2024年7月3日 星期三

Maisha Yanayoongozwa Na Malengo (Siku Ya Kumi na Tatu kwa Ishirini na Moja)

 


Siku ya Kumi na Tatu: Ibada Impendezayo Mungu

Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho

yako yote na kwa akilizako zote na kwanguvu zako zote.

Marko 12:30 (NIV)

Mungu anakutaka wewe mzima.

Mungu hapendi sehemu tu ya maisha yako. Anapenda umpe moyo wako wote, roho yako yote, akili zako zote, na nguvu zako zote. Mungu hafurahii kujitoa nusu, nusu utii, na mabaki ya muda na pesa zako. Anatamani kujitoakwako kikamilifu, siyo sehemu ndogo tu za maisha yako.

Wakati Fulani, Mwanamke Msamaria alijaribu kuwa na mjadala na Yesu kuhusu muda sahihi, mahali pa kuabudu, na namna ya kuabudu. Yesu alijibu kwamba haya mambo ya nje hayana maana. Mahali unapoabudia si muhimu kama kwa nini unaabudu na kiasi gani unajitoa unapomwabudu Mungu. Kuna njia sahihi na isiyo sahihi katika kuabudu. Biblia inasema, “Tuwe na shukurani nakumwabudu Mungu katika njia inayompendeza.” Waebrania 12:28 (TEV) Aina ya kuabudu inayompendeza Mungu ina sifa nne:

Mungu anafurahia kuabudu kwetu kunapokuwa sahihi. Mara nyingi watu husema, “Napenda kumfikiri Mungu kama ….,” na kisha wanaeleza mawazo yako kuhusu aina ya Mungu ambaye wangependa kumwabudu. Lakini hatuwezi kujitengenezea sura ya Munguinayotupendeza au ya kisiasa nakuiabudu. Hiyo ni ibada ya sanamu.

Ibada ya kumpendezea Munguni ya hisia za kina na mafundisho ya Imani ya kina. Tutatumia moyo na vichwa vyetu pamoja.

Ibadaa lazimaijengwe kwenye kweli ya maandiko, si maoni yetu kuhusu Mungu. Yesualimwambiamwanamke Msamaria, “Waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli, kwa kuwa hao ndio waabuduo Baba anaowatafuta.” Yohana 4:23 (NIV)

Kuabudu katika kweli” maana yake ni kumwabudu Mungu kama kweli ilivyofunuliwa katika Biblia.

Mungu anafurahia kuabudu kwetu kunapokuwa halisi. Yesu aliposema ni lazima “kuabudu katika roho,” hakuwa akimaanisha Roho Mtakatifu, lakini roho yako. Ukiwa umeumbwa kwa mfano wa Mungu, wewe ni roho inayoishi katika mwili, na Mungu alibuni roho yako iwasiliane naye. Kuabudu ni roho yako inaitikia kwa Roho waMungu.

Yesu aliposema, “Mpende Mungu wako kwa moyo na roho” alimaanisha kwamba kuabudu lazima kuwe kweli na kuguse moyo. Si jambo la kusema tu maneno sahihi; ni lazima umaanishe unachokisema. Sifa zisizotoka moyoni si sifa hata kidogo. Hazifai na nikumtukana Mungu.

Tunapoabudu, Mungu haangalii maneno kwanza huangalia nia ya moyo wetu. Biblia husema, “Mwanadamu huangalia mwonekano wanje, lakini Bwana huangalia moyo.”1 Samweli 16:7b (NIV)

Kwa kuwa kuabudu kumehusisha kumfurahia Mungu, kunahusisha hisia zako. Mungu alikupa hisia ili uweze kumwabudu na hisia za kina – lakini hisia hizo lazima ziwe halisi na siyo za kuigiza. Mungu anachukia unafiki. Hapendi kujionyesha, au kuigiza au sauti za ajabu ajabu. Anapenda upendo wetu halisi. Tunaweza kumwabudu Mungu si kikamlifu lakini tunaweza kunaweza kumwabudu kiukweli.

Ukweli peke yake hautoshi; unaweza kuwa mkweli lakini katika makosa. Ndio maana vyote viwili ukweli na roho vinahitajika. Kuabudu lazima kuwe sahihi na kweli. Ibada ya kumpendeza Mungu ni ya hisia za kina na mafundisho ya imani ya kina. Tunatumia moyo na vichwa vyetu pamoja.

Watu wengi siku hizi wanalinganisha mvuto wa muziki kwa hisia na kule kuvutwa na Roho, lakini haya mawili si sawa. Kuabudu halisi hutokea pale roho yako inamwitikia Mungu na siyo sauti ya muziki. Hakika nyimbo nyingine zenye mguso wa hisia zetu za ndanihuzuiakuabudu kwa sababu hutuondoa katika kumwelekea Mungu na badala yake tunaelekea kwenye hisia zetu. Kizuizi kikubwa katika kuabudu ni wewe mwenyewe – mambo uyapendayo na hofu zako kuhusu watu wengine wanakufikiriaje.

Njia bora ya kuabudu ni ile inayoonyesha kwa uhalisi upendo wako kwa Mungu.

Wakristo wanatofautiana kuhusu njia sahihi au inayofaa zaidi kumsifu Mungu, lakinihojahizimara nyingi huonyesha tofauti za watu na mazingira yao. Biblia imetaja namna mbalimbali za kusifu, kama vile kutubu,kuimba,kupiga kelele za shangwe, kushuhudia, na kuinua mikono. (Waebrania 13;15; Zaburi 7:17; Ezra 3:11; Zaburi 149:3; 150:3; Nehemia 8:6) Njia bora ya kuabuduni ile inayoonyesha kwa uhalisi upendo wako kwa Mungu, kwa kuzingatia mazingira na hali ya utu wako uliyopewa na Mungu.

Rafiki yangu Gary Thomas aligundua kwamba wakristo wengi huonekana kuzama katika shimo la kuabudu-jambo la kila mara lisilotosheleza-badala ya kuwa na urafiki uliochangamka na Mungu, kwa sababu hujilazimisha kufuata taratibu za kujitoa au mitindo yakuabudu ambazo haziwiani na jinsi Mungu alivyowaumba.

Gary alishangaa, kama Mungu alituumba tofauti, yawezekanaje kila mtu atazamiwe kumpenda Mungu kwa njia moja? Aliposoma maandishi ya Kikristo ya siku hizi na kuwasaili waamini waliokomaa, Gary aligundua kwamba Wakristo wanatumia njia nyingi tofauti kwa miaka 2000 kufurahia uhusiano wa karibu na Mungu: Kukaa nje ya nyumba, kujifunza, kuimba, kusoma, kucheza, kutengeneza Sanaa, kuwatumikia wengine, kuwa pekee, kushirikiana na wengine, na kushiriki katika shughuli mbalimbali.

Katika kitabu chaake, Njia Takatifu, Gary anataja njia tisa ambazo kwanza watu humkaribia Mungu: wapendao uumbaji wa asili (naturalists) wanasukumwa kumpenda Mungu nje ya majumba, katika mazingira ya asili. Watu wenye mvuto wa milango ya fahamu (sensates) humpenda Mungu kwa milango yao ya fahamu na hupenda ibada nzuri inayohusisha kuona, kuonja, kunusa, kugusa, na siyo masikio yao tu. Watu wa desturi (traditionalists) humwendea Mungu kwa kufuata njia za kanuni za kidini, liturujia, alama, na mifano isiyobadilika. Watu wenye kujikana (ascetics) humpenda Mungu kwa kukabili uovu, kupigania haki, na kuufanya ulimwengu uwe mahali bora. Waangalizi (caregivers) humpenda Mungu kwa kuwapenda wengine na kuwatimizia mahitaji yao. Watu wenye shauku (enthusiasts) humpenda Mungu kwa sherehe. Watu wa kutafakari (contemplatives) humpenda Mungu kwa njia ya kusujudu. Watu wenye akili nyingi (intellectuals) humpenda Mungu kwa kujifunza kwa kili zao. (Gary Thomas, njia takatifu, (Grand Rapids: Zondervan, 2000).

Hakuna “njia moja” inayofaa kwa watu wote kumwabudu na kufanya urafiki na Mungu. Jambo moja ni bayana: Huwezi kuleta utukufu kwa Mungu kwa kujaribu kuwa mtu Fulani ambaye hukukusudiwa kuwa. Mungu anakutaka uwe wewe mwenyewe. “Hao ndio aina yawatu Baba anawatufuta: wale ambao husimama mbele za Mungu katika hali rahisi yauhalisi wao katika kuabudu kwao. Yohana 4:23 (Msg)

Mungu anafurahia ibada yetu inapokuwa na kutafakari. Amri ya Yesu ya “Mpende Mungu kwa akili zako zote” imerudiwa mara nne katika Agano Jipya. Mungu hafurahii nyimbo zisizo na kufikiri, kusali sala za harakaharaka bila kujali, au maneno ya ovyo ya “Bwana asifiwe,” Kwa sababu hatuna neno jingine tunaloweza kusema kwa wakati huo. Kama kuabudu hakuhitaji akii, basi hakuna maana yoyote. Ni lazima utumie akili zako.

SIKU YA KUMI NA TATU:

IBADA IMPENDEZ AYO MUNGU

Yesu aliita ibada isiyo na kufikiri “Kupayuka payuka.”Mathayo 6:7 (KJV) Hata maneno ya kibiblia yanaweza kuzoeleka endapo yatatumiwa bila kiasi, hatimaye tutaacha kufikiri hata juu ya maana yake. Ni rahisi sana katika ibada kutumia maneno yaliyozoeleka badala ya kufanya bidii kumwabudu Mungu kwa Maneno mapya na njia mpya. Ndiyo maananakutia moyo usome maandiko kutoka tafsiri mbalimbali. Hii itapanua wigo wa kujieleza katika kuabudu.

Jaribu kumtumikia Mungu bila kutumia maneno kama Bwana asifiwe, haleluya, asante, au amina. Badala ya kusema, “Tunataka kukutukuza,” fanya orodha ya maneno yanayofanana kama vile tamani, heshimu, thamini, kucha, inua, na shukuru.

Pia uwe na uhalisi. Kama mtu Fulani angekuja kwako na kurudiarudia, “Nakusifu!” mara kumi, labda ungefikiri, kwa nini? Ni bora ungepokea sifa mara mbili za kitu halisi kuliko ishirini za jumla. Hata Mungu ni hivyo.

Wazo jingine ni kuorodhesha majina ya Mungu na kuyaangalia kwa makini. Majina ya Mungu hayakuwekwa tu; yanatueleza kuhusu mambo mbalimbali kuhusu tabia yake. Katika Agano la kale, Mungu alijifunua hatua kwa hatua kwa kutambulisha majini yake mapya, na anatuagiza kulisifu jina lake. (Angalia mlolongo 11 wa kanda kanda za majina ya Mungu, “Jinsi Mungu Anavyokutana na Mahitaji Yako Ya Ndani,” na Wachungaji wa Saddleback (1999), www.pastors.com

Mungu anapenda ibada yetu ya pamoja iwe ya kufikiri pia. Paulo aliandika sura nzima kwa ajili ya jambo hili katika 1Wakorintho 14 na anahitimisha hivi, “Kila kitu kifanyike kwa njia inayokubalika na kwa utaratibu.” 1 Wakorintho 14:40 (NIV)

Sawa na hili, Mungu anasisitia kwamba ibada yetu ya pamoja ieleweke kwa wasioamini wanapohudhuria mikusanyiko ya kuabudu. Paulo alisema, “Fikiri wageni wamehudhuria katika ibada yenu, mnapomtukuza Mungu katika roho zenu. Kama hawatawaelewa, watajuaje kusema “Amina”? Mnaweza kuwa mnamwabudu Mungu katika njia nzuri, lakini hakuna hata mwingine atakayesaidika.” 1 Wakorintho 14:16-17 (NIV) Kuwajali wasioamini wanaotembelea mikusanyiko yenu ya kuabudu ni amri ya kibiblia. Kutokujali amri hii ni kutotii na kukosa upendo. Kwa maelezo ya kina kuhusu jambo hili angalia sura inayohusu “Kuabudu Kunaweza Kuwa Ushuhuda”katika kitabu cha Kanisa Linaloongozwa Na Malengo.

Mungu anafurahia kuabudu kwetu kukiwa na matendo. Biblia inasema, “Itoeni miili yenu kama dhabihu iliyo hai, takatifu naya kumpendeza Mungu – hili ndilo tendo lenu la kiroho la kuabudu.” Warumi 12:1 (NIV) Kwa nini Mungu anapendaa mwili wako? Kwa nini hasemi, “Toa roho yako?” Kwa sababu bila mwili wako huwezi kufanya chochote katika sayari hii. Mbinguni utapokea mwili mpya wa kiwango cha juu, lakini unapokuwa hapa duniani, Mungu anasema, “nipe ulicho nacho!” Anahitaji matendo katika kuabudu.

Umesikia watu wakisema, “Leo siwezi kuja katika ibada lakini nitakuwa pamoja nanyi katika roho.” Unajua hiyo ina maana gani? Hakuna. Haina maana yoyote! Maadamu bado uko duniani, roho yako yaweza kuwepo tu mwili wako ulipo. Kama mwili wako haupo pale, basi hata roho yako haiko hapo.

Katika kuabudu tunatoa “miili yetu kama dhabihu iliyo hai.” Sasa mara nyingi tunaunganisha wazo la “dhabihu” na kitu kilichokufa, lakini Mungu anakutaka uwe dhabihu hai. Anapenda umwishie! Lakini, tatizo la sadaka hai ni kwamba inaweza kutambaa kutoka madhabahuni, na mara nyingi tunafanya hivyo. Tunaimba, “Twende mbele, Askari Wakristo,” siku ya Jumapili; na siku ya Jumatatu tumetoroka jeshini.

Katika Agano la Kale Mungu alifurahia dhabihu nyingi za ibada kwa vile zilikuwa kielelezo cha sadaka ya Yesu msalabani kwa ajili yetu. Sasa Mungu anafurahishwa na sadaka mbali mbali za kuabudu, kama vile: shukurani, sifa, unyenyekevu, toba, pesa, sala, kuwatumikia wengine, na kuwasaidia wahitaji. Zaburi 5:14 (TEV); Waebrania 13:15 (CEV); Zaburi 51:17; 54:6 (NIV); Filipi 4:18 (NIV); Zaburi 141:2 (GWT); Waebrania 13:16; Marko 12:33 (Msg); Warumi 12:1 (TEV).

Kuabudu halisi kuna gharama. Daudi alijua hivi na akasema, “Sitamtolea Bwana wangu sadaka ambazo hazikunigharimu chochote.” 2 Samweli 24:24 (TEV)

Jambo moja ambalo kuabudu hutugharimu ni ubinafsi wetu. Huwezi kumwinua Mungu na ukajinua mwenyewe kwa wakati mmoja. Hauabudu ili uonekane na wengine au kujipendezesha nafsi yako. Kwa makusudi kabisa unaacha kujielekea nafsi yako.

Yesu aliposema, “Mpende Mungu wako kwa nguvu zako zote,alionyesha kwamba kuabudu huchukua bidi na nguvu. Mara nyingi si tendo rahisi na la kufurahia, na wakati mwingine kuabudu ni tendo la kukusudia katika utashi-sadaka ya kupenda. Ibada isiyotokkana na utashi wetu ni upuuzi tu.

Unapomsifu Mungu hata pale hujisikii, unapotoka kitandani ili kuabudu ukiwa umechoka, au unapowasaidia wengine na wakati wewe mwenyewe uko hoi, unatoa dhabihu ya kuabudu kwa Mungu. Hivyo humfurahisha Mungu sana.

Matt Redman, kiongozi wa kuabudu huko Uingereza, anaeleza jinsi Mchungaji wake alivyofundisha Kanisani maana ya kuabudu. Kuonyesha kuwa kuabudu ni zaidi ya muziki, aliondoa uimbaji katika ibada zote kwa muda fulani huku wakijifunza kuabudu kwa njia nyingine. Mwisho wa muda huo, Matt alikuwa ameandika wimbo wa kisasa uitwao “Moyo wa kuabudu”:

Nitakuletea zaidi ya wimbo,

Kwa sababu wewe huhitaji wimbo peke zake.

Unachunguza ndani zaidi Kuliko mambo yanayoonekana.

Unaona moyoni mwangu.

Matt Redman, Moyo wa kuabudu (Kingsway’s Thankyou Music, 1997)

Kiini cha jambo ni jambo la kiini.

SIKU YA KUMI NA TATU

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Mungu ananitaka mimi mzima.

Kifungu cha Kukumbuka: Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote na kwa nguvu zako zote.Marko 12:30 (NIV)

Swali la kujiuliza: Je, ni jambo gani linalomfurahisha zaidi Mungu sasa hivi – ibada ya pamoja na wengine au ibada yangu binafsi? Je, nitafanya nini kuhusu hili?


Siku ya Kumi Na Nne: Wakati Mungu Anapoonekana kuwa Mbali

Mungu amejificha kutoka kwa watu wake, Lakini namwamini na kuweka

tumaini langu kwake.

Isaya 8:17 (TEV)

Mungu yupo haijalishi unajisikiaje.

Ni rahisi kumwabudu Mungu mambo yanapokuwa yanakuendea vizuri maishani – anapokuwa amekupa chakula, marafiki, jamaa, afya, na hali ya kupendeza. Lakini mazingira hayawi ya kupendeza siku zote. Je, unamwabudu Mungu vipi basi? Unafanyaje wakati Mungu anapoonekana kuwa maili milioni moja mbali nawe?

Kiwango cha kina sana cha kuabudu ni kumsifu Mungu hata katika maumivu, kumshukuru Mungu wakati wa majaribu, kumwamini unapojaribiwa, kujisalimisha huku unaumia, na kumpenda anapoonekana kuwa mbali.

Urafiki mara nyingi unajaribiwa kwa kutengana au ukimya; mnatengwa kwa umbali wa mahali au kwa kutoongea. Katika urafiki wako na Mungu, hutajisikia wakati wote kuwa karibu naye. Philip Yancey amesema kwa hekima kwamba, “Uhusiano wowote huwa na nyakati za ukaribu na nyakati za kuwa mbali, na katika uhusiano na Mungu, haijalishi ukaribu uliopo, kutakuwa na hali ya kuwa karibu na kutokuwa karibu.” Philip Yancey, Kusoma Kwa Ajili ya Mungu Asiyeonekana (Grand Rapids: Zondervan, 2000), 242. Ndipo hapo kuabudu huwa kugumu.

Ili kukomaza urafiki wenu, Mungu ataujaribu kwa wakati unaoonekana kama kutengana – nyakati unapojisikia kama amekuacha au amekusahau. Unamsikia Mungu kama yupo maili milioni moja mbali nawe. St. John of the Cross aliziita siku hizi za ukavu wa kirobo, mashaka, na kutengwa na Mungu kama “usiku wa giza kwa roho.” Henri Nouwen aliziita nyakati hizi “huduma ya kutokuwepo.” A.W. Tozer aliziita nyakati hizo “huduma ya usiku.” Wengine huziita “kiangazi cha moyo.”

Mbali na Yesu, Daudi labda alikuwa na ukaribu kwa Mungu zaidi ya mtu yeyote. Mungu alifurahia kumwita “mtu aupendezaye moyo wa Mungu.” 1 Samweli 13:14; 13:22 Lakini bado Daudi alilalamika juu ya Mungu kuwa mbali. “Bwana, mbona umekaa kando na uko mbali sana? Kwa nini umejificha ninapokuhitaji sana?”Zaburi 10:1 (LB) “Kwa nini umeniacha? Kwanini uko mbali hivyo?”“Kwa nini hujali kilio changu kwa ajili ya msaada?” Zaburi 22:1 (NLT) “Mbona umeniacha?” Zaburi 43:2 (TEV); Zaburi 44:23 (TEV); 74:11 (TEV).

Kwa kweli, Mungu hakuwa amemwacha Daudi, na hakuachi. Ameahidi mara nyingi, “sitakuacha wala kukupungukia kamwe.” Kumbukumbu 31:8; Zaburi 37:28; Yohana 14:16-18; Ebrania 13:5. Lakini Mungu hajaahidi kwamba “siku zote utahisi uwepo wangu.” Hakika, Mungu anasema wazi kwamba wakati mwingine anaficha uso wake toka kwetu. Ayubu 23:8-10 (NLT) Kuna nyakati anapoonekana kutokuwa katika matendo maishani mwako.

Floyd McClung hueleza nyakati hizo kama hivi: “Unaamka siku moja asubuhi na hisia zako zote za kiroho zinatoweka. Unasali lakini hakuna linalotokea. Unamkemea Shetani, lakini hakuna badiliko lolote. Unafanya mazoezi ya kiroho … rafiki zako wanakuombea … unatubu kila dhambi unayoidhania, kisha unazunguka kuomba msamaha kwa kila unayemfahamu. Unafunga … Bado hakuna kitu. Unaanaza kushangaa giza hili la kiroho litakwisha lini. Siku? Wiki? Mwezi? Je, kweli litakwisha? … inaonekana kama sala zako zinagonga dari. Katika kukata tamaa kabisa, unalia “Nina tatizo gani?” Floyd McChung, Kupata kufanya na Mungu (Ann Arbot, MI: Vine books 1992, 186.)

Mungu anasema wazi kwamba wakati mwingine anaficha uso wake toka kwetu.

Ukweli ni kwamba, wewe huna tatizo! Hii ni sehemu ya kawaida ya kujaribiwa na kukuza urafiki wako na Mungu. Kila Mkristo hupitia hali hiyo angalau mara moja au zaidi. Inaumiza na kusumbua, lakini ni ya muhimu kwa maendeleo ya Imani yako. Kujua ukweli huu kulimpa Ayubu tumaini wakati alipoacha kuhisi uwepo wa Mungu maishani mwake. Alisema “Naenda mashariki, lakini hayupo. Naenda magharibi, lakini simpati, simwoni. Kasikazini, kwa kuwa amejificha. Nageuka kusini, lakini simpati, Lakini anajua ninakoenda. Na akisha kunijaribu kama dhahabu katika moto, atanidhihirisha kuwa mwenye haki.” Ayubu 23:8-10 (NLT)

Wakati Mungu anaonekana kuwa mbali, unajisikia kwamba amekukasirikia au anakuadhibu kwa sababu ya dhambi Fulani. Ni kweli, dhambi hututenganisha kutoka ushirika wa karibu na Mungu. Tunamhuzunisha Roho wa Mungu na kuzimisha uhusiano wetu kwa kutotii, ugomvi na watu wengine, shughuli nyingi, urafiki na dunia, na dhambi nyingine. Zaburi 51; Efeso 4:29-30; 1 Wathesalonike 5:19; Yeremia 2:32; 1 Wakorintho 8:12; Yakobo 4:4 (NLT).

Lakini mara nyingi hali hii ya kujisikia kuachwa au kutengwa na Mungu haihusiani na dhambi. Ni kipimo cha Imani– jambo ambalo sote lazima litupate: Je, utaendelea kumpenda, kumwamini, kumtii, na kumwabudu Mungu, hata kama huhisi uwepo wake au ushahidi unaoonekana wa wazi maishani mwako?

Kosa linalofanywa na Wakristo wengi katika kuabudu siku hizi ni kutafuta uzoefu badala ya kumtafuta Mungu. Wanatafuta hisia, na iwapo itatokea wanaamini kuwa sasa wameabudu. Ni makosa! Kwa kweli, mara nyingi Mungu huondoa hisia ili tusizitegemee. Kutafuta hisia, hata hisia ya ukaribu na Kristo, siyo ibada.

Unapokuwa mkristo mchanga, Mungu hukupa hisia nyingi za uthibitisho na mara nyingine anajibu sala nyingi za uchaga na ubinafsi – ili ujue yupo. Lakini unapokua katika Imani, anakuachisha hali ya utegemezi.

Kosa linalofanywa na wakristo katika kuabudu siku hizi ni kutafuta uzoefu badala ya kumtafuta Mungu.

Uwezo wa Mungu na udhihirisho wa uwepo wa Mungu ni vitu viwili tofauti. Moja ni halisi; jingine mara nyingi ni hisia. Mungu siku zote yupo, hata pale unapokuwa huna habari naye, na uwepo wake ni wa ajabu mno hauwezi kupimwa na hisia.

Ndiyo, anapenda wewe uhisi uwepo wake, lakini anajali sana umwamini zaidi kuliko unavyomhisi. Imani, na siyo hisia, ndiyo inayompendeza Mungu.

Nyakati zitakazokuza Imani yako ni pale maisha yako yanapoonekana yanasambaa na Mungu hapatikani. Hii ilitokea kwa Ayubu. Kwa siku moja alipoteza kila kitu – jamaa yake, miradi yake, afya yake, na kila alichokuwa nacho. Sura thelathini za kukatisha tamaa, Mungu hakusema kitu!

Utamtukuzaje Mungu wakati huelewi kinachoendelea maishani mwako na Mungu amenyamaza? Utakaaje katika uhusiano wakati wa shida bila mawasiliano? Utawekaje macho yako katika Yesu yakiwa yamejawa na machozi?

Fanya alivyofanya Ayubu: “Kisha alianguka katika nchi akasujudu na kusema:Nilitoka katika tumbo la mama nchi, na nitaondoka nchi. BWANA alitoa na BWANA ametwaa; Jina la Bwana na libarikiwe.” Ayubu 1:20-21 (NIV)

Mwambie Mungu ukweli unavyohisi. Mimina moyo wako kwa Mungu. Tua mzigo wa hisia zako ulizonazo. Ayubu alifanya hivyo aliposema, “Siwezi kunyamaza! Nimekasirika na nina uchungu. Ni lazima niseme!” Ayubu 7:11 (TEV) Alilia Mungu alipoonekana kuwa mbali: “Ee, kwa siku ambazo nilikuwa katika kufanikisha, wakati urafiki wa karibu na Mungu ulibariki nymba yangu.” Ayubu 29:4 (NIV) Mungu atachukuliana na mashaka yako, hasira, woga, huzuni, kuchanganyikiwa, na maswali yako.

Je, ulijua kwamba kukiri kwa Mungu hali yako ya kukata tamaa yaweza kuwa ni maneno ya Imani? Akiwa anamwamini lakini akisikia kukata tamaa, Daudi aliandika, “Naamini, hivyo nilisema, ‘Nimeangamizwa kabisa’” Zaburi 116:10 (NCV) Hii inaonekana kama kupingana: Namwamini Mungu lakini nimefutiliwa Mbali! Uwazi wa Daudi hakika anafunua Imani ya kina: Kwanza, alimwamini Mungu. Pili aliamini Mungu angesikia sala yake. Tatu, aliamini Mungu angemruhusu aseme alivyojisikia nabado aendelee kumpenda.

Anglia zaidi Mungu ni nani – asili yake isiyobadilika. Pamoja na mazingira na jinsi unavyojihisi ng’ang’ania tabia ya Mungu isiyobadilika. Jikumbushe yale unayojua kuwa ni ya kweli milele kuhusu Mungu: Yeye ni mwema,ananipenda, yuko pamoja nami, anajua yanayonipata, anajali, anao mpango mzuri kwa maisha yangu. V. Raymond Edman alisema, “Usitilie mashaka unapokuwa gizani yale Mungu aliyokuambia nuruni.”

Maisha ya Ayubu yalipoharibiwa, na Mungu alikuwa kimya Ayubu bado alikuwa na vitu vya kumsifia Mungu:

l  Kwamba ni mwema na wa upendo. Ayubu 10:12

l  Kwamba ni mwenye nguvu zote. Ayubu 42:2; 37:5; 28

l  Kwamba anajua kila kitu katika maisha. Ayubu 23:10; 31:4

l  Kwamba anatawala kila kitu. Ayubu 34:13

l  Kwamba ataniokoa. Ayubu 19:25

Mwamini Mungu katika kutunza ahadi zake. Nyakati za ukavu wa kiroho lazima uwe na subira katika kuzitengemea ahadi za Mungu, siyo hisia zako, na uelewe kwamba anakupeleka katika kiwango cha kina cha kukua kiroho. Urafiki unaotegemea hisia ni wa juu juu tu.

Hivyo usisumbuliwe na usumbufu. Mazingira hayawezi kubadili asili ya Mungu. Neema ya Mungu bado ni timilifu; bado yuko upande wako, hata unapokuwa huna hisia hiyo. Katika mazingira magumu, Ayubu alilishika neno la Mungu. Alisema, “Sijayaacha maagizo ya kinywa chake; nimeyatunza maneno ya kinywa chake kuliko mkate wangu wa kila siku.” Ayubu 23:12 (NIV)

Imani hii katika Neno la Mungu ilimfanya Ayubu kukaa mwaminifu ingawa hakuna alilolielewa. Imani yake ilikuwa imara katikati ya maumivu: “Mungu anaweza kuniua, lakini bado nitamwamini.” Ayubu 13:15 (CEV)

Unapohisi kuachwa na Mungu bado endelea kumwamini bila kujali hisia hizo, mwabudu kwa kina zaidi.

Kumbuka yale Mungu ameshakutendea. Kama Mungu hajakufanyia chochote kamwe, bado anastahili sifa zako daima maisha yako yote kwa sababu ya alichokifanya Yesu msalabani. Mwana wa Mungu alikufia! Hii ni sababu kubwa ya kuabudu.

Unapohisi kuachwa na Mungu bado endelea kumwamini, mwabudu kwa kina zaidi.

Kwa bahati mbaya, tunasahau mambo magumu ya kina ya sadaka ya maumivu makali aliyoitoa Mungu badala yetu. Mazoea huleta kutosheka. Hata kabla ya kusulubishwa kwake, Mwana wa Mungu alivuliwa nguo, akapigwa vibaya sana, akadhihakiwa na kuchekwa, akavikwa taji ya miiba, na akatemewa mate. Alidhalilishwa na kudhihakiwa na watu waovu, akatendwa vibaya kuliko mnyama.

Kisha, akiwa karibu kuzimia kwa sababu ya kupoteza damu nyingi, alilazimishwa kubeba msalaba kwenda mlimani, alipigwa misumari juu yake, na aliachwa afe pole pole, kifo cha mateso ya kusulubishwa. Damu yake ya uhai ilipomwagika, watu wenye maudhi walisimama na kumtukana huku wakimpa changamoto ya kuhoji uhusiano wake na Mungu.

Akisha Yesu kuchukua dhambi ya binadamu na hukumu yake, Mungu alitazama pembeni mwa sehemu hiyo ovu, na Yesu alilia katika hali ya kulemewa sana, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? “Yesu angeweza kujiokoa mwenyewe –lakini asingekuwa amekuokoa.

Maneno hayatoshi kueleza giza la wakati huo. Kwa nini Mungu aliruhusu na kuvumilia mateso maovu kiasi hicho. Kwa nini? Hii ni ili wewe uweze kuokolewa na kuzimu ya milele! Biblia inasema, “Kristo hakuwa na dhambi, lakini kwa ajili yetu Mungu alimfanya ashiriki dhambi yetu ili kwamba katika kushirikiana naye tuweze kushiriki haki ya Mungu.” 2 Wakorintho. 5:21 (TEV)

Yesu aliacha vyote ili wewe upate vyote. Alikufa ili wewe uishi milele. Jambo hilo tu linatosha kukufanya umshukuru na kumsifu daima. Usijiulize kamwe jambo la kushukuru.

SIKU YA KUMI NNE

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Mungu ni halisi, haijalishi ninahisi vipi.

Kifungu cha Kukumbuka:Kwa kuwa Mungu amesema, ‘Sitakuacha kamwe, sitakupungukia kamwe.’”  Waebrania 13:5 (TEV)

Swali la Kujiuliza: Je, nawezaje kudumu katika kuutazamia uwepo wa Mungu, hasa anapoonekana kuwa mbali?

Siku ya Kumi na Tano: Uliumbwa kwa Ajili Ya Jamii Ya Mungu

Mungu ndiye aliyeumba vitu vyote, na vitu vyote ni kwa ajili ya utukufu wake.

Alitaka watoto wake wengi washiriki utukufu wake.

Waebrania 2:10a (NCV)

Oneni jinsi gani Mungu anavyotupenda sana, Kwa kuwa anaturuhusu

tuitwe watoto wake, Na kweli ndivyo tulivyo!

1 Yohana 3:1 (NLT)

Ulimbwa kwa ajili ya jamii ya Mungu. Mungu anapenda jamii, na alikuumba uwe sehemu ya hiyo jamii. Hili ni lengo la pili la Mungu kwa maisha yako, alilolipanga kabla hujazaliwa. Biblia nzima ni hadithi ya Mungu akijenga jamii ya watu watakaompendeza, kumheshimu, na kutawala naye milele. Imeandikawa, “Mpango wake usiobadilika umekuwa siku zote ni kutufanya kuwa wa jamii yake kutuleta kwake kwa kupitia Yesu Kristo. Na jambo hili lilimpa furaha kubwa.” Waefeso 1:5 (NLT)

Kwa sababu Mungu ni upendo, anathamini mahusiano. Asili yake ni uhusiano, na anajitambulisha katika hali ya kijamaa: Baba, Mwana, na Roho. Utatu ni uhusiano wa Mungu kwake mwenyewe. Ni kielelezo kikamilifu cha umoja katika uhusiano, na ni lazima tujifunze kutokana na kielelezo hicho.

Mungu daima ameishi katika uhusiano wa upendo yeye mwenyewe, hivyo hajawahi kuwa na upweke. Hakuhitaji jamaa-alitamani kuwa nayo, na kutushirikisha vyote alivyo navyo. Hili humpa Mungu furaha. Biblia inasema, “Ilikuwa ni siku ya furaha kwake alipotupa sisi maisha yetu mapya, kwa njia ya ukweli wa Neno lake, na tukawa, kama alivyokuwa, wazaliwa wa kwanza katika jamaa yake mpya.” Yakobo 1:18 (LB)

Tunapoweka imani yetu kwa Kristo, Mungu anakuwa Baba yetu, tunakuwa watoto wake, waamini wengine wanakuwa kaka na dada zetu, na kanisa linakuwa jamii yetu ya kiroho. Jamii ya Mungu ni pamoja na waamini wa siku zilizopita, na wakati huu, na ule ujao.

Kila binadamu aliumbwa na Mungu, lakini si kila mmoja ni mtoto wa Mungu. Njia pekee ya kuingia katika jamii ya Mungu ni kwa kuzaliwa mara ya pili. Unakuwa mmoja wa jamii ya kibinadamu kwa kuzaliwa kwa mara ya kwanza, lakini unakuwa katika jamii ya Mungu kwa kuzaliwa mara ya pili. Mungu, “ametupatia upendeleo wa kuzaliwa kwa mara ya pili, ili kwamba sasa tuwe watu wa jamii ya Mungu.” 1 Petro 1:3 (LB); Rumi 8:15-16 (TEV)

Mwaliko wa kuingia katika jamii ya Mungu ni kwa watu wote. (Marko 8:34; Matendo 2:21; Rumi 10:13; 2 Petro 3:9.) Lakini kuwa sharti moja: Imani katika Yesu. Biblia inasema, “Ninyi nyote ni watoto wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.” Wagalatia 3:26 (NLT)

Jamii yako ya kiroho ni bora zaidi kuliko ya kimwili kwa sababu itadumu milele Jamii zetu duniani ni zawadi nzuri kutoka kwa Mungu, lakini ni za muda mfupi na ni rahisi kuvunjika, mara nyingi zinavunjwa na talaka, kutengwa na umbali, kuzeeka, na kifo. Kwa upande mwingine, jamii yetu ya kiroho-uhusiano wetu kwa waamini wengine-utadumu milele. Ni uhusiano imara zaidi, wa kudumu kuliko ule wa damu. Kila Paulo alipotulia na kutafakari juu ya kusudi la Mungu kwetu sote alijikuta akibubujika katika sifa: “Ninapofikiri juu ya hekima na upeo wake napiga magoti yangu na kumwomba Baba wa jamii yote kubwa ya Mungu-wengine wao wako mbinguni tayari na wengine hapa dumiani,” Wafeso 3:14-15 (LB)

FAIDA ZA KUWA KATIKA JAMII YA MUNGU

Mara ulipozaliwa katika jamii ya kiroho, ulipewa zawadi bora za siku ya kuzaliwa ambazo ni: jina la jamaa, uhusiano wa karibu kijamaa, na urithi wa kijamaa!” (1 Yohana 3:1; Rumi 8:29; Wagalatia 4:6-7; Rumi 5:2; 1 Wakorintho 3:23; Waefeso 3:12; 1 Petro 1:3-5; Warumi 8:17.) Biblia inasema, “Kwa kuwa wewe ni mototo wake, kila ulicho nacho ni mali yake.” Wagalatia 4:7b (NLT)

Jamii yako ya kiroho ni bora kuliko ya kimwili kwa sababu itadumu milele.

Agano jipya hutoa mkazo mkubwa kuhusu “urithi” wetu mkubwa. Hutuambia, “Mungu wangu atawatimizieni mahitaji yenu yote kulingana na utajiri wa utukufu wake katika Kristo Yesu.” Wafilipi 4:19 (NIV) Kama watoto wa Mungu tunashiriki baraka za kijamii. Hapa duniani tumepewe “utajiri … neema yake … wema … subira … utukufu … hekima … nguvu … na rhema.” (Waefeso 1:7; Warumi 2:4; 9:23; 11:33; Waefeso 3:16; 2:4.) Lakini katika maisha ya milele tutapata zaidi ya hapo.

Paulo alisema, “Nataka mtambue utajiri na utukufu wa urithi aliowapatia watu wake.” Waefeso 1:18b (NLT) Je, urithi huo una nini? Kwanza, tutakuwa na Mungu milele. (1 Wathesalonike 5:10; 4:17) Pili, tutabadilishwa kabisa na kuwa kama Kristo. (1 Yohana 3:2; 2 Wakorintho 3:18) Tatu, tutawekwa huru kutoka maumivu yote, kifo na mateso. (Ufunuo 21:4) Nne, tutapewa zawadi na kutunukiwa nafasi za huduma. (Marko 9:4; 10:30; 1 Wakorintho 3:8; Waebrania 10:35; Mathayo 25:21, 23) Tano, tutashiriki katika utukufu wa Kristo. (Warumi 8:17; Kolosai 3:4; 2 Wathesalonike 2:14; 2 Timotheo 2:12; 1 Petro 5:1) Ni urithi wa ajabu: Wewe ni tajiri mno kuliko unavyodhani.

Biblia inasema, “Mungu amewatunzia urithi wa thamani watoto wake. Umetunzwa mbinguni kwa ajili yenu, safi usio na taka, hauwezi kubadilika wala kuoza.” 1 Petro 1:4 (NLT) Hii ina maana kuwa urithi wako wa milele hauna kipimo cha thamani, ni safi, wa kudumu, na unalindwa. Hakuna mtu anayeweza kukuondolea; hauwezi kuharibiwa na vita, uchumi mbovu, au majanga ya asili. Urithi huu wa milele, siyo mapumziko ya uzeeni, ndicho kiwe kitu unachokitazamia na kukifanyia kazi. Paulo alisema, “Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kama kumfanyia kazi Bwana, na siyo watu, kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi kutoka kwa Bwana kama zawadi.” Wakolosai 3:23-24a (NIV) Mapumziko ya uzeeni ni lengo la muda mfupi. Ni lazima uishi katika mtazamo wa milele.

UBATIZO: KUJULIKANA KATIKA JAMII YA MUNGU

Jamaa bora hujivunia jamaa zao; wanajamaa hiyo hawaoni aibu kujulikana kama wanajamaa hiyo. Lakini, nimekutana na waamini wengine ambao hawajajitambulisha hadharani kuwa ni wanajamaa wa jamii ya kiroho kama Yesu alivyoagiza-kwa kubatizwa.

SIKU YA KUMI NA TANO:

ULIUMBWA KWA AJILI YA JAMII YA MUNGU

Ubatizo siyo tendo la kuchagua kufanya au la, kuchelewesha au kuahirishwa. Huonyesha kulingizwa kwako katika jamii ya Mungu. Ni tendo la kutangaza hadharani kwa ulimwengu kuwa, “Mimi sioni haya kuwa mmoja katika watu wa jamii ya Mungu.” Je, umebatizwa? Yesu aliagiza tendo hili zuri kwa ajili ya watu wote wa jamii yake. Alituambia, “Nendeni mkafanye wanafunzi wa mataifa yote, mkiwabatiza kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Ntakatifu.” Mathayo 28:19 (NLT)

Kwa miaka mingi nilishangaa kwanini Agizo Kuu la Yesu linatoa umuhimu sawa Kati ya ubatizo na wajibu wa uinjilisti na mafundisho. Kwa nini ubatizo ni wa muhimu? Kisha nikatambua kuwa ni sababu ni kielelezo cha lengo la pili la Mungu kwa maisha yako: Kuwa mshirika katika jamii ya Mungu la milele.

Ubatizo una maana kubwa. Ubatizo wako ni tangazo la imani yako, kushiriki kuzikwa na kufufuka kwa Kristo, huonyesha kufa kwa utu wako wa kale, na hutangaza maisha yako mapya katika Kristo. Pia ni sherehe ya wewe kuingizwa Katika jamii ya Mungu.

Ubatizo wako ni tangazo la nje la ukweli wa kiroho. Huwakilisha kilichotokea pale Mungu alipokuingiza katika jamii yake: “Wengine wetu ni Wayahudi, wengine Mataifa, baadhi ni watumwa, na wengine huru. Lakini sisi sote tumebatizwa katika mwili wa Kristo kwa Roho mmoja, na wote tumempokea Roho huyo mmoja.” 1 Wakrintho 12:13 (NLT)

Ubatizo haukufanyi mwanajamaa wa jamii ya Mungu. Imani katika Kristo tu ndiyo hufanya kazi hiyo. Ubatizo huonyesha kuwa wewe ni mmoja wa jamii ya Mungu.

Kama pete ya harusi ni ukumbusho unaoonekana wa mkataba wa ndani uliofanywa moyoni mwako. Ni tendo la kuingizwa hatua nyingine (initiation), siyo kitu cha kufanya unapokuwa umekomaa kiroho. Sharti pekee la kibiblia ni kwamba unaamini. (Matendo 2:41; 8:12-13, 35-38)

Katika Agano Jipya, watu walibatizwa mara tu walipoamini. Siku ya Pentekoste, watu 3,000 walibatizwa siku ile ile walipompokea Kristo. Penginepo, towashi wa Kushi alibatizwa pale pale alipoongoka; Paulo na Sila waliwabatiza mlinzi wa gereza pamoja na jamaa jake usiku. Hakuna kuchelewesha ubatizo katika Agano jipya. Kama hujabatizwa kama kielelezo cha imani yako katika Kristo. Fanya hivyo haraka iwezekanavyo, Kama Kristo alivyoagiza.

UPENDELEO MKUBWA KATIKA MAISHA

Kuingizwa katika jamii ya Mungu ni heshima ya hadi ya juu na upendeleo mkubwa sana unaoweza kuupata

Biblia inasema, “Yesu na watu anaowafanya kuwa watakatifu wote ni wa jamii moja. Ndiyo maana haoni haya kuwaita ndugu na dada zake.” Wabrania 2:11 (CEV) Hebu ukweli huu wa ajabu uzame ndani yako. Wewe ni sehemu ya jamii ya Mungu, na kwa sababu Yesu anakufanya mtakatifu, Mungu anajivunia! Maneno ya Yesu hayana makosa: “Yesu aliwaambia wanafunzi wake, akisema, ‘hawa ndio mama na ndugu zangu. Yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu!” Mathayo 12:39-50 (NLT) Kuingizwa katika jamii ya Mungu ni heshima ya hali ya juu na upendeleo mkubwa sana unaoweza kuupata. Hakuna chochote cha kulinganisha. Unapojihisi hufai, hupendwi au huko salama, kumbuka wewe ni mali ya nani.

 

SIKU YA KUMI NA TANO

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Niliumbwa kwa ajili ya jamii ya Mungu.

Kifungu cha Kukumbuka:Mpango wake usiobadilika umekuwa siku zote ni kutufanya kuwa watu wa jamii yake kwa kutuleta kwake kupitia Yesu Kristo.” Waefeso 1:5a (NLT)

Swali la kujiuliza: Je? Naweza kuanza kuwatendea waamini wengine kama watu wa jamii yangu mwenyewe?

 Siku ya Kumi na Sita: Kitu Cha Muhimu Zaidi

Haijalishi ninachosema, ninachoamini, na ninachofanya,

Mimi sina kitu kabisa kama sina upendo

1 Wakorintho 13:36 (Msg)

Upendo maana yake ni kuishi kama Mungu alivyotuagiza tuishi.

Kama mlivyosikia tangu mwanzo, amri yake ni hii,

muishi maisha ya upendo.

2 Yohana 1:6 (NCV)

Maisha yanahusu upendo.

Kwa sababu Mungu ni upendo, somo la muhimu analotaka wewe ujifunze hapa duniani ni jinsi ya kupenda. Ni katika kupenda ndiyo tunafanana naye, hivyo upendo ni msingi wa kila amri aliyotupatia: “Sheria yote inaweza kujumlishwa katika amri moja: Wapende wengine kama unavyojipenda mwenyewe.” Wagalatia 5:14 (LB)

Kujifunza kupenda pasipo ubinafsi siyo kazi rahisi. Ni kinyume cha hali yetu ya ubinafsi. Ndiyo maana tunapewa muda wa maisha yetu yote kujifunza kupenda. Bila shaka, Mungu anatutaka tumpende kila mtu, lakini hasa anatutaka tujifunze kuwapenda watu wengine katika jamii yake. Kama tulivyokwishakuona, hili ni lengo la pili la maisha yako. Petro anatuambia, “Onyesheni upendo maalum kwa watu wa Mungu.” 1 Petro 2:17b (CEV) Paulo pia anatoa maelezo ya namna hiyo: “Tunapokuwa na nafasi ya kumsaidia mtu yeyote, tufanye. Lakini tuwape kipaumbele wale walio wa jamii ya waaminio.” Wagalatia 6:10 (NCV)

SIKU YA KUMI NA SITA

KITU CHA MUHIMU

Kwa nini Mungu anakazia kwamba tutangulize waamini katika kuonyesha upendo wetu? Kwa nini wapate upendeleo huo? Kwa sababu Mungu anapenda jamii yake ijulikane kwa upendo walio nao kuliko kingine chochote. Yesu alisema kuwa upendo watu kati yetu sisi-siyo mafundisho wa imani-ndiyo ushuhuda wetu mkubwa kwa ulimwengu. Alisema, “Upendo wenu imara kati yenu utathibitisha kwa ulimwengu kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.” Yohana 13:35 (LB)

Mbinguni tutaifurahi jamii ya Mungu milele, lakini tunayo kazi kubwa ya kufanya hapa duniani ili kujiandaa kwa kutupatia “Wajibu wa kijamii,” na wajibu mkubwa ni kupendana.

Mungu anakutaka uwe katika ushirika wa karibu na wa mara kwa mara na waamini wengine ili uweze kukuza ujuzi wako katika kupenda. Lazima uwe karibu na watu-watu wanaoudhi, wasio wakamilifu, na wa kuvunja moyo. Kwa kushirikiana tunajifunza kweli muhimu tatu.

MATUMIZI MAZURI YA MAISHA NI UPENDO

Upendo lazima uwe kitu cha kwanza, lengo kuu, na tamanio lako kuu maishani. Upendo si kipengele kizuri katika maisha yako, ni sehemu ya muhimu kuliko zote katika maisha. Biblia inasema, “Upendo na uwe lengo lenu kuu.” 1 Wakorintho 14:1a (LB)

Haitoshi kusema, “moja ya vitu ninavyotaka maishani ni kuwa na upendo,” kama vile ni kitu cha kwanza katika orodha ya vitu kumi. Uhusiano upewe kipaumbele katika maisha yako kuliko vyote. Kwa nini?

Maisha bila upendo hayana thamani. Paulo anatoa hoja hii: “Haijalishi ninachosema, ninachoamini, mimi sina kitu kabisa kama sina upendo.” 1 Korintho 13:3 (Msg)

Mara nyingi tunatenda kama vile uhusiano ni kitu tunachoweza kukibana na kukiingiza kwenye ratiba zetu. Tunaongea juu ya kutafuta muda kwa ajili ya watoto wetu au kutenga muda kwa ajili ya watu wetu. Hiyo huonyesha kwamba uhusiano ni sehemu ya maisha yetu pamoja na shughuli nyinginezo. Lakini Mungu anasema uhusiano ndiyo maisha yalivyo.

Amri nne kati ya amri kumi zinahusu uhusiano wetu na Mungu na zile sita zinahusu uhusiano wetu na wetu. Lakini zote kumi zinahusu uhusiano. Baadaye Yesu alijumlisha na kuonyesha kilicho cha muhimu zaidi sana kwa Mungu katika kauli mbili. Mpende Mungu na wapende watu. Alisema, “Ni lazima umpende Mungu kwa moyo wako wote ..’ Hii ndiyo amri ya kwanza na kuu kuliko zote. Ya pili nayo ni muhimu sawa na hiyo: Mpende jirani yako kama nafsi yako. Amri nyingine zote na maagizo yote ya manabii yanategemea amri hizi mbili.” Mathayo 22:37-40 (NLT) Baada ya kujifunza kumpenda Mungu (kuabudu), kujifunza kuwapenda wengine ni lengo la pili kwa maisha yako.

Uhusiano si mafanikio ya mali, ndiyo kitu cha muhimu zaidi maishani. Sasa kwa nini tunaruhusu uhusiano uchukue sehemu ndogo maishani? Ratiba zetu zinapokuwa zimejaa kupita kiasi, tunaanza kupitapita juutu mambo ya uhusiano, tunapunguza muda, nguvu na usikivu kwa matarajio ya uhusiano yalivyotakiwa. Jambo ambalo ni muhimu zaidi kwa Mungu linaloondolewa na jambo la dharura.

Shughuli nyingi ni adui mkubwa wa uhusiano. Tunachukuliwa na kutafuta maisha, kufanya kazi zetu, kulipa madeni, kutekeleza malengo kama vile shughuli hizi ndizo lengo kuu la maisha. La hasha! Lengo la maisha ni kujifunza kupenda-Mungu na watu. Maisha yasiyo na upendo ni bure.

Upendo utadumu milele. Sababu nyingine Mungu anayotupa ili tufunye upendo kitu cha kwanza ni kwamba upendo ni wa milele: “Mambo haya matatu yatadumu milele: Imani, tumaini, na upendo. Na lililo kubwa kuliko yote ni upendo.”           1 Wakorintho 13:13 (NCV)

Upendo huacha kumbukumbu. Jinsi unavyowatendea watu wengine, siyo utajiri au mafanikio yako ndicho kitu kinachodumu unachoweza kuacha duniani. Kama Mama Teresa alivyosema, “Sivyo unavyotenda, lakini kiasi gani cha upendo unaweka katika tendo hilo ndilo jambo la muhimu sana.” Upendo ni siri ya urithi wa kudumu.

Nimekuwa kando ya kitanda cha watu wengi wanaokuwa katika kufa, wanaposimama pembezoni mwa umilele, na sijiasikia yeyote akisema, “Nileteeni vyeti vyangu! Nataka kuviona mara moja tena. Nionyesheni zawadi zangu, medali zangu, ile saa ya dhahabu niliyopewa.” Maisha yanapokoma duniani, watu hawajizungushii vitu. Tunachotaka kituzunguke ni watu-watu tuwapendao na tulio na uhusiano nao.

Katika dakika zetu za mwisho wote tunang’amua kwamba maisha ni uhusiano. Hekima ni kujifunza ule ukweli mapema na siyo baadye. Usingoje mpaka utakapokuwa katika kitanda cha kifo ili ufahamu kuwa hakuna chenye thamani zaidi.

Tutatathminiwa katika upendo wetu. Sababu ya tatu ya kufanya kujifunza kupenda liwe lengo la maisha yako ni Kwamba ndicho kigezo kitakachotumika kututathmini katika umilele. Njia moja wapo Mungu hutumia kupima upevu wa kiroho ni ile thamani ya uhusiano wako. Mbinguni Mungu hatasema, “Niambie kuhusu taaluma yako, akaunti yako ya benki, na mambo uyapendayo,” Badala yake ataangalia ulivyowatenda watu wengine, hasa wale wenye mahitaji. (Mathayo 25:40) Yesu alisema njia yaa kumpenda ni kupenda jamii yake na kuangalia mahitaji yao ya kila siku: “Nawaambieni ukweli, kama mlivyowatendea wadogo hawa walio watu wa jamii ya Mungu, mlinitendea mimi.” Mathayo 25:34-46 (NRSV)

Maisha ni uhusiano.

Utakapohamia katika umilele, utaacha kila kitu nyuma. Utakachopeleka ni tabia yako. Ndiyo maana Biblia inasema, “Jambo pekee la muhimu ni imani inayojidhihirisha katika upendo.” Wagalatia 5:6 (NIV)

Tukijua hili, napendekeza kwamba unapoamka kila asubuhi, piga magoti kando ya kitanda chako, au kaa juu yake, na usali hivi: “Mungu, hata kama nitafanya chochote, nataka kuhakikisha kwamb natumia muda kukupenda wewe na kuwapenda watu wengine – kwa sababu hayo nidiyo maisha. Sitaki kupoteza siku hii.” Kwa nini Mungu akupe siku nyingine kama utaipoteza?

UDHIHIRISHO MZURI WA UPENDO NI MUDA

Umuhimu wa vitu unaweza kupimwa kwa kiasi cha muda tunaoutumia kwa vitu hivyo. Ukitumia muda mwingi kwa kitu fulani, ndivyo anaonyesha umuhimu wa kitu hicho kwako. Ukitaka kujua mambo ya muhimu kwa mtu, angalia tu jinsi wanavyotumia muda wao.

Mudaa ni zawadi ya thamani sana kwa sababu una kiasi maalum tu cha muda. Unaweza kutengeneza pesa nyingi, lakini huwezi kutengeneza muda zaidi. Unapompa mtu fulani muda wako unampa sehemu ya maisha yako ambayo hutaipata tena. Muda wako ni maisha yako. Ndiyo maana zawadi kuwa unayoweza kumpa mtu ni muda wako.

Zawadi kubwa unayoweza kumpa mtu ni upendo wako.

Haitoshi tu kusema kwamba uhusiano ni muhimu; tunatakiwa kuthibitisha kwa kuwekeza muda katika huo. Maneno matupu si kitu. “Watoto wangu, upendo wetu usiwe wa maneno tu; ni lazima uwe upendo halisi, unaojionyesha katika matendo.” 1 Yohana 3:18 (TEV) Uhusiano unachukua muda na juhudi.

Kiini cha upendo siyo tunavyofikiri au kufanya au kuwapa watu wengine, lakini ni kiasi gani tunajitoa sisi wenyewe. Wanaume hasa hawalewi jambo hili mara nyingi. Wengi wao wameniambia, “Siwaelewi mke wangu na watoto wangu, nawapatia kila kitu wanachotaka. Wanaahitaji nini Zaidi?” Wanakuhitaji wewe! Macho yako, masikio yako, muda wako, usikivu wako, uwepo wako, kujali kwako-mudaa wako. Hakuna kinachoweza kuziba pengo hilo.

Zawadi ya upendo inayotamaniwa na wengi siyo almasi au maua, au chokoleti. Watu wanahitaji uskivu usiogawanyika. Upendo unamjali mtu mwingine kwa makini kiasi kwamba unajisahau mwenyewe kwa muda huo. Usikivu husema “ninakujali wewe sana kiasi cha kukupa mali yangu ya thamani sana-muda wangu.“ Kila unapotoa muda wako, unatoa sadaka, na sadaka ni kiini cha upendo. Yesu alitoa kielelezo cha jambo hili. “Mjawe upendo kwa wengine, mkifuata kielelezo cha Kristo aliyewapenda na akajitoa nafsi yake kwa Mungu kama sadaka ili kuondoa dhambi zenu.” Wafeso 5:2 (LB)

Unaweza kutoa bila upendo, lakini huwezi kupenda bila kutoa. “Mungu aliupenda ulimwengu sana hata akamtoa …” (Yohana 3:16a) Upendo humaanisha kuachilia-kutoa nivpendavyo, furaha, malengo, usalama, pesa nguvu, au muda kwa faida ya mtu mwingine.

WAKATI MZURI WA KUPENDA NI SASA

Wakati mwingine kuahirisha kunakubalika hasa kwa mambo madogo madogo. Lakini kwa sababu upendo ndicho kitu cha muhimu zaidi, unahitaji kupewa nafasi ya kwanza. Biblia hukazia jambo hili mara nyingi, “Tunapokuwa na nafasi, tuwatendee mema watu wote.” Wagalatia 6:10 (NLT) “Kila unapoweza, watendee wema wale wanaouhitaji. Efeso 5:16 (NCV) Usimwambie jirani yako asubiri mpaka kesho kama unaweza kuwasaidia sana.” Mithali 3:27 (TEV)

Kwa nini sasa ndiyo muda mwafaka wa kuonyesha upendo? Kwa sababu hujui utakuwa na muda mpaka lini. Mazingira hubadilika. Watu hufa. Watoto hukua. Huna dhamana ya kesho. Kama unataka kuonyesha upendo, ni bora ufanye sasa.

Ukijua kwamba siku moja utasimama mbele za Mungu, hapa kuna maswali unayopaswa kujiuliza: Je, utazielezeaje zile nyakati ambazo miradi au vitu ndivyo vilikuwa vitu vya muhimu zaidi kuliko watu? Nani ambaye unahitaji kuanza kutumia muda zaidi naye? Je, ni kitu gani unahitaji kukiondoa katika ratiba yako ili uweze kutimiza haya? Je, unahitaji kutoa sadaka gani?

Matumizi mazuri ya maisha ni upendo. Udhihirisho wa upendo ni muda. Wakati mzuri wa kupenda ni sasa.

SIKU YA KUMI NA SITA

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Maisha ni kupenda.

Kifungu cha Kukumbuka:Shria yote imejumlishwa katika amri moja; mpende jirani yako kama nafsi yako.” Wagalatia 5:14 (NIV)

Swali la Kujiuliza: Kusema ukweli, je uhusiano naupa nafasi ya kwanza? Je, nawezaji kuhakikisha kwamba nafanya hivyo?

 Siku ya Kumi na Saba: Mahali Pa Kuwa

Ninyi mumekuwa watu wa jamii ya Mungu, raia wa taifa la

Mungu nanyi ni watu wa nyumbani mwa

Mungu pamoja na kila Mkristo.

Waefeso 2:19b

Jamii ya Mungu ni kanisa la Mungu aliye hai,

Nguzo ya msingi wa ile kweli.

1 Timotheo 3:15b (GWT)

Umeitwa kuwa mshiriki, siyo tu kuamini.

Hata katika mazingira makamilifu yasiyo na dhambi ya Edeni, Mungu alisema, “Si vyema mtu kuwa peke yake.” (Mwanzo 2:18) Tumeumbwa kuwa katika jamii, tukatengenezwa kuwa na ushirika, na tukaumbwa tuwe jamii, na hakuna mmoja wetu anayeweza kutimiza malengo ya Mungu peke yake.

Bilia haielewi chochote juu ya watakatifu wanaoishi peke yao au watu wa rohoni wanaojitenga kutoka waamini wengine na kujinyima ushirika na wengine. Biblia inasema tumewekwa pamoja, tumeungwa pamoja, tumejengwa pamoja, tu warithi pamoja,  na tutanyakuliwa pamoja. (1 Wakorintho 12:12-13; Waefeso 2:21,22; 3:6; 4:16; Kolosai4:17.) Huko peke yako tena.

Wakati uhusiano wako kwa Kristo ni kati yako na yeye, Mungu hakukusudia uwe wa binafsi. Katika jamii ya Mungu umeunganishwa na kila mwamini mwingine, na kila mtu ni sehemu ya mwingine milele. Biblia inasema, “Katika Kristo sisi ambao ni wengi tumekuwa mwili mmoja, na kila mmoja ni sehemu ya wengine wote.” Warumi 12:5 (NIV)

Kumfuata Kristo ni pamoja na kuwa mshirika, siyo tu kuamini. Sisi ni viungo vya mwili wake-yaani kanisa. C.S. Lewis alisema kuwa neon ushirika (membership) lina asili ya Ukristo, lakini ulimwengu umeliondolea maana yake ya asili Masoko hutoa punguzo la bei kwa “washirika” wake, na watangazaji hutumia jina la mwanachama kutengeneza orodha ya usafirishaji. Katika kanisa ushirika ni kuandikisha jina lako au Bila masharti au wajibu.

Kwa Paul, Kuwa “mshirika” wa kanisa alimaanisha kuwa kiungo cha mwili ulio hai, hiungo muhimu, kilichoshikamana na viungo vingine katika mwili wa Kristo. (Warumi 12:4-5; 1 Wakorintho 6:15; 12:12-27.) Tunahitaji kurudia na kutenda sawasawa na maana ya kibiblia ya “ushirika.” Kanisa ni mwili, siyo jengo, kiumbe na siyo chama.

Tunagundua wajibu wetu katika maisha kwa njia ya uhusiano na wengine.

Ili viungo vya mwili wako viweze kufanya kazi yake, lazima viwe vimeungwa kwenye mwili. Hii ndivyo ilivyo kwako kama sehemu ya mwili wa Kristo. Uliumbwa kwa ajili ya kazi maalum, lakini utakosa lengo hili la pili kwa maisha yako kama haukushikana na kanisa la mahali lililo hai. Utagundua wajibu wako katika maisha kwa njia ya uhusiano na watu wengine. Biblia inatuambia, “Kila kiungo hupata maana katika mwili mzima, siyo kinyume cha hapo. Mwili tunaozungumzia ni mwili wa Kristo wa watu waliochaguliwa. Kila mmoja wetu hupata maana na wajibu kama sehemu ya mwili wake. Lakini kama kidole kilichokatwa kisivyokuwa na maana yoyote, hata sisi hatuwezi kufaa.” Warumi 12:4-5 (Msg)

Kama kiungo kimeondolewa kwenye mwili wake, kitasinyaa na kufa. Hakiwezi kuishi peke yake, na hata wewe huwezi. Ukiwa umetengwa na kukatwa toka kwenye damu ya uhai ya kanisa la mahali, maisha yako ya kiroho yatanyauka na hatimaye yatakoma. (Waefeso 4:16) Ndiyo maana dalili ya kwanza ya kuanguka kiroho mara nyingi nikutohudhuria mara kwa mara katika ibada na mikusanyiko mingine ya waamini. Tunapoacha kujali kuhusu ushirika, kila kitu kingine huanza kuteleza pia.

Ushirika katika jamii ya Mungu ni jambo la muhimu si la kudharau. Kanisa ni mjadala wa Mungu kwa ulimwengu. Yesu alisema, “Nitalijenga kanisa langu, na nguvu za kuzimu hazitalishinda.” Mathayo 16:18 (NLT) Kanisa haliharibiwi na litadumu milele. Litakuwepo hata baada ya ulimwengu huu, ndivyo ilivyo hata kwa wajibu wako ndani yake. Mtu anayesema “Sihitaji kanisa,” ni mwenye majivuno au haelewi. “Kristo alilipenda kanisa na akatoa maisha yake kwa ajili yake.” Waefeso 5:25 (GWT)

Kanisa litakuwepo hata baada ya ulimwengu huu, ndivyo ilivyo hata kwa wajibu wako ndani yake.

Biblia huliita kanisa “bibi arusi kwa Kristo” na “mwili wa Kristo.” (2 Wakorintho 11:2; Efeso 5:27; Ufunuo 19:7.) Siwezi kufikiri kumwambia Yesu, “nakupenda lakini simpendi mke wako.” Au “nakupokea lakini naukataa mwili wako.” Lakini tunafanya hivyo kila tunaposusia au kulidharau, na kulinung’unikia kanisa. Badala yake, Mungu anatuamuru kulipenda kanisa kama Yesu mwenyewe anavyolipenda. Biblia inasema, “Ipendeni jamii yenu ya kiroho.” 1 Petro 2:17b (Msg) Inahuzunisha kwamba Wakristo wengi hulitumia kanisa lakini hawalipendi.

USHIRIKA WAKO WA MAHALI

Mara nyingi kila neon kanisa linapotumika katika Biblia linamaanisha kusanyiko la mahali linaloonekana, isipokuwa tu kwa matumizi machache sana, humaanisha waamini wote katika historia. Agano Jipya linaonyesha kuwa kila mwamini ni mshirika wa kanisa la mahali. Wakristo pekee ambao hawakuwa washiriki wa kanisa la mahali ni wale waliokuwa kwenye marudio ya kanisa ambao wameondolewa kwa sababu ya dhambi za hadharani. (1 Wakorintho 5:1-13; Wagalatia 6:1-5.)

Biblia husema Mkristo ambaye hana kanisa la nyumbani ni kama kiungo kisicho na mwili, kondoo asiye na kundi, au mtoto asiye na jamaa. Ni hali isiyo ya kawaida. Biblia inasema, “Ninyi ni watu wa nyumbani mwa Mungu pamoja na kila Mkristo mwingine.” Waefeso 2:19b (LB)

Mila ya leo ya ubinafsi na kujitegemea imesaababisha kuwepo yatima wa kiroho wengi- “Wakristo wa majina” wanaozunguka kutoka kanisa moja hadi jingine bila utambulisho, kuwajibika, wala kujitoa. Wengi huamini eti mtu anaweza kuwa “mwamini mzuri” bila kujiunga (au hata kuhudhuria) katika kanisa la mahali; lakini Mungu hatakubaliana nao kabisa. Biblia hutoa sababu nyingi za maana kuhusu kuwa mshirika mwaminifu na hai katika kanisa la mahali.

KWA NINI UNAHITAJI JAMII YA KANISA

Jamii ya kanisa hukutambulisha kama mwamini halisi. Siwezi kudai kuwa mimi namfuata Kristo kama mimi si mmoja wa kikundi maalum cha wafuasi wake. Yesu alisema, “Upendo wenu kati yenu utathibitisha kwa ulimwengu kwamba ninyi ni wafuasi wangu.” Yohana 13:35 (NLT)

Tunapokutanika katika upendo kama jamii ya kanisa kutoka mazingira tofauti, rangi, au daraja za kijamii tofauti, ni ushuhuda mkubwa kwa ulimwengu. Wagalatia 3:28 (Msg); Yohana 17:21. Wewe si mwili wa Kristo peke yako. 1 Wakorintho 12:27 (NCV)

Jamii ya kanisa hukuondoa kutoka upweke wa ubinafsi. Kanisa la mahali ni darasa la kujifunza jinsi ya kuendelea katika jamii ya Mungu. Ni mahali pa kujizoeza kutokuwa na uchoyo,upendo wenye huruma. Kama mshiriki mtendaji unajifunza kuwajali wengine na kushiriki katika mambo yao: “Kama kiungo kimoja cha mwili kitaugua, viungo vingine vyote huugua pamoja nacho. Au kama kiungo kimoja cha mwili wetu kitatukuzwa, viungo vingine vyote hushiriki heshima hiyo.” 1 Wakorintho 12:26 (NCV) Kaika kushiriki na waamini kwa kawaida, wasio wakamilifu, ndipo tunajifunza ushirika halisi na uzoefu wa ukweli wa Agano Jipya wa kuwa katika mshikamano na kutengemeana mmoja kwa mwingine. (Waefeso 4:16; Warumi 12:4-5; Wakolosai 2:19, 1 Wakorintho 12:25.)

Ushirika wa kibiblia ni sisi kushikamana kama tunavyoshikamana na Kristo. Mungu anatutegemea kutoa maisha yetu kwaa ajili ya wenzetu. Wakristo wengi wanaofahamu Yohana 3:16 hawafahamu 1 Yohana 3:16. “Yesus Kristo alitoa maisha yake kwa ajili yetu. Imetupasa na sisi kutoa maisha yetu kwa ajili ya wengine.” 1 Yohana 3:16 (NIV) Huu ni mfano wa upendo wa jujitoa sadaka ambao Mungu anatutaka tuwaonyeshe waamini wengine-kuwapenda kama Kristo anavyokupenda.

Jamii ya kanisa hukusaidia kukomaa kiroho. Huwezi kamwe kukomaa kwa kuhudhuria ibada tu na kuwa mtazamaji. Ni katika kushriki kikamilifu katika maisha ya kanisa la mahali ndipo utajengwa kiroho. Biblia inasema, “Kama kila kiungo kinafanya kazi yake maalum, husaidia viungo vingine kukua, kiasi kwamba mwili wote unakuwa na afya na kukua, na kuwa na upendo tele.” Waefeso 4:16b (NLT)

Zaidi ya mara hamsini katika Agano Jipya maneno “kati yenu” au “mmoja kwa mwenzake” yametumiwa. Tumeagizwa kupendana mmoja kwa mwenzake, kuombeana, kutiana moyo, kuonyana, kusalimiana, kutumikiana, kufundishana, kupokeana, kuheshimiana, kubebeana mizigo, kusameheana, kunyenyekeana, kujitoa mmoja kwa mwenzake na kazi nyinginezo za kutendeana. Huu ndio ushirika wa kanisa la mahali. Je, unafanya majukumu haya na nani?

Inaweza kuonekana rahisi kuwa mtakatifu kunapokuwa hakuna mtu yeyote karibu wa kukuvuruga mambo yako, lakini huu ni utakatifu usio wa kweli na ambao haujajaribiwa. Kujitenga huleta udanganyifu, ni rahisi kujidanganya kuwa tumepevuka iwapo hakuna watu wa kutupa changamoto. Upevu wa kweli huonekana katika uhusiano.

Tunahitaji Zaidi ya Biblia ili tukue; tunahitaji waumini wengine. Tunakua haraka na wenye nguvu kwa kujifunza kutoka kwa wenzetu na kuwajibika kwa kila mmoja wetu. Wengine wanaposhirikisha yale Mungu anawafundisha tunajifunza na kukua pia.

Mwili wa Kristo unakuhitaji. Mungu ana jukumu maalum kwa ajili yako ulifanye katika jamii yake. Hili huitwa “huduma” yako, na Mungu amekupa vipawa kwa ajili ya jukumu hili: “Karama ya kiroho imetolewa kwa kila mmoja wetu kama njia ya kulisaidia kanisa lote.” 1 Wakorintho 12:7 (NLT)

Kanisa lako la mahali ndipo Mungu alipkuandalia wewe ili ugundue, uendeleze, na kutumia vipawaa vyako. Unaweza pia kuwa na huduma pana, lakini hiyo ni nyongeza kwa huduma yako katika kanisa la mahali. Yesu hakuahidi kujenga huduma yako, aliahidi kujenga kanisa lake.

Utashiriki katika huduma ya Mungu kwa ulimwengu. Yesu alitembea hapa duniani; Mungu alitembea kupitia mwili halisi wa Kristo. Kanisa ni chombo cha Mungu duniani. Hatupaswi kuonyesha upendo wa Mungu kwa kupendana sisi tu, lakini tunatakiwa kuupeleka pamoja kwa ulimwengu nzima. Huu ni upendeleo mkubwa tuliopewa kwa pamoja. Kama viungo katika mwili wa Kristo, sisi ni mikono yake, miguu yake, na moyo wake. Anafanya kazi ulimwenguni kupitia sisi. Sisi kila mmoja ana mchango wake wa kutoa. Paulo anatuambia, “Anatuumba kila mmoja wetu kwa njia ya Kristo ili kujiunga naye katika kazi anayoifanya, kazi njema aliyotuandalia tuifanye, kazi ambayo yatupasa tuifanye.” Waefeso 2:10 (Msg)

Yesu hakuahidi kuijenga huduma yako; aliahidi kujenga kanisaa lake.

Jamii ya kanisa inakusadia usirudi nyuma. Hakuna kati yetu aliyesugu wa majaribu. Katika mazingira mwafaka, wewe na mimi tunaweza kutenda dhambi. (1 Wakorintho 10:12; Yeremia 17:9; 1Timotheo 1:19.) Mungu analijua hili, hivyo ametupatia wajibu kila mmoja kumwangalia mwingine. Biblia inasema, “Tianeni moyo ninyi kwa ninyi kila siku … ili kwamba asiwepo mmoja wenu atakaye fanywa kuwa na moyo mgumu kwa sababu ya dhamibi.” Waebrania 3:13 (NIV) “Jali mambo yako” siyo msemo wa Kikristo, tumeitwa na kuagizwa kuhusika na maisha ya wenzetu. Kama unamjua mtu fulani ambaye anayumba kiroho sasa hivi, ni wajibu wako kumwendea na kumrejeza katika ushirika. Yakobo anatuambia, “Kama mnawajua watu waliotoka na kwenda mbali ya kweli ya Mungu, msiwaache. Wafuateni. Warejezeni.” Yakobo 5:19 (Msg)

Faida nyingine kama hiyo ya kanisa la mahali ni kwamba hutoa ulinzi wa kiroho wa viongozi wacha Mungu. Mungu anawapa viongozi wachungaji jukumu la kulinda, kutunza, kupigania, na kuangilia maslahi ya kundi lake. (Matendo 20:28-29; 1 Petro 5:1-4; Waebrania 13:7, 17.) Tunaambiwa, “Kazi yao ni kuangalia nafsi zenu na wanajua kuwa watatoa hesabu kwa Mungu.” Waebrania 13:17 (NLT)

Shetani hupenda waamini waliojitenga, waliojiondoa kwenye uhai wa mwili, waliojitenga na jamii ya Mungu, na wasiotoa hesabu kwa viongozi wa kiroho, kwa kuwa anajua hao hawana kinga wala nguvu dhidi ya mbinu zake.

YOTE YAKO KANISANI

Katika kitabu change, Kanisa Linaloongozwa Na Malengo, nimeelezea jinsi ambavyo kuwa sehemu ya kanisa imara ni muhimu kwa kuishi maisha ya ushindi. Natumaini utasoma kitabu hicho pia, kwa sababu kitakusaidia kuelewa jinsi Mungu alivyolibuni kanisa lake ili likusaidie kutimiza yale malengo matano aliyo nayo kwa ajili ya maisha yako. Alilitengeneza kanisa kukidhi mahitaji yako matano ya kina: lengo la kuishi, watu wa kuishi nao, kanuni za kuishi, ukiri wa kuishi, na nguvu za kuishi. Hakuna sehemu nyingine yoyote duniani unakoweza kupata faida zote hizi tano sehemu moja.

Malengo ya Mungu kwa kanisa lake yanafanana na malengo yake matano kwako. Kuabudu hukusaidia kumtazama Mungu, ushirika hukusaidia kukabili matatizo ya maisha; mafundisho hukusaidia kuimarisha imani yako; huduma hukusaidia kupata vipawa vyako; uinjilisti hukusaidia kutimiza wito wako. Hakuna kingine duniani kilicho kama kanisa.

UCHAGUZI WAKO

Kila mtoto anapozaliwa, mara moja yeye huwa ni sehemu ya jamaa ya watu wote duniani. Lakini pia mtoto huyo anahitaji kuwa mshirika wa jamaa maalum ili kupata malezi ili akue na kustawi. Jambo hili ni la kweli hata kiroho. Ulipozaliwa mara ya pili, mara moja ulijiunga na jamii ya Mungu ya waamini wote, lakini unahitaji pia mahali utakaposhiriki kama jamii ya Mungu.

Tofauti ya kuwa mhudhuria kanisani na mshirika wa kanisa ni kule kujitoa. Wahudhuriaji ni watazamaji kutoka pembeni; washirika huhusika na huduma. Wahudhuriaji ni watumiaji tu, washirika ni watoaji. Wahudhuriaji hutaka faida ya kanisa bila kushiriki majukumu. Hawa ni kama watu wawili wanaotaka kuishi pamoja bila kujitoa kufunga ndoa.

Kwa nini ni muhimu sana kujunga na jamii ya kanisa la mahali? Kwa sababu inathibitisha kwamba umejitoa kushirikiana na ndugu na dada kikweli, sio kwa nadharia. Mungu anakutaka upende watu halisi, sio watu wa mawazoni tu. Unaweza kutumia muda wote wa maisha yako ukitafuta kanisa kamilifu, Lakini hutalipata. Umeitwa kupenda watu wasio wakamilifu na wakosaji, kama Mungu anavyowapenda.

Katika Matendo ya Mitume, Wakristo walikuwa makini katika kujitoa mmoja kwa mwenzake. Walikuwa wamejitoa kwa ushirika. Biblia inasema, “Walidumu katika mafundisho ya mitume, maisha ya pamoja, kula pamoja, na kusali.” Matendo 2:42 (Msg) Mungu anakutarajia udumu katika kufanya mambo kama hayo siku hizi.

Maisha ya Kikristo ni Zaidi ya kujitoa kwa Kristo, ni pamoja na kujitoa kushiriki na Wakristo wengine. Wakristo kule Makedonia walilijua jambo hili. Paulo alisema, “Kwanza walijitoa nafsi zao kwa Bwana, kisha, kwa mapenzi ya Mungu, na walijitoa kwetu pia.” 2 Kakorintho 8:5 (TEV) Kujiunga na ushirika wa kanisa la mahali ni hatua inayofuata baada ya kuwa Mwana wa Mungu. Unakuwa mshirika wa kanisa kwa kujitoa kushiriki katika kikundi maalum cha waamini. Uamuzi wa kwanza huleta wokovu, uamuzi wa pili huleta ushirika.

SIKU YA KUMI NA SABA

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Nimeitwa kuwa mshirika siyo kuamini tu.

Kifungu cha Kukumbuka:Katika Kristo sisi tulio wengi tunafanya mwili mmoja, na kila kiungo ni sehemu ya viungo vingine.” Warumi 12: 5 (NIV)

Swali la kujiuliza: Je kuhusika kwangu katika kanisa langu la nyumbani kunadhihirisha kwamba naipenda na kujitoa kwa ajili ya jamii ya Mungu?

 Siku Ya Kumi Na Nane: Maisha Ya Pamoja

Kila mmoja wenu ni sehemu ya mwili wa Kristo, na

Mlichaguliwa ili muishi pamoja kwa amani.

Wakolosai 3:15 (CEV)

Ni ajiabu, na inapendeza sana, kwa watu wa Mungu

Kuishi pamoja kwa umoja!

Zaburi 133:1

Maisha ni kushirikiana.

Mungu anatukusudia tushirikiane katika maisha. Biblia huita hali hii ya kushirikiana ushirika (fellowship). Siku hizi, lakini neno hili limepoteza maana yake ya kibiblia. “Ushirika” mara nyingi sasa humaanisha mazungumzo ya kawaida, mahusiano, chakula, na burudani Swali, “Je, unashiriki wapi?” humaanisha “Unahudhuria kanisa gani?” “Kaa baada ya ushirika,” humaanisha “subiri vinywaji.”

Ushirika halisi ni Zaidi ya kuonekana tu katika ibada. Ni kushiriki maisha pamoja. Ni pamoja na upendo usio na choyo, kushirikishana kwa uaminifu, kutumika, kutoa kwa moyo, kufariji kwa kuhurumiana, na amri nyinginezo zote za Agano Jipya za “mmoja kwa mwingine.”

Inapokuja kuhusu ushirika, ukubwa wa kikundi ni muhimu: kikundi kidogo ni bora zaidi. Unaweza kuabudu na kundi, lakini huwezi kushirikiana nalo. Mara kundi linapokuwa kubwa kuliko watu wapatao kumi, wengine huanza kutoshiriki-hasa mtu mkimya-na watu wachache tu hutawala kikundi.

Yesu alihudumu katika mazingira ya kikundi kidogo cha wanafunzi. Angeweza kuchagua wengi, lakini alijua kuwa kumi na mbili ni kiwango cha juu cha watu katika kikundi kidogo iwapo kila mmoja atatakiwa kushiriki.

Mwili wa Kristo. Kama mwili wako, ni mkusanyiko wa chembechembe nyingi. Uhai wa mwili wa Kristo, kama mwili wako, uko katika chembechembe. Kwa sababu hii, kila Mkristo anatakiwa kushiriki katika kikundi kidogo kanisani mwake, chaweza kuwa kikundi kidogo cha nyumbani, darasa la Jumapili, au kikundi cha kujisomea Biblia. Hapa ndipo ushirika halisi kutokea, si katika mikusanyiko mikubwa. Kama unalifikiri kanisa lenu kama meli, basi vile vikundi vidogo ni kama zile meli za kuokoa zilizofungwa hapo.

Mungu amefanya ahadi kubwa kuhusu vikundi vidogo vya waamini: “Kwa kuwa wawili au watatu wakikusanyika kwa jina langu, niko hapo katikati yao.” Mathayo 18:20 (NASB) Kwa bahati mbaya, hata kuwa katika kikundi kidogo hakutuhakikishii kwamba utapata ushirika halisi. Madarasa mengi ya shule za Jumapili na vikundi vidogo vimezama kwenye taratibu za kawaida na hawana habari kabisa na ushirika halisi ni upi. Je, tofauti ni ipi kati ya ushirika halisi na ule wa kuigiza?

Katika ushirika wa kweli watu hupata uhalisi. Ushirika halisi si wa kuigiza, mazungumzo ya juu juu tu. Ni wa kweli, wa kutoka moyoni, wakati mwingine mazungumzo ya kina. Hii hutokea wakati watu wanapokuwa waaminifu juu ya wao ni ndani na nini kinatokea maishani mwao. Hushirikishana mambo yanayo waumiza, hufunua hisia zao, hukiri kushindwa kwao, hufunua mashaka yao, hukiri hofu zao, hukubali udhaifu wao, na kuomba msaada na maombi.

Uhalisi ni kinyume cha unachokikuta katika baadhi ya makanisa. Badala ya mazingira ya uaminifu na unyenyekevu, kuna kuigiza, kujionyesha, kufanya siasa, na upole wa nje tu lakini mazungumzo duni. Watu huvaa kifuniko cha uso, wakijilinda na kutenda kama vile kila kitu ni shwari maishani mwao. Hali za namna hii ni kifo cha ushirika wa kweli.

Ushirika wa kweli hutokea

wakati watu wanapokuwa

Waaminifu juu ya wao ni nani

na nini kinatokea maishani mwao.

Ni pale tu tunapokuwa wazi kuhusu maisha yetu ndipo tunapata ushirika halisi. Biblia inasema, “Kama tukiishi nuruni, kama vile Mungu alivyo nuruni, tunaweza kuwa na ushirika kati yetu … Kama tukisema hatuna dhambi, tunajidanganya wenyewe.” 1 Yohana 1:7-8 (NCV) Ulimwengu unadhani ukaribu hutokea gizani, lakini Mungu anasema hutokea nuruni. Giza hutumika kuficha maumivu yetu, makosa, hofu kushindwa, na upungufu. Lakini nuruni, tunayaleta yote wazi na kukiri jinsi tulivyo.

Kwa kweli, kuwa mkweli huhitaji ujasiri na unyenyekevu. Humaanisha kukabili hofu zetu za kuwekwa wazi, kukataliwa na kuumizwa tena. Kwa nini mtu yeyote ajihatarishe hivyo? Kwa sababu ndiyo njia pekee ya kukua kiroho na kuwa na hisia nzuri. Biblia husema, “Fanyeni jambo hili daima: ungamianeni dhambi ninyi kwa ninyi na kuombeana ili muishi pamoja kwa amani na kuponywa.” Yakobo 5:16a (Msg) Tunakuwa tu kwa kujihatarisha, na hatari kubwa zaidi ni kule kuwa wakweli kwetu wenyewe na kwa wengine.

Katika ushirika wa kweli watu hutegemeana. Kutegemeana (mutuality) ni maisha ya kutoa na kupokea. Ni Kutegemeana. Biblia husema, “Mungu alivyoibuni miili yetu ni kielelezo cha kuelewa maisha yetu pamoja kama kanisa: kila kiungo hutegemea kila kiungo kingine.” 1 Wakorintho 12:25 (Msg) Kutegemeana ni kiini cha ushirika: kujenga uhusiano wa kutendeana, kushirkiana wajibu, na kusaidiana. Paulo alisema, “Nataka tusaidiane kila mmoja na mwenzake kwa imani tuliyo nayo. Imani yenu itanisaidia, na Imani yangu itawasaidia.” Warumi 1:12 (NCV)

Sisi sote Imani yetu huwa imara pale watu wengine wanatembea nasi na kututia moyo. Biblia inahimiza kila mtu kuwajibika kwa mwenzake, kutiana moyo, kutumikiana, na kuheshimiana. Warumi 12:10 (NRSV) Zaidi ya mara hamsini katika Agano Jipya tumeagizwa “kututendeana.” Biblia husema, “Fanyeni bidii katika yale yanayoleta amani ya kujengana ninyi kwa ninyi.” Warumi 14:19 (NIV)

Hauwajibiki kwa kila mtu katika mwili wa Kristo, lakini unawajibika kwao. Mungu anakutarajia kufanya uwezavyo kuwasaidia.

Katika ushirika wa kweli watu hupata huruma (sympathy). Huruma siyo kutoa ushauri au msaada wa haraka; huruma ni kuzama ndani na kushiriki maumivu ya wengine. Huruma husema, “Naelewa unachopata, na unavyojihisi siyo wenda wazimu au wehu.” Siku hizi watu wengine huita “kumwelewa mtu” (empathy), lakini Biblia hutumia neno “huruma” (sympathy). Biblia husema, “Kama watu watakatifu … muwe na huruma, wema, wanyenyekevu, wapole na wavumilivu.” Wakolosai 3:12 (GWT)

Huruma husaidia mahitaji mawili makuu ya binadamu: hitaji la kueleweka na hitaji la hisia za mtu kukubalika. Kila wakati unapoelewa na kukubali hisia za mtu mwingine unajenga ushirika. Tatizo ni kwamba, mara nyingi tunaharaka ya kushughulikia mambo na hatuna muda na watu. Au tumechukuliwa sana na matatizo yetu. Kujihurumia binafsi huondoa huruma kwa watu wengine.

Kuna viwango tofauti vya ushirika, na kila kiwango kinafaa kwa wakati wake. Viwango rahisi vya ushirika ni ushirika wa kushirikishana na ushirika wa kujifunza neno la Mungu pamoja. Kiwango cha kina ni kile cha ushirika wa kutumika, kama tunapohudumu pamoja katika safari za umisheni au miradi ya rehema. Kiwango cha kina kuliko zote ni ushirika wa mateso, (Wafilipi 3:10; Waebrania 10:33-34) ambapo tunaingia katika maumivu na huzuni za mwenzetu na kubebeana mizigo. Wakristo wanaoelewa kiwango hiki vyema ni wale walio katika nchi za mateso, wakidharauliwa na kuuwawa kwa ajili ya Imani yao.

Biblia inaagiza, “Shirikianeni katika matatizo na shida za kila mmoja wenu, na kwa njia hii mpate kuitii sharia ya Kristo.” Wagalatia 6:2 (NLT) Ni katika wakati wa matatizo mazito, msiba, na mashaka ndipo tunahitajiana sana. Mazingira yanapotugandamiza kiasi kwamba Imani yetu inadhoofika, ndipo tunapowahitaji sana marafiki waamini. Tunahitaji vikundi vidogo kuwa na Imani kwa ajili yetu ili kututia nguvu za kuendelea. Katika kikundi kidogo, mwili wa Kristo ni dhahiri hata kama Mungu anaonekana kuwa mbali. Hiki ndicho Ayubu alikihitaji mno wakati wa mateso yake. Alilia, “Mtu aliyevunjika moyo anahitaji faraja wa rafiki zake, hata kama ataiacha hofu ya Mwenyezi Mungu.” Ayubu 6:14 (NIV)

Katika ushirika wa kweli watu hupata rhema (mercy). Ushirika ni sehemu ya neema, ambapo makosa hayatunzwi bali kuondolewa. Ushirika hutokea pale rehema inashinda hukumu.

Sote tunahitaji rehema, kwa kuwa sote tunajikwaa na kuanguka na kuhitaji msaada ili kurudi katika njia. Tunahitaji kurehemiana na kuwa tayari kupokea kutoka kwa wenzetu. Mungu anasema, “Watu wanapotenda dhambi, wasameheni na huwatia moyo, ili wasikate tamaa.” 2 Wakorintho 2:7 (CEV)

SIKU YA KUMI NA NANE:

MAISHA YA PAMOJA

Hamwezi kuwa na ushirika bila husameheana. Mungu anaonya, “Msiwe na uchungu moyoni,” Wakolosai 3:13 (LB) kwa sababu nchungu na chuki mara nyingi huharibu ushirika. Kwa kuwa hatuko wakamilifu, na ni wenye dhambi ni wazi kuwa tunaumizana tunapokuwa pamoja kwa muda wa kutosha. Wakati mwingine tunaumizana kwa makusudi na wakati mwingine bila kukusudia, lakini kati ya hayo, inahitajika rehema na neema nyingi ili kutengeneza ushirika. Biblia inasema, “Ni lazima mchukuliane katika makosa na kumsamehe mtu anayewakosea. Kumbukeni, Bwana aliwasamehe, hivyo imewapasa kuwasamehe wengine.” Wakolosai 3:13 (NLT)

Rehema ya Mungu kwetu ni kichocheo cha kuonyesha rehema kwa wengine. Kumbuka hautaelezwa kumsamehe mtu mwingine saidi ya alivyokusamehe Mungu.

Unapoumizwa na mtu fulani, unao uchaguzi wa kufanya: Je, nitatumia nguvu na hisia zangu kulipa kisasi au kusuluhisha? Huwezi kufanya yote mawili.

Watu wengi husita kuonyesha rehema kwa sababu hawaelewi tofauti ya imani na msamaha. Kusamahe ni kuyaacha yaliyopita. Imani inahusika na tabia ya mbele.

Kusamehe lazima kufanywe mara moja, bila kujali kama mtu ameomba msamaha huo au la. Imani inajengeka kwa muda kitambo. Imani inahitaji ufuatiliaji mrefu. Kama mtu atakuumiza mara nyingi, umeagizwa na Mungu kuwasamahe mara moja, lakini hutazamiwi kuwaamini mara moja. Wala hutemegewi kuwaruhusu kuendelea kukuumiza. Ni lazima wathibitishe kuwa wamegeuka kadiri muda unavyopita. Mahali mwafaka pa kurejeza imani ni katika mazingira ya kikundi kidogo cha kutiana nguvu ambacho hutia moyo na kuwajibishana.

Kuna faida nyingine nyingi utakazozipata kwa kujiunga na kikundi kidogo kilichojitoa kuwa na ushirika wa kweli. Ni sehemu ya muhimu ya maisha yako ya Kikristo ambayo hutakiwi kuyapuuza. Kwa Zaidi ya miaka 2,000 Wakristo wamekuwa wakikusanyika kwenye vikungi vidogo vidogo vya ushirika. Kama hujawahi kuwa katika kikundi au darasa la namna hii, kwa kweli hujui unachokikosa.

Katika sura inayofuata tutaona ni nini kinatakiwa ili kuweza kuunda jumuiya kama hii na waamini wengine, lakini natumaini sura hii imekujengea hamu ya kupata uhalisi, kutegemeana, huruma, na rehema katika ushirika wa kweli. Uliumbwa kwa ajili ya jamii.

SIKU YA KUMI NA NANE

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Nawahitaji wengine maishani mwangu.

Kifungu cha Kukumbuka:Saidianeni katika shida na matatizo, ili muitimize sharia ya Kristo.” Wagalatia 6:2 (NLT)

Swali la Kujiuliza: Je, ni hatua gani moja ninayoweza kuchukua leo ili kujenga uhusiano na mwamini mwingine katika hali ya kweli kutoka moyoni?

 Siku ya Kumi na Tisa: Kukuza Jamii

Mnaweza kujenga jamii yenye afya na yenye kustawi, ambayo inaishi sawa mbele za Mungu na kufurahia matunda yake iwapo mtafanya bidii kuwa na amani kati yenu, mkiheshimiana.

Yakobo 3:18 (Msg)

Walijitoa kupokea mafundisho ya mitume, kuishi kwa pamoja, wakila pamoja, na kusali pamoja.

Matendo 2:42 (Msg)

Ushirika wa jamii huhitaji kujitoa.

Ni Roho Mtakatifu peke yake anayeweza kujenga ushirika wa kweli kati ya waamini lakini huukuza kwa kuzingatia uchaguzi wetu nakujitoa kwetu. Paulo anautaja wajibu huu wa aina mbili kwa kusema, “Mumeungwa pamoja kwa amani kwa njia ya Roho Mtakatifu, hivyo fanyeni bidii katika kudumu pamoja.” Waefeso 4:3 (NCV) Inahitajika nguvu ya Mungu na bidii yetu ili kupata jamii ya Kikristo yenye upendo.

Kwa bahati mbaya, watu wengi hukua katika jamaa zenye uhusiano duni, hivyo wanakuwa hawana ujuzi wa mahusiano unaotakiwa kwa ajili ya ushirika halisi. Ni lazima wafundishwe jinsi ya kuhusiana na wengine katika jamii ya Mungu. Inapendeza kwamba, Agano Jipya limejaa maelekezo ya namna ya kushirikiana pamoja kimaisha. Paulo aliandika, “Nakuandikia mambo haya … ili ujue inavyopaswa kuishi katika jamii ya Mungu, jamii hiyo ni kanisa.” 1 Timotheo 3:14-15 (NCV)

Kama umechoka na ushirika usio halisi na ungependa kujenga ushirika wa kweli na jamii yenye upendo katika kikundi chako kidogo, shule ya Jumapili, na kanisa, utahitaji kufanya maamuzi magumu na kuchukua hatua.

Kujenga ushirika wa jamii huhitaji uaminifu. Utahitaji kuwa mtu mwenye kujali ili useme ukweli katika upendo, hata wakati ambapo ungekaa kimya na kupuuzia jambo fulani. Ingawa ni rahisi kunyamaza wakati wengine karibu yetu wanaumizana au wengine wanatenda dhambi, huu siyo upendo. Watu wengi hawana mtu anayewapenda kiasi cha kuwaeleza ukweli (hata kama inaumiza), hivyo wanadumu katika njia za kujiangamiza. Mara nyingi tunajua kile kinachostahili kusemwa kwa mtu fulani, lakini woga wetu hutuzuia kusema chochote. Ushirika mbalimbali umevunjika kwa sababu ya hofu: Hapa kuwa na mtu yeyote wa kusema kitu wakati maisha ya mshirika fulani yalikuwa hatarini.

Biblia inatuambia, “Semeni ukweli katika upendo.” (Waefeso 4:15) Kwa sababu hatuwezi kuwa na ushirika wa kijamii bila unyofu. Suleimani alisema, “Jibu la uaminifu ni ishara ya urafiki wa kweli.” Mithali 24:26 (TEV) Wakati mwingine itamaanisha kuonyesha upendo kwa kumwendea moja kwa moja ndugu anayetenda dhambi au anayejaribiwa kutenda dhambi, “Ndugu zangu wa kiume na wa kike, kama mmoja wenu katika kikundi akitenda kosa, ninyi mlio wa kiroho lazima mwende kwa mtu huyo na kumsaidia kwa upole apate kurejea.”Wagalatia 6:1-2 (NCV)

Ushirika mwingi wa kanisa na vikundi vidogo vidogo hubaki wa juu juu tu kwa sababu watu wanaogopa migogoro. Kila kunapotokea jambo ambalo linaweza kusababisha machafuko, mara moja linafunikwa ili kutunza amani ya uongo. Tatizo halitatuliwi na kila mmoja anaishi katika hali ya kukata tamaa. Kila mtu anajua juu ya tatizo hilo, lakini hakuna anayelizungumzia wazi. Hali hii huumba mazingira mabaya ambamo siri na usengenyaji hujikita. Suluhisho la Paulo lilikuwa wazi. “Hakuna tena uongo. Hakuna tena kuigiza. Mwambie jirani yako ukweli. Katika mwili wa Kristo sisi sote tumeunganishwa pamoja pia. Unapowadanganya wengine unajidanganya mwenyewe.” Waefeso 4:25 (Msg)

Migongano inapotatuliwa ipasavyo, tunaendelea kuwa karibu zaidi mmoja kwa mwingine.

Ushirika halisi, iwe katika ndoa, urafiki, kanisani mwenu, hutegemea uwazi. Kwa kweli, migogoro ni njia ya kuelekea uhusiano wa karibu mpaka kuonyesha kujali kiasi cha kukabili na kutatua vikwazo, haiwezekani kukua na kufikia uhusiano wa karibu. Migogoro inapotatuliwa kwa uangalifu tunakuza ukaribu kwa kukabili na kuondoa tofauti zetu. Biblia inasema, “Hatimaye watu hufurahia uwazi kuliko kujipendekeza.” Mithali 28:23 (NLT)

Uwazi siyo kibali cha kusema chochote unachotaka, popote na saa yoyote. Siyo ujeuri. Biblia hutuambia kuna wakati mwafaka na njia sahihi ya kufanya killa kitu. Mhubiri 8:6 (TEV) Maneno ya bila kufikiri huacha vidonda vya kudumu. Mungu anatuagiza na kusema pamoja katika kanisa kama wanajamii wenye upendo: “Usitumie maneno makali unapomrekebisha ndugu alivye mzee, lakini sema naye kama baba yako: Ongea na vijana kama vile ni ndugu zako, akina mama wazee kama vile mama zako, na wasichana kama vile dada zako.” 1 Timotheo 5:1-2 (GWT)

La kusikitisha, vikundi maelfu vimeharibiwa kwa kukosa uaminifu. Paulo aliwakemea kanisa la Korintho kwa ukimya wao kwa kuruhusu zinaa katika ushirika wao. Kwa kuwa hapakuwepo mtu jasiri wa kukemea hali hiyo, Paulo alisema, “Hampaswi kutazama pembeni na kufikiri mambo yatakwisha yenyewe. Liwekeni wazi na mlishughulikie … Bora uharibifu na kuudhika kuliko hukumu … Malipita tu kama jambo dogo, lakini ni jambo ambalo … hampaswi kutenda kama vile kila kitu kiko sawa wakati Mkristo mwenzenu ni mwovu au amepotoka, hajali Mungu au ni jeuri kwa wenzake, analewa au ni mchoyo, na mnyang’anyi. Huwezi kuyakubali haya tu, kuyafanya ati kama ni tabia zinazokubaliwa. Sihusiki na walio nje, lakini je, hatuna wajibu kwa wale wa jamii ya waamini?” 1 Wakorintho 5:3-12 (Msg)

Kujenga ushirika wa jamii huhitaji unyenyekevu. Kujiona kwa muhimu na kujikinai, na kiburi huharibu ushirika haraka sana kuliko chochote. Kiburi hujenga ukuta kati ya watu; unyenyekevu hujenga daraja. Unyenyekevu ni mafuta yanayolainisha na kuvuta mahusiano. Ndiyo maana Biblia inasema, “Jivikeni unyenyekevu katika kuhusiana kwenu.” 1 Petro 5:5 (NIV) Vazi sahihi kwa ajili ya ushirika ni moyo wa unyenyekevu.

Sehemu iliyobaki ya kifungu hicho husema, “… kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi lakini huwapa wanyenyekevu neema.” 1 Petro 5:5c (NIV) Hii ni sababu nyingine ya sisi kuwa wanyenyekevu: Kiburi huzuia neema ya Mungu maishani mwetu, ambayo tunaihitaji ili tukue, tubadilike, tuweze kuponya na kusaidia wengine. Tunapokea neema ya Mungu kwa kukiri kwa unyenyekevu kuwa tunaihitaji. Biblia inasema, wakati wowote tukiwa na kiburi, tunaishi tukipingana na Mungu! Hayo ni maisha ya Kipumbavu na ya hatari.

Unyenyekevu siyo kufikiri

haufai; ni kufikiri juu ya nafsi

yako kidogo

Unaweza kukuza unyenyekevu kwa njia halisi kabisa: Kwa kukiri udhaifu wako, kwa kuwavumilia wengine katika udhaifu wao, kwa kuwa tayari udhaifu wao, kwa kuwa tayari kusahihishwa na kuwa mwazi kwa wengine. Paulo anasema “Muishi katika amani. Msijaribu kujiona bora kuliko wengine. Na msifikiri mnajua yote.” Warumi 12:16 (NCT) Kwa Wakristo wa Filipi aliwaandikia, “Wapeni heshima wengine Zaidi kuliko nafsi zenu. Msichukuliwe tu na mambo ya maisha yenu, lakini yaangalieni maisha ya wengine.” Wafilipi 2:3-4 (NCV)

Unyenyekevu siyo kufikiri hufai, ni kufikiri juu ya nafsi yako kidogo. Unyenyekevu ni kufikiri juu ya wengine Zaidi. Watu wanyenyekevu wana mwelekeo mkubwa sana katika kuwatumikia wengine; hawajifikirii nafsi zao.

SIKU YA KUMI NA TISA:

KUKUZA JAMII

Kujenga ushirika huhitaji adabu. Adabu ni kuheshimu tofauti zetu, kujali hisia za wenzako, na kuwavumilia wengine wanaotukera. Biblia inasema, “Inatupasa kuchukua mzigo wa kujali mashaka na hofu za wengine.” Warumi 15:2 (LB) Paulo alimwambia Tito, “Watu wa Mungu inawapasa kuwa na moyo mkuu na adabu.” Tito 3:2 (Msg)

Katika Kila kanisa na katika kila kikundi kidogo, kuna walau mtu mmoja “mgumu,” mara nyingi ni Zaidi ya mmoja. Watu hawaa wanaweza kuwa na kitaji maalum la kihisia, hofu ya ndani, tabia ya kuudhi, au ujuzi duni wa kijamii. Ni lazima uwaone kama watu Wanaohitaji Neema ya Ziada.

Mungu aliwaweka watu hawa katikati yetu kwa faida yao na yetu pia. Hutupatia nafasi ya kukua na kupima ushirika: Je, tutawapenda kama kaka na dada zetu na kuwapa heshima?

Katika jamaa, kukubaliwa hakutegemei usafi, uzuri, au vipawa vya mtu. Hutegemea ukweli kwamba sisi sote ni wamoja. Tunaitetea na kuilinda jamaa. Mmoja wa jamaa anaweza kuwa mpumbavu kidogo, lakini yeye bado ni mmoja wetu. Vivyo hivyo, Biblia husema, “Shirikianeni ninyi kwa ninyi kama jamii yenye upendo. Mzidi sana katika huheshimiana.” Warumi 12:10 (GWT)

Ukweli ni kwamba, sisi sote tuna mapungufu na tabia za kuchukiza. Lakini ushirika huhusiani na kuiana. Msingi wa ushirika ni uhusiano wetu kwa Mungu: Sisi ni jamii.

Ufunguo wa adabu ni kuelewa watu wanatokea wapi, utaelewa Zaidi. Badala ya kufikiri ni mwendo gani bado wanatakiwa kwenda, fikiri wametoka umbali gani na maumivu yao.

Sehemu nyingine ya adabu ni kuepuka kupuuza hofu za wengine. Ikiwa wewe huogopi kitu fulani, si kwamba hiyo ndiyo hisia sahihi. Watu huwa katika ushirika wa kweli wanapojua kuwa kuna usalama wa kutosha kushirikisha wengine mashaka na hofu zao bila kuhukumiwa.

Ushirikiano wa kanisa ni muhimu Zaidi kuliko mtu yoyote binafsi.

Kujenga jamii huhitaji siri. Ni katika mazingira salama tu, yenye kukaribisha na uaminifu wa kuaminika ndipo watu watafunguka na kushirikisha maumivu yao ya ndani, mahitaji na makosa. Siri siyo kukaa kimya wakati kaka au dada yako anatenda dhambi. Ila kilichozungumzwa katika kikundi kinabaki katika kikundi tu, na kikundi kinatakiwa kushughulikia jambo hilo, na siyo kusengenya kwa wengine.

Mungu anachukia usengeyaji, na hasa inapowekwa kama “maombi” kwa ajili ya mtu mwingine. Mungu anasema, “Usengenyaji huenezwa na watu waovu; huchochea matatizo na kuvunja urafiki.” Mithali 16:28 (TEV) Usengenyaji mara nyingi husababisha mavumivu na matengano, na huharibu ushirika, na Mungu yuko wazi kabisa kwamba lazima tuwakemee wale waletao matengano kati ya Wakristo. Tito 3:10 (NIV) Wanaweza kukasirika au kuondoka kwenye kikundi au kanisani kama utawakemea tabia yao inayoleta mgawanyiko, lakini ushirika wa kanisa ni muhimu Zaidi kuliko mtu yeyote binafsi.

Kujenga jamii huhitaji kufanywa mara nyingi. Ni lazima kukutana na kundi lako mara kwa mara ili kujenga ushirika halisi. Mahusiano huhitaji muda. Biblia inatuambia, “tusiache kukuktanika pamoja, kama wengine wanavyofanya. Badala yake, tutiane moyo.” Waebrania 10:25 (TEV) Tunatakiwa kujenga tabia ya kukutana pamoja. Tabia ni jambo unalofanywa mara kwa mara, siyo kwa muda fulani. Unapaswa kutumia muda na watu-muda mwingi-kujenga uhusiano wa kina. Ndiyo maana ushirika katika makanisa mengi ni duni, hatutumii muda wa kutosha pamoja, na muda tunaotumia mara nyingi ni kumsikiliza mtu mmoja akiongea.

Jamii haijengwi kwa wakati unaokubalika (“tutakusanyika nikijisikia”), lakini katika kweli kwamba naihitaji kwa ajili ya afya yangu kiroho. Kama unataka kujenga ushirika wa kweli, itamaanisha kukutana hata pale unapokuwa hujisikii kufanya hivyo, kwa sababu unaamini ni muhimu. Wakristo wa kwanza walikutana kila siku! “Waliabudu pamoja hekaluni kila siku, wakakusanyika katika vikundi vidogo nyumbani kwa ajili ya ushirika, na wakashirikiana vyakula vyao kwa furaha kubwa na shukrani.” Matendo 2:46 (LB) Ushirika huhitaji kuwekeza muda.

Kama wewe ni mshirika wa kikundi kidogo au darasa, nakushauri kufanya agano la kikundi ambalo lina sifa tisa za ushirika wa kibiblia: Tunashirikisha hisia zetu halisi (uhalisi), kutiana moyo (kutegemeana), kutiana nguvu (kuhurumiana), kutiana moyo (kutegemeana), kutiana nguvu (kuhurumiana), Kusameheana (rehema), kusema ukweli katika upendo (uaminifu), kukiri udhaifu wetu (unyenyekevu), kuheshimu tofauti zetu (adabu), hapana kutetana (kutunza siri), na kuweka kipaumbele kwa kikundi (kukutana mara kwa mara).

Tunapoangalia orodha ya sifa hizo, ni wazi kwa nini ushirika halisi ni vigumu kuupata. Maana yake ni kuacha ubinafsi wetu na kujitegemea ili tuweze kufikia hali ya kutegemeana. Kushirikiana kuna faida kubwa kuliko gharama, na kunatuandaa kwa ajili ya mbinguni.

SIKU YA KUMI NA TISA

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la kutafakari: Ushirika wa kijamii huhitaji kujitoa.

Kifungu cha kukumbuka: “Tunaelewa upendo ni kitu gani tunapofahamu kwamba Kristo alitoa maisha yake kwa ajili yetu. Hii maana yake ni kwamba inatupasa kutoa maisha yetu kwa ajili ya waamini wengine.” 1 Yohana 3:16 (GWT)

Swali la kujiuliza: Je, nawezaje kusaidia leto kujenga sifa za ushirika wa jamii ulio halisi katika kundi langu dogo na kanisa?

Siku ya Ishirini: Kurejeza Uhusiano Uliovunjika

Mungu amerejesha uhusiano wetu naye kwa njia ya Kristo,

na ametupatia sisi huduma hii ya kurejesha mahusiano.

2 Wakorintho 5:18 (GWT)

Uhusiano unastahili kurejeshwa.

Kwa kuwa maisha ni juu ya kujifunza kupenda, Mungu anatutaka tuthamini uhusiano na kufanya bidii kuutunza badala ya kuutupilia mbali mara kunapokuwepo kupishana, maumivu, au migogoro. Kwa kweli, Biblia inatuambia kwamba Mungu ametupatia huduma ya kurejeza uhusiano. 2 Wakorintho 5:18 (GWT) Kwa sababu sehemu kubwa ya Agano Jipya inatufundisha jinsi ya kuishi pamoja. Paulo aliandika. “Kama mumepata chochote kwa kumfuata Kristo, kama upendo wake umefanya badiliko lolote, kama kuwa katika ushirika wa Roho Mtakatifu kuna maana yoyote kwenu, … kubalianeni, pendaneni, iweni na urafiki wa kutoka moyoni.” Wafilipi 2:1-2 (Msg) Paulo alifundisha kwamba uwezo wetu wa kuishi vyemaa na wengine ni alama ya ukomavu wetu kiroho. Warumi 15:5 (Msg)

Kwa kuwa Kristo anapenda kanisa lake lijulikane kwa upendo wake wa ndugu, (Yohana 13:35) basi kuvunjika kwa uhusiano ni ushuhuda wa aibu kwa wasioamini. Ndiyo maana Paulo alikuwa amedhuzunishwa kwa washirika wa kanisa la Korintho kugawanyika katika vikundi vilivyopigana vita na hata kupelekana mahakamani. Aliwaandikia, “Aibu kwenu! Kwa hakika hakuna walau mtu mmoja mwenye hekima katika ushirika wenu anayeweza kumaliza mgogoro katik ya Wakristo wenzake.” 1 Wakorintho 6:5 (TEV) Alishangazwa kwamba hapakuwepo yeyote kanisani aliyekuwa amekomaa kiroho kuweza kutatua mgogoro kwa amani. Katika barua hiyo hiyo, alisema, “Nitalifanya kuwa ni jambo la dharura kama niwezavyo: Ni lazima mpatane.” 1 Wakorintho 1:10 (Msg)

Kama unataka baraka za Mungu kwa maisha yako na unataka kujulikana kama mtoto wa Mungu, ni lazima ujifunze kuwa mpatanishi. Yesu alisema, “Mungu huwabariki wale wanaotafuta amani, kwa kuwa wataitwa watoto wa Mungu.” Mathayo 5:9 (NLT) Angalia Kristo hakusema, “wamebarikiwa wapenda amani,” kwa sababu kila mtu hupenda amani. Wala hakusema “wamebarikiwa walio na amani,” wala wasiosumbuliwa na chochote. Yesu alisema, “wamebarikiwa wale waitafutao amani” –wale wanaofanya bidii kutatua migogoro. Watafuta amani ni wachache kwa sababu upatanishi ni kazi ngumu.

Kwa sababu uliumbwa ili uwe sehemu ya jamii ya Mungu na lengo la pili la maisha yako hapa duniani ni kujifunza jinsi ya kupenda na kuhusiana na wengine, upatanishi ni moja ya ujuzi unaotakiwa kujifunza. Kwa bahati mbaya, wengi wetu hatukufundishwa namna ya kutatua migogoro.

Kutafuta amani siyo kuepuka mgogoro, kukimbia mgogoro, kujifanya hakuna tatizo au kuogopa kuliongelea tatizo huo ni woga kwa hakika. Yesu, mfalme wa amani, hakuogopa kamwe migogoro. Mara nyingine aliuchochea ukatokea kwa faida ya wote. Wakati mwingine tunatakiwa kuepuka migogoro, wakati mwingine kuisababisha, na wakati mwingine tunahitaji kuitatua. Ndiyo maana tunapaswa kuomba uongozi wa Roho Mtakatifu daima.

Kuleta amani siyo kuktuliza hasira. Mara nyingi unakubaliana, unakuwa kama jamvi, na unawaruhusu wengine wakukanyage sivyo alivyokusudia Yesu. Alikataa kuacha mambo kama yalivyo, na akachukua msimamo mbele za upinzani wa waovu.

JINSI YA KUREJESHA UHUSIANO

SIKU YA ISHIRINI:

KUREJEZA UHUSIANO ULIOVUNJI KA

Kama waamini, Mungu “ametuita kurejeza uhusiano baina yetu.” 2 Wakorintho 5:18 (Msg)

Kusema na Mungu kabla ya kusema na mtu. Jadili tatizo na Mungu. Kama utaomba kwa ajili ya mgogoro huo kabla ya kusengenya na rafiki, mara nyingi utagundua kwamba Mungu anabadili moyo wako au anambadili yule mwingine bila msaada wako. Mahusiano yako yote yangekuwa shwari kama ungeyaombea zaidi.

Kama Daudi alivyofanya na zaburi zake, tumia sala kupata uhusiano wa juu na Mungu. Mwambie Mungu mashaka yako. Mlilie. Hashangazwi wala kukatishwa tamaa na hasira yako, maumivu, hofu, au hisia nyingine zozote. Hivyo mwambie ukweli wa unavyojihisi.

Migogoro mingi chanzo chake ni uhitaji. Baadhi ya mahitaji haya yanaweza kutimizwa tu na Mungu. Unapomtazamia mtu yeyote-rafiki, mume au mke, mkuu wa kazi, au mwanajamaa-kutimiza hitaji ambalo linaweza tu kutimizwa na Mungu, unajiweka katika hili ya kuvunjika moyo na uchungu. Hakuna mtu yeyote anayeweza kutimiza mahitaji yako yote isipokuwaa Mungu.

Mtume Yakobo alisema kuwa migogoro yetu mingi inatokana na maisha ya kutokusali, “Nini kinasababisha vita na ugomvi kati yenu? … mnataka kitu lakini hampati … hampati kwa sababu hamwombi Mungu.” Yakobo 4:1-2 (NIV) Badala ya kumtazama Mungu tunawatazama watu ili tupate furaha na tunakasirika wanaposhindwa kutusaidia. Mungu anasemaa, “mbona huji kwangu kwanza?”

Kila ara chukua hatua za kwanza. Si kitu kama wewe ni mkosaji au umekosewa: Mungu anakutazamia kuchukua hatua za kwanza. Usisubiri kwa ajili ya upande ule mwingine waendee kwanza. Kurejeza uhusiano uliovunjika ni muhimu, Yesu aliagiza kwamba jambo hili lifanywe hata kabla ya kukusanyika katika kikundi cha kuabudu. Alisema, “Kama ukiingia sehemu ya kuabudu na, unataka kutoa sadaka, ukakumbuka ghafla kwamba rafiki yako ana neno dhidi yako, acha sadaka yako, ondoka mara moja, nenda kwa rafiki huyo na kuweka mambo sawa. Hapo ndipo unaweza kuja na kumtolea Mungu.”1 Petro 3:7; Methali 28:9

Ushirika unaposongwa au kuvunjika, panga mkutano wa upatanisho mara moja. Usiahirishe, usitoe sababu wala kuahidi “nitalishughulikia siku fulani.” Andaa mkutano wa uso kwa uso haraka iwezekanavyo. Kuchelewa huongeza chuki na kufanya mambo kuwa mabaya zaidi. Katika migogoro, muda hauponyi kitu, husababisha maumivu kuongezeka.

Kuchukua hatua haraka pia hukupunguzia maumivu ya kiroho. Biblia husema dhambi, pamoja na mgogoro ambao haujatatuliwa,” pia hutufanya tuwe na huzuni. Marafiki wa Ayubu walimkumbusha, “Kuhofu kiasi cha kufa ukijaa uchungu ni upumbavu na kitu kisicho ch busara” na “unajiumiza nafsi yako kwa hasira.” Ayubu 5:2 (TEV); 18:4 (TEV)

Kufanikiwa kwa mkutano wa kutafuta amani hutegemea uchaguzi wa wakati na mahali mwafaka katika kukutana. Msikutane mmoja wenu akiwa amechoka au ana haraka au atapata usumbufu fulani. Muda mzuri ni ule ambao nyote mko tayari.

Wahurumie katika hisia zao. Tumia masikio yako zaidi kuliko mdomo wako. Kabla ya kujaribu kutatua mgogoro wowote ni lazima kwanza usikilize hisia za watu. Paulo alishauri, “Yatafuteni mambo yanayowapendeza wenzenu, siyo tu mambo yenu.” Wafilipi 2:4 (TEV) Neno “yatafuteni” ni neno la kiyunani skopos, kutokana nalo tunapata neno teleskopu na mikroskopu. Ina maana ya kuweka uangalifu wa karibu sana! Ziangalie sana hisia zao, sio ule ukweli. Anza na huruma sio suluhisho.

Usijaribu kuwasema watu kulingana na wanavyohisi kwanza. Wewe sikiliza tu na wamimine hisia zao bila kuhisi kujilinda. Tikisa kichwa kuonyesha kuwa unawaelewa hata kama hukubaliani nao. Hisia haziko sahihi au za busara – mara nyingi Hakika, uchungu hutufanya tufikiri na kutenda kipumbavu. Daudi alikiri, “Fikra zangu zilipojaa uchungu na hisia zangu zikaumizwa, nilikuwa mpumbavu kama mnyama.” Zaburi 73:21-22 (TEV) Sisi sote hutenda kinyama tunapokuwa tumeumizwa.

Kinyume na hapa Biblia husema, “Hekima ya mtu humpa subira, ni utukufu kwake kutohesabu makosa.” Mithali 19:11 (NIV) Subira hutokana na hekima, na hekima huja kwa kusikiliza maoni ya wengine. Kusikia husema, “Najali maoni yako, najali uhusiano wetu, na wewe ni wa muhimu kwangu.” Mesemo huu ni wa Kweli: Watu hawajali mambo tunayojajua mpaka wajue kwamba tunajali.

Ili kurejeza ushirika “Ni lazima tubebe ‘mzigo’ wa kujali mashaka na hofu za wengine … Na tumfurahishe mwenzetu, na siyo nafsi zetu, na kufanya yanayomfaa.” Wafumi 15:2 (LB)     Ni kujitoa sadaka kumeza kwa uvumilivu hasira za watu wengine, hasa kama jambo hilo si la kweli. Kumbuka, hivi ndivyo Yesu alivyokutendea. Alivumilia hasira ya uongo na uonevu ili akuokoe: “Kristo hakufuatisha hisia zake … kama maandiko yasemavyo: matusi yao wakutukanayo yaliniangukia.” Warumi 15:3 (NJB)

Kiri sehemu yako ya mgogoro. Kama unamaanisha kibisa kuhusu kurejeza uhusiano, unatakiwa uanze na kukiri makosa yako au dhambi. Yesu alisema ni njia ya kuona mambo dhahiri: “Kwanza toa boriti ndani ya jicho lako; kisha labda utaona vyema kuondoa kibanzi kwenye jicho la rafiki yako.” Mathayo 7:5 (NLT)

Kwa kuwa sote tuna maeneo ya giza maishani, utahitaji kuuliza mtu wa tatu asaidie kutathmini matendo yako kabla ya kukutana na mtu uliye na mgogoro naye. Pia mwombe Mungu akuonyeshe ni kiasi gani cha tatizo ni kosa lako. Uliza, “Je, mimi ni tatizo? Je, mimi si mkweli, sijali, au najali sana?” Biblia inasema, “Kama tutasema kwamba hatuna dhambi, tunajidanganya tu wenyewe.” 1 Yohana 1:8 (Msg)

Toba ni chombo chenye nguvu katika kuleta upatanisho. Mara nyingi namna tunavyoshughulikia mgogoro huleta maumivu makubwa kuliko hata lile tatizo la kwanza. Unapoanza kwa kukiri kinyenyekevu makosa yako, hupunguza makali ya hasira ya yule mwingine na huondoa nguvu ya mashambulizi kwa kuwa walitegemea utajitetea. Usitoe udhuru wala kuhamishia lawama kwa wengine; kwa uaminifu kubali makosa yako katika mgogoro huo. Kubali kuwajibika kwa makosa yako na uombe msamaha.

Shambulia tatizo na siyo mtu. Huwezi kutatua tatio kama umekusudia tu kuondoa lawama. Ni lazima uchague kati ya hayo mawili. Biblia inasema, “Jawabu la upole hutuliza hasira, lakini ulimi mkali huwasha hasira.” Mithali 15:1 (Msg) Hutaweza kupitisha jambo lako kwa kuwa na hasira, hivyo chagua maneno yako kwa busara. Jibu laini mara nyingi ni bora kuliko jeuri.

Katika kusuluhisha migogoro, unavyosema ni muhimu kama ulichosema. Ukikisema kwa kukasirisha, litapokelewa kwa kujilinda. Mungu anatuambia, “Mtu mwenye hekima, mkomavu anajulikana kwa ufahamu wake. Kadiri maneno yake yanavyopendeza, ndivyo anavyokuwa na ushawishi mkubwa.” Mithali 16:21 (TEV) Kulaumu hakusaidii. Huwezi kuwa na ushawishi kama wewe ni jeuri.

Wakati wa Vita Baridi, pande zote mbili walikubaliana kwamba baadhi ya silaha zilikuwa za maangamizi sana hivyo zisitumiwe kamwe. Leo silaha za kikemia na kibaiolojia zilizopigwa marufuku, na maghala ya silaha za nyuklia yanapunguzwa na kuangamizwa. Kwa ajili ya ushrikiano, lazima uangamize ghala lako la silaha za uhusiano, ambazo ni lawama, dharau, kulinganisha, kuwapa watu majina, kututana, ubwana, na kutoa maneno makali. Paulo anajumlisha yote akisema, “Msitumie maneno yanayodhuru, lakini maneno yenye kusaidia, yenye kujenga na kutoa kila kinachohitajika, ili kwamba kile msemacho kiwajenge wanaosikia.” Efeso 4:29 (TEV)

Onyesha ushirikiano ipasavyo. Paulo alisema, “Fanyeni kila mwezalo kwa upande wenu ili kuishi kwa amani na watu wote.” Warumi 12:18 (TEV) Amani siku zote ina gharama. Wakati mwingine hugharimu majivuno yetu. Kwa ajili ya ushirika, jitahidi kujirekebisha, ukubalike na wengine, na uonyeshe kujali mahitaji yao. (Warumi 12:10; Wafilipi 2:3) Ufafanuzi wa heri ya saba ya Yesu husema, “Mumebarikiwa kama mkiwaonyesha watu namna ya kushirikiana badala ya kushindana au kugombana. Ndipo mnapogundua ninyi ni akina nani, na nafasi yenu katika ufalme wa Mungu.” Mathayo 5:9 (Msg)

Upatanisho hulenga uhusiano

Wakati usuluhisihi

hulenga tatizo

Kazia upatanisho siyo usuluhishi. Siyo kitu halisi kutegemea kuwa kila mtu atakubaliana na kila kitu. Upatanisho hulenga uhusiano, wakati usuluhishi hulenga tatizo. Tunapolenga utapanisho, tatizo hupoteza nguvu na mara nyingi linakuwa halina maana.

Tunaweza kurejeza uhusiano hata kama hatuwezi kuondoa tofauti zetu. Wakristo mara nyingi wana mambo ambayo wanatofautiana kwa halali na wana maoni tofauti ya kweli, lakini tunaweza kutokukubaliana kimaoni bila kukataana sisi wenyewe. Almasi moja huonekana tofauti toka pande tofauti tofauti. Mungu anatarajia umoja, siyo kufanana, na tunaweza kutembea mkono kwa mkono bila kuonana jicho kwa jicho kwa kila kitu.

Hii haina maana kwamba basi uache kutafuta suluhu. Mnaweza kuendelea kujadili na kuwa na kongamano-lakini mnafanya hivyo katika roho ya amani. Upatanisho maana yake unasemehe yaliyopita na si lazima lile jambo.

Je, ni nani unahitaji kumwona baada ya kusoma sura hii? Je, unahitaji kurejeza uhusiano na nani? Usichelewe dakika nyingine. Tulia sasa na uzungumze na Mungu kuhusu mtu huyo. Sasa chukua simu na anza kuchukua hatua. Hatua hizi saba ni rahisi, lakini si nyepesi. Huhitajiki juhudi kubwa kerejeza uhusiano. Ndiyo maana Petro alisihi, “Jitahidini kuishi kwa amani baina yenu.” 1 Petro 3:11 (NLT) Ndiyo maana Mungu anawaita wapatanishi kuwa ni watoto wake. Mathayo 5:9

SIKU YA ISHIRINI

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Uhusiano ni wa muhimu kuurejeza.

Kifungu cha Kukumbuka: “Fanyeni kila mwezalo kwa upande wenu ili kuishi kwa amani na watu wote.” Warumi 12:18 (TEV)

Swali la Kujiuliza: Je, ni nani ninahitaji kurejeza uhusiano naye leo?

Siku ya Ishirini na Moja: Kuhifadhi Kanisa Lako

Mmeunganishwa pamoja kwa amani kwa njia ya Roho Mtakatifu, hivyo

fanyeni kila bidii ili kuendelea pamoja katika hali hiyo.

Waefeso 4:3 (NCV)

Zaidi ya yote, upendo uongoze maisha yenu, kwa nijia hiyo kanisa lote

litakaa pamoja katika amani kamilifu.

Wakolosai 3:14 (LB)

Ni kazi yako kuutunza umoja wa kanisa lako.

Umoja wa kanisa ni muhimu jambo kiasi kwamba Agano Jipya limelipa mkazo zaidi kuliko hata mbingu au kuzimu. Mungu anapenda sana tuwe na umoja na amani baina yetu.

Umoja ndiyo uhai wa ushirika. Ukiuharibu, umeondoa moyo kwenye mwili wa Kristo. Ni Kiini, na asili ya jinsi Mungu anavyotukusudia tuwe na maisha ya pamoja katika kanisa lake. Mfano mzuri kwetu wa umoja ni Utatu. Baba, mwana, na Roho Mtakatifu wameunganika kikamilifu katika umoja. Mungu mwenyewe ni kielelezo cha juu katika upendo wa kujitoa sadaka, kuwajali wengine kwa unyenyekevu, na umoja mkamilifu.

Kama vile kila mzazi, Baba yetu wa mbinguni kufurahi akituona watoto wake pamoja katika amani. Katika saa yake ya mwisho, kabla ya kukamatwa, Yesu aliomba kwa moyo kwa ajili ya umoja wetu. (Yohana 17:20-23) Umoja wetu ndio ulichukua nafasi kubwa katika mawazo yake muda ule alipokuwa katika kuugua moyoni.

Hakuna kitu cha thamani

duniani kama kanisa lake.

Hakuna kitu cha thamani duniani kama kanisa lake. Alilipa gharama kubwa kwa ajili yake, na anapenda lilindwe sana kutokana na uharibifu unaosababishwa na mgawanyiko, migongano, na machafuko. Kama wewe nsi sehemu ya jamii ya Mungu, ni wajibu wako kutunza umoja pale unaposhiriki. Umeagizwa na Kristo kufanya kila uwezalo kutunza umoja, kulinda ushirika na kutimiza amani katika jamii ya kanisa lako na katika waamini wote. Biblia inasema, “Fanyeni kila bidii kuutunza umoja wa Roho kwa kifungo cha amani.” Waefeso 4:3 (NIV) Je, tutafanyaje jambo hili? Biblia inatupa ushauri.

Kukazia mambo yanayotuhusu wote na siyo tofauti zetu. Paulo anatuambia, “Tuyaangalie mambo yaletayo amani, na yale yanayoleta tabia njema kwa kila mtu.” Warumi 14:19 (NIV) Kama waamini tunashiriki Bwana mmoja, mwili mmoja, ubatizo mmoja, na upendo mmoja. (Warumi 10:12; 12:4-5; 1 Wakorintho 1:10; 8;6; 12:13; Waefeso 4:4; 5:5; Wafilipi 2:2.) Tunashiriki wokovu ule ule, maisha yale yale, na hatima moja-mambo haya ni ya muhimu sana kuliko tofauti zozote tunazoweza kuzitaja. Haya ndiyo mambo, siyo tofauti zetu binafsi, tunayoweze kuyajadili zaidi.

Ni lazima tukumbuke kwamba ni Mungu aliyechagua kutupatia hali tofauti, mazingira tofauti, rangi, na mambo tuyapendayo, hivyo yatupasa kuthamini na kuzifurahia tofauti hizo, sio tu kuzivumilia. Mungu anapenda umoja siyo kufanana. Lakini kwa ajili ya umoja tusiruhusu tofauti zitugawe. Ni sharti tuyatazame zaidi mambo ya muhimu. Kujifunza kupendana kama Kristo alivyotupenda na kutimiza malengo ya Mungu matano kwa maisha ya kila mmoja wetu na kanisa lake.

Migogoro ni dalili ya kwamba tumeanza kuyaagalia mambo yasiyo muhimu, Biblia huyaita mambo hayo “mambo yanayotatiza.” (Warumi 14:1; 2 Timotheo 2:23) Tunapokazania hulka za watu, matakwa, tafsiri, mitindo, na njia, migawanyiko hutokea mara nyingi. Lakini tunapoelekeza nguvu zetu katika kupendana na kutimiza malengo ya Mungu, amani hutokea. Paulo alisihi kwa ajili ya jambo hili, “Kuweni na umoja wa kweli ili kusiwe na mgawanyiko kanisani. Nawasihi muwe na nia moja, mkishikamana katika wazo na lengo.” 1 Wakorintho 1:10 (NLT)

Kuwa na matazamio halisi. Ukishagundua Mungu anavyotaka ushirika halisi uwe, ni rahisi kuvunjwa moyo na bonde lililopo kati ya matarajio na hali halisi kanisani mwako. Lakini lazima tulipende kanisa kwa moyo bila kujali mapungufu yake. Kutamani hali ya matarajio huku ukilaumu hali halisi iliyopo ni ushahidi wa uchanga. Kwa upande mwingine, kuridhika na hali halisi badala ya kutia bidii kufikia matarajio ni kujikinai. Kukua ni kuishi katika mvutano.

Lazima tulipende kanisa

bila kujali mapungufu yake.

Waamini wengine watakuvunja moyo na kukutupa, huo siyo udhuru wa kukoma kufanya ushirika nao. Wao ni jamii yako, hata kama hawatendi ipasavyo, na huwezi hujitenga nao. Badala yake anatuambia. “Vumilieni, mkichukuliana katika makosa yenu kwa sababu upendo wenu.” Waefeso 4:2 (NLT)

Watu huvunjwa moyo na kanisa kwa sababu nyingi zinazoeleweka. Orodha yaweza kuwa ndefu: migogoro, maumivu, unafiki, kutokujali, kuonekana kutofaa, sharia na dhambi nyingine. Badala ya kushangaa, lazima tukumbuke kwamba kanisa lina watu wenye dhambi, ikiwa ni pamoja na sisi. Kwa sababu tu wenye dhambi tumeumizana, kwa makusudi au bila kukusudia. Lakini badala ya kuliacha kanisa, tunapaswa kukaa na kutafuta utatuzi. Upatanisho, siyo kukimbia, ni njia ya kuelekea ukomavu wa tabia na ushirika wa kina.

Kuliacha kanisa lako kwa dalili ya kwanza ya kuvunjwa moyo ni dalili ya uchanga. Mungu ana mambo anayotaka kukufundisha, na wengine pia. Zaidi, hakuna kanisa kamilifu la kikimbilia. Kila kanisa lina mapungufu na matatizo yake. Si muda mrefu utavunjwa moyo tena.

Groucho Marx alijulikana kwa kusema asingetaka kuwa kwenye chama chochote ambacho kingemwingiza ndani. Kama kanisa litakuwa kamili kukutosheleza, basi ukamilifu huo huo utakuondoa kwenye ushirika, kwa sababu wewe si mkamilifu!

Dietrich Bonhoeffer, Mchungaji wa kijerumani aliyeuawa kwa kupinga utawala wa Nazi, aliandika kitabu cha ushirika kinachopendwa kitwacho, Maisha ya Pamoja. Ndani yake anapendekeza kwamba kuvunjwa moyo na kanisa letu la mahali ni jambo zuri kwa sababu huharibu matarajio yetu potofu juu ya ukamilikfu. Mara tunapoacha ndoto hiyo ya kuwa kanisa lazima liwe kamilifu ili tulipende, ndipo tunaacha kuigiza na tunaanza kukiri kuwa sote si wakamilifu na tunahitaji neema. Huu ndiyo mwanzo wa ushirika halisi wa kijamii.

Kila kanisa linaweza kuweka ilani ikisema Hakuna mtu yeyote anahitaji kutuma maomlbi. Hapa ni pahali tu pa watu waliokiri kuwa wenye dhambi, wahitaji neema, na wanaotaka kukua.

Bonhoeffer alisema, “Yeye apendaye ndoto yake ya jamii kuliko jamii ya Kikristo yenyewe huwa mharibifu wa jamii ya Kikristo … Kama hatutoi shukrani kila siku kwa ajili ya ushrika wa Kikristo tulimowekwa, hata kama hakuna mambo makubwa, hakuna utajiri, lakini udhaifu mwingi, Imani mdogo, na magumu, na kama badala yake tunadumu kulalamika kwamba kila kitu ni duni na hakifai, basi tunamzuia Mungu kukukza ushikrika wetu.” ( Marumi 14:13; Yakabo 4:11; Waefeso 4:29; Mathayo 5:9; Yakobo 5:9)

Chagua kutia moyo badala ya kulaumu. Ni rahisi kusimama kando na kuwashambulia wanaotumika kuliko kuhusika na kutoa mchango wako. Mungu anatuonya tena na tena tusilaumu, tusijilinganishe, wala tusihukumiane. Warumi 14:4 (CEV) Kama utalaumu anachofanya Mkristo mwingine kwa Imani na uthabiti wa moyo, unaingilia kazi ya Mungu. “Una haki gani kumhukumu mtumishi wa mtu mwingine? Ni Bwana wake tu anayeweza kuamua kama wanafanya vyema.” Warumi 14:10 (Ph)

Paulo anaongeza kwamba hatupaswi kuhukumu au kudharau waamini wengine ambao wanaamini tofauti nasi. “Kwa nini basi, unalaumu matendo ya ndugu yako, kwa nini unamdhalilisha? Sote tutahukumiwa siku moja, si kwa kutumia vigezo vyetu, lakini kwa vigezo vya Kristo.” Ufunuo 12:10

Ninapomhukumu mwamini mwingine, mambo manne hutokea mara moja: napoteza ushirika na Mungu, nadhihirisha majivuno na hofu zangu, najiweka kuhukumiwa na Mungu, na ninaathiri ushirika wa kanisa. Roho ya kuhukumu ni jambo la hatari.

SIKU YA ISHIRINI NA MOJA:

KUHIFADHI KANISA LAKO

Biblia humwita Shetani, “Mshtaki wa ndugu zetu.” Warumi 14:19 (Msg) Ni kazi ya Ibilisi kulaumu kunung’unika, na kuhukumu washirika wa jamii ya Mungu. Saa yoyote tukifanya hivyo, basi tunafanya kazi ya Shetani. Kumbuka washirika wengine haijalishi mumepishana kiasi gani, wao si adui halisi. Tunapochukua muda kulaumu au kujilinganisha na waamini wengine ni muda ambao ungetumika kujenga umoja wa ushirika wetu. Biblia inasema, “Tukubaliane kutumia nguvu zetu zote kuishi kwa amani kati yetu. Tukiwasaidia wengine na maneno ya kutia moyo; tusiwaangushe kwa kuwatafutia makosa.” (Mithali 17:4; 16:28; 26:20; 25:9; 20:19.)

Kataa kusikiliza masengenyo. Kusengenya ni kusema habari ambao haikuhusu wala huhusiki kusuluhisha. Unajua kueneza usenganyaji ni kosa, lakini usiusikilize, iwapo unataka kulinda kanisa lako. Kusikiliza masengenyo ni kama kupokea mali ya wizi, na inakufanya uhukumiwe kwa kosa lilelile.

Mtu anapoanza kusengenya kwako chukua ujasiri kumweleza, “Tafadhali acha, sihitaji kujua hili. Je umemweleza mhusika moja kwa moja jambo hili?” Watu wanaosengenya kwako watakusengenya pia. Hawaaminiki. Ukisikiliza masengenyo, Mungu anasema, wewe ni mleta matatizo. Mithali 17:4 (CEV) “Wasumbufu husikiliza wasumbufu wenzao.” Yuda 1:19 (Msg) “Hawa ndio wanaogawa makanisa, wakijifikiri wenyewe tu.” Wagalatia 5:15 (Amp)

Ni huzuni kwamba katika kundi la Mungu, majeraha makubwa mara nyingi hutokana na kondoo wengine, sio mbwa mwitu. Paulo alionya juu ya Wakristo “wala nyama”. “Wanaokulana” na kuharibu ushirika. Mithali 20:19 (NRSV) Biblia inasema watu wa aina hii waepukwe. “Masengenyo hufunua siri, hivyo usishirikiane na msengenyaji.” Mithali 26:20 (LB) Njia ya haraka ya kukomesha mgogoro kanisani au katika kikundi kidogo ni kuwaonya wazi kwa upendo wale wasengenyaji waache kabisa. Sulemani alisema, “Moto huzimika kwa kukosa mafuta, na ugomvi hutoweka usengenyaji unapokoma.” Mathayo 18:15-17a (Msg)

Tumia njia ya Mungu ya kutatua migogoro. Kwa nyongeza ya kanuni zilizotajwa katika sura iliyopita, Yesu alilipa kanisa njia rahisi yenye hatua tatu: “Kama mwamini mwenzako atakosea, nenda kamwambie-malizeni kati yenu wawili. Akisikia, umempata rafiki yako. Asipokusikiliza, wachukue ndugu wawili au watatu pamoja nawe ili kutunza ushahidi halali, na ujaribu tena. Asiposikiliza tena liambie kanisa.” (Mathayo 18:17; 1 Wakorintho 5:5)

Wakati wa mgogoro, ni rahisi kulalamika kwa mtu wa tatu badala ya kusema kijasiri ukweli katika upendo kwa mtu aliyekuudhi. Hii hufanya tatizo kuwa baya zaidi. Badala yake, mwendee moja kwa moja mtu anayehusika.

Kumwendea mtu binafsi ndiyo hatua ya kwanza, na lazima ufanye hivyo haraka iwezekanavyo. Kama hamwezi kuyamaliza ninyi wawili, hatua ya pili ni kuchukua ndugu mmoja au wawili wasaidie kuthibitisha tatizo na kupatanisha uhusiano. Je, utafanya nini kama mtu huyo bado jeuri? Yesu alisema chukua tatizo hilo kwa kanisa. Kama mtu huyo bado hataki kusikiliza baada ya hapo, unamwona mtu huyo kama yule asiyeamini. Waebrania 13:17 (Msg)

Waunge mkono mchungaji na wazee wa kanisa. Hakuna viongozi wakamilifu, lakini Mungu huwapa viongozi majukumu na mamlaka ya kutunza umoja wa kanisa.

Kunapokuwepo migogoro baina ya watu hiyo si kazi ya kufurahia. Wachungaji huwa na kazi ngumu ya kuwa wapatanishi kati ya washirika walioumizwa au walio kwenye mgogoro. Pia wanapewa jukumu gumu la kujaribu kufanya kila mtu afurahi, kazi ambayo hata Yesu hakuifanya!

Tunalinda ushirika wa kuwaheshimu wale wanao tutumikia kwa kuongoza.

Biblia iko wazi juu ya namna ya kuhusiana na watumishi wetu: “Watiini wenye kuwachunga na kuwaongoza. Sikilizeni ushauri wao. Wao wako macho juu ya hali za maisha yenu na wanafanya kazi chini ya usimamizi mkali wa Mungu. Basi shangilieni katika furaha ya uongozi wao, na sio kuwakatisha tamaa. Kwa nini mfanye kazi yao kuwa ngumu?” Waebrania 13:17 (NIV)

Wachungaji siku moja watasimama mbele za Mungu na kutoa hesabu ya jinsi walivyowaangalia vizuri. “Wao huwaangalia kama watu watakaotoa hesabu.” (2 Timotheo 2:14,23-26; Waf 10-11.) Lakini wewe pia utatoa hesabu ya jinsi ulivyowafuata viongozi wako.

Biblia inawapa wachungaji maagizo maalum ya namna ya kufanya na watu waletao matengano katika ushirika. Wanapaswa kuepuka mabishano, kuwafundisha kwa upole wale wapinzani huku wakiwaombea wabadilike, kuwaonya wabishi, kusihi kuwa na amani na umoja, kuwakemea wanaodharau uongozi, na kuwaondoa waletao matengano kanisani kama wakidharau maonyo mawili. 1 Wathesalonike 5:12-13a (Msg)

Tunalinda ushirika kwa kuwaheshimu wale wanaotutumikia kwa kuongoza. Wachungaji na wazee wanahitaji maombi yetu, kutiwa moyo, kuwashukuru na kuwapenda. Tumeamriwa, “Waheshimuni wale viongozi wanaofanya kwa bidii kwa ajili yenu, ambao wamepewa jukumu la kuwasihi na kuwaongoza katika utii wenu. Washukuruni na kuwapenda!” 1 Wakorintho 10:24 (NLT)

Nakupa changamoto la kupokea wajibu wako wa kulinda na kukuza umoja wa kanisa lako. Weka juhudi zote kwa jambo hili, na Mungu atafurahi. Haitakuwa rahisi daima. Wakati mwingine utatakiwa kufanya lililo bora kwa mwili wa Kristo, si kwako, kuonyesha kipaumbele kwa wengine. Hiyo ni sababu moja ya Mungu kutuweka katika jamii ya kanisa – kujifunza kutokuwa na ubinafsi. Katika jamii tunajifunza kusema “sisi” badala ya “mimi” na “yetu” badala ya “yangu.” Mungu anasema, “Usifikirie manufaa yako tu. Fikiri juu ya Wakristo wengine na kile kinachowafaa.”

Mungu hubariki makanisa yaliyo na umoja. Katika kanisa la Saddleback, kila mshirika husaini mkataba ambao pia unaahadi ya kuhifadhi umoja wa ushirika wtu. Matokeo yake, kanisa halijawahi kuwa na mgogoro wa kugawa ushirika wetu. Ilivyo muhimu, kwa kuwa ni ushirika wenye umoja, na upendo, watu wengi wanapenda kuwa sehemu yake! Katika miaka saba iliyopita kanisa limebatiza zaidi ya waamini wapya 9,100. Mungu anapokuwa na kundi la waamini wachanga anaotaka wazaliwe, anatafuta kanisa lenye joto zuri.

Je, wewe unafanya nini ili kulifanya kanisa lako liwe jamii yenye uchangamfu wa upendo? Kuna watu wengi katika jamii yenu wanaotafuta upendo na mahali pa kuwa washirika. Ukweli ni kwamba, kila mmoja anapenda na anahitaji kupendwa, na watu wanapopata kanisa ambapo washirika wake wanapendana na kujaliana kikweli, utalazimika kufunga mlango ili wasije maana nafasi haitatosha.

 

SIKU YA ISHIRINI NA MOJA

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Ni wajibu wangu kuhifadhi umoja wa kanisa langu.

Kifungu cha kukumbuka:Tuyaangalie mambo yanayoleta amani na kukua kwa ushirika wetu kwa pamoja.” Warumi 14:19 (Ph)

Swali la Kujiuliza: Je, sasa hivi mimi ninafanya nini ili kulinda umoja katika jamii ya kanisa langu?


 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

沒有留言:

張貼留言