wote wa
Mungu walikuwa watu wadhaifu.” Udhaifu wa Musa ulikuwa hasira, ilimsababisha
kumwua Mmisri, kupiga mwamba uliotakiwa kuusemesha, na kuvunja mbao za amri kumi.
Lakini Mungu alimgeuza Musa kuwa “mtu mpole kuliko wote duniani.” (Hesabu 12:3)
Udhaifu wa Gidioni ulikuwa kutokujiamini na hali ya hofu kuu.
Lakini Mungu alimgeuza kuwa “mtu shujaa.”
Wamuzi 6:12 (KJV) Udhaifu wa Ibrahimu ulikuwa uoga. Si mara moja, mara mbili
alidai mke wake alikuwa dada yake ili ajilinde. Lakini Mungu alimgeuza Ibrahimu
na kuwa “Baba wa walio na imani.” Warumi 4:11 (NLT) Petro mwenye haraka na asiye na msimamo
alkuwa “mwamba.”
Mathayo 16:18 (TEV) Daudi mzinzi alikuwa “mtu aupendezaye
moyo wangu.” Matendo 13:22 (NLT) Na Yohana mmoja wa watoto wa ngurumo wenye
majivuno, akawa “Mtume wa upendo.”
Orodha inaweza kuendelea. “Ingelihitaji muda
mrefu kutoa imani ya … Baraka, Samsoni, Yefta, Daudi, Samweli, na manabii wote
… udhaifu wao uligeuzwa kuwa nguvu.” Waebrania
11:32-34 (NLT) Mungu ni bingwa wa kugeuza udhaifu kuwa nguvu. Anapenda kuchukua
udhaifu wako mkubwa na augeuze.
Shirikisha
udhaifu wako kwa uaminifu. Huduma huanza na udhaifu. Kadiri
unavyoacha kujilinda, ukavua vazi la bandia, na ukashirikisha wengine vita
vyako, ndipo Mungu ataweza kukutumia kuwatumikia wengine. Paulo alitoa
kielelezo cha udhaifu wake katika nyaraka zake.
l Kushindwa kwake: “ninapotaka kutenda mema nashindwa, ninapojaribu
nisitende mabaya nayatenda.” Warumi 7:19 (NLT)
l Hisi zake: “nimewaambia hisia zangu zote.” 2 Wakorintho 6:11 (EB)
l Mambo ya kuvunja moyo: “tulivunjwa moyo
kiasi cha kushindwa kabisa, na tukafikiri tusingeweza kuishi kabisa.” 2 Wakorintho 1:8 (NLT)
l Hofu zake: “nilipokuja kwenu, nilikuwa mdhaifu na
mwenye hofu na kutetemeka.” 1 Wakorintho 2:3 (NCV)
Kwa kweli ni hatari. Laweza kuwa jambo la kuogofya kupunguza
ulinzi wako na kuweka wazi maisha yako kwa watu wengine. Unapofunua kushindwa
kwako, hisia, mambo ya kukuvunja moyo, na hofu, unajiweka katika hali ya
kukataliwa. Lakini faida zake zinastahili hatari hiyo. Udhaifu huleta uhuru kihisia.
Kujiweka wazi huleta ahueni ya moyo, huondoa hofu zako, na ni hatua ya kwanza
katika kupata uhuru.
Tumeona kwamba Mungu “huwapa neema wanyenyekevu,” lakini wengi hawaelewi vyema unyenyekevu. Unyenyekevu siyo
kujiweka chini au kukana nguvu zako; badala yake, ni kuwa wazi kuhusu udhaifu
wako. Kadiri unavyokuwa wazi ndivyo unavyopata neema ya Mungu zaidi. Pia
utapokea neema kutoka kwa wengine. Kukubali udhaifu ni sifa ya kudumu; kwa asili
tunavutwa na watu wanyenyekevu. Maigizo hufukuza lakini uhalisi huvuta, na
kukubali udhaifu ni mlango wa uhusiano wa karibu.
Siku ya
Thelathini na Tano: Nguvu Ya Mungu Katika Udhaifu Wako
Sisi
tu dhaifu … lackini kwa nguvu za Mungu tutaishi naye ili kuwatumikia.
2 Wakorintho 13:4 (NIV)
Mimi
niko pamoja nawe; hiyo inakutosha. Nguvu yangu
hudhihirika vyema katika watu dhaifu.
2 Wakorintho 12:9 a (LB)
Mungu hupenda kutumia watu dhaifu.
Kila mtu ana udhaifu. Kusema ukweli, una lundo la makosa na
mapungufu: ya kimwili, kihisia, kiakili, na kiroho. Unaweza pia kuwa na
mazingira yaliyo zaidi ya uwezo wako yanayokudhoofisha, kama vile mapungufu ya
kifedha au mahusiano. Jambo la muhimu ni kile unachokifanya na hali hizi. Mara
nyingi tunakana udhaifu wetu, tunatetea, tunatoa udhuru, tunaficha, na
kuchukia. Hii humzuia Mungu kutumia udhaifu huo kama upendavyo.
Mungu ana mtazamo tofauti kwa udhaifu wako. Anasema, “Mawazo
yangu na njia zangu ziko juu kuliko zenu.”
Isaya 55:9 (CEV) Hivyo mara nyingi yeye hutenda kinyume kabisa na mategemeo
yetu. Tunafikiri Mungu hupenda tu kutumia nguvu zetu, lakini pia anapenda
kutumia udhaifu wetu kwa ajili ya utukufu wake.
Biblia inasema, “Mungu kwa makusudi alichagua … kilicho
dhaifu machoni pa ulimwengu ili kuviaibisha vyeye nguvu.” 1 Wakorintho 1:27 (TEV) Madhaifu yako siyo bahati mbaya. Mungu
aliyaruhusu kwa makusudi kabisa, kwa lengo la kudhihirisha nguvu zake kupitia
wewe.
Mungu kamwe hajapendezwa na nguvu na utoshelevu wa binafsi.
Hakika, anavutwa na watu dhaifu, wenye kukubali hivyo. Yesu alihesabu utambuzi
wa uhitaji wetu kuwa kama, “mashini wa rohoni.” Huu ndio msimamo wa kwanza anaoubariki. (Mathayo 5:3)
Biblia imejaa mifano ya namna Mungu anavyopenda kutumia watu wa
kawaida wenye mapungufu kufanya mambo yasiyo ya kawaida bila kujali udhaifu
wao. Kama Mungu angetumia tu watu wakamilifu, hakuna ambacho kingetendeka, kwa
sababu hakuna mmoja wetu asiye na mapungufu. Kwamba Mungu anatumia watu wenye
mapungufu ni habari ya kututia moyo sisi sote.
Udhaifu, au “mwiba”
kama Paulo alivyouita, (2 Wakorintho 12:7) siyo dhambi au uovu au tabia mbaya
unayoweza kuibadili, mfano, ulafi, au kukosa uaminifu. Udhaifu ni upungufu
wowote uliorithi au huna uwezo wa kuubadili. Unaweza kuwa upungufu wa kimwili, kama ulemavu, ugonjwa usiopona au nguvu kidogo. Waweza kuwa
upungufu wa kihisia,
kama vile kovu la hofu kuu, tumbukumbu inayoumiza, udhaifu wa nafsi, au
mwelekeo wa kurithi. Au waweza kuwa upungufu wa kipawa au akili.
Sote si watu wenye akili nyingi au kipawa.
Kama Mungu angetumia tu watu wakamilifu hakuna
ambacho kingetendeka. |
Kiri
udhaifu wako. Ukikubali upungufu wako. Acha
kujifanya una kila kitu. Uwe mkweli kwako mwenyewe. Badala ya kuishi kwa kukana
na kutoa udhuru, chukua muda kuainisha udhaifu wako. Unaweza kufanya orodha
yake.
Ukiri mkubwa wa aina mbili katika Agano Jipya unaelezea
unachohitaji ili kuishi maisha ya utoshelevu. Ukiri wa kwanza ulitolewa na
Petro, alimwambia Yesu “Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu
aliye hai.” Mathayo 16:16 (NIV) Ukiri wa pili ni ule wa Paulo alipowaeleza
kundi lililotaka kumwabudu kama Mungu, “Sisi ni wanadamu
tu kama ninyi.” Matendo 14:15 (NCV) Kama
unataka Mungu akutumie, lazima ujue Mungu ni nani na ujue wewe ni nani.
Wakristo wengi, hasa viongozi, husahau ukweli huu wa pili: sisi ni binadamu tu!
Kama italazimu ufikwe na tatizo ili ukubali ukweli huu, Mungu hatasita
kuliruhusu, kwa sababu anakupenda.
Ridhika
na udhaifu wako. Paulo anasema, “Nafurahi
kujisifia udhaifu wangu, ili kwamba nguvu ya Kristo ifanye kazi kupitia mimi.
Kwa kuwa nafahamu yote ni kwa ajili ya Kristo. Nimeridhika kabisa na udhaifu
wangu.” 2 Korintho 12:9-10a (NLT) Mwanzoni hili halileti maana.
Tunataka kuwekwa huru kutoka udhaifu wetu. Haturidhiki nao! Lakini kuridhika ni
udhihirisho wa imani katika wema wa Mungu. Ni kusema, “Mungu naamini unanipenda
na unajua nini kinanifaa zaidi.”
Paulo anatupatia sababu kadhaa za kuridhika na udhaifu wetu wa
kuzaliwa nao. Kwanza, zinatufanya tumtegemee Mungu. Akirejea kwenye udhaifu
wake mwenyewe ambao Mungu alikataa kumwondolea, Paulo alisema, “Nina
furaha sana juu ya mwiba … kwa kuwa ninapokuwa dhaifu ndipo nina nguvu … nikiwa
na kidogo ndipo ninapomtegemea zaidi.”
2 Wakorintho 12:10 (LB) Unapojihisi dhaifu, Mungu anakukumbusha kumtegemea.
Udhaifu watu pia huzuia majivuno. Hutufanya wanyenyekevu. Paulo
anasema, “Ili nisiwe na kiburi, nilipewa zawadi ya
udhaifu. Ili kunifanya kila wakati nijue mipaka yangu.” 2 Wakorintho 12:7 (Msg) Mara nyingi Mungu huambatanisha udhaifu
mkubwa na uwezo mkubwa ili kudhibiti ubinafsi wetu. Upungufu unaweza kufanya
kazi kama kizuizi cha kutufanya tusiende kasi zaidi na kumtangulia Mungu.
Gidioni alipotayarisha jeshi la watu 32,000 ili kupigana na
Wamidiani Mungu alilipunguza mpaka watu 300 tu, akifanya maajabu ya watu 450
kwa mtu mmja walipoenda kupigana na jeshi la watu 135,000. Ilionekana kuwa
kujiletea janga kubwa, lakini Mungu alifanya hivyo ili Israel wajue kwamba
ilikuwa ni nguvu za Mungu, siyo nguvu zao wenyewe zilizowaokoa.
Huduma yako bora zaidi itatokana na maumivu yako ya
kina. |
Zaidi ya yote, udhaifu wetu huongeza uwezo wetu wa huruma na
huduma. Tunaweza kuwa na huruma zaidi na kujali udhaifu wa wengine. Mungu
anakutaka uwe na huduma kama ya yesu duniani. Maana yake watu wengine watapata
uponyaji katika vidonda vyako. Ujumbe wako mkubwa katika maisha na huduma yako
bora zaidi itatokana na maumivu yako ya kina. Mambo yanayokuudhi na kuyaonea
haya zaidi, na usiyapende kuyasema, ndiyo sana Mungu anazoweza kutumia kwa
nguvu sana kuponya wengine.
Mmishenari mkubwa Hudson Taylor alisema, “Watu maarufu wote wa
Mungu walikuwa watu wadhaifu.” Udhaifu wa Musa ulikuwa hasira, ilimsababisha
kumwua Mmisri, kupiga mwamba uliotakiwa kuusemesha, na kuvunja mbao za amri kumi.
Lakini Mungu alimgeuza Musa kuwa “mtu mpole kuliko wote duniani.” (Hesabu 12:3)
Udhaifu wa Gidioni ulikuwa kutokujiamini na hali ya hofu kuu.
Lakini Mungu alimgeuza kuwa “mtu shujaa.”
Wamuzi 6:12 (KJV) Udhaifu wa Ibrahimu ulikuwa uoga. Si mara moja, mara mbili
alidai mke wake alikuwa dada yake ili ajilinde. Lakini Mungu alimgeuza Ibrahimu
na kuwa “Baba wa walio na imani.” Warumi 4:11 (NLT) Petro mwenye haraka na asiye na msimamo
alkuwa “mwamba.”
Mathayo 16:18 (TEV) Daudi mzinzi alikuwa “mtu aupendezaye
moyo wangu.” Matendo 13:22 (NLT) Na Yohana mmoja wa watoto wa ngurumo wenye
majivuno, akawa “Mtume wa upendo.”
Orodha inaweza kuendelea. “Ingelihitaji muda
mrefu kutoa imani ya … Baraka, Samsoni, Yefta, Daudi, Samweli, na manabii wote
… udhaifu wao uligeuzwa kuwa nguvu.” Waebrania
11:32-34 (NLT) Mungu ni bingwa wa kugeuza udhaifu kuwa nguvu. Anapenda kuchukua
udhaifu wako mkubwa na augeuze.
Shirikisha
udhaifu wako kwa uaminifu. Huduma huanza na udhaifu. Kadiri
unavyoacha kujilinda, ukavua vazi la bandia, na ukashirikisha wengine vita
vyako, ndipo Mungu ataweza kukutumia kuwatumikia wengine. Paulo alitoa
kielelezo cha udhaifu wake katika nyaraka zake.
l Kushindwa kwake: “ninapotaka kutenda mema nashindwa, ninapojaribu
nisitende mabaya nayatenda.” Warumi 7:19 (NLT)
l Hisi zake: “nimewaambia hisia zangu zote.” 2 Wakorintho 6:11 (EB)
l Mambo ya kuvunja moyo: “tulivunjwa moyo
kiasi cha kushindwa kabisa, na tukafikiri tusingeweza kuishi kabisa.” 2 Wakorintho 1:8 (NLT)
l Hofu zake: “nilipokuja kwenu, nilikuwa mdhaifu na
mwenye hofu na kutetemeka.” 1 Wakorintho 2:3 (NCV)
Kwa kweli ni hatari. Laweza kuwa jambo la kuogofya kupunguza
ulinzi wako na kuweka wazi maisha yako kwa watu wengine. Unapofunua kushindwa
kwako, hisia, mambo ya kukuvunja moyo, na hofu, unajiweka katika hali ya
kukataliwa. Lakini faida zake zinastahili hatari hiyo. Udhaifu huleta uhuru kihisia.
Kujiweka wazi huleta ahueni ya moyo, huondoa hofu zako, na ni hatua ya kwanza
katika kupata uhuru.
Tumeona kwamba Mungu “huwapa neema wanyenyekevu,” lakini wengi hawaelewi vyema unyenyekevu. Unyenyekevu siyo
kujiweka chini au kukana nguvu zako; badala yake, ni kuwa wazi kuhusu udhaifu
wako. Kadiri unavyokuwa wazi ndivyo unavyopata neema ya Mungu zaidi. Pia
utapokea neema kutoka kwa wengine. Kukubali udhaifu ni sifa ya kudumu; kwa asili
tunavutwa na watu wanyenyekevu. Maigizo hufukuza lakini uhalisi huvuta, na
kukubali udhaifu ni mlango wa uhusiano wa karibu.
SIKU YA
THELATHINI NA TANO: NGUVU YA MUNGU KATIKA UDHAIFU WAKO |
Katika maisha yako ufikie kuamua kama unataka kuwapendeza watu au kuwavutia
watu. Unaweza kuwapendeza watu kutoka kwa mbali lakini ni vizuri uwe karibu nao
ili uwavute. Na unapofanya hivyo, wataweza kuyaona mapungufu yako Hiyo ni sawa
tu. Sifa muhimu sana kwa uongozi siyo ukamilifu, lakini ni kuaminika. Watu
lazima waweze kukuamini au hawatakuamini. Je, unajengaje uaminifu? Siyo kwa
kuigiza kuwa mkamilifu, lakini kwa kuwa mkweli.
Jisifie
udhaifu wako. Paulo anasema “Nitajisifia
tu jinsi nilivyo dhaifu na jinsi Mungu alivyo mkuu kuweza kutumia udhaifu huo
kwa utukufu wake.” 2 Wakorintho 12:5b (LB) Badala
ya kujitumainia mwenyewe kama mtu asiyeweza kushindwa kitu, jione mwenyewe kama
kumbukumbu ya neema. Shetani anapotaja udhaifu wako, mkubalie na ujaze moyo
wako na sifa kwa Yesu ambaye “anaelewa kila udhaifu wetu.” Waebrania 4:1a (CEV) Na kwa Roho Mtakatifu ambaye “hutusaidia
udhaifu wetu.” Warumi 8:26a (NIV)
Wakati mwingine, lakini, Mungu hugeuza nguvu kuwa udhaifu ili
atutumie zaidi. Yakobo alikuwa mwenye hila aliyetumia maisha yake kwa kufanya
hila na kukimbia matokeo yake. Usiku mmoja alipambana na Mungu na kusema “Sitakuacha
uende hadi unibariki. “Mungu alisema, “Sawa.” Lakini hapa alikamata paja la Yakobo
na kulitegua mfupa. Maana yake ni nini?
Mungu alikamata nguvu za Yakobo (msuli wa paja ndio wenye nguvu
kuliko zote mwilini) na kuugeuza katika udhaifu. Tangu siku hiyo na kuendelea, yakobo
alitembea kwa kuchechemea hivyo asingeweza kukimbia na kutoroka tena.
Ilimfundisha kumtegemea Mungu apende au asipende. Ukitaka Mungu akubariki na
akutumie sana, lazima uwe tayari kutembea kwa kuchechemea maisha yako
yaliyobaki, kwa sababu Mungu hutumia watu dhaifu.
SIKU YA THELATHINI NA TANO KUFIKIRA JUU YA LENGO
LANGU Jambo la Kutafakati: Mungu hutenda kazi vyema ninapokubali
udhaifu wangu. Kifungu cha Kukumbuka: “Neema yangu
yakutosha, nguvu zangu hukamilika katika udhaifu.” 2 Wakorintho 2:9a (NIV) Swali la kujiuliza: Je, nazuia nguvu ya Mungu katika maisha
yangu kwa kujaribu kuficha udhaifu wangu? Je, nahitaji kuwa mkweli katika
jambo gani ili kuwasaidia wengine? |
沒有留言:
張貼留言