2024年7月4日 星期四

Maisha Yanayoongozwa Na Malengo (Siku Ya Ishirini na Mbili kwa Ishirini na Nane )


LENGO LA 3


        ULIUMBWA ILI UFANANE NA KRISTO

Mizizi yenu ikue na kuzama udani ya Kristo na kupata lishe kutoka kwake. Hakikisheni

kwamba mnaendelea kukua katika Bwana, na mpate kuwa na nguvu katika ile kweli.

Wakolosai 2:7 (LB)

Siku ya Ishirini na Mbili: Uliumbwa Ili Ufanane na Kristo

Mungu alijua alichokuwa anafanya tangu mwanzo. Aliamua tangu mwanzoni

kuyafanya maisha ya wale wampendao yafanane na maisha ya mwana wake …

Tunaona sura ya asili na iliyokusudiwa ya maisha yetu katika yeye.

Warumi 8:29 (Msg)

Tunamwangalia mwana huyu na kuona lengo la asili la Mungu

katika kila kilichoumbwa.

Wakolosai 1:15 (Msg)

Tuliumbwa ili tufanane na Kristo.

Tangu mwanzo, mpango wa Mungu umekuwa ni kukufanya wewe uwe kama Mwana wake, Yesu Kristo. Hii ndiyo hatima yako na lengo la tatu la maisha yako. Mungu alitangaza kusudi hili wakati wa uumbaji, “Kisha Mungu akasema, ‘Na tufanye wanadamu katika sura na mfano wetu.’” Mwanzo 1:26 (NCV)

Katika uumbaji wake wote, ni binadamu tu ndio wameumbwa “katika mfano wa Mungu.” Huu ni upendeleo mkubwa na hutupa heshima. Hatujui yote huhusu kifungu hiki cha maneno, lakini tunajua baadhi ya vipengele: kama Mungu, sisi ni viumbe vya kiroho-roho zetu hazifi na zitaishi hata baada ya miili yetu ya duniani kufa; sisi tuna akili-tunaweza kufikiri kutatua matatizo; kama Mungu, tuna busara-tunaweza kutoa na kupokea upendo; na tuna hali ya uadilifu-tunaweza kujua mema na mabaya, ambayo kutufanya kutoa hesabu kwa Mungu.

Biblia inasema kwamba watu wote, sio waamini tu, wana sehemu ya sura ya Mungu, ndiyo maana uuaji na utoaji mimba ni dhambi. (Mwanzo 9:6; Zaburi 139:13-16; Yakobo 3:9.) Lakini sura hii si kamilifu imeharibiwa na dhambi. Hivyo Mungu alimtuma Kristo na kazi ya kuja kurejeza sura kamili ambayo tumeipoteza.

Je, sura na “mfano wa Mungu” kamili ukoje? Huonekana kama Kristo! Biblia husema Yesu ni “Mfano halisi wa Mungu,” “Sura ya Mungu asiyeonekana,” na “Mwakilishi halisi wa nafsi yake.” 2 Wakorintho 4:4 (NLT); Wakolosai 1:15 (NLT)

Watu mara nyingi hutumia maneno, “Kama baba kama mwana” kumaanisha kufanana katika jamaa. Watu wanapoona mfano wangu katika watoto wangu, hunifurahisha. Mungu anapenda watoto wake kuwa na sura na mfano wake pia. Biblia inasema, “Ninyi … mliumkbwa ili muwe kama Mungu, wenye haki na watakatifu kweli.” Waefeso 4:24 (GWT)

Ngoja niwe wazi zaidi: Kamwe hutakuwa Mungu, au hata mungu. Uongo huo wa kiburi ni jaribu la zamani la Shetani. Shetani aliwaahidi Adamu na Hawa kwamba kama wangefuata ushauri wake, “Mtakuwa kama miungu.” Mwanzo 3:5 (KJV) Dini nyingi na falsafa za wakati mpya (New Age) bado wanaendeleza uongo huu wa kale kwamba sisi ni miungu au tunaweza kuwa miungu.

Tamaa hii ya kuwa Mungu hujitokeza kila wakati tunapotaka kutawala mazingira yetu, hatima yetu, na watu wanaotuzunguka. Lakini kama viumbe, hatutakuwa muumba kamwe. Mungu hapendi wewe uwe Mungu; anakutaka uwe mcha Mungu (godly)-ukichukua matakwa yake, nia na tabia zake. Biblia husema, “Vaeni njia mpya ya maisha-maisha ya kimungu, maisha yaliyofanywa upya kutoka ndani na kujitokeza katika tabia yenu kama Mungu anavyodhihirisha bayana tabia yake ndani yenu.” Waefeso 4:22 (Msg)

Lengo la Mungu kwa maisha yako duniani siyo faraja, lakini kukuza tabia. Anapenda ukue kiroho na uwe kama Kristo. Kuwa kama Kristo haimaanishi kupoteza nafasi yako au uwe kama kiumbe kisicho na akili. Mungu alikuumba wa kipekee, hivyo bila shaka hapendi kukuangamiza. Kufanana na Kristo ni kuhusu kubadilisha tabia yako, siyo nafsi yako.

Lengo kuu la mungu kwa maisha yako siyo faraja lakini kukuza tabia yako.

Mungu anakutaka ukuze tabia kama ile iliyoelezwa katika heri za Yesu, (Mathayo 5:1-12) tunda la Roho, (Wagalatia 5:22-23) sura ya upendo ya Paulo, (1 Kakorintho 13) na sifa zilizoorodheshwa na Petro za maisha yanayofaa. (2 Petro 1:5-8) Kila unaposahau kwamba tabia ni moja ya malengo ya Mungu kwa maisha yako, utavunjwa moyo na mazingira yako. Utashangaa, “Kwa nini linanitokea? Kwa nini Napata muda mgumu namna hii?” Jibu moja ni kwamba maisha yanapaswa kuwa magumu! Ndicho hutuwezesha kukua. Kumbuka dunia si mbingu!

Watu wengi huelewa vibaya ahadi ya Yesu ya “uzima tele” (Yahana 10:10) kama kumaanisha afya kamilifu, maisha ya raha, furaha daima, kutimiza ndoto zako zote, na kupata nafuu mara moja kutoka matatizoni kwa njia ya Imani na maombi. Kwa maneno mengine, wanategemea maisha ya Kikristo kuwa rahisi. Wanategemea mbingu duniani.

Mtazamo huu wa ubinafsi humwona Mungu kama jinni ambaye yupo tu kukutumikia kafika kutimiza tamaa zako. Lakini Mungu siyo mtumishi wako, na kama utachukuliwa na wazo la kwamba maisha lazima yawe mepesi, basi utapotoka vibaya sana au utaishi katika hali ya kukana ukweli.

Usisahau kwamba maisha si juu yako! Upo kwa sababu ya lengo la Mungu, na si kinyume cha hapo. Kwa nini Mungu akupe mbingu duniani wakati ameandaa kitu halisi kwa ajili yako katika umilele? Mungu hutupa muda wetu wa duniani ili kujenga na kuimarisha tabia yetu kwa ajili ya mbinguni.

KAZI YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO

Ni kazi ya Roho Mtakatifu ndani yako kukupa tabia ya Kristo ndani yako. Biblia inasema, “Kama Roho wa Bwana anavyofanya kazi ndani yetu, tunafanana naye zaidi na zaidi na kudhihirisha utukufu wake zaidi.” 2 Wakorintho 3:18b (NLT) Mchakato huu wa kutubadilisha ili tuwe kama yesu unaitwa utakaso, ni lengo la tatu la maisha yako duniani.

Huwezi kudhihirisha tabia Kristo kwa nguvu zako mwenyewe. Maazimio ya mwaka mpya, nguvu ya utashi, na nia njema havitoshi. Ni Roho Mtakatifu peke yake aliye na nguvu za kufanya mabadiliko anayotaka kufanya Mungu katika maisha yetu. Biblia inasema, “Mungu anatenda kazi ndani yenu, akiwapa nia ya kumtii na nguvu za kufanya kile kimpendezacho.” Wafilipi 2:13 (NLT)

Ukitaja “nguvu za Roho Mtakatifu,” watu wengi hufikiri juu ya udhihirisho wa

SIKU YA ISHIRINI NA MBILI:

ULIUMBWA ILI UFANANE NA KARISTO

miujiza na hisia za hali ya juu. Roho Mtakatifu hutolewa katika maisha yako taratibu, bila wewe kujua wala kuhisi. Mara nyingi yeye hutujia “kwa sauti nyororo.” 1 Wafalme 9:12 (NIV)

Sura ya Kristo haipatikani kwa kuigiza, lakini kwa kukaa ndani. Tunamruhusu Kristo kuishi kupitia sisi. “Kwa kuwa siri ni hii: Kristo anaishi ndani yesu.” Kolosai 1:27 (NLT) Je, hii inatokeaje katika maisha halisi? Kwa uchaguzi tunaoufanya. Tunachagua kufanya kitu sahihi katika mazingira fulani na kisha tunamwamini Roho Mtakatifu kutupatia nguvu zake, upendo, imani na hekima ya kutenda. Kwa kuwa Roho wa Mungu anaishi ndani yetu, mambo haya yanapatikana siku zote kwa kuyaomba.

Lazima tushirikiane na kazi ya Roho Mtakatikfu. Katika Biblia nzima tunaona ukweli muhimu ukionyeshwa tena na tena: Roho Mtakatifu hutoa nguvu zake mara unapochukua hatua ya imani. Wakati Yoshua alipokabiliwa na kizuizi kisichopitika, mafuriko ya mto Yordani yalitoweka baada ya viongozi kukanyaga kwenye mkondo wa maji kwa utii na imani. (Yoshua 3:13-17) Utii hufungulia nguvu za Mungu.

Mungu anakusubiri utende kwanza. Usingoje uwe na nguvu au ujisikie kujiamini. Songa mbele katika udhaifu wako, ukifanya kitu sahihi pamoja na hofu zako na hisia zako. Hivyo ndivyo unavyoshirikiana na Roho Mtakatifu, na ndivyo tabia yako inavyokua.

Biblia hulinganisha kukua kiroho na mbegu, jengo, na mtoto anayekua. Kila kielelzo huhitaji kushiriki kimatendo: mbegu lazima zipandwe na kulimwa, majengo lazima yajengwe-hayatokei tu-na watoto lazima wale na kufanya mazoezi ili wakue.

Wakati bidii haina chochote kuhusu wokovu wako, ina kazi kubwa kwa kukua kwako kiroho. Angalau mara nane katika Agano Jipya tumeambiwa “kutia bidii” Luka 13:24; Warumi 14:19; Waefeso 4:3; (zote NIV); 2 Timotheo 2:15 (NCV) Waebrania 4:11; 12:4; 2 Petro 3:14 (zote NIV). Katika kukua kwenu na kuwa katika mfano wa Kristo. Hakai tu na kusubiri itokee.

Paulo anaeleza katika Waefeso 4:22-24 wajibu wetu wa aina tatu katika kuwa kama Kristo. Kwanza, lazima tuchague kuziacha tabia zetu za zamani. “Kila kitu … kinachohusiana na maisha ya zamani lazima kiachwe. Kimeoza kabisa, kiondoeni!” Waefeso 4:22 (Msg)

Pili, lazima tubadili namna tunavyofikiri. “Roho Mtakatifu abadili namna mnavyofikiri.” Waefeso 4:23 (CEV) Biblia inseam “tunabadilishwa” kwa kufanywa upya nia zetu. (Warumi 12:2) Neno la Kiyunani la kubadilishwa ni metamorphosis (limetumiwa katika Warumi 12:2 na 2 Wakorintho 3:18), linatumiwa leo kuelekeza badiliko la ajiabu analopitia kiwavi na kuwa kipepeo. Ni kielelezo kizuri kwa kile kinachotokea kwetu kiroho tunapomruhusu Mungu kuongoza mawazo yetu: Tunabadilishwa toka nadani kuja nje, tunavutia zaidi, na tunawekwa huru kuruka katika anga jipya.

Tabia yako hasa ni jumla ya mazoea yako.

Tatu, ni lazima “tuvae” tabia ya kristo kwa kukuza tabia mpya za kimungu. Tabia yako hasa ni jumla ya mazoea yako; ni jinsi utendavyo mara kwa mara. Biblia inaema, “Vaeni utu mpya ulioumbwa kuwa kama Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.” Waefeso 4:24 (NIV)

Mungu hutumia Neno lake, watu na mazingira kukufinyanga. Mambo haya matatu ni ya muhimu katika kukuza tabia. Neno la Mungu hutupa kweli tunayoihitaji ili tukue, watu wa Mungu hutupa msaada tunaohitaji kukua, na mazingira hutupa mazingira tunayohitaji kukfanyia mazoezi ya kufanana na Kristo. Unaposoma na kulifanyia kazi Neno la Mungu, ushirikiane na waamini wengine, na ujifunze kumtumaini Mungu katika mazingira magumu, na kuhakikishia utakuwa na mfano wa Kristo. Tutaviangalia hivi kila kimoja katika sura zilizoko mbele.

Watu wengi hudhani ili kukua kiroho kinachohitajika ni kusoma Biblia na maombi. Lakini baadhi ya mambo maishani hayatabadilishwa na kusoma Biblia au maombi peke zake. Mungu hutumia watu. Hupenda kufanya kazi kupitia watu zaidi kuliko miujiza, ili tutegemeane kwa ajili ya ushirika. Anapenda tukue pamoja.

Katika dini nyingi, watu wanaofikiriwa kuwa wamekomaa kiroho na watakatifu ni wale wanaojitenga na wengine na kwenda katika nyumba za watawa milimani, ambako wanaishi bila kuchafuliwa na watu wengine. Lakini huu ni uelewa potofu. Upevu wa kiroho siyo kujitenga na watu kutafuta mambo ya binafsi! Huwezi kukua katika hali ya mfano wa Kristo katika upweke ni lazima kuwa karibu na watu na kuwa na uhusiano nao. Unahitaji uwe mshirika wa kanisa na jamii. Kwa nini? Kwa sababu kukua kiroho halisi ni juu ya kujifunza kupenda kama Yesu, na huwezi kutenda kwa mfano wa Kristo bila kuwa na uhusiano na watu wengine. Kumbuka, yote ni juu ya upendo-kumpenda Mungu na kuwapenda wengine.

Kuwa kama Kristo ni mchakato mrefu wa kukua na wa polepole. Kukua kiroho si tendo la mara moja au linalotokea lenyewe tu; ni tendo la taratibu, linalotokea hatua kwa hatua ambalo litachukua maisha yako yote. Akizungumzia mchakato huu, Paulo alisema, “Jambo hili litaendelea mpaka hapo sisi … tumepevuka kama Kristo alivyo, na tutakuwa kama yeye kabisa.” Waefeso 4:13 (CEV)

Unafanya kazi katika kuendelea. Mageuzi yako ya kiroho katika kukuza tabia ya Kristo yatachukua maisha yako yote, na hata hapo hayatakuwa kamilifu hapa duniani.

Yatakamilika utakapofika mbinguni au pale Yesu akirudi. Kwa wakati huo, kazi yoyote ambayo haijamalizika juu ya tabia yako itakamilishwa. Biblia inasema kwamba tutakapomwona Yesu kikamilifu, tutakuwa wakamilifu kama Yeye: “Hatuwezi hata kufikiri tutakavyokuwa Kristo atakaporudi. Lakini tunajua kwamba atakapokuja tutakuwa kama Yeye. Kwa kuwa tutamwona halisi kama alivyo.” 1 Yohana 3:2 (NLT)

Mungu anajali zaidi wewe ni nani kuliko unachofaanya.

Vurugu nyingi katika maisha ya Kikristo hutokana na kutokujali ukweli rahisi kwamba Mungu anapenda zaidi kujenga tabia yako kuliko mambo mengine. Tunahofu Mungu anapoonekana kunyamaza katika mambo muhimu kama vile “Ni kazi gani nichague?” Ukweli ni kwamba, kuna kazi nyingi ambazo zinaweza kuwa mapenzi ya Mungu kwa maisha yako. Mungu anachojali zaidi ni kwamba kila ukifanyacho ukifanye kwa namna ya mfano wa Kristo. (1 Wakorintho 10:3-12; 16:14; Wakolosaid 3:17, 23).

Mungu anajali zaidi wewe ni nani kuliko unachofanya. Sisi ni wanadamu, si watendaji. Mungu anahusika zaidi kuhusu tabia yako kuliko kazi yako, kwa sababu utachukua tabia yako hadi katika umilele, na siyo kazi yako.

Biblia inaonya, “Msijifananishe sawa sawa kabisa na mila na desturi zenu bila kufikiri. Badala yake, mtazameni Mungu. Mtabadilishwa kutoka ndani kuja nje … tofauti na mila inayowazunguka, kila wakati ikiwavuta mrudi katika uchanga, Mungu anawaandaa vyema, akiwakuza kukfikia utu uzima.” Warumi 12:2 (Msg) Lazima ufanye maamuzi kupingana na mila ili kuelekea hali ya kufanana na Kristo. Vinginevyo, nguvu nyingine kama ya marafiki, wazazi, wafanyakazi, na mila vitajaribu kukufinyanga katika sura yake.

Inasikitisha, ukipitia kwa haraka vitabu vingi vya Kikristo vinavyopendwa na watu huonyesha kwamba waamini wengi wameacha kumwishia Mungu kwa malengo makubwa na wamezamia mambo ya binafsi na kujenga hisia zao. Hiyo ni kujipendezesha na siyo kumfuata Kristo. Yesu hakufa msalabani ili tuishi kwa raha mstarehe duniani. Lengo lake ni la kina sana: anapenda kutufanya tufanane naye kabla hajatuchukua mbinguni. Huu ni upendeleo mkubwa kwetu, ni wajibu watu sasa, na hatima yetu huu.

 

 

      SIKU YA ISHIRINI NA MBILI

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Niliwekwa wakfu nifanane na Kristo.

Kifungu cha Kukumbuka: “Kadiri Roho wa Bwana anavyofanya kazi ndani yetu, tunakuwa kama Yeye zaidi na zaidi na tunadhihirisha utukufu wake zaidi.” 2 Wakorintho 3:18b (NLT)

Swali la Kujiuliza: Je, ni katika eneo gani la maisha yangu nahitaji kuomba nguvu za Roho Mtakatifu ili niwe kama Kristo leo?

 

 

 

 

 

 

 

Siku ya Ishirini na Tatu: Jinsi Tunavyokua

Mungu anapenda tukue … kama Kristo katika kila kitu.

Waefeso 4:15a (Msg)

Hatukukusudiwa kukaa kama watoto.

Waefeso 4:14a (Ph)

Mungu anapenda ukue.

Lengo la Baba yako a mbinguni ni wewe ukue ufikie kiwango cha tabia za Kristo. Inasikitisha, mamilioni ya Wakristo wanazeeka bila kukua kiroho. Wamezama katika utoto wa kiroho, wakikaa katika mavazi ya kitoto. Sababu ni kwamba hawana mpango na kukua.

Kukua kiroho si tendo linalotokea tu. Huhitaji kuchukua hatua za maksudi. Lazima utake kukua, uamue kukua, fanya bidii kukua na udumu katika kukua. Kuwa mwanafunzi (discipleship) – mchakato wa kuwa kama Kristo – daima huanza na uamuzi. Yesu anatuita, na sisi tunaitika: “Njoo uwe mwanafunzi wangu, Yesu alimwambia. Hivyo Mathayo aliinuka na kumfuata.” Mathayo 9:9 (NLT)

Wanafunzi wa kwanza walipoamua kumfuata Yesu, hawakuelewa matokeo yote ya uamuzi wao. Wao waliitikia tu mwaliko wa Yesu. Ndivyo unavyohitaji kuanza: Amua kuwa mwanafunzi.

Hakuna kinachobadilisha maisha yako zaidi kuliko uamuzi unaouchukua. Maamuzi yako yaweza kukuendeleza au kukuharibu, lakini kati ya hayo, yataonyesha wewe ni nani. Niambie ni jambo gani umejitoa kwalo, nami nitakuambia utakuwa nani miaka ishirini ijayo. Tunakuwa katika hali kulingana na uchaguzi tuliojitoa kuuishia.

Ni katika kujitoa huku kwamba watu wengi hulikosa lengo la Mungu kwa maisha yao. Watu wengi wanaogopa kujitoa kwa ajili ya kitu chochote, hivyo wao hujiendea kiholela katika maisha. Watu wengine hujitoa nusu kufuata mambo yanayopingana maishani, jambo ambalo husababisha maisha ya huzuni na uvuguvugu. Watu wengine hujitoa kikamilifu kwa mambo ya ulimwengu, kama vile kuwa tajiri au kujulikana, na mwisho wake ni kukatishwa tamaa pamoja na uchungu mwingi. Kila uchaguzi una matokeo ya milele, hivyo bora uchague kwa busara. Petro anaonya, “Kwa kuwa kila kitu kinachotuzunguka kitayeyuka na kutoweka, basi mnatakiwa kuishi maisha matakatifu yenye kumcha Mungu!” 2 Petro 3:11 (NLT)

Tunakuwa katika hali kulingana na uchaguzi tuliojitoa kuuishia.

Upande wa Mungu na upande wako. Kufanana na Kristo ni matokeo ya kufanya uchaguzi kama wa Kristo na kwa kutegemea Roho wake akusaidie kutimiza uchaguzi huo. Unapoamua kutilia mkazo kuwa kama Kristo, ni lazima uanze kutenda kwa njia mpya. Utahitaji kuyaacha mambo ya kila siku uliyozoea, kukuza mazoea mapya na kwa makusudi kabisa ubadili namna ya kufikiri. Unaweza kuwa na uhakika kwamba Roho Mtakatifu atakusaidia katika mabadiliko hayo. Biblia inasema, “Endeleeni kuutumikia wakovu wenu kwa hofu na kutetemeka, kwa kuwa ni Mungu atendaye kazi ndani yenu katika kunia na kutenda sawa sawa na lengo lake zuri.” Wafilipi 2:12-13 (NIV)

Kifungu hiki huonyesha pande mbili za kukua kiroho: “kuutumikia” na “atendaye.” “Kuutumikia” ni wajibu wako, na “atendaye” ni wajibu wa Mungu. Kukua kiroho ni kazi ya kushirikiana wewe na Roho Mtakatifu. Roho wa Mungu hufanya kazi pamoja nasi, siyo tu ndani yetu.

SIKU YA ISHIRINI NA TATU:

JINSI

TUNAVYOK UA

Kifungu hiki, kiliandikwa kwa waamini, hakihusu namna ya kuokoka, lakini jinsi ya kukua. Hakisemi “fanyeni kazi kupata wokovu”, kwa sababu huwezi kuongeza chochote kwa kile alifanya tayari. Katika kufanya mazoezi ya mwili, hufanyi hivyo ili kupata mwili, ila kuukuza mwili wako.

Unapocheza mchezo wa mafumbo (puzzle), tayari unavyo vipande vyote-kazi yako ni kuviunganisha. Wakulima hufanya kazi shambani siyo kupata ardhi, lakini kuendeleza kile tayari wanacho. Mungu amekupa wewe maisha mapya; sasa una wajibu wa kuyaendeleza “Kwa hofu na kutetemeka.” Maana yake ni kuchukua kwa makini ukuaji wako wa kiroho! Watu wanapoacha kujali kukua kwao kiroho, inaonyesha hawaeliwi matokeo yake ya milele (kama tulivyoona katika sura ya 4 na 5)

Kubadilisha mwongozo wako. Ili kubadili maisha yako, lazima ubadili unavyofikiri. Nyuma ya kila ufanyalo kuna wazo lako. Kila tabia hutokana na imani, na kila tendo linachochewa na msimamo. Mungu alifunua ukweli huu miaka elfu iliyopita kabla ya wanasaikolojia kuelewa: “Angalia unavyofikiri; maisha yako yanafinyangwa na mawazo yako.” Mithali 4:23 (TEV)

Hebu fikiri kwamba umepanda mtumbwi wa kazi ziwani ukienda bila nahodha ila umefungiwa mashine kwenda mashariki. Ukiamua kuugeuza mtumbwi huu kuelekea magharibi, una njia mbili unazoweza kutumia kubadili uelekeo wa mtumbwi huu. Njia ya kwanza ni kushika usukani na kutumia nguvu kuugeuza kuelekea upande mwingine kutoka kwenye mwelekeo wa kwanza. Kwa nguvu ya utashi unaweza kuishinda ile mashine inayojipeleka tu, lakini utasikia kizuizi wakati wote. Mikono yako inaweza kuchoka, unaweza kuuachia usukani, na mtumbwi mara moja unaweza kuelekea mashariki, njia ambayo ilipangwa ndani yake.

Hivi ndivyo hutokea unapojaribu kubadili maisha yako kwa nguvu na nia yako; unasema, “Nitajilazimisha kula chakula kidog … kufanya mazoezi … ache kutokuwa na mipango na kuchelewa chelewa.” Ndiyo, nguvu ya utashi inaweza kutoa matokeo ya muda mfupi, lakini hujenga usumbufu wa daima ndani yako kwa sababu hujashughulikia mzizi wa tatizo. Badiliko haliwi la asili kwako, hivyo mwisho unakata tamaa, unarudia mlo wako, na unaacha mazoezi. Mara moja unarudia kawaida yako ya nyuma.

Kuna njia bora na rahisi: badili mwongozo wako-jinsi unavyofikiri. Biblia inasema, “Mruhusuni Mungu awabadili na kuwafanya mtu mpya kwa kubadili jinsi mnavyofikiri.” Warumi 12:2b (NLT) Hatua yako ya kwanza katika kukua kiroho ni kubadili unavyofikiri. Mabadiliko daima huanzia katika akili. Unavyofikiri huchochea unavyohisi, na unavyohisi huwa na mvuto wa unavyotenda. Paulo alisema, “Lazima kuwe na kufanywa upya kirobo kwa fikra na nia zenu.” Waefeso 4:23 (NLT)

Kuwa kama Kristo lazima ukuze nia ya Kristo ndani yako. Agano Jipya huita tendo hilo la akili toba, ambalo kwa kiyunani maana yake ni “kubadili nia yako.” Unatubu mara unapobadili namna unavyofikiri kwa kuanza kufikiri Mungu anavyofikiri-kuhusu wewe, dhambi Mungu, watu wengine, maisha, hatima yako, na kila kitu. Unachukua mtazamo wa Kristo.

Tumeagizwa “kufikiri kama Kristo alivyofikiri.” Wafilipi 2:5 (CEV) Kuna sehemu mbili za kufanya hili. Nusu ya kwanza ya badiliko hili la kiakili ni kuacha kufikiri mawazo ya kichanga, ambayo ni ubinafsi na kutafuta mambo ya binafsi. Biblia inasema, “Acheni kufikiri kama watoto, kuhusu maovu iweni watoto lakini katika kufikiri kwenu iweni watu wazima.” 1 Wakorintho 14:20 (NIV) Watoto wachanga kwa asili ni wenye ubinafsi kabisa. Wanajifikiri wao tu na mahitaji yao. Hawawezi kutoa, wanawena tu kupokea. Huko ni kufikiri kwa mtu mchanga. Kwa bahati mbaya, watu wengi hawakui kupita kiwango hicho cha kufikiri. Biblia inasema kuwa kufikiri katika ubinafsi ni asili ya matendo ya dhambi, “wale wanaoishi kwa kufuata nia zao za dhambi hufikiri vitu vile tu ambavyo nafsi zao zenye dhambi zinataka.” Warumi 8:5 (NCV)

Nusu ya pili ya kufikiri ni kuanza kufikiri ki-utu uzima, ambayo ni kuwaangalia wengine na siyo wewe. Katika sura yake kuu ya upendo, Paulo alihitimisha kusema kwamba kuwafikiri wengine ni alama ya ukomavu: “Nilipokuwa mtoto niliongea kama mtoto, niliamua kama mtoto. Nilipokuwa mtu mzima, niliacha mambo ya kitoto.” 1 Wakorintho 13:11 (NIV)

Siku hizi watu wengi hudhani upevu wa kiroho unapimwa kwa kiasi cha habari ya Biblia na mafundisho uliyo nayo. Wakati ufahamu ni moja ya vipimo vya ukomavu, siyo mwisho. Maisha ya Kikristo ni zaidi ya mafundisho, na imani yetu; ni pamoja na mwenendo na tabia. Matendo yetu lazima yafanane na mafundisho yetu, na imani yetu lazima iwe msingi wa mwenendo wetu wa mfano wa Kristo.

Ukristo siyo dini au falsafa, lakini ni uhusiano na mtindo wa maisha. Kiini cha mtindo huu wa maisha ni kufikiri juu ya wengine, kama Yesu alivyofanya, badala ya nafsi zetu. Biblia inasema, “Tufikirie yaliyo mema kwao na kujaribu kuwasaidia kwa kufanya yale yanayowapendeza. Hata Kristo hakujaribu kujipendeza nafsi yake.” Warumi 15:2-3a (CEV)

Kuwajili wengine ni icha ya kufanana na Kristo na uthibitisho imara wa kukua kiroho. Namna hii ya kufikiri siyo ya siyo ya asili, ni kinyume cha desturi, ni ngumu na nadra. Mungu ashukuriwe tuna msaada: “Mungu umetupatia Roho wake. Ndiyo maana hatufikiri kama watu wa ulimwengu huu wanavyofikiri.” 1 Wakorintho 2:12a (CEV) Katika sura chache zifuatazo tutaangalia zana anazotumia Roho Mtakatifu kutusaidia kukua.

SIKU YA ISHIRINI NA TATU

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Hujachelewa kamwe kuanza kukua.

Kifungu cha Kukumbuka:Mruhusuni Mungu awabadili ndani kwa kuwabadili kabisa nia zenu. Kisha mtaweza kujua mapenzi ya Mungu – yaliyo mema na yenye kumpendeza na kamili.” Warumi 12:2b (TEV)

Swali la Kujiuliza: Je, ni eneo gani moja ambao nahitaji kuacha kufikiri nionavyo tu na kuanza kufikiri kwa njia ya Mungu?


Siku ya Ishirini na Nne: Kubadilishwa na Kweli

Watu wanahitaji zaidi ya mkate kwa ajili ya maisha yao; Lazima wale

kila Neno kutoka kwa Mungu.

Mathayo 4:4 (NLT)

Neno la neema … la Mungu laweza kuwafanya muwe apendavyo na

Kuwapatieni kila kitu mnachoweza kuhitaji.

Matendo 20:32 (Msg)

Ukweli unatubadili.

Kukua kiroho ni mchakato wa kuondoa uongo na kuweka ukweli Yesu aliomba, “Uwatakase kwa ile kweli, Neno lako ndiyo kweli.” Yohana 17:17 (NIV) Utakaso unahitaji ufunuo. Roho Mtakatifu hutumia Neno la Mungu kutanya tufanane na Mwana wa Mungu. Kuwa kama Yesu, ni lazima tujaze maisha yetu na Neno lake. Biblia inasema, “Kwa njia na Neno tumewekwa pamoja na kutayarishwa kwa ajili ya kazi alizonazo Mungu kwe ajili yetu.” 1 Timotheo 3:17 (Msg)

Neno la Mungu si kama neno lolote lile. Liko hai. (Waebrania 4:12; Matendo 7:38; 1 Petro 1:23.) Yesu alisema, “Maneno niliyosema kwenu ni roho na ni uzima.” Yohana 6:63 (NASB) Mungu anaposema, mambo hubadilika. Kila kitu kinachozunguka-viumbe vyote-vinaishi kwa sababu “Mungu alisema.” Aliposema vyote vikawa. Bila Neno la Mungu usingeweza kuwa hai. Yakobo anasema, “Mungu aliamua kutupa uzima kwa njia ya Neno la kweli ili tuwe watu wa muhimu zaidi katika vyote alivyoumba.” Yokobo 1:18 (NCV)

Roho wa Mungu hutumia neno la mungu kutufanya tufanane na mwana wa Mungu

Biblia ni zaidi ya kitabu chenye mafundisho ya mwongozo wa imani Neno la Mungu hutoa uzima, huumba imani huleta mabadiliko, humtisha Iblisi, husababisha miujiza, huponya mioyo, hujenga tabia, hubadili mazingira, huleta furaha, hushinda dhiki, hushinda majaribu, huleta tumaini, hutia nguvu hutakasa nia zetu huleta vitu katika uwepo, na hutuhakikishia hatima yetu milele! Hatuwezi kuishi bila Neno la Mungu! Usichukulie kirahisirasi tu. Lazima ulione kuwa muhimu kwa maisha yako kama chakula. Ayubu alisema, “Nimeyatunza maneno ya kinywa chake kuliko chakula change cha kila siku.” Ayubu 23:12 (NIV)

Neno la Mungu ni lishe ya kiroho ni unayohitaji ili utimize lengo lako. Biblia inaitwa maziwa yetu, mkate, chakula kigumu, na matunda matamu. (1 Petro 2:2; Mathayo 4:4; 1 Wakorintho 3:2; Zaburi 119:103.) Chakula hiki ni chakula cha Roho kwa ajili ya nguvu za kiroho na kukua kiroho. Petro anashauri, “Tamanini maziwa safi ya kiroho, ili kwamba kwa hayo mpate kukua katika wokovu wenu.” 1 Petro 2:2 (NIV)

KUKAA KATIKA NENO LA MUNGU

Siku hizi kuna Biblia nyingi zimepigwa chapa kuliko hapo nyuma, lakini Biblia kwenye shelfu haina faida yoyote. Mamilioni ya waamini wamepatwa na ugonjwa wa kiroho wa kutokula, wanafufa kwa njaa ya kiroho. Kuwa mwanafunzi wa Yesu mwenye afya, kujilisha Neno la Mungu lazima liwe jambo lako kuu katika maisha. Yesu aliliita “Kukaa.” Alisema, “Mkikaa katika Neno langu, basi ninyi ni wanafunzi wangu kweli.” Yohana 8:31 (NASB, 1978 edition) Katika maisha ya kila siku, kukaa katika Neno la Mungu ni pamoja na mambo matatu:

Ni lazima nikubali mamlaka yake. Biblia lazima iwe ndicho kipimo chenye mamlaka kwa maisha yangu: dira ya maisha yangu, ushauri ninaousikiliza kwa kufanya maamuzi yangu, na kigezo ninachotumia kutathmini kila kitu. Biblia lazima iwe na kauli ya mwanzo na ya mwisho katika maisha yangu.

Matatizo mengi hutupata kwa sababu tunaweka msingi wa maamuzi yetu kwenye mamlaka zisizoaminika: Mila (“kila mtu anafanya”), desturi (“tumefanya hivi siku zote”), fikra (“inaonekana kuwa na maana”) au hisia (“nilihisi vizuri”). Haya yote manne yameharibiwa na Anguko. Tunachohitaji ni kipimo kikamilifu ambacho hakitatuongoza kimakosa. Ni neno la Mungu tu ndilo linafikia kiwango hicho. Sulemani anatukumbusha, “Kila Neno la Mungu halina kasoro,” Mithali 30:5 (NIV) na Paulo anasema, “Kila kitu katika maandiko ni Neno la Mungu. Lote linafaa kwa mafundisho na kusaidia watu na kwa kuwa sahihisha na kuwaonyesha namna ya kuishi.” 2 Timothy 3:16 (CEV)

Miaka ya mwanzoni ya huduma yake, Billy Graham alipitia kipindi ambapo alihangaishwa na mashaka juu ya usahihi na mamlaka ya Biblia. Usiku mmoja wa mbalamwezi alipiga magoti kwa machozi na kumwambia Mungu kwamba, pamoja na vifungu vilivyomchanganya na kutokuvielewa, tangu hapo na kuendelea ataiamini Biblia kama mamlaka pekee kwa maisha yake na huduma. Tangu siku hiyo na kuendelea, maisha Billy yalibarikiwa na nguvu zisizo za kawaida na utendaji bora.

Uamuzi wa muhimu sana unaoweza kuufanya leo ni kuamua ni nini kitakuwa mamlaka ya mwisho kwa maisha yako. Amua kwamba bila kujali mila yako, desturi, fikra, au hisia, unachagua Biblia kuwa mamlaka yako ya mwisho. Azimia kujiuliza kwanza, “Je, Biblia inasemaje?” katika kufanya uamuzi. Amua kwamba Mungu anaposema kufanya kitu fulani, utaliamini Neno la Mungu na kulitenda hata kama linaleta maana au la hujisikii kulifanya. Chukua maneno ya Paulo kuwa uthibitisho wa imani yako: “Naamini kila kitu kinachokubaliana na sharia na kile kilichoandikwa katika manabii.” Matendo 24:14 (NIV)

Ni lazima nijae ukweli wa Biblia. Haitoshi tu kuamini mamlaka ya Biblia, ni lazima nijaze akili yangu na kweli yake ili kwamba Roho Mtakatifu anibadilishe na kweli hiyo. Kuna njia tano za kufanya: unaweza kulipokea, kulisoma, kulitafiti, kulikumbuka, na kulitafakari.

Kwanza unalipokea Neno la Mungu unapolisikia na kulipokea kwa nia wazi ya kupokea. Mfano wa mpanzi ni kielelezo cha namna ya kupokea kwetu kunavyowezesha Neno la Mungu kuwa na mizizi ndani yetu na kuzaa matunda au la. Yesu alitaja misimamo mitatu isiyo ya kupokea-nia iliyofungwa (udongo mgumu), nia ya kuigiza (udongo usio na rutuba) na nia iliyopotoka (udongo wenye magugu)-na kisha alisema, “Angalieni sana jinsi mnavyosikia.” Luka 8:18 (NIV)

Mara unapohisi kwamba hujifunzi chochote kutoka na mahubiri au mafundisho ya mwalimu wa Biblia, angalia msimamo wako, hasa kuhusu kiburi, kwa sababu Mungu anaweza kusema hata kupitia mwalimu anayechosha sana unapokuwa mnyenyekevu na mwenye kupokea. Yakobo anashauri, “Katika roho ya unyenyekevu (upole, kiasi) pokeeni na kulikaribisha Neno ambalo limepandwa na kuota mizizi moyoni mwenu lina nguvu ya kuokoa nafsi zenu.” Yakobo 1:21b (Amp)

Pili, sehemu kubwa ya historia ya miaka 2000 ya kanisa, ni mapadri ndio walisoma Biblia moja kwa moja, lakini sasa mabilioni yetu tunayo mikononi. Pamoja na hayo, waamini wengi ni waaminifu kusoma gazeti la kila siku kuliko Biblia yao. Haishangazi kwamba hatukui. Hatuwezi kutazama televisheni kwa masaa matatu, na kisha tusome Biblia kwa dakika tatu halafu tutegemee kukua.

Watu wengi wanaodai kuiamini Biblia “kutoka ukurasa hadi ukurasa” hawajawahi kuisoma ukurasa kwa ukurasa. Lakini kama utaisoma Biblia dakika kumi na tano kila siku, utaisomo yate katika mwaka mmoja. Kama utatenga dakika thelathini za televisheni kila siku na badala yake usome Biblia, utaisoma Biblia mara mbili kwa mwaka.

Kusoma Biblia kila siku itakuweka katika mazingira ya kuisikia sauti ya Mungu. Ndiyo maana Mungu aliwaagiza wafalme wa Israeli kutunza nakala ya Neno lake daima karibu nao: “Analazimika kulitunza Neno karibu naye wakati wote na kulisoma kila siku ya maisha yao.” Kumbukumbu 17:19a (NCV) Lakini usilitunze tu karibu yako; lisome mara kwa mara! Dhana rahisi inayoweza kusadia kufanya jambo hili ni kuwa na mpango wa kila siku wa kusoma Biblia. Mpango huu utakuzuia kurukia kurasa mbalimbali bila mpango na kuacha sehemu nyingi. Kama ungependa nakala yako ya mpango wa kila siku wa kusoma Biblia angalia nyongeza ya 2.

Tatu, kutafiti, au kujifunza Biblia ni njia nyingine ya kukaa katika Neno. Tofauti kati ya kusoma na kujifunza Biblia ni kuongezeka kwa kazi nyingine mbili: kuuliza maswali ya kifungu na kuandika mambo uliyojifunza.Hujajifunza Biblia mpaka umeandika mawazo yako chini katika karatasi au kompyuta.

Nafasi hainiruhusu kueleza njia tofauti za kujifunza Biblia. Kuna vitabu kadhaa juu ya kujifunza Biblia , pamoja na kile nilichoandika miaka ishirini iliyopita. (Rick Warren, Mbinu 12 za kujifunza Biblia Binafsi. Kitabu hiki kimetafsiriwa katika lugha sita. Hupatikana www.pastors.com) Siri ya kujisomea Biblia vizuri ni kuuliza maswali sahihi tu. Njia tofauti hutumia maswali tofauti. Utagundua zaidi kama ukitulia na kuuliza maswali kama nani? Nini? Wapi? Kwa nini? Na vipi? Biblia inseam, “Watu wenye furaha kweli ni wale wanaojifunza sharia kamilifu ya Mungu ambayo kuwaweka watu huru, na wanaendelea kujifunza. Hawasahau walichojifunza, lakini wanatii mafundisho ya Mungu yanavyosema. Wale wanaofanya hivi watakuwa na furaha.” Yokobo 1:25 (NCV)

Njia ya nne ya kukaa katika Neno la Mungu ni kwa kulikumbuka. Uwezo wako wa kukumbuka ni kipawa toka kwa Munkgu. Unaweza kufikiri huna kumbukumbu nzuri, lakini ukweli ni kwamba, una mamilioni ya mawazo, kweli na mifano ambayo umekariri. Unakumbuka kilicho muhimu kwako. Kama Neno la Mungu ni muhimu utachukua muda kulikumbuka.

Kuna faida nyingi za kukariri vifungu vya Biblia. Itakusaidia kushinda majaribu, kufanya maamuzi ya busara, kupunguza mahangaiko ya moyo, kujenga kujiamini, kutoa ushauri mzuri, na kushirikisha imani yako kwa wengine. (Zaburi 119:105; 119:49-50; Yeremia 15:16; Mithali 22:18; 1 Petro 3:15.)

Kumbukumbu yako ni kama msuli. Kadiri unavyoitumia zaidi, ndivyo inakuwa na nguvu, na kukariri Maandiko kutakuwa rahisi. Unaweza kuanza kwa kuchagua vifungu vichache vya Biblia kutoka kitabu hiki ambavyo vimekugusa na kuviandika kwenye kadi ndogo unayoweza kubeba. Kisha virudie kwa sauti siku nzima. Unaweza kukariri Maandiko popote: kazini au mazoezini au ukiendesha gari, ukisubiri au wakati wa kulala. Funguo tatu za kukariri Maandiko ni kurudia, kurudia, na kurudia tena! Biblia inasema, “Kumbukeni yale aliyofundisha Kristo na Neno lake liwajae maishani na kuwafanya wenye hekima.” Kolosai 3:16a (LB)

Njia ya tano ya kukaa katika Neno la Mungu ni kulifikiri, Biblia huita “kutafakari.” Kwa wengi, wazo la kutafakari lina maana ya kuacha kufikiri na kuacha akili yako ianze kutangatanga. Hii ni kinyume kabisa na kutafakari Kibiblia. Kutafakari ni kufikiri kwa mwelekeo. Huhitaji juhudi kubwa. Unachagua kifungu, na kufikiri tena na tena akilini mwako.

Kama nilivyotaja katika sura ya 11, kama unajua jinsi ya kuhofu, tayari unajua namna ya kutafakari. Hofu ni kufikiri kwa mwelekeo katika jambo lisilofaa. Kutafakari ni kufanya jambo hilo hilo, lakini kwa kuelekea Neno la Mungu badala ya matatizo yako.

Hakuna tabia yoyote inayoweza kugeuza maisha yako zaidi na kukufanya kama yesu kuliko kutafakari Neno la Mungu kila siku. Tunapochukua muda kulitafakari Neno la Mungu, huku tukimfikiri Kristo kwa makini, “tunabadilishwa na kuchukua mfano wake na utukufu unaozidi.”2 Korintho 3:18 (NIV)

Ukiangalia nyakati zote ambazo Mungu huzungumzia kutafakari katika Biblia, utashangazwa na faida alizoahidi kwa wale wanaochukua muda kulitafakari Neno lake siku nzima. Sababu moja wapo ya Mungu kumwita Daudi “mtu aupendezaye moyo wangu” Matendo 13:22 (NIV) ni kwamba Daudi alipenda kutafakari Neno la Mungu. Alisema, “Nayapenda mafundisho yako! Nayafikiri mchana kutwa.” Zaburi 119:97 (NCV) Kutafakari kwa makini ukweli wa Mungu ni ufunguo kwa maombi kujibiwa na siri ya maisha yenye mafanikio. (Yohana 15:7; Yoshua 1:8; Zaburi 1:2-3.)

Ni lazima niweke katika vitendo kanuni za Neno la Mungu. Kupokea, kusoma, kutafiti, kukumbuka na kutafakari Neno la Mungu yote hayafai kama hatutendi yale tuliyopata. Lazima tuwe “watendaji wa Neno.” Yokobo 1:22 (KJV) Hii ndiyo hatua ngumu zaidi ya zote, kwa sababu Shetani huipiga vita kali. Hajali kama utaenda kwenye kujifunza Biblia ili mradi chochote na kile ulichojifunza.

Kweli itakuweka huru, lakini kwanza inaweza kukufanya uwe na huzuni!

Tunajidanganya wenyewe tunapodhani kwamba kwa kuwa tumesikia au kusoma au kujifunza kweli, basi tumeyatunaza mioyoni mwetu maneno hayo. Hakika unaweza kuwa na bidii kwenye darasa lifuatalo, au semina, au mkutano wa Biblia kiasi kwamba mkakosa muda wa kuyatendea kazi uliyojifunza. Unasahau unapokuwa njiani kwenda kujifunza mambo mengine. Bila utekelezaji, kujifunza kwetu Biblia hakuna maana. Yesu alisema, “Kila asikiaye maneno yangu haya na kuyatenda ni sawa na mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.” Mathayo 7:24 (NIV) Yesu pia alisema kwamba Baraka za Mungu huja kwa kutii ile kweli, sit u kuielewa. Alisema, “Kwa kuwa sasa mnajua haya, mtabarikiwa kama mkiyatenda.” Yohana 13:17 (NIV)

Sababu nyingine kwa nini tunaepuka utekelezaji kwa mtu binafsi ni kwa sababu ni vigumu au hata kuleta maumivu. Kweli itakuweka huru, lakini kwanza inaweza kukufanya uwe na huzuni! Neno la Mungu hufunua nia yetu ya ndani, hudhihirisha makosa yetu, hukemea dhambi yetu, na kututegemea kubadilika. Ni asili ya binadamu kupinga badiliko, hivyo kutekeleza Neno la Mungu ni kazi ngumu. Ndiyo maana ni vigumu kujadili utekelezaji wako binafsi na watu wengine.

Siwei nikakazia kupita kiasi umuhimu wa kuwa mmoja katika kikundi kidogo cha kujifunza Biblia. Mara nyingi tunajifunza kweli nyingi kutoka kwa wengine ambazo tusingejifunza kama tungekuwa peke yetu. Watu wengine watakusaidia kufahamu mambo ambayo usingeyaona na kuweka katika matendo ile kweli ya Mungu.

Njia bora ya kuwa “mtendaji wa Neno” ni kuandika daima hatua za kuchukua kutekeleza ulichojifunza kwa kusoma, kutafiti au kutafakari Neno la Mungu. Kuza tabia ya kuandika kile unachokusudia kufanya. Hatua hii ya utekelezaji lazima iwe ya binafsi (ikuhusishe wewe), inayotekelezeka (kitu unachoweza kufanya), na inayothibitika (weka muda maalum). Kila hatua ya utekelezaji itahusisha uhusiano wako na Mungu, au uhusiano wako na wengine, au tabia yako binafsi.

Kabla ya kusoma sura inyofuata tumia muda fulani kufikiri juu ya swali hili: Je, Mungu amekueleza nini katika Neno lake ambacho hujaanza kukifanya bado? Kisha andika chini maneno machache ya utekelezaji ambayo yatakusaidia utende unachojua. Unaweza kumweleza rafiki ambaye atakuwajibisha. Kama D.L. Moody alivyosema, “Biblia haikutolewa ili kuongeza ufahamu wetu bali kubadilisha maisha yetu.”

SIKU YA ISHIRINI NA NNE

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Kweli hunigeuza.

Kifungu cha Kukumbuka:Mkikaa katika Neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” Yohana 8:31-32 (KJV)

Swali la Kujiuliza: Je, Mungu amenieleza nini katika Neno lake ambacho sijaanza kukifanya bado?

Siku ya Ishirini na Tano: Kubadilishwa na Taabu

Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia

 utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana.

2 Wakorintho 4:17 (NIV)

Ni moto wa mateso ambao hutoa dhahabu ya utauwa.

Madame Guyon

Mungu ana lengo kwa kila tatizo.

Yeye hutumia mazingira kukuza tabia yetu kwa kweli. Yeye hutegemea zaidi mazingira katika kutufanya tufanane na Kristo kuliko anavyotegemea usomaji wetu wa Biblia. Sababu iko wazi: Unakabiliana na mazingira masaa ishirini na nne kila siku.

Yesu alituonya kwamba tutakuwa na matatizo ulimwenguni. (Yohana 16:33) Hakuna aliye sugu kwa matatizo au amefunikwa asipatwe na mateso, wala hakuna aliye huru mbali na matatizo katika maisha. Maisha ni mfululizo wa matatizo. Kila unapotatua moja, jingine linasubiri kutokea. Si yote makubwa, lakini yote yana maana kwa Mungu katika kukuza tabia yako. Petro anatuhakikishia kwamba matatizo ni ya kawaida, “Msishangazwe wala kushtushwa mnapopitia katika mnapopitia katika majaribu yenye moto mbele yenu, kwa kuwa hili si geni, ni jambo la kawaida ambalo litawapata.” 1 Petro 4:12 (LB)

Mungu anatumia matatizo kukusogeza karibu yake. Biblia inasema, “Mungu yuko katibu yao waliopondeka mioyo, huwaokoa wale waliopondeka rohoni.” Zaburi 34:18 (NLT) Wakati wako mzuri wa kuwa na ibada ya karibu na Mungu unaweza kuwa siku zile za giza sana-moyo wako unapokuwa umepondeka, unapohisi kuachwa, unapokuwa huna uchaguzi, maumivu yanapokuwa makubwa-na unamgeukia Mungu peke yake. Ni wakati wa taabu ndipo tunajifunza kusali sala za kweli na uaminifu kutoka moyoni. Tunapokuwa katika maumivu, hatuna nguvu za sala za juu juu.

Wakati wako mzuri wa kuwa na ibada ya karibu na Mungu unaweza kuwa siku zile za giza sana.

Joni Eareckson Tada anasema, “Maisha yakiwa ya raha, tunawezaa kumfahamu Yesu juu juu tu, tukimwiga na kumnukuu na kusema juu yake. Lakini ni tatika taabu ndipo tutamjua Yesu.” Tunajifunza mambo katika Mateso, mambo ambayo hatuwezi kujifunza kwa njia nyingine yeyote.

Mungu angeweza kuzuia Yusufu asitiwa gerezani, (Mwanzo 39:20-22) angezuia Danieli asitupwe kwenye shimo la simba, (Danieli 6:16-23) angezuia Yeremia asitupwe katika shimo la matope, (Yeremia 38:6) angezuia Paulo asivunjikiwe na jahazi mara tatu, (2 Wakorintho 11:25) na angewazuia vijana watatu Waebrania wasitupwe katika tanuru la moto (Danieli 3:26) – lakini hakufanya hivyo. Aliruhursu matatizo hayo kutokea, na matokeo yake kila mmoja wao alimsogelea Mungu karibu zaidi.

Matatizo hutulazimisha kumtazama Mungu na kumtegemea badala ya nafsi zetu wenyewe. Paulo alishuhudia kuhusu faida hii, “Tulihisi tuliwekewa kufa na tuliona jinsi tulivyokuwa hatuna nguvu za kujisaidia wenyewe; lakini ilikuwa vyema, kwa kuwa hapo tuliweka kila kitu mikononi mwa Mungu, ambaye peke yake angeweza kutuokoa.” 2 Wakorintho 1:9 (LB) Kamwe hutajua kwamba unachohitaji ni Mungu tu mpaka pale utakapojikuta umebaki na Mungu tu.

Bila kujali chanzo, hakuna tatizo lolote linaloweza kukupata bila ruhusa ya Mungu. Kila kinachotokea kwa mtoto wa Mungu kinachujwa na Baba, na amekusudia kukitumia kuleta mema ingawa Shetani na watu wengine wanakusudia mabaya.

Kila kinachotokea kwako kina umuhimu wa kiroho

Kwa kuwa Mungu anatawala yote, ajali ni matukio tu katika mpango mzuri wa Mungu kwa ajili yako. Kwa sababu kila siku ya maisha yako iliandikwa kwenye kalenda ya Mungu kabla hujazaliwa, (Zaburi 139:16) kila kinachotokea kwako kina umuhimu wa kiroho. Kila kitu! Warumi 8:28-29 inaeleza kwa nini, “Tunajua kwamba Mungu husababisha kila kitu kufanya kazi pamoja kwa ajili ya mema ya wale wampendao Mungu na wameitwa kulingana na lengo lake kwa ajili yao. Kwa kuwa Mungu aliwajua watu wake kabla, na akawachagua wafanane na Mwana wake.” Warumi 8:28-29 (NLT)

KUELEWA WARUMI 8:28-29

Hiki ni kifungu ambacho hunukuliwa na kueleweka vibaya katika Biblia. Hakisemi, “Mungu husababisha kila kitu kufanya kazi kama ninavyopenda mimi.” Hii si kweli. Wala hakisemi, “Mungu husababisha kila kitu kufanya kazi ili kuleta maisha ya furaha duniani.” Hisi kweli pia. Kuna miisho ya huzuni duniani.

Tunaishi katika ulimwengu ulioanguka. Ni mbinguni tu mdiko mambo yanatendeka kikamilifu kama Mungu alivyokusudia. Ndiyo maana tumeelezwa kusali, “Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.” Mathayo 6:10 (KJV) Ili kuelewa vyema Warumi 8:28-29 ni lazima uangalie kwa makini kila fungu la maneno.

“Tunajua”: Tumaini letu wakati wa magumu hutegemei kufikiri chanya, kufikiri kwa kutarajia, au kule kutegemea mazuri kwa kawaida. Huu ni uhakika uliojengwa kwenye kweli ya kwamba Mungu anatawala kikamilifu ulimwengu na kwamba anatupenda.

“Kwamba Mungu husababisha.” Kana mbunifu nyuma ya kila kitu. Maisha yako siyo matokeo ya bahati mbaya, ajali, au bahati nzuri. Kuna msanifu nyuma. Historia ni hadithi yake. Mungu anavuta nyuzi. Tunafanya makosa, lakini Mungu hakosei kamwe. Mungu hawezi kufanya kosa-kwa sababu yeye ni Mungu.

“Kila kitu.” Mpango wa Mungu kwa maisha yako unahusisha yote yanayokutokea – pamoja na makosa yako, dhambi zako, na maumivu yako. Pia ni pamoja na magonjwa, madeni, majanga, talaka, kifo cha uwapendao. Mungu anaweza kuleta mema kutokana na jambo ovu sana. Alifanya hivyo pale Kalvari.

“Kufanya kazi pamoja”: Siyo kwa kipekee au kwa kujitegemea. Matukio katika maisha yako hufanya kazi pamoja katika mpango wa Mungu Siyo matukio yaliyojitenga, lakini matukio yanayotegemeana katika mchakato mzima wa kukufanya ufanane na Kristo. Ili kutengeneza keki lazima utumie unga wa ngano, chumvi, yai bichi, sukari, na mafuta. Kama kila kimoja kikiliwa peke yake hakina ladha nzuri au hata ni kichungu. Lakini ukivioka pamoja vinakuwa chakula kitamu. Kama ukimpa Mungu maono yako yote mabaya, matukio yasiyopendeza, atayaunganisha pamoja kuwa kitu chema.

“Kwa ajili ya mema”: Hii si kwamba kila kitu maishani ni chema. Mengi yanayotokea katika ulimwengu ni maovu na mabaya, lakini Mungu ni mtaalam wa kutoa mema kutokana na hayo. Katika ukoo wa Yesu Kristo, Mathayo 6:10 (KJV) wanawake wanne wameorodheshwa: Tamari, Ruthu, Rahabu, na Bethsheba. Tamari alimhadaa baba mkwe wake. Rahabu alikuwa kahaba. Ruthu hakuwa Myahudi na alivunja sheria kwa kuolewa na Myahudi. Bethsheba alitenda uzinzi na Daudi, jambo lililoleteleza mauaji ya mume wake. Hizi hazikuwa ni sifa nzuri, lakini Mungu alileta mema kutokana na mabaya, na Yesu akaja kupitia ukoo wao. Kusudi la Mungu ni kubwa kuliko matatizo yetu, maumivu yetu na hata dhambi yetu.

“Ya wale wampendao Mungu na wameitwa”: Ahadi ya Mungu ni kwa watoto wa Mungu tu. Si kwa kila mmoja. Kila kitu hufanya kazi pamoja kwa ubaya kwa wale wanaoishi wakimpinga Mungu na kukazia kufuata njia zao.

“kulingana na lengo lake.” Lengo hilo ni lipi? Ni kwamba sisi “tufanane na Mwana wake.” Kila kitu Mungu anachokiruhusu kutokea katika maisha yako kinaruhusiwa kwa kusudi hilo!

KUJENGA TABIA YA MFANO WA KRISTO

Sisi ni kama lulu, tumechongwa kwa nyundo na tezo ya taabu nyingi. Kama nyundo ya sonara haina nguvu sana kuweza kuondoa mikwaruzo, Mungu atatumia nyundo nzito zaidi. Kama sisi ni jeuri zaidi, anatumia nyundo nzito ya kunyanyuliwa na chombo maalum. Atatumia chochote kile.

Kila tatizo ni nafasi ya kujenga tabia, na kadiri linavyokuwa gumu zaidi, ndivyo kunakuwa na matokeo makubwa katika kujenga msuli wa kiroho na uadilifu. Paulo alisema, “Tunajua kwamba mateso haya yanaleta subira. Na subira huleta tabia bora.” Warumi 5:3-4 (NCV) Kile kinachotokea kwa maisha yako ya nje si cha muhimu sana kama kile kinachotokea ndani yako. Mazingira yako ni ya muda mfupi, lakini tabia yako itadumu milele.

Biblia hufananisha majarikbu na moto wa kusafisha madini ambao huchoma takataka zote. Petro alisema, “Mateso haya huja ili kuthibitisha kwamba imani yenu ni safi. Usafi huu wa imani ni bora sana kuliko dhahabu.” 1 Petro 1:7a (NCV) Mfua fedha aliulizwa, “Je, unafahamu vipi kwamba sasa fedha ni safi? Alijibu, “ninapoona sura yangu ndani yake.” Unapokuwa umesafishwa kwa majaribu, watu wanaweza kuiona sura ya Kristo ndani yako. Yakobo alisema, “Katika matatizo, maisha yenu ya imani yanajitokeza nje na kuonyesha rangi yake halisi.” Yakobo 1:3 (Msg)

Kila kinachotokea kwa maisha yako ya nje si cha muhimu kama kile kinachotokea ndani yako.

Kwa kuwa Mungu anakusudia kukufanya ufanane na Kristo, atakupitisha katika yale Yesu aliyoyapitia. Hii ni pamoja na upweke, majaribu, dhiki, kulaumiwa, kukataliwa, na matatizo mengine mengi. Biblia inasema Yesu “Alijifunza kutii kwa njia ya mateso” na “alikamilishwa kwa njia ya mateso.” (Waebrania 5:8-9) Kwa nini Mungu atuepushe kutoka yale aliyomruhusu Mwana wake kuyapata? Paulo alisema, “Tunapitia mambo yale yale ambayo Kristo anayapitia. Kama tutapitia nyakati ngumu pamoja naye, basi kwa hakika tutakwenda kupita katika nyakati njema pamoja naye!” Warumi 8:17 (Msg)

KUPOKEA MATATIZO KAMA KRISTO

Matatizo hayaleti mara moja yale Mungu anakusudia. Watu wengi huwa na uchungu, badala ya kufurahi, na kamwe hawakui. Unapaswa kuyapokea kama vile Kristo angeyapokea.

Kumbuka mpango wa Mungu ni mwema. Mungu anajua kilicho bora kwako na anakutakia mema moyoni mwake. Mungu alimwambia Yeremia, “Mipango niliyo nayo kwa ajili yenu ni mipango ya kuwapa mafanikio na wala si kuwapa mabaya, mipango ya kuwapatia tumaini na hatima njema.” Yeremia 29:11 (NIV) Yusufu alielewa ukweli huu alipowaeleza ndugu zake waliomuuza utumwani, “Ninyi mlinikusudia mabaya, lakini Mungu aliyakusudia kwa mema.” Mwanzo 50:20 (NIV) Hezekia naye alionyesha mtazamo huo huo alipopata tisho la kufo kwa ugonjwa: “Ilikuwa ni kwa ajili ya faida yangu kwamba nilipatwa na wakati mgumu kama huo.” Isaiah 38:17 (CEV) Mungu akisema hapana unapoomba kupata nafuu, kumbuka, “Mungu anafanya kilicho chema kwetu, akitufundisha kuishi katika utakatifu wa Mungu ipasavyo.” Waebrania 12:10b (Msg)

Ni jambo la muhimu kwamba utazame mpango wa Mungu daima, si maumivu wala matatizo yako. Hivi ndivyo Kristo alivyoweza kuvumilia maumivu ya msalaba, na tunashauriwa kufuata kielelezo hiki: “Mtazameni Kristo, kiongozi wetu na makufunzi wetu. Alikuwa tayari kufa kifo cha aibu msalabani kwa sababu ya furaha aliyofahamu ataipata baada ya hapo.” Waebrania 12:2a (LB) Carrie ten Boom, aliyeteseka katika magereza ya Nazi ya kifo, alieleza nguvu ya kuwa na mwelekeo: “Ukiutazama ulimwengu, utafadhaishwa. Ukitazama ndani utahuzunika. Lakini ukimtazama Kristo, utapata pumziko!” Mwelekeo wako utakuwa kigezo cha hisia zako. Siri ya uvumilifu ni kukumbuka kwamba maumivu yako ni ya muda mfupi lakini zawadi yako ni ya milele. Musa alivumilia maisha ya matatizo ya milele. “Kwa kuwa aliyatazamia malipo.” Waebrania 11:26 (NIV) Paulo alivumilia magumu vilevile. Alisema, “Mateso yetu ya sasa ni madogo na hayatadumu kwa muda mrefu sana. Lakini yanatuletea utukufu usiopimika ambao utadumu milele.” 2 Wakorintho 4:17 (NLT)

Usiwe mtu wa kufikiri kwa karibu. Kaza macho kwa matokeo ya mwisho: “Kama tutashiriki utukufu wake, ni lazima pia tushiriki mateso yake. Mateso tunayopata sasa si kitu chochote ukilinganisha na utukufu atakaokupatia baadaye.” Warumi 8:17-18 (NLT)

Furahi na kushukuru. Biblia inatuambia “Shukuruni katika kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 1 Wathesalonike 5:18 (NIV) Inawezekanaje? Angalia, Mungu anatuambia kushukuru “Katika kila jambo” siyo “Kwa kila jambo.” Mungu hategemei wewe umshukuru kwa mabaya, kwa dhambi, kwa mateso, au kwa matokeo ya mambo haya yenye maumivu katika ulimwengu. Badala yake, Mungu anakutaka umshukuru kwamba atatumia matatizo yako kutimiza malengo yake.

SIKU YA ISHIRINI

NA TANO:

KUBADILIS HWA NA TAABU

Biblia inasema, “Furahi katika Bwana siku zote.” Wafilipi 4:4 (NIV) Haisemi, “Furahieni maumivu yenu.” Hiyo ni hali ya watu ambao kufurahia maumivu. Unafurahi “Katika Bwana.” Bila kujali kinachotokea, unaweza kufurahi katika upendo wa Mungu, uangalizi wake, hekima, nguvu uaminifu wake. Yesu alisema, “Iweni na furaha nyingi kwa wakati huo, kwa sababu mnayo zawadi kubwa ikiwangojeeni mbinguni.” Luka 6:23 (NCV)

Tunaweza kufurahi pia katika kujua kwamba Mungu yuko pamoja nasi katika maumivu hayo. Hatumtumikii Mungu aliye mbali na kujitenga ambaye anatupa maneno ya juu juu tu kututia moyo akiwa amekaa pembeni! Badala zake yeye huingia katika mateso yetu. Yesu alifanya hivyo kwa kuchukua ubinadamu wetu, na Roho wake anafanya hivyo ndani yetu sasa. Mungu kamwe hatatuacha peke yetu.

Kataa kukata tamaa. Uwr mvumilivu na udumu. Biblia husema, “Mchakato huo na uendelee mpaka uvumilivu wenu uimarishwe, na mpate kuwa watu wenye tabia iliyopevuka … bila mawaa ya udhaifu.” Yokobo 1:3-4 (Ph)

Kujenga tabia ni mchakato wa polepole. Kila tunapojaribu kuepuka au kutoroka magumu katika maisha, tunakatisha mchakato huo, na kuchelewesha kukua kwetu, na hakika mwisho wetu unakuwa na maumivu mabaya zaidi-hali ya kutokufaa inayoambatana na kukana na kuepuka. Ukielewa matokeo ya milele ya kukua kwa tabia yako, utasali mara chache sala za “Nifariji” (“Nisaidie njihisi vizuri”) na utasali mara nyingi sala za “Nifananaji.” (“Tumia jambo hili kunifanya nifanane na wewe zaidi”)

Unafahamu kwamba unakua unapoanza kuona mkono wa Mungu katika mazingira magumu, ya ajabu na yasiyo na maana maishani.

Kama unakabiliwa na matatizo sasa hivi, usiulize, “Kwa nini mimi?” Badala yake uliza, “Mungu unataka nijifunze nini?” Kisha mwamini Mungu na dumu katika kutenda yaliyo haki. “Mnahitaji kusimama imara, mkikaa katika mpango wa mungu ili mpate kuwepo kwenye ahadi ya utimilifu.” Waebrania 10:36 (Msg) Usikate tamaa-kua!

 

SIKU YA ISHIRINI NA TANO

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: kuna kusudi nyuma ya kila tatizo.

Kifungu cha Kukumbuka:Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi kuwapatia mema wale wampendao, wale walioitwa kwa kusudi lake.” Warumi 8:28 (NIV)

Swali la Kujiuliza: Ni tatizo gani katika maisha yangu limenisababisha kukua kwa kiwango kikubwa?

Siku Ya Ishirini Na Sita: Kukua Kwa Njia Ya Majaribu

Heri mtu yule asiyetenda dhambi anapojaribiwa, kwa kuwa baada ya hapo atapokea

zawadi ya taji la uzima ambayo Mungu amewaahidi wale wampendao.

Yakobo 1:12 (LB)

Majaribu yangu yamekuwa ni shahada yangu ya juu

Katika mambo ya Mungu.

Martin Luther.

Kila jaribu ni nafasi ya kutenda mema.

Katika kuelekea kukua kiroho, hata majaribu huwa ni jiwe la kukanyaga badala ya jiwe la kukwaza unapotambua kwamba ni wakati mwingine wa kutenda jema badala ya kutenda baya. Majaribu huleta uchaguzi. Wakati majaribu ni silaha kuu ya Shetani ili kukuharibu, Mungu anapenda kuyatumia kukukuza. Kila unapochagua kufanya jema badala ya dhambi, unakua katika tabia ya Kristo.

Kuelewa jambo hili, ni lazima kwanza uziainishe sifa za tabia ya Kristo. Moja ya maelezo mafupi ya tabia yake ni tunda la Roho: “Roho Mtakatifu anapotawala maisha yetu, atazaa tunda kama vile: Upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu, upole na kiasi.” Wagalatia 5:22-23 (NLT)

Sifa hizi tisa ni upanuzi wa Amri Kuu na huonyesha picha nzuri ya Yesu. Yesu ni mkamilifu katika upendo, furaha, amani, uvumilivu na matunda mengine yote yalikuwa ndani ya huyu mtu mmoja. Kuwa na tunda la Roho Mtakatifu ni kuwa kama Yesu.

Je, jinsi gani basi, Roho Mtakatifu anatoa matunda haya tisa katika maisha yako? Je, utaamka siku moja na kukuta ghafla hizi sifa zimekuwa ndaani yako? Hapana. Tunda daima hukua na kuiva polepole.

Mungu hukuza tunda la Roho katika maisha yako kwa kukuruhusu upite katika mazingira ambayo unajaribiwa kutenda kinyume kabisa cha sifa ya tunda la Roho.

Sentensi ifuatayo ni moja ya kweli muhimu za kiroho utakazoweza kujifunza: Mungu hukuza tunda la Roho katika maisha yako kwa kukuruhusu upite katika mazingira ambayo unajaribiwa kutenda kinyume kabisa cha sifa ya tunda la Roho! Kukua kwa tabia daima kunahusu uchaguzi, na majaribu hutoa nafasi hiyo.

Kwa mfano Mungu hutufundisha upendo kwa watu wasiopendeka karibu yetu. Haihitaji tabia kupenda watu wanaopendeka na pia wanaokupenda. Mungu hutufundisha furaha halisi katikati ya huzuni tunapomgeukia. Raha (happiness) hutegemea mazingira ya nje, lakini furaha (joy) hutegemea uhusiano wako na Mungu.

Mungu hukuza amani halisi ndani yetu, siyo kwa kufanya mambo yatendeke kama tulivyopanga, lakini kwa kuruhusu nyakati za machafuko na vurugu. Mtu anaweza kuwa na amani akitazama machweo ya jua yanayopendeza au akistarehe mapumzikoni. Tunajifunza amani halisi kwa kuchagua kumwamini Mungu katika mazingira ambayo tunajaribiwa kuhofu au kuogopa. Vivyo hivyo, uvumilivu unakuzwa katika mazingira ambayo tunalazimika kusubiri na tunajaribiwa kukasirika.

Mungu hutumia mazingira ya kinyume cha kila tunda ili kutupa uchaguzi. Huwezi kudai kuwa mwema kama hujajaribiwa kuwa mbaya. Huwezi kudai kuwa mwaminifu kama hujawahi kupata nafasi ya kutokuwa mwaminifu. Uaminifu unajengwa kwa kushinda jaribu la kutokuwa mwaminifu, unyenyekevu hukua tunapokataa kuwa na majivuno; na uvumilivu hukua kila wakati unapokana jaribu la kukata tamaa. Kila unaposhinda jaribu, unakuwa kama Kristo zaidi!

JINSI JARIBU LINAVYOFANYA KAZI

Inasaidia kufahamu kwamba Shetani anaweza kueleweka kabisa. Ametumia mkakati ule ule na mbinu za zamani tangu uumbaji. Majaribu yote hufuata mfumo ule ule. Ndiyo maana Paulo alisema, “Tunazifahamu hila zake za uovu.” 2 Wakorintho 2:11 (NLT) Kutoka Biblia tunajifunza kwamba jaribu hufuata mchakato wa hatua nne, ambao ndio shetani aliutumia kwa Adamu na Hawa na kwa Yesu pia.

Katika hatua ya kwanza, shetani anaainisha tamaa ndani yako. Inaweza kuwa tamaa ya dhambi, kama tamaa ya kulipa kisasi au kutawala wengine, au yaweza kuwa tamaa njema, kama vile tamaa ya kupendwa na kuthaminiwa au kuhisi furaha. Jaribu huanza pale Shetani anapopendekeza (kwa wazo) kwamba ufuate tamaa mbaya, au utimize ile tamaa njema kwa njia mbaya au kwa wakati usio sahihi. Wakati wote jihadhari na njia mbaya au kwa wakati usio sahihi. Wakati wote jihadhari na njia za mkato.Mara nyingi ni majaribu! Shetani ananong’oneza, “Unastahili hicho! Kichukue sasa! Kitafurahisha … au kitakufanya ujisikie vizuri.”

Tunadhani jaribu liko karibu nasi, lakini Mungu anasema linaanzia ndani yetu. Kama usingekuwa na tamaa ya ndani, jaribu lisingekuvuta, jaribu mara nyingi huanzia akilini mwako, siyo katika mazingira. Yesu alisema, “Kwa kuwa kutoka ndani ndani ya moyo wa mtu, hutoka mawazo mabaya, zinaa, wizi, uuaji, uzinzi uchoyo, ufisadi, uongo, tamaa mbaya, husuda, masingizio, kiburi, na upumbavu. Mambo yote haya maovu hutoka ndani.” Marko 7:21-23 (NLT) Yakobo hutuambia kwamba kuna “Jeshi zima la tamaa mbaya ndani yako.” Yakobo 4:1 (LB)

Tunadhani jaribu liko karibi nasi lakini Mungu anasema linaanzia ndani yetu.

Hatua ya pili ni mashaka. Shetani hujaribu kukufanya utili mashaka yale Mungu aliyosema kuhusu dhambi: Je, kweli ni vibaya? Je, Mungu kweli alisema tusilifanye? Je, Mungu hakumaanisha katazo hili kwa mwingine au kwa wakati mwingine? Je, Mungu anapenda niwe na furaha? Biblia inaonya, “Jiangalieni! Msiruhusu mawazo mabaya au mashaka yamfanye mmoja wenu ageuke na kumuacha Mungu aliye hai.” Waebrania 3:12 (CEV)

Hatua ya tatu ni udanganyifu. Shetani hawezi kusema ukweli na anaitwa “Baba wa Uongo.” (Yohana 8:44) Chochote atakachokuambia kitakuwa uongo au nusu ukweli tu. Shetani hutoa uongo wake badala ya kile Mungu alichokwisha sema katika Neno lake. Shetani anasema, “Hamtakufa, mtakuwa na hekima kama Mungu. Unaweza kuchukua. Kakuna atakayefehamu. Itatatua tatizo lako. Zaidi ya hapo kila mmoja anafanya jambo hili. Ni dhambi ndogo tu.” Lakini dhambi ndogo ni kama kuwa na mimba ndogo: Baadaye itajitokeza tu.

Hatua ya nne ni kutokutii. Hatimaye unatendea kazi yale mawazo ambayo umekuwa unaumba akilini mwako. Kile kilichoanza kama wazo kinazaliwa katika tabia. Unatenda kile ambacho kimekuvutia. Unaamini uongo wa Shetani na kuanguka katika mtego ambao yakobo anaonya: “Tunajaribiwa pale tunapovutwa na kunaswa na tamaa yetu mbaya. Kisha tamaa yetu mbaya huchukua mimba na kuzaa dhambi; na dhambi inapokomaa, huzaa mauti. Msidanganyike, rafiki zangu wapendwa!” Yakobo 1:14-16 (TEV)

KUSHINDA MAJARIBU

Kuelewa jinsi jaribu linavyofanya kazi ni msaada mkubwa, lakini kuna hatua maalum unazotakiwa kuchukua ili kushinda jaribio hilo.

Kataa kutishwa. Wakristo wengi huogopa na kuvunjwa moyo kwa mawazo ya majaribu, kuhisi hukumu, kwamba hawako “juu” ya majaribu. Wanahisi aibu kwa kujaribiwa. Huu ni uelewa potofu kuhusu kukua kiroho. Kamwe hutakua kiasi cha kutojaribiwa.

Kwa maana nyingine yaone majaribu kama heshima. Shetani hawezi kuwajaribu wale ambao tayari wanafanya matakwa yake maovu; wao ni wa kwake tayari. Jaribu ni alama kwamba Shetani anakuchukia, siyo dalili ya udhaifu au kuwa mtu wa dunia. Pia ni sehemu ya kawaida ya wanadamu na kuishi katika ulimwengu ulioanguka. Usishangae wala kushitushwa, au kuvunjwa moyo. Ukubali hali halisi kuhusu ulazima wa kujaribiwa; hutaweza kuepuka kujaribiwa kabisa. Biblia inasema, “Mnapojaribiwa, … siyo “kama.” Paulo alishauri, “Kumbukeni kwamba majaribu yanayokuja katika maisha yenu hayana tofauti na yale yanayowapata wengine.” 1 Wakorintho 10:13 (NLT)

Siyo dhambi kujaribiwa. Yesu alijaribiwa, lakini hakutenda dhambi. (Waebrania 4:15) Jaribu huwa dhambi unapolikubali. Martin Luther alisema, “Huwezi kuzuia ndege wasiruke juu ya kichwa chako lakini unaweza kuwazuia wasijenge kiota kwenye nywele zako.” Huwezi kumzuia Ibilisi asilete mawazo kwako, lakini unaweza kuchagua kutoyatafakari na kuyatendea kazi.

Mfano, watu wengi hawajui tofauti ya mvuto wa kimwili au kusisimuka kingono, na tamaa mbaya (lust). Haviko sawa. Mungu alimuumba kila mmoja wetu na tamaa za tendo la ndoa, na hiyo ni vyema. Kuvutiwa na kusisimka ni mwitikio wa asili na wa kawaida na kwa uzuri wa mwili-mwitikio huo tulipewa na Mungu-wakati tamaa

Jaribu ni alama kwamba shetani anakuchukia, Siyo dalili ya udhaifu au kuwa mtu wa dunia

mbaya ni tendo la maksudi la utashi. Tamaa mbaya ni uamuzi unaouchukua akilini juu ya kile ambacho ungependa kufanya na mwili wako. Unaweza kuvutwa au hata kusisimka bila kuamua kutenda dhambi kwa tamaa mbaya. Watu wengi, hasa Wakristo wanaume, huhisi hatia kwamba maono yao waliyopewa na Mungu yanafanya kazi. Mara wanapoona mwanamke anayevutia, wanadhani ni tamaa mbaya na hujisikia aibu na kuhukumiwa. Lakini kuvutiwa siyo tamaa mbaya mpaka utakapoanza kutafakari kwa makini.

Kwa Kweli, kadiri unavyokua na kuwa karibu na Mungu, ndivyo Shetani atazidi kukujaribu. Mara ulipoanza kuwa mtoto wa Mungu, Shetani alikuwekea “mkataba.” Wewe ni adui yake, na anapanga namna ya kukuangusha.

Wakati mwingine unapokuwa unasali Shetani atakuchanganya au kuleta mawazo machafu ili tu akuvuruge na kukuaibisha. Usitishwe wala kuaibishwa na hili, lakini tambua kwamba Shetani anaogopa sala zako na atajaribu kila kitu kuzizuia. Badala ya kujihukumu mwenyewe kwa kufikiri “Je, niliwezaje kufikiri wazo hilo?” lione kama ni usumbufu kutoka kwa Shetani na mara moja mwelekee Mungu.

Elewa mfumo wako wa kujaribiwa na uwe tayari kwa huo. Kuna hali fulani ambazo hukufanya uwe dhaifu zaidi kwa majaribu kuliko nyingine. Mazingira mengine yatakufanya ujikwae mara moja ambapo mengine hayakusumbui sana. Mazingira haya ni ya pekee kwa udhaifu wako, na unahitaji kuyaainisha kwa sababu Shetani anayajua hakika! Anajua ni nini hukuweka tayari kuanguka, na daima anafanya kazi ili kukuingiza katika mazingira hayo. Petro anaonya, “Jihadharini. Shetani amejiweka tayari kuvamia, na angependa kuwakamata kwa kuwashtukiza mkiwa usingizini.” 1 Petro 5:8 (Msg)

Jiulize mwenyewe, “Lini ninajaribiwa kwa kiasi kikubwa?” Siku gani ya juma? Wakati gani wa siku? Jiulize, “Ni wapi ninajaribiwa zaidi?” Nyumbani? Kazini? Kwa jirani? Kwenye baa ya michezo? Kwenye kiwanja cha ndege au hotelini nje ya mji?

Jiulize, “Nani yuko nami ninapojaribiwa zaidi? Rafiki? Wafanyakazi wenzangu? Wageni? Ninapokuwa peke yangu?” Pia jiulize, “Najisikiaje ninapokuwa nimejaribiwa zaidi?” Yaweza kuwa unapokuwa umechoka, uko mpweke, au umechoshwa, umesongwa na mambo mengi. Inawezekana unapokuwa umeumizwa, au umekasirika, au umehofu, au baada ya mafanikio makubwa, au umefaulu kiroho.

Unapaswa kutambua mfumo wako wa kajaribiwa na ujiandae kuepuka mazingira hayo kadiri iwezekanavyo. Biblia inatuambia mara nyingi kujiandaa na kuwa tayari kukabiliana na majaribu. (Mathayo 26:41; Waefeso 6:10-18; 1 Wathesalonike 5:10-18; 1 Petro 1:13; 4:7; 5:8.) Paulo alisema, “Msimpe Ibilisi nafasi.” Waefeso 4:27 (TEV) Kupanga kwa busara hupunguza majaribu. Fuata ushauri wa Mikthali: “Panga kwa uangalifu kile Unachokifanya … Epuka uovu na uende kwa unyoofu. Usiende hatua moja nje na njia sahihi.” Mithali 4:26-27 (TEV) “Watu wa Mungu huepuka njia za uovu, na wanajilinda kwa kuangalia wanakokwenda.” Mithali 16:17 (CEV)

Omba msaada wa Mungu. Mbingu ziko tayari masaa ishirini na nne kupokea mwito wa hali ya hatari. Mungu anapenda umwombe msaada katika kushinda majaribu. Anasema, “Ukaniite wakati wa mateso. Nitakuokoa na utaniheshimu.” Zaburi 50:15 (GWT)

SIKU YA ISHIRINI NA SITA:

KUKUA KWA NJIA YA MAJARIBU

Naita hii kuwa sala ya mawimbi madogo (microwave) kwa sababu ni ya haraka na inataja jambo halisi: Saidia! Wakari majaribu yanapojitokeza, huna muda mrefu wa mazungumzo na Mungu; wewe unamlilia tu. Daudi, Danieli, Petro Paulo na mamilioni ya wengine waliomba aina hii ya sala ya mara moja kupata msaada wakati wa shida.

Biblia inatuhakikishia kwamba kilio chetu kitasikilizwa kwa sababu Yesu anatuhurumia katika kuhangaika kwetu. Alipatwa na majaribu kama yetu. “Yeye anaelewa udhaifu wetu, kwa kuwa alipitia majaribu kama tunayopata sisi, lakini hakutenda dhambi.” Waebraniaa 4:15 (NLT)

Kama Mungu anasubiri kutusaidia ili tushinde majaribu, kwa nini hatumgeukii mara nyingi? Kusema wazi, wakati mwingine hatuhitaji kusaidiwa! Tunataka kuingia katika jaribu ingawa tunajua ni vibaya. Na kwa wakati huo tunadhani tunajua kinachofaa kwetu kuliko Mungu anavyojua.

Nyakati nyingine tunajisikia vibaya kumwomba Mungu msaada kwa sababu tunaingia katika jaribu hilo mara kwa mara. Lakini Mungu haudhiki, hachoshwi, wala hawi bila subira tunapoendelea kumwendea tena. Biblia inasema, “Na tuwe na ujasiri basi, tukiendee kiti cha enzi cha Mungu, ambapo kuna neema. Hapo tunapokea rehema na kupata neema ya kutusaidia tunapoihitaji.” Waebrania 4:16 (TEV)

Upendo wa Mungu ni wa milele, na uvumilivu wake hudumu milele. Kama unaweza kumlilia Mungu mara mia mbili kwa siku moja akusaidie kushinda jaribu fulani bado atakuwa tayari kukupa neema na rehema, hivyo mwendee na ujasiri. Mwombe nguvu za kutenda kitu sahihi na mtumaini atakupatia.

Majaribu hutusaidia kuendelea kumtegemea Mungu. Kama vile mizizi inavyopata nguvu upepo unapovuma dhidi ya mti, hivyo kila wakati unaposhinda jaribu unazidi kufanana na Yesu. Unapojikwaa-kitu ambacho utafanya-siyo kifo chako. Badala ya kukubali jaribu au kukata tamaa, mtazame Mungu, mtumaini akusaidie, na kumbuka thawabu inayokungojea: “Watu wanapojaribiwa na wakadumu kuwa imara, wanafurahi. Baada ya kuthibitisha imani yao, Mungu atawapa thawabu ya uzima wa milele.” Yakobo 1:12 (NCV)

SIKU YA ISHIRINI NA SITA

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Kila jaribu ni nafasi ya kutenda mema.

Kifungu cha Kukumbuka:Mungu huwabariki watu wale wanaovumilia majaribu. Baada ya hapo wataipokea taji ya uzima ambayo Mungu amewaahidi wale wampendao.” Yakobo 1:12 (NLT)

Swali la Kujiuliza: Je, ni sifa gani ya mfano wa tabia ya Kristo naweza kuikuza kwa kushinda jaribu la mara kwa mara linalonipata?

 Siku Ya Ishirini Na Saba: Kushinda Majaribu

Kimbia kutoka katika chochote kinachokupa mawazo mabaya … lakini

kaa karibu na chochote kinachokufanya utake kutenda mema.

2 Timothy 2:22 (LB)

Kumbukeni kwamba majaribu yanayowapata maishani mwenu hayana

tofauti na yale yanayowapata wengine. Na Mungu ni mwaminifu.

Atalifanya jaribu lisiwe kubwa kuliko uwezo wenu wa kustahimili.

Mnapojaribiwa, atawaonyesha mlango wa kutokea ili msije mkaanguka.

1 Wakorintho 10:13 (NLT)

Siku zote kuna mlango wa kutokea.

Unaweza kuhisi kwamba wakati mwingine jaribu ni zito mno kwako kulibeba, lakini huo ni uongo kutoka wa Shetani. Mungu ameahidi kamwe hataweka mzigo mzito juu yako kuliko anachoweka ndani yako ili kustahimili. Hataruhusu jaribu lolote ambalo huwezi kushinda. Lakini, ni lazima wewe pia ufanye sehemu yako kwa kuweka katika matendo funguo nne za kibiblia katika kushinda majaribu.

Weka mawazo yako kwa kitu kingine. Inaweza kukushangaza kwamba hakuna sehemu yoyote katika Biblia tumeambiwa “kupinga majaribu.” Tumeambiwa “kumpinga Shetani,” (Yakobo 4:7) lakini hiyo ni tofauti, kama nitakavyoeleza baadaye. Badala yake tumeambiwa kuelekeza mawazo yetu kwa sababu kupinga mawazo yetu haiwezekani. Badala yake huzidisha mwelekeo wetu katika kitu kibaya na kuongeza mvuto wake. Ngoja nieleze:

Vita dhidi ya dhambi unaishinda au kushindwa katika akili yako. Chochote kinachogusa ufahamu wako kitakupata.

Kila wakati unapojaribiwa kuzuia wazo katika mawazo yako, ndipo unapolizamisha zaidi katika kumbukumbu yako. Kwa kulipinga ni Dhahiri kwamba unalipa nguvu zaidi. Hii ni kweli hasa kuhusu jaribu. Huwezi kushinda jaribio kwa kupigana na hisia zako. Kadiri unavyopigana na hisia, ndivyo linavyozidi kukumaliza na kukutawala. Linaongezeka nguvu kila unapolifiria.

Kwa kuwa jaribu huanza na wazo, njia ya haraka ya kumaliza mvuto wake ni kuelekeza mawazo yako katika kitu kingine. Usipigane na wazo hilo, wewe bedilisha tu mwelekeo wa mawazo yako na kuhusika na wazo jingine. Hii ni hatua ya kwanza katika kushinda majaribu.

Vita dhidi ya dhambi unaishinda au kushindwa katika akili yako. Chochote kinachogusa ufahamu wako Kitakupata. Ndiyo maana Ayubu alisema, “Nilifanya agano na macho yangu yasitazame msichana kwa tamaa mbaya.” Ayubu 31:1 (NLT) Na Daudi aliomba, “Unigeuze macho yangu, nisitazame yasiyofaa.” Zaburi 119:37a (TEV)

Je, umewahi kuona tangazo la chakula katika televisheni na ghafla ukahisi njaa? Je, umewahi kumsikia mtu anakohoa na ghafla ukahisi kusafisha koo lako? Je, umewahi kumwona mtu akipiga mwayo na wewe ukatamani kupiga mwayo? (unaweza hata kupiga mwayo unaposoma hii!) Hiyo ndiyo nguvu ya pendekezo. Mara nyingi ni kawaida kwetu kuelekea kule tunakoelekezea mawazo yetu. Kadiri unavyofikiri juu ya kitu fulani, ndivyo kinavyokushika.

Ndiyo maana kurudiarudia “Ni lazima niache kula mno … au kuvuta sigara … au kutamani” ni mkakati wa kujishinda wenyewe. Hukufanya uelekeze mawazo yako katika kitu ambacho hutaki. Ni kama kutangaza, “Sitafanya kile ambacho mama yangu alifanya. “Unajiweka sawa kukirudia.

Mambo ya kutawala lishe hayafanikiwi mara nyingi kwa sababu hukufanya ufikiri juu ya chakula kila wakati, ili mradi tu upatwe na njaa. Vivyo hivyo, msemaji anajisemea mwenyewe, “usiongope!” anajiandaa kuogopa! Badala yake anatakiwa kuelekeza mawazo yake kwenye jambo jingine isipokuwa hisia zake- ajielekeze kwa Mungu, umuhimu wa hotuba yake, au kwa mahitaji wasikilizaji wake.

Majaribu huanza kwa kuteka mawazo yako. Kinachoshika mawazo yoko husisimua hisia zako. Kisha hisia zako huchochea matendo yako, na unatenda kufuata ulivyojisikia. Kadiri unavyojielekeza kwenye “sitaki kufanya hili, “ndivyo linavyokuvuta kukuingiza kwenye mtandao wake.

Majaribu huanza kwa kuteka mawazo yako. Kinachoshika mawazo yako husisimua hisia zako. Kisha hisia zako huchochea matendo yako, na unatenda kufuata ulivyojisikia. Kadiri unavyojielekeza kwenye “sitaki kufanya hili,” ndivyo linavyokuvuta kukuingiza kwenye mtandao wake.

Kupuuza jaribu ni bora zaidi kuliko kulipinga. Mara mawazo yako yanapoelekea kwenye kitu kingine, lile jaribu hupoteza nguvu zake. Hivyo jaribu linapokupigia simu, usibishane nalo wewe kata simu tu!

Wakati mwingine inabidi kuondoka kutoka kwenye mazingira ya jaribu. Huu ni wakati unaokubalika kukimbia. Inuka na ufunge televisheni. Ondoka kwenye kikundi kinachosengenya. Ondoka kwenye ukumbi wa filamu. Ili kuepuka kuumwa na nyuki kaa mbali na nyuki. Fanya kila liwezekenalo ili kugeuza na kuelekeza mawazo yako kwa kitu kingine.

Kiroho, akili yako ni kiungo kilicho dhaifu. Ili kupunguza kujaribiwa, jaza mawazo yako na Neno la Mungu na mawazo mengine mazuri. Unashinda mawazo mabaya kwa kufikiri jambo zuri. Hii ni kanuni ya kubadilisha. Unashinda ubaya kwa wema. (Warumi 12:21) Shetani hawezi kupata usikivu wako pale mawazo yako yanapokuwa yamejaa kitu kingine. Ndiyo maana Biblia inatuambia kwa kurudiarudia kuyapa mwelekeo mawazo yetu: “Elekezeni mawazo yenu kwa Yesu.” Waebrania 3:1 (NIV) “Fikirini daima juu na yesu.” 2 Timotheo 2:8 (GWT) “Jazeni akili zenu na mambo yale yaliyo mema yanayostahili sifa: mambo yaliyo ya kweli, yenye sifa njema, ya haki, yasiyo na taka, yakupendeza, na ya heshima.” Wafilipi 4:8 (TEV)

Kama umeamua kushinda majaribu ni lazima uitawale akili yako na kutawala unavyopewa taarifa. Mtu mwenye hekima duniani alionya kuwa. “Angalia unavyofikiri? Maisha yako yanafinyangwa na mawazo yako.” Mithali 4:23 (TEV) Usiruhusu takataka kuingia akilini mwako bia kuchuja. Uwe na upembuzi. Chagua kwa uangalifu unachofikiri. Fuata kielelezo cha Paulo: “Tunateka nyara kila fikra ipate kushuka na kumtii Kristo.” 2 Wakorintho 10:5 (NCV) Hii ni kazi ya kufanya maisha yote, lakini kwa msaada wa Roho Mtakatifu unaweza kupanga upya unavyofikiri.

Weka wazi vitu vyoko kwa rafiki mcha Mungu au kikundi cha kusaidiana. Hauhitaji kuutangazia ulimwengu mzima, lakini unahitaji walau mtu mmoja unayeweza kumshirikisha wazi vita vyako. Biblia inasema, “Ni vyema ukiwa na rafiki kuliko kuwa peke yako … ukianguka, rafiki yako aweza kukuinua. Lakini ukianguka bila kuwa na rafiki karibu, hakika utapata taabu.” Mhubiri 4:9-10 (CEV)

SIKU YA ISHIRINI

NA SABA:

KUSHINDA MAJARIBU

Ngoja niwe wazi: Kama unashindwa vita dhidi ya tabia fulani mbaya inayokusonga daima, au jaribu, na umezama katika mzunguko wa nia njema-kuanguka-hukumu, hutapona wewe mwenyewe tu! Unahitaji msaada wa watu wengine. Majaribu mengine yanashindwa tu kwa msaada wa rafiki anayekuombea, anayekutia moyo, na kukuwajibisha.

Mpango wa Mungu katika kukua kwako na kukupa uhuru unahusisha Wakristo wengine. Ushirika halisi, na wa kweli ndiyo dawa ya vita vya peke yako dhidi ya dhambi zisizotaka kutoka. Mungu anasema ndiyo njia pekee itakayokuwezesha kuwa huru: “Ungamianeni dhambi ninyi kwa ninyi na kuombeana ili kwamba mpate kuponywa.” Yokobo 5:16 (NIV)

Je, ni kweli unataka kuponywa na hilo jaribu la daima ambalo linakuangusha mara kwa mara? Suluhisho la Mungu ni Dhahiri: Usilizuie ndani; kiri! Usilifiche; lifichue. Kufunua hisia zako ni mwanzo wa kuponywa kwako.

Kuficha maumivu yako hufanya yawe mazito zaidi. Matatizo hukua gizani yakawa makubwa zaidi, lakini yakiwekwa wazi katika nuru ya ile kweli, yanasinyaa. Unakuwa mgonjwa sawa na siri zako. Hivyo ondoa vazi la maigizo, acha kuigiza kuwa u mkamilifu, na utembee katika uhuru.

Ukweli ni kwamba kitu chochote ambacho huwezi kukizungumzia tayari kimeshavuka uwezo wako wa kukitawala katika maisha yako.

Hapa katika Kanisa la Saddleback tumeona nguvu ya ajabu ya kanuni hii ya kuvunja vifungo vya mazoea yasiyotegemewa kuachwa na majaribu ya daima kwa kupitia mpango tuliyoanzisha na unaitwa Sherehekea Kupona (Celebrate Recovery). Ni mchakato wa kibibilia wenye hatua nane wenye misingi katika Heri za Yesu (Beatitudes) na kujengwa kwenye vikundi vidogo vidogo vya kusaidiana. Katika miaka humi iliyopita zaidi ya watu 5,000 wamewekwa huru kutoka katika tabia mbali mbali, maumivu na mazoea mabaya. Leo mpango huu unatumiwa katika maelfu ya makanisa. Napenda mpango huu utumike kanisani mwake.

Shetani anapenda ufikiri kwamba dhambi na majaribu yako ni ya kipekee hivyo lazima uyatunze kama siri. Ukweli ni kwamba, ssisi sote tuko katika mtumbwi mmoja. Sote tunapigana na majaribu yale yale, (1 Wakorintho 10:3) na “Sisi sote tumetenda dhambi.” (Warumi 3:23) Mamilioni ya watu wamewahi kujihisi kama unavyojihisi na wamepatwa vita kama ulivyo navyo sasa.

Sababu ya kuficha makosa yetu ni kiburi. Tunataka wengine wafikiri sisi “tunatawala” kila kitu. Ukweli ni kwamba, kitu chochote ambacho kuwezi kukizungumzia, tayari kimeshavuka uwezo wako wa kukitawala katika maisha yako: matatizo yako ya kifedha, ndoa, watoto, mawazo, zinaa, tabia za siri, au chochote. Kama ungeweza kulimaliza mwenyewe tayari ungekwisha fanya hivyo. Lakini huwezi. Uwezo wa utashi na suluhisho la binafsi havitoshi.

Matatizo mengine yamezama sana, yamekuwa mazoea, na ni makubwa sana kiasi cha wewe kutoyatatua mwenyewe. Unahitaji kikundi kidogo au rafiki ambaye mtawajibishana ambaye atakutia moyo, atakusaidia, atakuombea, atakupenda bila mashariti, na atakuwajibisha. Na kisha unaweza kuwatendea vivyo hivyo.

Kila mtu anapoeleza siri yake, “Sijamwambia jambo hili mtu yeyote mpaka sasa,” napata furaha kwa ajili yake kwa sababu najua sasa mtu huyu anakwenda kupata nafuu na uhuru. Msongo wake unakwenda kuondolewa, na kwa mara ya kwanza wanakwenda kupata mwanga mdogo wa matumaini ya mbele. Hii hutokea mara kwa mara tunapofanya yale Mungu anayotuagiza kwa kukiri mambo yanayotusumbua kwa rafiki mcha Mungu.

Hebu nikuulize swali gumu: Je, ni kitu gani unajifanya kusema si tatizo maishani mkwako? Unaogopa kuzungumzia nini? Hutaweza kulitatua mwenyewe. Ndiyo, inatunyenyekesha kukiri udhaifu wetu kwa wengine, lakini kukosa unyenyekevu ndicho kitu kinachokuzuia kupona. Biblia inasema, “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa neema wanyenyekevu. Basi nyenyekeeni mbele za Mungu.” Yakobo 4:6-7a (NLT)

Mpinge Shetani: Baada ya kunyenyekeza nafsi zetu na kumtii Mungu, tunaambiwa sasa kumpinga Ibilisi. Sehemu inayobaki ya Yakobo 4:7 inasema, “Mpingeni Ibilisi naye atawakimbia.” Hatukai tu na kuyaangalia mashambulizi yake. Lazima tujibu mashambulizi.

Agano Jipya huyaeleza maisha ya Kikristo kama vita vya kiroho dhidi ya nguvu za uovu, kwa kutumia maneno ya kivita kama vile kupigana, kushinda, kupambana, kuzidi nguvu. Wakristo mara nyingi wamelinganishwa na askari wanaopigana katika himaya ya adui.

Je, tunaweza kumpinga Ibilisi? Paulo anatuambia, “Vaeni wokovu kama chepeo yenu, na kuchukua upanga wa Roho, ambao ni Neno la Mungu.” Wafeso 6:17 (NLT) Hatua ya kwanza ni kupokea wokovu wa Mungu. Huwezi kumwambia Shetani hapana mpaka uwe tayari umesema ndiyo kwa yesu. Bila Yesu sisi hatuna ulinzi wa kumzuia Ibilisi, lakini tukiwa na “chapeo ya wokovu” akili zetu zimelindwa na Mungu. Kumbuka hili: Kama wewe ni mwamini, Shetani hawezi kukulazimisha kufanya chochote. Anaweza tu kutoa pendekezo.

Pili, lazima utumie Neno la Mungu kama silaha yako dhidi ya Shetani. Yesu alitoa kielelezo cha namna hii alipojaribiwa jangwani. Kila wakati Shetani alipopendekeza Jaribu, Yesu alijibu kwa kunukuu Maandiko. Hakubishana na Shetani. Hakusema, “sina njaa,” alipojaribiwa kutumia uwezo wake ili kutimiza hitaji lake binafsi. Yeye alichukua tu Maandiko kutoka katika kumbukumbu yake. Lazima tufanye vivyo hivyo. Kuna nguvu katika Neno la Mungu, na Shetani huliogapa.

Usijaribu kamwe kubishana na Ibilisi. Yeye ni bingwa wa kubishana kuliko wewe, amekuwa na uzoefu wa miaka maelfu. Huwezi kumlaghai Shetani kwa kutumia akili yako au maoni yako, lakini unaweza kutumia silaha inayomfanya atetemeke-ile kweli ya Mungu. Ndiyo maana kukariri Maandiko ni muhimu katika kushinda majaribu. Unayapata mara moja pindi unapojaribiwa. Kama Yesu, unayo ile kweli moyoni mwako, tayari kukumbukwa.

Kama huna vifungu vya Biblia ulivyokariri, huna risasi katika bunduki yako! Nakupa changamoto ya kukariri kifungu kimoja kila wiki kwa maisha yako yaliyobaki. Utakuwa na nguvu sana.

Usijaribu kamwe kubishana na ibilisi. Yeye ni bingwa wa kubishana kuliko wewe. Amekuwa na uzoefu wa miaka maelfu.

Elewa udhaifu wako. Mungu anatuonya kamwe tusijifanye. Wajuaji na wenye kujiamini zaidi; hivyo ni vichocheo vya majanga. Yeremia alisema, “Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote na hauna tiba.” Yeremia 17:9 (NIV) Hii ina maana kwamba sisi tuna uwezo wa kujidanganya wenyewe. Kukiwa na mazingira mwafaka, yeyote kati yetu anaweza kutenda dhambi yoyote. Tusije tukaacha kujichunga tukidhani kuwa sisi tumeshavuka kiwango cha kujaribiwa.

Usijingize bila uangalifu kwenye mazingira yanayoleta majaribu. Yaepuke. Mithali 14:16 (TEV) Kumbuka ni rahisi kukaa nje ya jaribu kuliko kutoka kwenye jaribu. Biblia inasema, “Msiwe wajinga sana na wenye kujiamini. Hakuna aliye maalum. Mnaweza kuanguka chini kabisa kama yeyote yule. Sahauni mambo ya kujiamini, haifai. Jengeni ujasiri katika Mungu.” 1 Wakorintho 10:12 (Msg)

 

SIKU YA ISHIRINI NA SABA

KUFIKIRI KWA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Kuna mlango wa kutokea daima.

Kifungu cha Kumbukumbu:Mungu ni mwaminifu. Atalifanya jaribu lisiwe zito sana kiasi cha wewe kutoweza kulishinda. Unapojaribiwa, atakuonyesha na mlango wa kutokea ili kwamba usije ukaanguka katika jaribu hilo.” 1 Wakorintho 10:13b (NLT)

Swali la Kujiuliza: Je, nimwombe nani awe mwenzangu wa kiroho ili anisaidie katika kushinda jaribu linalonisonga daima kwa kuniombea?

Siku ya Ishirini na Nane: Huchukua Muda

Kila kitu hapa duniani kina wakati wake na majira yake.

Mhubiri 3:1 (CEV)

Nina uhakika kwamba Mungu aliyeanza kazi njema ndani yenu ataendelea kuwasaidia

 ili mkue katika neema yake hadi hapo kazi yake ndani yenu itakapokuwa

imekamilika katika siku ile Kristo atakaporudi.

Wafilipi 1:6 (LB)

Hakuna njia ya mkato katika kukua.

Huchukua miaka mingi kwetu kukua na kuwa watu wazima, na huchukua kipindi kizima cha majira kwa tunda kukua na kuiva. Ndivyo ilivyo hata kwa tunda la Roho. Kukua katika tabia ya mfano wa Kristo hakuwezi kupelekwa haraka. Kukua kiroho, kama ilivyo kukua kimwili, huchukua muda.

Unapojaribu kuivisha tunda haraka, hupoteza ladha yake. Katika nchi ya Marekani, nyanya huchumwa zikiwa mbichi ili zisikwaruzwe wakati wa kupelekwa ghalani. Kisha, kabla ya kuuzwa, nyanya hizi hupuliziwa gesi ya kaboni dioksaidi (CO2) ili kuzigeuza kuwa nyekundu mara moja. Nyanya zenye gesi hii zinalika, lakini hazina ladha sawa na zile zilizoachwa zikakomaa taratibu na kuivia shinani.

Wakati sisi tunahofu kuhusu tunavyokua karaka, Mungu anahusika na kiasi cha nguvu tulizoongeza. Mungu hutazama maisha yetu katika mtazamo wa umilele, hivyo hana haraka kamwe.

Wakati sisi tunahofu kuhusu tunavyokua haraka, Mungu anahusika na kiasi cha nguvu tulizoongeza.

Lane Adams aliwahi kulinganisha mchakato wa kukua kiroho na ule makakati uliotumiwa na Washirika katika Vita Vya Pili Vya Dunia ili kukomboa visiwa vya Pasifiki Kusini. Kwanza “walikilainisha” kisiwa, wakadhoofisha upinzani kwa kupiga mabomu kwenye ngome za adui kutoka kwa meli zilizokuwa mbali na nchi kavu. Kisha kikundi kidogo cha askari wa majini walishambulia kile kisiwa na kutengeneza kichwa cha ufukweni (beach head), sehemu ndogo ya kisiwa ambayo wangeitawala. Baada ya kichwa-cha-ufukweni kupatikana, wangeanza sasa mchakato mrefu wa kukikomboa kisiwa chote, sehemu ndogo kwa mara moja. Hatimaye kisiwa chote kiliweza kutawaliwa, lakini siyo bila vita vikali.

Adams alitoa kielelezo hiki: Kabla Kristo hajavamia maisha yetu wakati wa kuongoka, wakati mwingine anapaswa “kutulainisha” kwa kuruhusu matatizo tusiyoweza kuyastahimili. Hapo baadhi hufungua maisha yao kwa Kristo mara ya kwanza anapogonga langoni kwao, wengi wetu hupinga na kujilinda. Hali yetu kabla ya kuokoka ni Yesu anasema, “Tazama nasimama mlangoni na kupiga bomu.

Mara unapofunguka kwa ajili ya Kristo, Mungu anapata “kichwa-cha-ufukweni” maishani mwako. Unaweza kufikiri umejisalimisha maisha yako yote kwake, lakini ukweli ni kwamba, kuna mambo mengi maishani mwako ambayo hata huyajui. Unaweza tu kumpa Mungu kiasi chako unachokifahamu kwa wakati huo. Sawa, mara Kristo anapopewa kichwa – cha – ufukweni, anaanza mkakati wa kuchukua sehemu zaidi za utawaha hadi hapo maisha yako yote atakapoyachukua. Kutakuwa na mapambano na vita, lakini matokeo hayatakuwa na mashaka kamwe. Mungu ameahidi kwamba, “Yeye alivyeanza kazi njema ndani yenu ataiendeleza hadi ikamilike.” Wafilipi 1:6 (NIV)

Kufanya wanafunzi ni mchakato wa kufanana na Kristo. Biblia inasema, “Tunafikia kiwango halisi cha kukua – kiwango cha kukua kinachomaanishwa na utimilifu wa Kristo.” Waefeso 4:13 (Ph) Mfano wa Kristo ndio hatima yako, lakini safari itadumu kwa muda wa maisha yako yote.

Mpaka hapa tumeshaona kwamba safari hii inahusu kuamini (kwa njia ya kuabudu), kuwa sehemu ya (kwa njia ya ushirika), na kuwa (kwa njia ya kuwa mwanafunzi). Kila siku Mungu nataka uwe kama Yeye kidogo: “Mmeanza kuishi maisha mapya, kwa hayo mnafanywa wapya na kuwa kama Yeye aliyewatengeneza.” Wakolosai 3:10a (NCV)

Siku hizi tumejawa na haraka, lakini Mungu anapenda nguvu na uimara kuliko wepesi. Tunataka suluhisho la mara moja, la njia ya mkato, na la papo kwa hapo. Tunataka mahubiri, semina au tendo fulani ambalo kwa mara moja litatatua tatizo, kuondoa jaribu, na kutuweka huru na maumivu. Lakini kukua halisi hakupatikani kwa tendo moja, haijalishi lina nguvu kiasi gani. Kukua ni hatua ya taratibu. Biblia inasema, “Maisha yetu yaking’aa taratibu na kupendeza zaidi kadiri Mungu anavyoingia katika maisha yetu na tunakuwa kama Yeye.” 2 Wakorintho 3:18b (Msg)

KWA NANI HUCHUKUA MUDA MREFU?

Ingawa Mungu angeweza kutubadilisha mara moja, amechagua kufanya hivyo polepole. Yesu anafanya kwa makusudi katika kuwaendeleza wanafunzi wake. Kama vile Mungu alivyowaruhusu wana wa Israeli kuichukua nchi ya ahadi “kidogo kidogo” (Kumbukumbu 7:22) ili wasije wakalemewa, anapenda kufanya hatua kwa hatua katika maisha yetu.

Kwa nini huchukua muda mrefu kubadilika na kukua? Kuna sababu kadhaa.

Sisi hujifunza polepole. Mara nyingi tunajifunza somo mara arobaini au hamsini ndipo tunaelewa sawa sawa. Matatizo yanaendelea kujirudia, na tunafikiri, “Lisirudie tena! Nimejifunza tayari!” – lakini Mungu anajua zaidi. Historia ya wana wa Israel hutupa kielelezo cha jinsi tunavyosahau haraka masomo Mungu anayotufundisha na jinsi ambavyo tunarudi haraka sana katika mwenendo wetu wa zamani. Tunahitaji kufundishwa kwa kurudiarudia.

Tuna mengi ya kuacha. Watu wengi huenda kupata ushauri wakiwa na tatizo la binafsi au la mahusiano ambalo limechukua miaka kukua na wanasema, “nahitaji unitatulie tatizo langu. Nina saa moja tu.” Kwa kutokuelewa wao hutegemea kupata suluhisho la mara moja kwa tatizo lililozamisha mizizi yake kwa muda mrefu. Kwa kuwa matatizo yetu yaliyo mengi-tabia zetu zote mbaya-hayakujitokeza usiku mmoja, si kweli kutegemea huyaondoa mara moja. Hakuna kidonge, sala, wala kanuni inayoweza kuondoa hapo hapo uharibifu wa miaka mingi. Huhitajika kazi ngumu ya kuondoa na kuweka upya. Biblia huita jambo hili “Kuondoa utu wa kale” na “kuvaa utu mpya.” (Warumi 13:12; Efeso 4:22-25; Kolosai 3:7-10, 14.) Ingawa ulipewa asili mpya wakati ulipookoka, bado unazo tabia za kale, mfumo, na matendo yanayohitaji kuondolewa na kuweka mapya.

Hakuna kukua bila kubadilika, hakuna kubadiliko bila hofu na hasara, na hakuna hasara bila maumivu.

Tunaogopa kukabili kwa unyenyekevu ukweli wetu binafsi. Nimekwisha sema kwamba ukweli utatuweka huru lakini mara nyingi hutuhuzunisha kwanza. Hofu ya yale tutakayoyagundua kama tungekabili kwa uaminifu madhaifu ya tabia yetu hutufanya tudumu kuishi katika kifungo cha kukana. Ni pale tu Mungu anapopewa nafasi kung’aza nuru ya kweli yake kwenye makosa yetu, kushindwa kwetu, na mazoea yetu, ndipo tunapoweza kuanza kuyashughulikia. Ndiyo maana huwezi kukua bila kuwa na msimamo wa unyenyekevu na kufundishika.

Kukua kunaumiza na kunaogopesha. Hakuna kukua bila kubadilika, hakuna kubadilika bila hofu au hasara, na hakuna hasara bila maumivu. Kila dadiliko huja na hasara fulani: ni lazima kuacha njia ya zamani ili upate zile mpya. Tunaogopa hasara hizi, hata kama njia zetu za zamani zilikuwa zinajikwamisha, kwa sababu, kama nguo iliyochakaa, ilikuwaa nzuri na umeizoea.

Watu mara nyingi hujenga utambulisho wa utu wao katika mapungufu yao. Tunasema, “Ni kama mimi tu kuwa …” na “ndivyo nilivyo tu.” Hofu iliyofichika ni kwamba kama nitaacha tabia yangu, maumivu yangu, mazoea yangu, je nitakuwa nani? Hofu hii bila shaka itapunguza kasi ya kukua kwako.

SIKU YA ISHIRINI

NA NANE:

HUCHUKUA MUDA

Mazoea huchukua muda kujengeka. Kumbuka kwamba tabia yako ni jumla ya mazoea yako. Huwezi kudai kuwa mwema mpaka uwe na mazoea ya wema – unaonyesha wema hata bila kufikiri. Huwezi kudai kuwa mwaminifu mpaka iwe mazoea yako kuwa mwaminifu. Mume aliye mwaminifu kwa mke wake mara nyingi huwa si mwaminifu kabisa! Mwenendo wako hueleza tabia yako.

Kuna njia moja tu ya kukuza mwenendo wa tabia ya mfano wa Kristo: Lazima ujizoeze-na hivyo huchukua muda! Hakuna mwenendo wa mara moja. Paulo alimsihi Timotheo, “Tenda mambo haya. Toa maisha yako kwa ajili ya hayo ili kila mtu ayaone maendeleo yako.” 1 Timotheo 4:15 (GWT)

Ukifanyia mazoezi kitu fulani, unakimudu. Marudio ni mama wa tabia na ujuzi. Mazoea haya yanayojenga tabia mara nyingi yanaitwa “maadili ya kiroho,” na kuna vitabu vingi vizuri vinavyoweza kukufundisha mambo haya. Angalia nyongeza ya 2 kwa ajili ya vitabu vilivyopendekezwa kusoma kwa ajili ya kukua kiroho.

USIHARAKISHE

Kadiri unavyokua kiroho, kuna njia kadhaa za kushirikiana na Mungu katika mchakato huo.

Amini Mungu anafanya katika maisha yako hata pale unapokuwa huhisi kitu. Kutua kiroho wakati mwingine ni kazi inayochosha, unapiga hatua moja ndogo kwa muda. Tegemea maendeleo ya polepole. Biblia inasema, “Kila kitu hapa duniani kina wakati wake na majira yake.” Mhubiri 3:1 (CEV) Kuna majira katika maisha yako ya kiroho pia. Wakati mwingine utakuwa na kipindi kifupi cha kukua (wakati wa vuli) kikifuatwa na kipindi cha kuimarishwa na kujaribiwa (kipupwe na masika).

Vipi kuhusu matatizo hayo, mazoea, na maumivu ambayo ungependa yaondolewe kimiujiza? Ni vyema kuomba ili kupata miujiza, lakini usivunjike moyo kama jibu litakuja katika mabadiliko ya taratibu. Baada ya muda, kijito cha maji cha polepole na cha kudumu kitamomonyoa mwamba mgumu na kugeuza miamba mikubwa kuwa vipande vidogo vidogo. Baada ya muda mrefu, mmea mdogo unaweza kugeuka na kuwa mti mkubwa wenye urefu wa futi 350.

Tunza kitabu cha kumbukumbu (journal) kwa ajili ya masomo uliyojifunza. Hiki siyo kijitabu cha matukio ya kila siku, lakini ni cha rekodi ya mambo unayojifunza. Andika ufahamu na masomo ya maisha Mungu anayokufundisha kumhusu, kuhusu wewe, kuhusu maisha, mahusiano, na kila kitu. Yaandike ili upate kuyarudia na kuyakumbuka na pia kuwapa kizazi kijacho. (Zaburi 102:18; 2 Timotheo 3:14.) Sababu ya kujifunza tena somo ni kwamba tunasahau. Kurudia kijitabu chako cha mambo yako ya kiroho mara kwa mara kwaweza kukuponya na maumivu mengi ya moyo yasiyo ya lazima. Biblia inasema, “Imetupasa kuyashika sana hayo tuliyosikia ili tusije tukapotoka.” Waebrania 2:1 (Msg)

Uwe mvumilivu kwa Mungu na kwako mwenyewe. Moja ya mambo ya kukatisha tamaa katika maisha ni kwamba ratiba ya Mungu ni mara chache sana hufanana na yetu. Mara nyingi sisi tuna haraka wakati Mungu hana haraka. Unaweza kuhisi kukata tamaa kwa maendeleo kidogo unayofanya katika maisha. Kumbuka kwamba Mungu kamwe hana haraka, lakini anatunza muda daima. Atatumia muda wa maisha yako yote kukuandaa kwa ajili ya maisha ya milele.

Mungu kamwe hana haraka lakini anatunza muda daima.

Biblia imejaa mifano ya jinsi Mungu anavyotumia mchakato mrefu kukuza tabia, hasa katika viongozi. Alichukua miaka themanini kumwandaa Musa, ikiwemo miaka arobaini ya jangwani. Kwa siku 14,600 Musa alisubiri huku akishangaa, “Muda bado?” Mungu aliendelea kusema “Bado.”

Kinyume na vitabu vingi vinavyopendwa, hakuna hatua rahisi za kufikia kukuka au siri za kuwa mtakatifu mara moja. Mungu anapotaka kutengeneza uyoga, hufanya hivyo kwa usiku mmoja, lakini anapotaka kutengeneza mti mkubwa (oak), huchukua miaka mia moja. Nafsi kuu zimejengwa kwa mapambano na dhoruba na majira ya mateso. Uwe mvumilivu na mchakato huo. Yakobo alishauri, “Msijaribu kutoka katika jambo fulani haraka. Acheni lifanye kazi yake ili mpate kuwa watu wazima waliokua sawasawa.” Yakobo 1:4 (Msg)

Usivunjike moyo. Habakuki alivunjika moyo kwa sababu hakufikiri Mungu alikuwa anatenda kazi haraka, Mungu alisema: “Mambo haya niyoyapanga hayatatokea mara moja. Polepole, kwa uthabiti, kwa uhakika, wakati unakaribia ambapo maono haya yatatimizwa. Kama inaonekana kuwa polepole, usikate tamaa, kwa kuwa mambo hayo kwa hakika yatatimia. Uwe na subira tu! Hayatakawia hata kwa siku moja.” Habakkuk 2:3 (LB) Kuchelewa sio kukanusha kutoka kwa Mungu.

Kumbuka ulikotoka, usiangalie tu umbali wa unakokwenda. Hauko pale unapotaka uwe, lakini pia hauko ulipokuwa zamani. Miaka mingi iliyopita watu walivaa kifungu chenye herufi PBPGINFWMY. Hii ilisimama badala ya “Tafaddhali vumilia, tafadhali uwe na subira, Mungu hajamaliza kazi yake kwangu bado.” Mungu bado hajamaliza na wewe, hivyo endelea kusonga mbele. Hata konokono alifika kwenye safina kwa uvumilivu!

 

SIKU YA ISHIRINI NA NANE

KUFIKIRI JUU YA LENGO LANGU

Jambo la Kutafakari: Hakuna njia ya mkato katika kukua.

KIfungu cha Kukumbuka:Mungu alianza kufanya kazi njema ndani yenu, na nina hakika ataiendeleza hadi itakapokamilika pale Yesu Kristo atakapokuja tena.” Wafilipi 1:6 (NCV)

Swali la kujiuliza: Je, ni katika eneo gani la kukua kwangu kiroho nahitaji uvumilivu na bidii zaidi?

 

 

  

 

 

 

 

 

 

 


沒有留言:

張貼留言